Monday, October 13, 2014

BIBI NA BWANA HARUSI WANUSURIKA KIFO

bibi harusiBibi harusi Mariamu mduwa aliyenusurika kifo katika ajali ya mitumbwi katika kijiji cha kalalangabo akiwa naendelea na matibabu katika hospital ya  mkoa wa Kigoma

 
 
 
wawili hawa wamenusurika katika ajali ya mtumbwi iliyogharimu vifo vya watua zaidi ya 10 baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama ziwa Tanganyika
Akiongea na mtandao huu katika wodu namba 5 katika Hospital ya Mkoa wa Kigoma alipolazwa bibi harusi huyo alisema kuwa alishikwa na bumbuwazi sana baada ya tukio hilo kwani mpaka sasa bado hajielewi.
”Sikumbuki kitu kwani baada ya mtumbwi kuzama kila mtu alikuwa anahangaika kujiokoa na kifo,kwakweli mimi naona kama mkosi siku ya harusi yangu watu wanakufa ila namshukuru mungu kwa kutunusuru na kifo na yote mimi nimemwachia mungu”alisema bibi harusi huyo
Muhanga mwingine aliyenusurika katika ajali hiyo Zabibu Issa alisema kuwa mitumbwi waliyokuwa wamepanda ilikuwa imejaza sana watu na mizigo ndiyo maana ilizidiwa uzito na kuzama baada ya kupigwa na wimbi.
”Safari ya kwenda kijijini kwetu lazima tupite njia za majini hakuna barabra kabisa sababu vijiji tunavyoishi vipo mwambao mwa ziwa Tanganyika kungekuwa na barabara tungepita barabrani”alisema Mhanga huyo
 


wahangaNdugu jamaa na wapambe wa bwana na bibi harusi walionusurika kifo baada ya ajali ya mtumbwi kutokea katika kijiji cha kalalangabo wakiwa wanaendelea na matibabu katika hospita ya Mkoa wa Kigoma
bibi harusi
 
Naye muuguzi wa wodi namba tano walipolazwa majeruhi hao alisema kuwa wamejuhi wote waliopo wodini hali zao zinaendelea vizuri na mpaka sasa wameshapokea jumla ya maiti sita.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kigoma Jafari Mohamed alisema kuwa mpaka sasa jumla ya watu 27 wameshaokolewa,na miili sita kuopolewa pamoja na walionusurika 11,lakini bado inahofiwa kuwa kuna miili mingine zaidi ambao bado haijapatikana kwani mitumbwi hiyo inakadiriwa kuwa ilikuwa na watu zaidi ya sabini.

 UOKOJIWaokoaji mbalimbali wakijindaa kwenda katika eneo ilipotokea ajali ya mitumbwi iliyobeba harusi kutoka kigoma mjini kwenda katika kijiji cha Kigalya kutafuta miili ya marehemu ambayo bado haijapatikana

KIJANA ATEMBEZWA UCHI MTAANI KWA KUTAFUTA PESA ZA KUFANYIWA TOHARA

Kijana mmoja nchini Kenya alilazimishwa kutembezwa akiwa mtupu mtaani ili kuchangisha fedha za kumuwezesha kufanyiwa tohara.
Hatua hiyo ilikuja baada ya kijana huyo kudai hana pesa ya kwenda kufanya tohara na wanaume wenzake kuamua kumtembeza mitaani ili aweze kusaidiawa kupatiwa kiasi cha pesa kitakachomwezesha kufanyiwa huduma hiyo.
Kiongozi wa kundi lililokua likimtembeza mitaani  Peter Mwogera alisema lengo la kumzungusha mitaani uchi ni kutaka jamii ya watu wa Githurai waamini kuwa kijana huyo alikua hajafanyiwa tohara.

WATU 27 WAMEOKOLEWA AJALI YA MTUMBWI ZIWA TANGANYIKA, 10 WAMEFARIKI


Na Mwajabu Hoza Kigoma.
WATU sita wamekufa 27 wameokolewa na wengine 11 kulazwa katika hospitali ya rufaa maweni iliyopo Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma baada ya boti walilokuwa wakisafiria kuzama katika ziwa Tanganyika mkoani humo.
Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari kamishina msaidizi wa polisi mkoa kamanda Jafar Mohamed alisema tukio hilo limetokea majira ya saa nne asubuhi katika kijiji cha Kalalangabo kilichopo mwambao wa ziwa Tanganyika kwenye halmashauri ya wilaya Kigoma.
Kamanda Mohamed alisema chanzo cha tukio hilo ni idadi kubwa ya watu waliokuwa katika boti hilo na kusababisha kuzama majini mita 200 kutoka nchi kavu na kwamba watu hao walikuwa wakielekea kwenye sherehe ya harusi katika kijiji cha Kigalye kilichopo jimbo la Kigoma Kaskazini mkoani humo.
Alisema watu waliopatikana ambao ni marehemu ni watu sita wakiwemo watoto wawili kati ya hao mmoja ametambuliwa kwa jina la Salama Juakali (37) huku wengine majina yao yakiwa hayaja tambuliwa hadi sasa.
Kamanda amesema hatua za uokoaji zinaendelea sanjari na taratibu za kuhakikisha waliohusika na tukio hilo wanafikishwa katika vyombo vya sheria kujibu tuhuma inayowakabili.
Kwa mujibu wa taarifa ya mwenyekiti wa wavuvi katika mwalo wa Kibirizi uliopo Manispaa ya Kigoma Ujiji Sedwe Ibrahimu alieleza idadi ya watu waliozama majini inasadikiwa kuwa zaidi ya watu 64 ambao walikuwa wakielekea harusini. 
Alisema mitumbwi iliyosababisha ajali ilikuwa miwili ambayo ni maalum kwa kuvulia samaki na dagaa hivyo ilitumika kusafirishia abiria baada ya kukodiwa kwa lengo la kuwfikisha maharusi katika kijiji cha Kigalye wakitokea katika kijiji cha Mwandiga jimbo la Kigoma Kaskazini ndipo walipokutwa na janga hilo.
Akifafanua kuhusu tukio hilo baada ya kupatiwa tarifa ya kuzama kwa mitumbwi miwili iliyokuwa imebeba watu waliokuwa katika magari matatu aina ya Hiace pamoja bodaboda tatu kiasi ambacho kinaashiria watu hao walikuwa wengi ukilinganisha na uwezo wa mitumbwi hiyo ambayo hubeba watu 20 tu wakati wa shughuli za uvuvi.
 
v
viongozi wa mkoa wa Kigoma wakiangalia kwa makini zoezi la uopoaji wa miili ya watu
Alieleza eneo ambalo walitumia kupakia abiria hao ilikuwa katika kijiji cha Kalalangabo ambapo si rasmi kwa kupakia abiria kisheria na hivyo kutakiwa kutumia eneo la kibirizi ambalo limetengwa kisheria.
Baaadhi ya wahanga wa tukio hilo akiwemo Zainabu Issa na Mariamu Juma (18) ambaye ni bibi harusi alisema chanzo ni baada ya mitubwi hiyo kukumbwa na wimbi la maji sambamba na idadi kubwa ya watu takribani 80 ambao walikuwa katika mitumbwi hiyo.
Muuguzi wa zamu katika wodi namba tano Haika Masula alisema wamepokea majuruhi 10 na maiti tatu mwanamke mmoja alitambuliwa kwa jina la Salama Juakali na watoto wawili waliochini ya umri wa miaka mitano.