Wednesday, August 27, 2014

OLIVER MTUKUZI AONYESHA MATOKEO YA VIPIMO VYAKE VYA UKIMWI HADHARANI


Mwanamziki mkongwe Oliver Mtukudzi, ameonyesha hadharani matokeo ya vipimo vyake vya ugonjwa wa ukimwi baada ya kuwepo kwa maneno maneno mtaani kwamba mwanamziki huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 60 kuwa mgonjwa wa ugonjwa huo hatari.

Hata hivyo katika majibu ya vipimo hivyo mwanamziki huyo alionekana kutokuwa na ugonjwa huo, alikiri kuwa ndugu zake wengi wamefariki kwa ugonjwa huo, lakini yeye anasumburiwa na ugonjwa wa kisukari na sio mwathirika wa Ukimwi.

DAKTARI KANJANJA AKUTWA NA MAITI DUKA LA DAWA ALILOGEUZA KAMA HOSPITALI


UKANJANJA! Jeshi la Polisi wilayani Ikungi, Singida linamshikilia daktari anayedaiwa kuwa ni feki, Prosper Samson (pichani) kwa madai ya kumtibu mgonjwa Jibuli Mahende, mkazi  Kijiji cha Iyumbu, Sepuka na kumsababishia kifo chake

Habari zinadai kuwa, Jibuli alifariki dunia hivi karibuni baada ya kutibiwa na mtu huyo anayejiita daktari kutokana na kile kilichodaiwa kuwa alizidishiwa dozi kwa kuongezewa chupa tisa za maji ya drip sanjari na vidonge sita ambavyo havikujulikana jina mara moja.

HISTORIA YA MAREHEMU
Kwa mujibu wa ndugu, marehemu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua, kiuno na mgongo ambapo daktari huyo alimpa dawa hizo muda mfupi baadaye Jibuli alipoteza maisha akiwa kwenye duka la dawa, nyumbani kwa Prosper.

GANGA MKUU WA WILAYA ASIMULIA
Akizungumza kwa niaba ya mganga mkuu wa Wilaya ya Ikungi, mmoja wa madaktari wa wilaya hiyo, Philip Kitundu alisema tukio hilo lilitokea juzikati saa nne asubuhi kwenye vyumba maalum vilivyotengwa na daktari huyo kwa ajili ya kutolea huduma mbalimbali za matibabu.

“Baada ya kupewa taarifa za kifo hicho na utete wake, kesho yake tulikwenda kukagua duka la dawa la mtu huyo,” alisema daktari huyo.

Kwa mujibu wa daktari huyo, walipofika dukani kwa Prosper anayejitangaza kuwa ni daktari wa magonjwa ya binadamu, walilikagua na kugundua kuwa hakuwa na leseni kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) inayomruhusu kufanya biashara hiyo na alikiri kuwa hakuwa na cheti  cha chuo chochote alichosomea udaktari.

“Hata tulipopekuwa dukani kwake tulikuta dawa ambazo haziruhusiwi kabisa kwenye maduka ya dawa muhimu, tulikuta dawa na sindano na dawa za vidonda. Alikuwa anawafunga vidonda watu, analaza na anatoa huduma za kujifungua kwa akina mama,” alifafanua daktari huyo.

YADAIWA NI MTU WA TATU KUFA
Daktari huyo wa wilaya aliongeza kusema kwamba katika ukaguzi huo walikuta pia dawa zilizokwisha muda wake wa matumizi na kuwa tukio la Jibuli kupoteza maisha ni la tatu kwa watu waliopatiwa matibabu katika duka hilo, wawili walifia nje ya duka.

MTUHUMIWA ATOA MAELEZO
Kwa upande wake daktari huyo anayedaiwa ni feki, licha ya kukiri kumpokea mgonjwa huyo akiwa na hali mbaya na kwamba baada ya kuchukua historia yake aligundua alikuwa akisumbuliwa na kifua na kabla ya kupelekwa kwake alianza matibabu kwa waganga wa tiba asilia.

“Walikuja kwangu ili wapate ushauri lakini jinsi nilivyomwona mgonjwa nikawashauri wafanye mikakati apelekwe sehemu nyingine kwani niligundua ana matatizo tangu Juni, mwaka jana,” alisema Prosper.

MTOTO WA MAREHEMU NAYE ANENA
Naye mtoto wa marehemu Jibuli aitwaye Jilala alisema siku ya tukio asubuhi alikwenda kumsalimia baba yake na kumkuta akiwa hoi, ndipo alipoamua kumpeleka kwenye duka hilo la dawa ambapo baada ya uchunguzi wa ‘daktari’ huyo aliambiwa baba yake alisumbuliwa na kifua, mgongo na kiuno.

“Baada ya dokta kunifahamisha ugonjwa unaomsumbua baba, niliondoka kurudi nyumbani kutafuta fedha za kumuondoa pale dukani ili  kumpeleka Hospitali ya Mkoa wa Singida kwa matibabu zaidi,” alifafanua mtoto huyo.

Akaendelea: “Hata hivyo, kabla ya baba hajapoteza maisha alipokuwa dukani kwa dokta alipewa vidonge sita vya dawa ambazo sikufahamu zinatibu ugonjwa gani na ilipofika saa nne asubuhi alifariki dunia, nikamsusia na kuita watu kuja kuiona maiti ya baba.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, SACP Godfrey Kamwela amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

TIZAMA MKUTANO WA VIONGOZI WA TAKUKURU KATIKA PICHA


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa viongozi wa TAKUKURU unaofanyika katika ukumbi wa Kuringe.

Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Dk Edward Hosea akizummza wakati wa Mkutano wa mkuu wa mwaka wa viongozi wa TAKUKURU .
Mkurugenzi wa idara ya elimu TAKUKURU ,Marry Mosha akitoa neno la shukurani mara baada ya mgeni rasmi kufungua mkutano huo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama akiteta jambo na Mkurugenzi wa TAKUKURU Dk Edward Hosea.
Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa wa Kilimanjaro pia walikuwa waalikwa katika mkutano huo.
Baadhi ya washiriki katika mkutano huo.
Dk Hosea akitoa zawadi kwa mgeni rasmi RC ,Gama.
Makundi mbalimbali yakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo.Na Dixon Busagaga wa Globu ya jamii kanda ya kaskazini.

RAIS KIKWETE AWAITA UKAWA IKULU....ATAKA MAMBO YENYE UTATA YAWEKWE KANDO


RAIS Jakaya Kikwete amesema yupo tayari kukutana na viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), ili kunusuru mchakato wa Katiba mpya.
 Kauli hiyo ya Rais Kikwete imekuja siku chache baada ya baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani kupinga hatua ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumtuma Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana, kusaka suluhu na viongozi wa Ukawa.Akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro juzi, mara baada ya kusoma risala yao na kuunga mkono Bunge la Katiba, Rais Kikwete alisema    hana sababu ya kutokutana na viongozi waliosusia vikao vya Bunge. Alisema kutokana na hali hiyo, yupo tayari kukutana nao, na kwamba wanajua namna ya kukutana naye ili waweze kufanya mazungumzo yatakayoliwezesha taifa kupata Katiba mpya.
 
“Mimi sina tatizo la kukutana nao. Wanajua jinsi ya kukutana nami ili tuweze kutafuta namna ya kumaliza tofauti hizi.
“Mimi naishi kwa matumaini. Naamini kuwa tutafika mwisho vizuri. Mchakato ni mgumu, lakini barabara ndefu haikosi kona. Tukidhamiria kweli kweli tutafika tuendako vizuri,” alisema Rais Kikwete.
Alisema anasikitishwa na tofauti za viongozi wa siasa na kuleta mfarakano kwa taifa, hali ya kuwa tangu awali aliwaambia kuwa wakijiruhusu kushindana na kuviziana ni wazi mchakato wa Katiba utakwama.
“Niliwaambia kuwa Katiba inayotafutwa siyo Katiba ya CCM, ama ya Chadema, ama ya NCCR, ama ya CUF. Niliwaambia kuwa hii ni Katiba ya wananchi wa Tanzania. Ni vyema tukakubaliana kuwa yenye kutugawa tukayaacha kwa sasa na kukubaliana kwa yale ambayo hatuna tofauti,”alisema.
Awali akisoma risala ya wanafunzi kwa Rais Kikwete, Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Boniface Juma, alisema wanaunga mkono mchakato wa Bunge Maalumu la Katiba kwa kuridhishwa na hatua iliyofikiwa.
 
“Mheshimiwa Rais, tunaridhishwa sana na hatua iliyofikiwa na Bunge Maalumu la Katiba, tunaamini kuwa mwafaka unawezekana kwa vipengele vingine vya Rasimu ya Katiba. Na imani yetu theluthi mbili za kupitisha Katiba Mpya inawezekana kupatikana,” alisema Juma.
 
TCD kuteta na JK
Wakati huo huo, taarifa kutoka Dodoma zinaeleza kuwa Ukawa watakutana wiki hii na Rais Kikwete kuzungumzia suluhu kuhusu mchakato wa Katiba mpya.
 
Julai mwaka huu, Ukawa walikacha mazungumzo na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi na Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta na hatimaye kugomea mchakato huo kwa kutohudhuria vikao vya Bunge hilo.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), John Cheyo, alisema azimio la kutaka kuonana na Rais Kikwete ni baada ya mazungumzo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam Agosti 23, mwaka huu na kuhudhuriwa na wenyeviti wa vyama vyote.
 
Cheyo alikataa kusema ajenda zitakazozungumzwa katika kikao hicho na Rais, lakini alisema jambo kubwa ni kuhusu mchakato wa Katiba mpya.
 
Alisema kikao cha maazimio ya kukutana na Rais kiliwakilishwa na viongozi mbalimbali ambapo CCM, iliwakilishwa na Katibu Mkuu wake, Kinana, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba na Makamu wake, Magdalena Sakaya na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
 
“Viongozi wa vyama vya siasa vinavyounda TCD waliketi katika mkutano wa wakuu wa vyama ambapo kwa pamoja walijadili na kutafakari maendeleo ya mchakato wa Katiba mpya.
 
“Viongozi hao katika kikao hicho, pamoja na mambo mengine, waliazimia kutafuta nafasi ya kuonana na Rais kwa lengo la kushauriana naye ambapo Rais amelipokea ombi hilo na ameahidi kuonana na viongozi hao mwisho wa wiki hii,” alisema Cheyo.
 
Hata hivyo, Cheyo, ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Magharibi (UDP), alipoulizwa ni kitu gani wanakwenda kuzungumza na Rais wakati mchakato wa Katiba umefika mbali, na nini kimeonekana kimekwenda sivyo hadi kufikia hatua ya kuomba kukutana naye kwa mashauriano, alikataa kuzungumzia hilo.
 
Alisema ajenda za kikao hicho ni siri, na kwamba viongozi wa vyama, walikubaliana kutosema hadi pale mazungumzo hayo yatakapokwisha.
 
“Nimesema ni kuhusu mchakato wa Katiba, hayo mambo mengine mtajazia wenyewe, si mnayajua,” alisema Cheyo.
 
Katibu Ukawa anena
Akizungumzia uamuzi wa kukutana na Rais Kikwete, Katibu wa Ukawa ndani ya Bunge, Julius Mtatiro, alisema suala la maridhiano kwa nia ya kupatikana Katiba mpya ni jambo jema ambalo halina matatizo kwao.
 
“Sisi hatuna matatizo na kukutana na Rais na tunajua kuwa kuna utaratibu ambao unatakiwa kufuatwa, hivyo endapo utashughulikiwa, tuko tayari kuonana na Rais ili tunusuru hali ya mvutano inayoendelea,” alisema Mtatiro.
 
Alisema kitendo cha Ukawa kususia mchakato huo ni kwa manufaa ya umma, kwani Katiba itakayoandikwa itakuwa ya Watanzania wote, hivyo ni vyema kuwa na Katiba ambayo itakubalika na wananchi.

MANISPAA YA IRINGA WAIPIKU MANISPAA YA MOSHI KWA USAFI



14tngfst
Manispaa ya Iringa imefanikiwa kuwa ya kwanza kwa usafi na kuchukua tuzo kwa kuipiku manispaa ya Moshi ambayo ina tuzo lukuki kwa usafi na kuwa mfano wa kuigwa na manispaa zingine nchini. Ingawa mwaka huu imepata upinzani mkali kutoka kwa Manispaa ya Iringa ambayo ndiyo imefanikiwa kuwa namba moja kwa usafi lakini manispaa ya Moshi imesema kuwa wao bado washindi.
Victoria Simakundi ambaye ni Afisa Afya wa Manispaa ya Moshi amesema kuwa vigezo viliyoweka vya usafi havihusu usafi tu moja kwa moja kuna masuala ya bajeti pamoja na masuala ya kuweka vitu vipya vya usafi.
7tngfst
Ameongeza kwa kusema Manispaa ya Iringa walikua chini hivyo kuna vitu ambavyo wameweza kuvipata kwa sasa na vinaonekana vipya lakini vitu kama hivyo Manispaa ya Moshi walishavifanya siku za nyuma.
Kuhusu watu wanaochafua Manispaa ya Moshi kuna adhabu amabazo wameziweka ambazo zinaanzia kiasi cha 10,000 hadi 50,000,Manispaa ya Moshi imeshika nafasi ya pili mwaka huu baada ya Manispaa ya Iringa.
2tngfst
Tangu mashindano haya yaanzishwe mwaka 1984 Manispaa ya Moshi imekuwa ikishika nafasi ya kwanza na katika miaka yote,ingawa imeshika nafasi ya pili mara mbili  katika miaka hii 30 ya mashindano haya.
Picha za tuzo zilizopata manispaa ya Moshi mpaka sasa.
10tngfst

11tngfst


FLORA MBASHA AFUNGUKA KUWA ANA MIMBA YA MBASHA NA SI YA MCH: GWAJIMA

Muimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania ambae pia ni Mke wa Emmanuel Mbasha amefunguka na kusema kuwa hana mahusiano yoyote ya kimapenzi na na Mchungaji wa Kanisa la kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima,
 
 mbashaz
Muimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania Flora Mbasha akichat Live katika ukurasa wa Facebook wa EATV.
Flora amesema hayo leo alipokuwa akichat Live kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live kinachofanyika kila siku ya Jumatano kuanzia saa Sita kamili.
Flora amesema kuwa hawezi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu ambae ni ndugu yake hivyo

Mchungaji Gwajima ni mjomba wake na si mpenzi wake kama ambavyo watu wamekuwa wakizusha kwa lengo la kumchafua na kumshushia hadhi."Hayo ni maneno tu ya watu mtaani ila Mchungaji
Gwajima ni mtumishi wa Mungu na ni uncle wangu ninawezaje kuwa na mahusiano na uncle wangu..? "Alihoji Flora.

wakati akijibu ya maswali ya mashabiki ambayo mengi yao yalikuwa yakimtuhumu na huku watu wengi wakitaka kujua ukweli juu ya ugomvi uliopo kati yake na Mumeo kama ni kweli au ni skendo tu za magazeti,Flora aliweka wazi kuwa kuna vyombo vya habari ambavyo vimekuwa na lengo la kumchafua na kumualibia sifa ndio maana walitumia gharama kubwa kufanya wanavyoweza ili kutimiza malengo yao,mbasha amedai kuwa alimua kukaa kimya kwa kuwa hakukuwa na ukweli wowote.

"Hizo stori mnazosikia hazina ukweli wowote na ndio maana niliamua kukaa kimya sikutaka kujibizana kwenye vyombo vya habari kwa uongo wa

baadhi ya magazeti ya udaku ila ninasikitika sana kwani kuna watu wamekaa na kujipanga kisawa sawa kwa ajili ya kuhakikisha wanaharibu huduma yangu kwa gharama zozote, lakini bado ninasonga mbele kwani mwanzilishi wa huduma yangu ni Mungu na huyo ndiye atakayeimaliza na sio mwanadamu. hata hivyo ninawashukuru kwa kuwa wamenitabilia nkuja kumiliki jumba na magari ya kifahari ingawa yote ni ubatili"



SIJAACHANA NA MBASHA KISA GWAJIMA
Flora Mbasha amesema kuwa watu wengi wanasema kuwa ameachana na Mumewe kisa Gwajima hilo swala halina ukweli wowote hajaachana na Mbasha sababu ya Gwajima na amedai kuwa bado anampenda sana ila anampenda Mungu zaidi.bali amekuwa na matatizo katika ndoa yake kati yake na mumewe na ni matatizo yao ya ndani ambayo asingependa kuyaweka wazi katika vyombo vya habari maana kufanya hivyo ni sawa na kumvunjia heshima mumewe,maana mambo ya chumbani ni siri yao wenyewe asingependa kuwa wazi sababu wanamtoto mkubwa sasa.

"Sijamwacha mume wangu sababu ya Gwajima na kweli bado napenda sana Mbasha lakini nampenda zaidi Mungu"

Wakati anazungumzia suala hili Flora ameweka wazi kuwa kwa sasa ni mjamzito na ujauzito huo ni wa Mume wake ambae ni Emmanuel Mbasha maana ameishi nae katika ndoa zaidi ya miaka kumi na katika kipindi chote hicho hajawahi hata siku moja kumsaliti Mumewe na kwenda kwenye michepuko hivyo huo ujauzito ni wa Mume wake Emmanuel Mbasha na siyo Gwajima.

MWANAFUNZI ABAKWA DAR


Denti wa darasa la saba aliyebakwa na muuza genge anayefahamika kwa jina la Juma Athumani (30)

 Kwenye Kituo cha Polisi cha Maturubai kilichopo Mbagala, Dar kuna faili la kesi namba MBL/RB/ 9817/2014- KUFANYA MAPENZI NA MWANAFUNZI ambalo linamsaka kijana Juma Athumani (30), mkazi wa Charambe, Mbagala kwa kosa la ubakaji wa mwanafunzi wa darasa la saba. Habari za kiintelijensia zilidai kwamba mtuhumiwa huyo ambaye ni muuza genge, alitenda kosa hilo Agosti, mwaka huu ambapo mwanafunzi huyo alikuwa ametumwa na mama yake gengeni.Ilisemekana kwamba jamaa huyo alimuomba denti huyo wazungumze kidogo ndipo akampeleka gesti kwa lazima. 

Akizungumza na wanahabari za mastaa na kijamii, mwanafunzi huyo alisema kuwa alipofika gesti, jamaa huyo alilipa fasta na kumvutia chumbani ambapo alianza kumshika maziwa yake kisha akamtupia kitandani na kumwingilia kimwili bila ridhaa yake.
Mama wa mwanafunzi aliyebakwa.
 Alisema kwamba, jamaa alipomaliza shida zake, alimpa tsh elfu tano (5,000/=) lakini alipokataa huku akilia ndipo mwanaume huyo akamuongezea hadi ikafika elfu kumi (10,000/=).
“Niliporudi nyumbani mama aliniuliza kwa nini nimechelewa kisha akaziona hela, akaniuliza nimezipata wapi, nikamwambia amenipa Juma ndiyo tukaenda hadi gengeni kwa Juma kuuliza ndiyo mama akagundua kuwa nimebakwa. 
“Baadaye mama alikwenda kuripoti polisi ndipo Juma akakamatwa na mimi nikapelekwa hospitali na kugundulika kweli nilikuwa nimebakwa,” alisema mwanafunzi huyo.
Habari zilizotufikia punde zilidai kwamba uchunguzi wa polisi unaendelea ili sheria ichukue mkondo wake.

RAIA WA ETHIOPIA AFARIKI DUNIA KWENYE KITUO CHA AFYA CHA CHALINZE KATA YA BWILINGU WILAYA YA BAGAMOYO MKOANI PWANI.


RAIA wa nchi ya Ethiopia Dawita Alalo (25) amekufa alipokuwa akipatiwa matibabu kwenye kituo cha afya cha Chalinze kata ya Bwilingu wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.Marehemu alikuwa ni kati ya raia 48 wa nchi hiyo walikamatwa wakiwa kwenye msitu wa kijiji cha Visakazi Ubena Zomozi tarafa ya Chalinze Agosti 22 mwaka huu, baada ya kuingia nchini bila ya kibali.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha kaimu kamanda wa polisi mkoani humo Mrakibu Mwandamizi (SSP) Athuman Mwambalaswa alisema kuwa marehemu ni miongoni mwa wahamiaji haramu 11 waliokuwa wamelazwa kituoni hapo wakipatiwa matibabu.

Kamanda Mwambalaswa alisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 26 majira saa 7:30 usiku alipokuwa akipatiwa matibabu kituoni hapo baada ya kuugua ugonjwa wa malaria.

Wakati huo huo mlinzi wa baa ya Silent Inn Jamat Mandama (55) amefariki dunia baada ya kunywa pombe nyingi bila ya kula chakula.

Alisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 27 mwaka huu majira ya saa 1 usiku huko Umwe kata ya Ikwiri wilayani Rufiji.

Aidha alisema kuwa mlinzi huyo alikutwa amekufa akiwa lindoni kwenye baa hiyo.