Wednesday, August 20, 2014

SITTA AKUTANA NA WAANDISHI KUZUNGUMZIA MAENDELEO YA KAMATI ZA BUNGE MAALUM


mkiti 1
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Samuel Sitta akizungumza na waandishi wa habari alipokutana nao leo kuhusu muhtasari wa kikao cha Kamati ya Uongozi wa Bunge hilo kilichokaa leo kutathmini kazi za kamati 12 za Bunge hilo lilipofikia pamoja kuridhia baadhi ya maependekezo ya kuongeza ibara na sura ndani Rasimu ya Katiba katika Kamati zao.
mkiti 2
mkiti 3

MAMA AMCHANA MWANAWE WA MIEZI MIWILI NA VIWEMBE SEHEMU YA HAJA KUBWA BAADA YA MTOTO KUZALIWA AKIWA HANA



Vitendo vya baadhi ya wananchi kujitibu pasipo kufuata maagizo na njia za kitaalamu vimeendelea kukithiri nchini ambapo hapa jijini Mwanza mama mmoja ameamua kumchanja kwa viwembe mwanae mwenye umri wa wiki mbili baada ya
mtoto huyo kuzaliwa akiwa hana sehemu ya Haja kubwa.

Tukio hilo limetokea hivi karibuni baada ya mama huyo aliyefahamika kwa jina la Anastazia Ngilitu kumchana kwa wembe zaidi ya mara tatu ili kumsaidia mwanae kupata haja kubwa kwa kile kilichodaiwa mtoto huyo kuzaliwa akiwa hana sehemu
ya haja kubwa.

Akiongea kwa uchungu mama huyo mkazi wa Tabora aishie jiini mwanza kwa sasa amesema kuwa alijifungua watoto mapacha watatu ndani ya Mtaro kisha wawili kufariki alipofikswa Hospitali na kusalia mtoto mmoja aliyekutwa na tatizo la Kutokuwa na sehemu ya haja kubwa.

Sambamba na hayo mama huyo amesema kuwa sababu za kumchana na wembe mwanawe ni baada ya kumuona mtoto wake anashindwa kupata haja kubwa hali
iliyopelekea tumbo kujaa na kulia.

Ameongeza kuwa wakati wa kujifungua mtoto huyo walimfanyia upasuaji katika hospitali ya Bugando ila hali ya kuziba ilijirudia tena na kuamua kumchana kwa
kutoakana na kutokuwa na uwezo wa kulipia gharama za upasuaji hospitali.

Katika hatua nyingine Mama huyo amesema kuwa kwa sasa hali yake ya Maisha siyo nzuri kwani watoto wake wanaishi kwa kunywa maji na kwamba hapo awali alikuwa anafanya kazi ya kufua nguo kwenye nyumba za watu ila kwa sasa hawezi
kutokana na kuwa na mototo mdogo.

Sambamba na hayo mama huyu anasema kuwa licha ya kuolewa na wanaume watatu kwa wakati tofauti na kila mmoja kumnyanyasa kwa kumpiga na mwingine kumdhurumu pesa zaidi amesikitishwa na kitendo cha Mume wake wa sasa hivi kumtaka kufanya mapenzi ikiwa tumbo la uzazi halijakaza hali anayotaja kumsababishia maumivu makali na kutokwa na damu nyingi baada ya mumewe
kumpiga.

 
Kitendo cha mama huyu kumchana mtoto wake kwa wembe kinatoakana na hofu ya kwenda hospitali kwani anasema hana uwezo wa pesa kwani kwa sasa yeye mwenyewe anasumbuliwa na uvimbe katika titi lake la kushoto na alipoenda Hospitali ya SEKOTURE aliambiwa gharama za upasuaji ni shilingi elfu 30 na
alipokosa alirudi nyumbani na kuendelea kujitibu kwa dawa za kienyeji.

Kwa upande wao baadhi ya kina majirani ambao wamekuwa wakimpa msaada mama huyu mara kwa mara,Wamesema kuwa mama huyu ana maisha magumu kwani mume wake humpiga na kumfukuza mara kwa mara hali inayomfanya aishi kwa kuomba omba na wakati mwingine kulala na watoto wake
bila kula.

 
Taarifa za awali zinaonyesha kuwa mama huyu aliolewa na mume wa kwanza mkazi wa eneo la maji moto mkoani Mara na waliachana baada ya kupigwa na kuchomwa kisu tumboni ikiwa ni pamoja na kupigiliwa msumali wa nchi sita katikati ya mkono
wake wa kushoto ikiwa ni sambamba na kumvuta hereni akimwambia kuwa ni dalili za kuwa malaya hali iliyomsababibishia masikio yake kuvimba.

Mume wa pili aliyemuoa mama huyo inaelezwa kuwa yeye alimdhurumu kiwanja walichouza milioni moja na laki saba kilichokuwa eneo la makaburi Bwiru kisha
kuzichukua na kuaga kwenda kuzifanyia biashara.

Kuhusu ndugu Bi Anastazia amesema kuwa wazazi wake wote wamefariki na kwamba aliyebaki ni bibi yake ambaye naye anamtaja kuwa ni mchawi kwani wakati alipoenda Tabora,bibi yake alimwambia ampe mkono wa mtoto ili usiku wa manane
amuamshe kwa kumpiga nao kichwani ili aende kazini.

Anastazia anasema kuwa kutokana na matatizo hayo aliwahi kushauriwa kumtupa mtoto huyo eneo la vichakani soko la sabasaba,ushauri aliopewa na rafiki yake mkazi wa Ilemela aliyemtaja kwa jina moja la Amina ambaye alimwambie mtoto wako hatapona,Jambo ambalo yeye alikataa na kusema kuwa anaogopa mkono wa Sheria.

Tatizo linalomsumbua mama huyo kwa sasa ni chakula na matibabu kwa mwanaye na yeye mwenyewe anayesumbuliwa na uvimbe katika titi la kushoto na kuwaomba wasamalia wema kumsaidia ili aendelee na shughuli zake aondokane na
kuombaomba.


MWONEKANO WA MASIKIO YAKE BAADA YA KUVUTWA HELENI NA MUMEWE WA KWANZA.

PAPA FRANCIS AJITABILIA KIFO



Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis kwa mara ya kwanza ametabiri hatima ya maisha yake duniani akisema kuwa anaamini Mungu anaweza kumpa muda wa miaka miwili au mitatu ya kuishi.Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ndege wakati akitoka ziarani Korea Kusini kurejea Vatican, Papa Francis alisema suala la kuendelea kuishi ni neema ya Mungu.

 Suala hili naliona kama neema tu ya Mungu kwa watu wake. Najaribu kutafakari kuhusu dhambi zangu na makosa yangu, siwezi kujivuna. Najua kwa sababu hali hii itadumu kwa muda mchache. Miaka miwili au mitatu nitakuwa nimeondoka na kwenda nyumbani kwa baba
alisema.Papa Francis (77), pia alizungumzia uwezekano wa kustaafu endapo atahisi kwamba afya yake hairuhusu kuendelea na kazi. 
Utamaduni wa kuachia madaraka ndani ya kanisa hilo linalotajwa kuwa na waumini wengi duniani uliasisiwa upya mwaka jana na mtangulizi wake, Papa Benedict XVI aliyeng’atuka kutokana na matatizo ya kiafya.Pamoja na kwamba Papa Francis hajawahi kuzungumza hadharani kuhusu ni lini pengine anaweza kufariki dunia, lakini baadhi ya vyanzo vya habari kutoka Vatican vinasema kuwa kiongozi huyo amekuwa akiwaambia watu wake wa karibu kuhusu siku zake chache zilizosalia duniani. 
Wachambuzi wa masuala ya kiimani kwa nyakati tofauti walisema huenda kiongozi huyo ana tatizo la kiafya ambalo halijawekwa wazi.Wakati hayo yakiendelea taarifa za ndani zinabainisha kwamba kiongozi huyo aliwahi kutolewa pafu moja baada ya kuathirika wakati akiwa kijana nchini Argentina

MAGAVANA WA BENKI YA PTA KUKUTANA TANZANIA


01
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Stephen Wasira (katikati) alipokuwa akiongea na waandishi wa habari jana mjini Dodoma juu ya mkutano wa 30 utakaofanyika      nchini mwishoni wiki hii. Kushoto ni Rais wa Benki ya Maendeleo ya Kusini na Mashariki ya Afrika (PTA), Admassu Tadesse na kulia ni Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba. 02

03Rais wa Benki ya Maendeleo ya Kusini na Mashariki ya Afrika (PTA), Admassu Tadesse (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana kuhusu mkutano wa miaka 30 ya wanahisa na magavana utakao shirikisha nchi 18 za Afrika, mkutano huo utafanyika kesho jijini Dar es Salaam. Katikati ni Waziri wa Ofisi ya Rais (Uratibu na Mahusiano), Steven Wasira akifuatiwa na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba. 04
05Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Stephen Wasira (kushoto) abibadilishana mawazo na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Kusini na Mashariki ya Afrika (PTA),  Admassu Tadesse mara baada ya mkutano na waandishi wa habari jana mjini Dodoma. Katikati ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile.
Na Eleuteri Mangi- MAELEZO
19/082014
Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Biashara Mashariki na Kusini mwa Afrika (PTA) itakuwa mkutano wa mwaka utakaofanyikia nchini jijini Dar es salaam tarehe 22 mwezi huu.
 
Hayo yamebainishwa jana mjini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Stephen Wasira alipokuwa akiongea na waandishi wa habari juu ya mkutano huo utakaofanyika mwishoni wiki hii.
 
“Huu ni mkutano wa kawaida wa mwaka wa Bodi ya Magavana wa nchi wanachama pamoja na Mawaziri wa Fedha, Tanzania ni mwanachama ndio maana mkutano wa 30 unafanyika hapa” alisema Wasira.
 
Wasira amesema kuwa katika mkutano huo mada mbalimbali zitajadiliwa ikiwemo masuala ya fedha na uchumi, maendeleo ya benki ya PTA na mafanikio yake kwa nchi washirika.
 
Vile vile Wasira amesema kuwa PTA ni benki ya Kiafrika na inafanyakazi nzuri ambapo inaonesha inakua kwa zaidi ya asilimia 30 kwa mwaka kwa miaka kadhaa hadi sasa na imekuwa na mizania ya Dola za Kimarekani mil. 2.8 ikiwa miongoni mwa benki za maendeleo zinazofanya vizuri katika bara la Afrika.
 
Aidha, Wasira ameongeza kuwa mkutano huo utatanguliwa na semina ya wafanyabiashara itakayofanyika Agosti 21 siku moja kabla ya mkutano mkuu wa Magavana hao ambapo Serikali itawakilishwa na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba.
 
Kwa upande wake Rais na Mtendaji Mkuu wa benki ya PTA Admassu Tadesse amesema kuwa Tanzania imekuwa mstari wa mbele na ni mwanachama hai ambapo imekuwa mfano mzuri kwa nchi wanachama kwa kutoa michango mbalimbali kwa wakati.
 
Zaidi ya hayo, Tadesse amesema kuwa benki hiyo mwaka huu inaadhimisha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake, Tanzania imepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa mkutano wa mwaka huu ili washerehekee na Watanzania.
 
Tadesse amesisitiza kuwa Benki ya PTA inatoa huduma zake kwa nchi wanachama ikiwa na lengo la kuwa tasisi ya kifedha inayoongoza Mashariki na Kusini mwa Afrika katika utoaji wa huduma za kibenki.
 
Benki ya PTA ilianzishwa mwaka 1985 ambapo hadi sasa ina jumla ya wanachama 22 ikiwemo nchi 18 ambazo ni Burundi, Comoros, Djibouti Congo, Kenya na Malawi.
 
Nchi nyinine ni Misri, Eritrea, Ethiopia, Mauritania, Rwanda, Seychelles, Somalia, Sudan, Uganda, Zambia, Zimbabwe na mwenyeji Tanzania
 
Aidha, PTA inashirikiana na nchi nyingine nje ya bara la Afrika ambazo ni Belarus na China.
Washirika wengine ni Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB), Kampuni ya Bima ya Mauritia iitwayo Eagle na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Mauritius.
 
Mkutano wa mwaka huu unafanyikia Tanzania ikiwa ni utaratibu wa benkiya PTA kufanya mikutano ya mwaka kwa mzunguko ambapo washiriki watakuwa Mawaziri wa Fedha, Magavana wa nchi wanachama, sekta binafsi, Mabalozi wanaowakilisha nchi mbalimbali nchini na Wawakilishi wa Mashirika ya kimataifa. 

MRADI WA KUZUIA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA KWA WANAWAKE WAZINDULIWA JIJINI MBEYA



Naibu Meya wa Jiji la Mbeya Chifoda Yesaya Fungo akizindua Mradi wa kuzuia ukatili wa kijinsia kwa wanawake katika ukumbi wa Halmashauri jiji Mbeya

Mrtibu wa MBEPAU Jane Lawa akitoa maelezo mafupi jinsi mradi huo utakavyofanya kazi kwa kushirikiana wadau mbalimbali katika jamii


Mratibu wa NGOS Victor Kabuye akifafanua zaidi jinsi mradi huo utakavyofanya kazi karibu na jamii 




 Chifu Kiongozi wa Kabila la Kisafwa Bwana Roketi Mwanshinga akitoa neno la shukrani kwa waratibu wamradi wa MBEPAU kuwa wameupokea mradi huo kwa mikono miwili na sasa kazi tu kushirikiana kutokomeza vitendo vya ukatili wa kinjinsia



Baadhi ya wageni waalikwa katika uzinduzi wa mradi huo wakimsikiliza kwa makini mgeni rasmi


MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAKRISTO MKOA WA MBEYA AKITOA NENO LA SHUKRANI


PICHA YA PAMOJA MARA BAADA YA KUZINDULIWA KWA MRADI HUO

Picha na Mbeya yetu

RASIMU YA KATIBA MPYA YA JAJI JOSEPH WALIOBA YACHANWA CHANWA DODOMA



Mwenyekiti wa Kamati Namba Tano ya Bunge la Katiba, Hamad Rashid akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana. Kulia ni makamu mwenyekiti wa kamati hiyo Assumpta Mshana. Picha na Emmanuel Herman

Dodoma.
Kuna kila dalili kwamba mabadiliko mengi yaliyopendekezwa katika Rasimu ya Katiba yakigusa miundo ya taasisi nyeti za umma yatawekwa kando na huenda Bunge Maalumu likatoa Katiba isiyokuwa na mabadiliko makubwa kama ilivyotarajiwa.

Gazeti hili limebaini kuwa kamati nyingi za Bunge hilo zimebadili mapendekezo mengi hasa yanayowagusa viongozi na taasisi nyeti kama Bunge, tofauti na ilivyopendekezwa katika Rasimu ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya uongozi wa Jaji Joseph Warioba.


Miongoni mwa mambo ambayo yamependekezwa kurejeshwa kama yalivyokuwa ni muundo wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambalo kwa mujibu taarifa kutoka kwenye kamati mbalimbali, ni kuendelea na muundo wa sasa unaowajumuisha wabunge kutoka Zanzibar.


Katika maelezo yake, Jaji Warioba alisema moja ya kero za muungano katika eneo la Bunge ni malalamiko kwamba wabunge kutoka Zanzibar wamekuwa wakishiriki katika Bunge la Muungano na kushiriki kujadili mambo yanayohusu Tanzania Bara.


Kupitia mfumo wa Serikali tatu, Rasimu ilikuwa na mapendekezo ya kuwapo kwa Bunge la Muungano lenye wabunge 75, lakini mapendekezo hayo pia yamefutwa katika kamati karibu zote na kurejesha mfumo wa sasa pamoja na uwapo wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar.


Mwenyekiti wa Kamati Namba Tano, Hamad Rashid Mohamed alisema jana kuwa suala la muundo wa Bunge lilisababisha mvutano mkubwa katika kamati yake na baadhi ya wajumbe walikuwa wakihoji uwakilishi mkubwa wa wabunge wa Zanzibar katika Bunge la Muungano hata kwa mambo ya Tanzania Bara.


Hata hivyo, alitetea hali hiyo akisema uwapo wa wabunge kutoka Zanzibar ni moja ya masharti yaliyowekwa na Katiba. “Hata Katiba ya sasa imeweka sharti la idadi ya wabunge wa Zanzibar, hilo nalo ni sharti la Katiba huwezi kuliondoa, kama unataka kuliondoa unapotunga Katiba maana yake ni lazima uvunje muungano.”


Alisema mwaka 1964 mambo yote ya Tanganyika yaliingizwa kwenye Serikali ya Muungano... “Kwa hiyo ni lazima ukafumue Muungano, useme haya ni ya Tanganyika na haya ni ya Muungano,” alisema.


Hamad alisema katika hadidu ya rejea, Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilikatazwa kugusa mambo ya Muungano. “Hivi wabunge 70 wanaokuja kutoka Zanzibar wakazungumzia mambo ya Bara, hivi kuna dhambi gani, sioni kosa kabisa.” Mwenyekiti huyo alisema kamati yake imebaini kwamba Rasimu ya Warioba ina upungufu mwingi kwani hata baadhi ya kero zilizotajwa zilishafanyiwa kazi na Serikali.


Hoja ya ushiriki wa Wazanzibari katika masuala ya Tanzania Bara iliripotiwa kuibuka katika Kamati Namba Moja ambako mmoja wa wajumbe, Ally Keissy alinikuliwa akihoji sababu za wajumbe wa Zanzibar kushiriki mambo ambayo wao siyo sehemu yake.


Mambo mengine
Mbali na muundo wa Bunge, kamati nyingi pia zimefuta mapendekezo kadhaa yaliyomo kwenye Rasimu ya Katiba ambayo ni pamoja na wabunge kutokuwa mawaziri, ukomo wa ubunge kwa vipindi vitatu vya miaka mitano mitano, wabunge kuwajibishwa na wananchi, kupunguzwa kwa madaraka na kinga ya rais.


Katika Kamati Namba Tano, Hamad alisema suala la wananchi kumuondoa mbunge lilikataliwa. “Hivi ni kigezo gani ambacho kinaonyesha mbunge hakuweza kuwaletea wananchi maendeleo. Nini utatumia cha kupima ufanisi wa huyu mbunge?”


Alisema kuliweka jambo hilo katika Katiba ni kuleta matatizo na kwamba wameliacha suala hilo mikononi mwa vyama vya siasa kuangalia kama mbunge anafanya kazi ya ilani zao au la.



Mgawanyiko mpya
Habari zaidi zinasema kuwekwa kando kwa mapendekezo mengi yaliyolenga kurekebisha mifumo ya uongozi na utawala, kumesababisha mgawanyiko hasa miongoni mwa wajumbe watetezi wa muungano wa serikali mbili, ambao awali, waliahidiwa kwamba muundo huo usingekuwa na sura yake ya sasa, bali ungeboreshwa.


Mmoja wa wabunge wa CCM alisema jana kwamba: “Tutawapa wapinzani sifa maana umma utaamini kwamba bila wao hakuna kinachoweza kubadilika, sasa kama tunarejesha kila kitu ambacho kiko kwenye Katiba tuliyonayo kuna maana gani ya kuwa na mchakato?”


Mmoja wa wenyeviti wa kamati za Bunge Maalumu naye alisema kinachoendelea ndani ya kamati nyingi ni kufuta mapendekezo ya Rasimu na kuleta mapendekezo mapya ambayo ni sawa na yaliyomo kwenye Katiba ya sasa.


“Ndani ya chama (CCM) tuliamua kupinga mapendekezo ya serikali tatu baada ya kuahidiwa kwamba tutakuja na muundo wa serikali mbili zilizoboreshwa, lakini hata hizo hatuzioni. Kwa hiyo wananchi wataamini kwamba kilichosemwa na Ukawa (Umoja wa Katiba ya Wananchi), ni cha kweli,” alisema mwenyekiti huyo.


Utata wa akidi
Mwenyekiti wa Kamati Namba Tatu, Dk Francis Michael aliamua kuahirisha kikao jana saa tano asubuhi kutokana na kile alichokiita kuwa ni kuwapa muda wajumbe waende kusoma zaidi sura ya tisa ambayo inahusu muundo wa Bunge.


Hata hivyo, habari ambazo zilikuwa zimelifikia gazeti hili mapema zinasema kuahirishwa kwa kikao hicho kulitokana na akidi kutotimia, taarifa ambazo Dk Michael alizikanusha kwa kuonyesha idadi ya wajumbe ambao walikuwa wamesaini karatasi ya mahudhurio.


Katika maelezo yake Mwenyekiti huyo alikiri kwamba hadi ilipotimu saa 4:00 asubuhi jana kamati yake ilikuwa ikikabiliwa na upungufu wa wajumbe wanne, hivyo waliwapigia simu na kubaini kwamba walikuwa katika shughuli nyingine ikiwamo kumpokea Rais Jakaya Kikwete.


“Baadhi ya wajumbe ni mawaziri kwa hiyo baada ya kukamilisha majukumu yao walifika na saa tano hivi akidi ilikuwa imetimia,” alisema Dk Michael.MWANANCHI

RAIS KIKWETE NA MAMA SALMA KIKWETE WAHANI MSIBA WA MAREHEMU JAJI MAKAME

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweha saini katika kitabu cha maombolezo alipokwenda kutoa pole nyumbani kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kwanza wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu, Mheshimiwa Lewis Makame Masaki jijini Dar es salaam aliyefariki  katika Hospitali ya AMI Trauma Centre Jijini Dar es Salaam tarehe Agosti 19, 2014.
 Mama Salma Kikwete akiweha saini katika kitabu cha maombolezo alipokwenda kutoa pole nyumbani kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kwanza wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu, Mheshimiwa Lewis Makame,  Masaki jijini Dar es salaam aliyefariki  katika Hospitali ya AMI Trauma Centre Jijini Dar es Salaam tarehe  Agosti 19, 2014.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwafariji wafiwa walipokwenda kutoa pole nyumbani kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kwanza wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu, Mheshimiwa Lewis Makame,  Masaki jijini Dar es salaam aliyefariki  katika Hospitali ya AMI Trauma Centre Jijini Dar es Salaam  Agosti 19, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na watoto wa marehemu pamoja na Jaji Mstaafu Mark Bomani alipokwenda kutoa pole nyumbani kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kwanza wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu, Mheshimiwa Lewis Makame Masaki,  jijini Dar es salaam aliyefariki  katika Hospitali ya AMI Trauma Centre Jijini Dar es Salaam tarehe Agosti 19, 2014.

CCM YAKUBALI YAISHE, YAKUBALI KUAHIRISHA BUNGE MAALUM LA KATIBA


Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili zinasema kwamba kikao cha dharura cha CCM kilichofanyika jana kimetaka Bunge la Katiba (BMK) liahirishwe. Hii ni baada ya kujiridhisha kwamba akidi ya 2/3 kutoka Zanzibar haitatimia, hivyo ni bora kuahirisha bunge hilo kuliko kuteketeza fedha za watanzania ambazo zingetumika kubosesha huduma za jamii zilizo taabani kama vile maji, afya, miundombinu na elimu.

Chanzo:Mtanzania

CHADEMA YAKANUSHA KUHUSIKA NA KIFO CHA MWANGOSI


Mkurugenzi  wa Habari na Mawasiliano wa Chadema, John Mnyika, akizungumza na waandishi wa habari

Baadhi ya viongozi wa Chadema kutoka kushoto ni Ofisa Habari, Tumaini Makene, Mbunge wa Ubungo Mh. John Mnyika, Ofisa Mwandamizi Mafunzo na Uendeshaji, Mohamed Mtoi, na mwenye gwanda ni Katibu Mtendaji, Ofisi ya Katibu Mkuu, Victor Kimesera. Waandishi wa habari wakifuatilia taarifa ya Chadema. Jengo la makao makuu ya Chadema yaliyoko Kinondoni, Dar.
 CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimekana shutuma zilizoelekezewa kwao kuwa wanahusika na kifo cha aliyekuwa mwandishi wa habari wa Channel Ten, Daudi Mwangosi. 

Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Chadema, Mhe. John Mnyika, ameeleza kuwa hawahusiki na mauaji hayo bali ni propaganda zinazoenezwa ili kuwasahaulisha wananchi juu ya suala la katiba linaloendelea. Mnyika alieleza kuwa wanaoeneza habari hizo ni wale ambao wanataka kuizuia Chadema na Ukawa kwa ujumla kuendelea na harakati za kupigania katiba ya wananchi ikiwemo kufanyika maandamano ya kitaifa iwapo Rais Kikwete hataingilia kati kulisimamisha zoezi la katiba mpya.

WATU 16 WADAIWA KUFARIKI KATIKA AJALI WILAYANI SIKONGE MKOANI TABORA


Baadhi ya miili ya marehemu.
Watu  zaidi ya 17 wanadaiwa kufariki dunia na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa  baada ya mabasi waliokuwa wakisafiria kugongana katka k ijiji  cha Mlogolo wilayani Sikonge mkoani Tabora.
Ajali hiyo imetokea leo hii jioni majira ya saa 11 jioni baada ya Basi la Kampuni ya Sabena lenye namba za usajiri T 110 ARV lililokuwa likitokea Mbeya kwenda  Mwanza kumegongana uso kwa uso na basi la AM Dreamline lenye namba za usajiri  T 803 ATN lililokuwa likitokea Mwanza kupitia Mpanda.Ajali hiyo imetokea maeneo ya Mlogolo takribani kilometa 3 kutoka wilayani   Sikonge.Pia inadaiwa kuwa dereva wa basi la Sabena aliyefahamika kwa jina la James Kombe amepoteza maisha baada ya kukatika kiwiliwili na kufa papohapo a kuwa jitihada za kutafuta kiwiliwili chake zilikuwa zikifanyika baada ya kupondeka vibaya.
Mashuhuda wa ajali hiyo wamedai kuwa chanzo cha ajali hiyo ni madereva hao kuwa ni wasaidizi( Day-worker)
Inakadiriwa kuwa karibu robo tatu ya basi la sabena imeharibiwa vibaya sana.
Mabasi yaliyohusisha ajali hiyo ni basi la  Sabena lililokuokea  Mbeya kwenda -Mwanza na AM Dreamline lililokuokea  Mwanza kwenda Mpanda.
Jitihada za kumpata Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP). Suzana Kaganda ili kuzungumzia ajali hiyo bado zinaendelea.
 
 

TAFADHALI PICHA HIZI SI NZURI SANA

 

 
 

 
 
 
Majeruhi niwengi katika hospital ya mkoa ya Tabora
Watu waliopoteza maisha ni watu Kumi na sita.