Thursday, August 14, 2014

UGONJWA WA EBOLA' WASABABISHA TAFRANI SHINYANGA



Wakazi wa Manispaa ya Shinyanga, kwa siku mbili mfululizo walikumbwa na kiwewe, baada ya kuenea uvumi kwamba kuna mgonjwa wa mwenye homa hatari ya ebola, aliyefikishwa katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga. 
Taarifa za kuwepo kwa mgonjwa huyo, zilidai kuwa mgonjwa huyo alitoka katika moja ya mitaa ya Manispaa ya Shinyanga na  alikuwa akitokwa damu puani na mdomoni kabla ya kuzimia.
Akizungumzia hali hiyo jana, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dk Ntuli Kapologwe alisema mgonjwa huyo ambaye alikuwa akitokwa damu mdomoni na puani, alifika hospitalini hapo juzi na baada ya kufika wauguzi na madaktari walitaharuki.
Kwa mujibu wa Dk Kapologwe, mgonjwa huyo alipelekwa chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), huku baadhi ya wauguzi na madaktari wakimkimbia hali iliyotia hofu kwa baadhi ya wahudumu na hata wagonjwa hospitalini hapo.
Hata hivyo, Dk Kapologwe alisema baada ya uchunguzi wa awali, ilibainika kuwa mgonjwa huyo ana matatizo ya kutokwa damu mara kwa mara na hajaambukizwa virusi hao wa ebola.
Akielezea namna mkoa ulivyojiandaa kukabiliana na ugonjwa huo uliokwishaua zaidi ya watu 1,000 katika nchi za Afrika Magharibi, Dk Kapologwe alisema waganga wakuu katika halmashauri zote sita za wilaya mkoani Shinyanga, wameshajiandaa.
Alisema wamekubaliana atakapogundulika mtu mwenye dalili za ugonjwa huo, taarifa itolewe mara moja katika ngazi ya mkoa, ambako kuna timu maalumu ya wataalamu iliyoandaliwa kushughulika na ugonjwa huo hatari.
Baada ya taarifa kutolewa kwa mujibu wa Dk Kapologwe, timu hiyo itathibitisha kama mgojwa ana dalili zote za ebola na taarifa kutolewa kwa umma.
Wakati ugonjwa huo ukisababisha kiwewe mkoani Shinyanga,   mkoani Kagera, Mkuu wa Mkoa, Fabian Massawe ameshauri wakazi wa mkoa huo kuwa macho na tayari kutoa taarifa kwenye vituo vya afya vilivyo jirani waonapo mtu mwenye dalili  za ugonjwa huo. 
Alitoa mwito huo kupitia kwa waandishi wa habari aliozungumza nao jana ofisini kwake mjini hapa, baada ya kuibuka taarifa kuwa Rwanda kulikuwa na mtu anayehisiwa kuwa na ebola. 
Hata hivyo, Waziri wa Afya wa Rwanda, Agnes Binagwaho alisema juzi kuwa mwanafunzi mmoja wa Ujerumani aliyefika nchini humo akitokea Liberia,  alihisiwa kuwa na ugonjwa huo lakini baada ya sampuli ya damu yake kupimwa katika maabara za kimataifa, hakukutwa na ugonjwa huo.
Massawe alisema Mkoa wa Kagera unapakana na nchi mbalimbali za Afrika Mashariki na pia upo mwingiliano wa watu na shughuli mbalimbali za kijamii. 
Alisema nchi jirani zikipata mlipuko wa ugonjwa huo, upo uwezekano wa kuvuka mipaka na kuingia mkoani Kagera, hivyo ni  wajibu wa kila mmoja kutoa taarifa akiona mtu anayedhaniwa kuwa na ugonjwa huo. 
Dalili za ugonjwa huo unaoenezwa na virusi vya ebola ni pamoja na  kutokwa na damu sehemu mbali mbali za mwili, kuumwa na kichwa, mwili kuishiwa nguvu, maumivu ya misuli na hatimaye kifo.
Ugonjwa huo unaambukizwa kwa kugusa damu na majimaji ya mgonjwa pamoja na kugusa vifaa au nguo za mgonjwa.
Massawe alisema Kagera wamechukua hatua kwa kuweka mikakati kuhakikisha mlipuko wa ugonjwa  hauingii nchini  kupitia mipakani.  
Miongoni mwa halmashauri ambazo zimeelekezwa kuchukua hadhari kutokana na kuwa mpakani mwa nchi, ni wilaya ya Bukoba, Missenyi, Karagwe, Kyerwa na Ngara.

ANGALIA JINSI TAFRANI ILIVYOKUWA JANA WAKATI MSIKITI WA MTAMBANI KINONDONI UKITEKETEA KWA MOTO


 Moto Mkubwa ukiendelea kuwaka katika eneo la juu la Jengo la Shule ya Sekondari ya Kiislam ya Mivumoni (Mivumoni Islamic Seminary) iliyopo ndani ya Msikiti wa Mtambani,Kinondoni B Jijini Dar es Salaam leo.

Eneo hilo ambalo lilikuwa likitumika kama Mabweni ya Wanafunzi wa Shule hiyo,Maabara na Ofisi za Walimu limeteketea kabisa kiasi kwamba hakuna kitu chochote kilichoweza kuokolewa.

Jitihada za kuuzima moto huo zimekuwa zikiendelea hadi hivi sasa,huku sehemu ya Waumini wa Kiislam wakijitokeza kwa wingi kusaidia juhudi hizo za kuuzima moto huo zilizokuwa zikiendesha na Kampuni ya Kuzima moto ya Ultimate,japo baadae gari hilo liliisha maji,hali iliyowapelekea Waumini hao kulijaza maji gari hilo kwa kutumia ndoo huku kazi ya Uzimaji moto huo ikiendelea.

Chanzo cha Moto huo,inadaiwa ni hitilafu ya Umeme iliyokuwepo kwenye Bweni la Wasichana Wanafunzi wa Shule hiyo.Hakuna mtu yeyote aliepoteza maisha wala kujeruhiwa katika tukio hilo.Picha zote na Othman Michuzi. 
 Moto mkubwa ukiendelea kuwaka kwenye eneo hilo.
 Ulinzi mkali wa Polisi ulitawala katika eneo la Msikiti huo wa Mtambani kuhakikisha Usalama unakuwepo kwenye eneo hilo.
 Sehemu ya Waumini wa Kiislam wakishirikiana kusombelea maji ili kuuzima moto huo. 
 Jitihada zikiendelea. 
  Gari la Zima Moto mali ya Kampuni ya Ultimate Security likijazwa maji kwa ndoo ili kuendelea na zoezi la uzimaji w amoto huo. 
  Likafika na gari hili kwa ajili ya kusaidia kuzima moto huo.
Mashuhuda wakiwa nje ya eneo hilo.CRDT JIACHIE BLOG

AFANDE SELE AFIWA NA MZAZI MWENZAKE ASHA aka 'MAMA TUNDA'

Afande Sele akiwa katika picha ya pamoja na familia yake (picha ni ya muda kidogo), kutoka kulia ni mama wa familia hiyo Marehemu Asha Msindi, Seleman Msindi .a.k.a dume la simba, aliyempakata ni mtoto wake mdogo anayeitwa Asante Sana na wa mwishoni Tunda.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook Afande Sele amepost taarifa ifuatayo kuhusiana na kifo cha mzazi mwenzake aneitwa Asha au Mama Tunda.
Pichani ni Afande Sele na mzazi mwenzake marehemu Asha aka Mama Tunda

Mtandao huu unatoa pole kwa Afande Sele pamoja, mtoto wao na familia nzima kwa ujumla. May her soul R.I.P

LORI LA MAFUTA LAANGUKA KIMARA MWISHO NA KUZIBA NJIA.WANAINCHI WAGOMBANIA KUCHOTA MAFUTA


watu wapo busy wanachota Mafuta  yan bahati mbaya ukitokea mlipuko ni majanga


Lori la mafuta baada ya kuanguka.
Foleni iliyosababishwa na ajali hiyo eneo la Kimara, Dar.
Polisi wakidumisha ulinzi eneo la ajali.
LORI lililokuwa na shehena ya mafuta lita 34,000 likitoka jijini Dar es Salaam kuelekea mikoani Singida limeanguka asubuhi hii eneo la Kimara Darajani, Dar na kusababisha foleni kubwa baada ya kuziba barabara huku wananchi wakiamua kuchota mafuta kutoka kwenye lori hilo ambalo ni mali ya Nassor Filling Station. Jeshi la Polisi liliamua kuingilia kati kuwatawanya wananchi hao waliokuwa wakigombea kuchota mafuta eneo la ajali.

HATIMAYE YULE TRAFIKI FEKI APELEKWA MAHAKAMANI



MKAZI wa Kijitonyama jijini Dar es Salaam, Robinson Mwakyusa (30), amepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kujibu mashitaka ya kujifanya askari wa Kikosi cha Usalama barabarani na kukutwa na vifaa vya Jeshi la Polisi.
 
Mwendesha mashtaka wa Serikali, Mwanaamina Kombakono, alimsomea mshitakiwa mashtaka matatu mbele ya Hakimu, Devotha Kisoka na kusema kuwa  kabla Mwakyusa  kuachishwa kazi alikuwa ni askari mwenye namba F 2460,

Katika kosa la Kwanza, Kambakono alidai kuwa Agosti 2, mwaka huu, katika maeneo ya Chamazi Muhimbili, Wilaya ya Temeke, mshitakiwa alijitambulisha isivyo halali kwamba ni mwajiriwa wa sekta ya umma  kitengo cha jeshi la polisi Tanzania na kwamba ni ofisa wa Kikosi cha Usalama barabarani akiwa na cheo cha Stafu Sajini.

Alisema katika shitaka la pili, siku hiyo hiyo ya Agosti 2, katika Kituo cha Polisi cha Mbagala, wilaya ya  Temeke, mshtakiwa alikutwa na sare za polisi wa kikosi cha usalama barabarani, simu ya upepo aina ya Motorola GP 380 pamoja na beji iliyoandikwa ER Mwakyusa kinyume cha sheria.

Ilidaiwa kuwa mshitakiwa alikutwa na vitu hivyo ambavyo ni mali ya jeshi la polisi, vinavyosadikiwa kuibwa au kupatikana isivyo halali.

Katika shitaka la tatu, mshitakiwa anadaiwa kukutwa maeneo ya Kijitonyama Mpakani B, wilaya ya Kinondoni, akiwa na nguo nne za kazi ya polisi, ambazo ni suruali tatu na mashati ya trafiki, koti moja la mvua la polisi, vikoti vinane vya trafiki vyenye mwanga, kofia ya trafiki ya Uhuru, bareti na mikanda minne mali ya jeshi hilo, ambavyo vinasadikiwa vimeibwa au kupatikana kwa njia isiyo halali.

Mshitakiwa alikana mashitaka hayo na mwendesha mashtaka alidai upelelezi haujakamilika hali iliyomfanya hakimu Devotha kutoa masharti ya dhamana ambapo ni mshitakiwa kutia saini saini bondi ya sh. milioni 50 na awe na wadhamini wawili ambao nao watatia saini bondi hiyo kila mmoja.

Mshitakiwa alitimiza masharti ya dhamana na kuachiwa hadi Septemba mosi, mwaka huu, kesi itakapotajwa.

WANAFUNZI WA CHUO CHA MZUMBE WAUA MWIZI WA LAPTOP CHUONI MOROGORO

Wanafunzi wa mzumbe main campus Morogoro wameua mwizi alyeiba laptop kutoka mabweni mawili tofauti, taarifa zaidi zinasema uuaji huo umetokana na hasira kali za wanafunzi hao kuibiwa laptop kila siku na pia mwanzafunzi mwenzao kuvamiwa barabarani na kujeruhiwa na visu siku zilzopita....