Wednesday, November 5, 2014

UKAWA WASAINI MAKUBALIANO MAPYA, NI KUACHIANA KWENYE UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA


VIONGOZI WA VUGUVUGU LA KATIBA YA WANANCHI, (UKAWA), WAKIONYESHA HATI YA MAKUBALIANO BAADA YA KUTIA SAINI  JUMANNE NOVEMBA 4, 2014 KWENYE OFISI ZA MAKAO MAKUU YA CUF, BUGURUNI JIJINI DAR ES SALAAM. CHINI YA MAKUBALIANO HAYO, YALIYOHUSISHA VYAMA VINNE, CHADEMA, CUF, NCCR-MAGEUZI NA NLD, YATAANZA KUTEKELEZWA KWENYE UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA UNAOTARAJIWA KUFANYIKA BAADAYE MWAKA HUU AMBAPO, UKAWA UTAMSIMAMISHA MGOMBEA ANAYEKUBALIKA KWENYE ENEO HUSIKA BILA YA KUJALI CHAMA. HATA HIVYO MWAKILISHI WA NLD HAKUWEPO NA IKAELEZWA KUWA ATASAINI BAADAYE

Sehemu yamakubaliano ya UKAWA yaliyotiwa saini
Mwenyekiti mwenza wa UKAWA, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, akizungumza kuhusu ushirikiano huo
Katibu Mkuu wa UKAWA, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa, akizungumza kwa kutumia nyaraka
Baadhi ya viongozi wa UKAWA, wakielekea kwenye ukumbi wa mkutano makao makuu ya CUF, Buguruni jijini Dar es Salaam, Jumanne Nov 4, 2014
Kutoka kushoto, Katibu Mkuu CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, wakisaini makubaliano hayo ya UKAWA
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, (Kulia), akizungumza baada ya kutiliana saini makubaliano hayo

TAARIFA KWA BLOGERS WOTE TANZANIA

http://3.bp.blogspot.com/-nVd6D5O3TK4/VFpxCgJnpQI/AAAAAAAGvqE/ulDVmljibuc/s640/1415213231614_Screenshots.png