Sunday, December 14, 2014

ROSE MUHANDO HAYA NI YA KWELI


Mwimbaji nyota wa muziki wa Injili Bongo, Rose Muhando wakati akifanya yake.
Mapema wiki hii, chanzo kimoja kilipiga simu katika chumba chetu cha habari na kusimulia kuhusu habari hiyo, kwamba, Rose ambaye hana mume, amenasa na muda wowote kuanzia sasa anaweza kuitwa mama.

Madai ya chanzo hicho yalieleza kwamba, staa huyo amekuwa akijichimbia nyumbani kwake mkoani Dodoma tofauti na siku za nyuma ambapo alikuwa hakauki jijini Dar.
“Kama hamsadiki ninayowaambia, najua ninyi mmebobea kwenye habari za uchunguzi ‘so’ fanyeni yenu mtaniambia,” kilidai chanzo hicho kikiomba chondechonde kisichorwe jina gazetini.


Ili kujiridhisha na habari hiyo, pasipo kwanza kuwasiliana na Rose, moja kwa moja, gazeti hili lilimpigia simu mmoja wa watu wa karibu wa nyota huyo (jina linahifadhiwa), alipopatikana, aliulizwa kuhusu ishu hiyo na haya ndiyo aliyoyaeleza:

Rose Muhando akipafomu na madansa wake.


“Yaani hadi leo mlikuwa hamjapata hii habari? Mimi siku zote nilikuwa najua labda kwenu siyo habari kwa sababu ujauzito huu ni wa siku nyingi. “Hata sasa hivi ukimuona alivyo unajua wazi kuwa kuna kichanga tumboni kwani tumbo limechomoza hatari.”
Mtu huyo wa karibu alisema anapokuwa nyumbani Dodoma mara nyingi amekuwa mtu wa kukaa ndani tu kutokana na watu kumshangaa.Alisema Rose amekuwa akijificha kwa sababu ya kuogopa macho ya watu na uchovu unaotokana na hali aliyonayo ‘kuchoka’.

NANI MHUSIKA?
Juu ya nani mhusika wa mimba hiyo, mtu huyo wa karibu, ambaye anafahamu kila kinachofanywa na nyota huyo wa Wimbo wa Facebook alisema kuwa, inadhaniwa kuwa ni ya mcheza shoo wake (jina kapuni).


Inadaiwa kwamba, Rose, mara kadhaa amekuwa akisisitiza kuwa ni lazima amzalie mtoto jamaa huyo kwa jinsi anavyompenda.“Huyo mcheza shoo ana uhusiano naye kwa muda mrefu kidogo na ameshasema kwa watu wengi tu kwamba endapo Mungu atapenda basi atafurahi kama atamzalia mtoto.
“Mimi hajaniambia mimba hasa ni ya nani, lakini naziona dalili zote kuwa ni ya huyo kijana,” alisema mtu huyo.Rose Muhando na madansa wake wakitoa burudani.


Baada ya kujiridhisha na maelezo ya mtu wake wa karibu, gazeti hili lilianza kumtafuta Rose, mama wa watoto watatu ambao wote amezaa na wanaume tofauti, lakini katika hali ya kushangaza, simu yake iliita hadi kukatika bila kupokelewa, hata baada ya kupigwa mara kadhaa.

Likiamini huenda alikuwa katika shughuli au mahali panapombana kuzungumza, gazeti hili lilimtumia ujumbe mfupi wa maneno (SMS) na kumsomea mashitaka hayo ili atoe ufafanuzi, lakini pia hakuweza kujibu.
Likiamini huenda simu yake haisomeki kwa mtumishi huyo wa Mungu, gazeti hili lilitumia simu nyingine ambayo nayo iliita kwa muda mrefu hadi kukatika pasipo kupokelewa na hata pia alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu wenye maelezo kuhusu hali yake ya sasa, pia haukujibiwa hivyo jitihada zinaendelea.


Endapo itathibitika, ujauzito wa Rose utakuwa ni wa mtoto wa nne ambapo mara kadhaa staa huyo amekuwa akisema hayupo tayari kuolewa hivyo kuwaacha baadhi ya watumishi midomo wazi wakiamini mtu wa sampuli yake haifai kuzaa nje ya ndoa.

Saturday, December 13, 2014

WAZAZI WA MWOZESHA BINTI YAO KWA NGUVU BAADA YA KUFUMWA AKIFANYA TENDO LA NDOA

Na Baraka lusajo,
   Binti mmoja mkazi wa  kijiji   Lugombo  kata  ya Kandete  Wilayani Rungwe Mkoani  Mbeya  Getina   Karinga  miaka  {24} ameingia katika wakati  mgumu  baada ya kuozeshwa  ndoa  ya mkeka  kwa  nguvu na  wazazi  wake  baada  ya  kufuniwa   na  mwanaume  wakati  akifanya  tendo la ndoa  chumbani  kwao.

  Tukio  hilo  la kushangaza  limetokea  baada  ya  kijana  huyo kwenda  kwa  wazazi  wa  binti  huyo   kwa lengo la  maongezi ya  kawaida   na  kujikuta akiambulia   kipigo  kikali kutoka kwa  mama  mtu baada  ya kufumwa  wakati  akifanya  tendo  hilo chumbani kwa  mama yake  na binti.
 Hata hivyo  kutokana na     hali  hiyo
mama  huyo aliweza  kuangua  kilio kikubwa  baada  ya   vijana hao kuto onyesha  ishara  ya kuacghana  na kitendo  hicho mara baada  ya kufumwa  wakati  wakifanya kitendo hicho  na kwamba  kabla ya  tukio  mama  mtu alifika  na  kuwa muru  kuondoka mara  moja  lakini kutokana  na    wapendanao  kunogewa   na  tendo hilo  walijikuta wakiendelea  kufanya  bila kujari uwepo  wa  mama yao na kupelekea  mama mtu kupatwa  na hasira  na kuchukua   mfagio  na kuwachapa .
 Kwa mujibu  wa  mama  huyo ambaye  hakutaka  kutajwa  jina lake   hadharani  alisema  mnamo  majila ya  sambili za usiku akiwa ametokea  kwenye  shughuri  zake za kawaida  aliweza   kukuta milango ya   nyumba   yake ikiwa wazi  na kuamua  kuingia  lakini baada ya  kumwita  binti  yake  alijibiwa arudi  aliko tokea   , lakini aliamua  kupiga  moyo  konde  na  kuamua  kosogea  zaidi  na kumkuta mtoto wake akifanya  kitendo hicho  na kuamua   kuita watu.
         “Nimeona  aondoke  nyumbani kwangu kwani amekuwa akinidharau  bila kujari  kwamba    mimi ni mama yake  na  hadi kufikia hatua  ya  kufanya  mapenzi  na mwanaume mwingine  nyumbani kwangu kitu ambacho ni dharau  kubwa ,  na mpaka sasa nimemwozesha  na kutoa  baraka zangu  zote  kwani nimechoka   vitendo anavyo nifanyia   kwani  mda  wote amekuwa akifika nyumbani akiwa amelewa  pombe  kupita  kiasi  na  mda mwingine  nimekuwa  nikimfuma  kwa  macho  yangu akiwa  anavuta  bangi na sigara.” Alisema mama mtu.
 Kwa  upande  wa    binti huyo alisema   yuko  tayari  kuolewa  na kijana  huyo   na kwamba   anawashukuru wazazi  wake  kwa  hatua  walio fikia kutokana  na kwamba amekaa miaka  mingi sana akiwa  nyumbani  kwao bila  kuolewa na kwamba sasa  atakuwa  huru  katika  kumpatia mme  huduma yake  muhimu, na  huku mwanaume akifurahia  ndoa  hiyo  kutoikana  na kwamba  muda wote  walikuwa  wakimbania  mwanamke   huyo wakidai anatabia  mbaya  kitu amacho kwake    si kweli..
 Mtendaji wa  kata  hiyo  huruma mwakyusa  mbali  na kukili kutokea  kwa  tukio  hilo  alisema wameshindwa  kuendelea na  kesi hiyo kutokana na kwamba  wazazi  wa  binti  huyo  wamekataa  kumpokea binti  yao  kwa madai  ya kuwachafua na kuamua   kumuodhesha  bila  mahali.

Thursday, December 11, 2014

KIJANA AMPA MIMBA MAMAYE WAHAMA MJI KUOGOPA MANENO

Kijana mmoja nchini zimbabwe katika kijiji cha pote amekimbia kijiji hicho baada ya kujikuta katika matatizo makubwa kufuatia kumtia mimba mama yake mzazi kwa mara ya pili.Ikumbukwe hapo nyuma kijana huyo aliwahi kutenda kitendo hicho ambapo wana kijiji walimsihi kutorudia tena kitendo hicho baada ya kijana huyo kumshawishi mama yake na kuitoa mimba hiyo.Simon Matsvara na mama yake Ethel Vhangare aliamua kuondoka baada ya waumini wa kanisa lao kugundua kuwa mimba hiyo ni batili.Miaka minne iliyopita, wawili hao waliripotiwa na kutozwa faini na viongozi wa kijiji kwa kosa la kutoa mimba.Chifu wa kijiji, Chinamhora alisema kuwa jamii ilikasirishwa na kitendo hicho na kwamba yeye aliamua kuwatuma wafanyakazi wake kuwatafuta wawili hao waliokuwa wameamua kuishi kama mume na mke.“Tunaenda kuwatafuta mpaka tuwapate na wakisha patikana ni lazima wapewe adhabu kali ili iwe fundisho kwa watu wengine wanoa jihusisha na vitendo kama hivyo ambavyo havikubaliki katika jamii”Alisema chifu huyo.Imeripotiwa kuwa wawili hao walianza mahusiano yao tangu mwaka 2008 wakati Matsvara alipopewa jukumu la kumuuguza baba yake mzazi mzee Agripah,ambae baadae alikufa.Mama huyo alipata mimba mara ya kwanza, wawili hao walitozwa faini na kuambiwa uhusiano wao ukomee hapo wasije wakarudia tena.Habari ya mimba ya pili ziligundulika baada ya mama huyo kuanza kuwakwepa wahumini wa kanisa lake walipokuwa wakimtembelea nyumbani kwake.Baada ya uchunguzi ndipo walipogundua kuwa mama huyo ni mjamzito wa miezi 5 na ujauzito huo kapewa na mwanae.

Wednesday, December 3, 2014

BILIONEA NIGERIA AMZIKA MAMA YAKE NDANI YA HUMMER


Bilionea Nigeria aliyeiwekea marembo gari la Humeer yenye thamani ya dola 1,000 na kumzika nayo mama yake katika mji wa Enugu nchini Nigeria.
Gari la Hummer lililobeba mwili wa marehemu likiingizwa kaburini

Bilionea akimzika mama yake ndani ya gari la Hummer nchini Nigeria.

ZITTO AMTAMBULISHA MCHUMBA WAKE

MBUNGE Jimbo la Kigoma Kaskazini Zitto Zuberi Kabwe amemtambulisha mchumba wake mpya anayetarajia kufunga nae pingu za maisha hivi karibuni. Mchumba huyoUtambulishio huo wa mchumba wa Zitto ulifanywa na Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila (NCCR-Mageuzi) wakati wa sherehe ya Harusi yake iliyofanyika kwenye ukumbi wa Annex.hali ilikuwa hivi; baada ya Kafulila kutambulisha ndugu zake pamoja na wazazi wake ndipo alianza kutambulisha wageni wengine na kuanza na mchumba mtarajiwa wa Zitto Kabwe aliyemtaja kwa jina la Anna.“Huyu wa kwanza anaitwa Anna anafanya kazi Ubalozi wa Ireland ni mchumba mtarajiwa wa Zitto Zuberi Kabwe, anayefuata kutoka kushoto kwa Anna wote mnamfahamu ndiyo Zitto mwenyewe na anayemfuata ni Mwalimu wangu wa chuo kikuu Kitila Mkumbo na mwisho ni mbunge mwenzangu David Silinde hao ndo walio nisindikiza

Tuesday, December 2, 2014

BASI LAACHA NJIA NA KUTUMBUKIA KORONGONI MLIMA KITONGA

 Basi liitwalo Easy Bus lenye namba za usajili T 298 BLZ lililokuwa likitokea Lilongwe Malawi likiwa katika mtaro wa Mlima Kitonga.
Foleni kubwa iliyosababishwa na basi hilo baada ya kuingia mtaroni na kuziba njia. Basi la abiria lenye namba za usajili T 298 BLZ likiwa linatolewa katika mtaro wa Mlima Kitonga mapema leo baada ya kutumbukia. Hali hii imesababisha foleni kubwa kwa magari huku mengine yakishindwa kuendelea na safari zake. Kwa  mujibu wa mashuhuda, chanzo cha gari hilo kutumbukia mtaroni ni kufuatia kupata hitilafu na hatimaye uamuzi wa kuliegesha kando ukafanyika kisha abiria wote  wakashuka ili kusubiri marekebisho hayo.

Haikupita muda mrefu baada ya abiria kushuka gari lilikosa balansi, likaanza kurudi kinyumenyume na kisha kuingia mtaroni. Hakuna mtu aliyefariki dunia wala kujeruhiwa katika ajali hiyo.

RAIS KIKWETE AMWAPISHA CAG MPYA, PROF MUSA JUMA ASSAD IKULU JIJINI DAR

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitia sahihi yake kwenye nyaraka baada ya kumuapisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad nyaraka baada ya kumuapisha Ikulu jijini Dar es salaa  Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuangalia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad akiweka sahihi yake kwenye nyaraka baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad na CAG Mstaafu Bw. Ludovick Utouh Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali, Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda, Jaji Mkuu Mhe Mohamed Chande Othman, Spika Anne makinda na Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad na wafanyakazi wa ofisi ya CAG  Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na familia ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
 (PICHA NA IKULU)

MZEE MSUYA AWASIHI WAKULIMU KUTOOGOPA NENO BIOTEKNOLOJIA


Kutokana na kuwepo kwa maneno yanayowatishia na kuwakatisha tamaa wakulima kuwa mbegu za kisasa ni mbegu za kibioteknolojia na hazifai kwa matumizi ya binadamuu, mzee Msuya amewasihi wakulima kuwabeza watu hao na maneno yao na kutoliogopa neno bioteknolojia kwani hilo ni neno la kisayansi ambalo halibadirishi uasili wa mmea wa aina yoyote ile.
Aliyasema hayo baada ya kuwepo kwa baadhi ya watu kumfuata na kumuuliza siri ya mafanikio yake katika kilimo na anapowaambia kuhusu mbegu za kibioteknolojia huingiwa na mshangao na kuogopa neno hilo
Mzee msuya ni miongoni mwa wazee maarufu katika wilaya ya Vunjo kutokana na juhudi zake katika kilimo na ndio wazee wenye pesa mjini hapo.
mzee huyo ambaye alisema siri ya mafanikio yake aliipata baada ya kukubali kung'oa miche yake ya zamani ya kahawa na kupanda miche mipya aliyoinunua katika taasisi ya utafiti wa kahawa ya TaCRI baada ya kupata ushauri kutoka kwa mtaalamu wa kilimo wa taasisi hiyo.
"mtafiti alinishauri nitoe miche ya kahawa yote iliyokuwapo shambani na kunpambia nikanunue miche mipya ya TaCRI kwani ni miche isiyokuwa na maambukizi ya magonjwa yanayosumbua zao la kahawa sikuamini lakini baadaye nikakubali na nikafanya kama nilivyaambiwa na sasa naitwa mchawi hapa kijijini kutokana na mazao ninayoyapata.


wanawake wakimsaidia mzee msuta kuchambua mahindi nyumbani kwake 



Mzee huyo ambaye sasa amekuwa mwalimu wa wakulima wenzake alisema kuwa Tanzania kama nchi nyingine haiwezi kukwepa maendeleo ya bioteknolojia kutokana na utandawazi na maendeleo ambayo yapo duniani kote, kwa kuwa bioteknolojia ni nyenzo muhimu katika kuboresha kilimo, uzalishaji viwandani, kwenye afya, hifadhi ya mazingira pia kukuza uchumi nchini
mzee huyo ambaye alisema alikuwa anapata kilo 250 mpaka 1500 kwa msimu lakini tangu miche mipya ianze kuzaa matunda napata kilo 5000 mpaka 8000 kwa msimu na kwa ukubwa ule ule wa shamba. kitu ambacho akiwaeleza wenzie wanashangaa sana na kutoamini anachowaeleza.

Akifafanua kuhusu neno bioteknolojia alisema kwa madaha  kuwa ni "taaluma ya kutumia michakato ya kibaolojia katika  viumbe hai ili kupata mahitaji na huduma kwa maendeleo na maisha bora ya binadamu" 


 
Msuya ambaye alisema hata sahau jinsi majirani zake walipomcheka na mumuita mpumbavu pale alipoamua kung'oa na kupanda miche mipya. Hata hivyo hakukatishwa tamaa na maneno yake bali alizingatia sana mafundisho aliyoyapata na kuyatendea kazi mpaka alipo fanikiwa na kubadirika kuwa mwalimu wa wengine
"Hivi sasa mimi nafuatwa na wakulima ili niwafundishe mbinu ninazotumia, lakini wengi wanashangaa ninapowaambia kuhusu mbegu mpya na utunzaji wa shamba vizuri wanaofuata ninayowaambia wanaona matunda yake.


 shamba la kahawa la mzee msuya likiwa limechanganywa na zao la migomba

Mzee huyo alisema kuwa anajivunia sana elimu aliyoipata kutoka kwa watafiti kwani wamemfanya kutoka kwenye kilimo cha kutafuta chakula pekee na kuwa mkulima mfanyabiashara kwani mazao anayoyapata kwa sasa yanakidhi mahitaji yake ya chakula na kupata kiasi kikubwa kwa ajili ya kuyauza kwenye makampuni makubwa hapa nchini.
"TaCRI imeniondolea umaskini kwani walinifundisha elimu ya kutumia mbegu bora kwa kila zao ninalotaka kulima pamoja na matumizi ya samadi ya wanyama nilionao nyumbani hivyo kwamgu mimi kila kitu ni faida kwani mashamba yanategemea mifigo kwa mbolea wakati mifugo inategemea kilimo kwa chakula". 

Hata hivyo aliwasii watafiti wote nchini kuwasaidia wakulima ili wapate elimu kuhusu matumizi ya mbegu bora ili kumkomboa mkulima kwani wakulima wengi wanadanganya na propaganda zinazoletwa na wafanyabiashara wengine wa bidhaa zao wakidai kuwa matumizi ya mbegu hizo si salama wakati ni uvumi usio wa kweli kabisa.

TaCRI ni taasisi ya utafiti wa kahawa nchini Tanzania na inafanya kazi  kwa msaada wa nchi za ulaya, hufanya uzalishaji kwa njia ya Tissue Culture ( uzalishaji kwa njia ya chupa) na kuzalisha kwa kutumia vikonya (kupachika mche mmoja juu ya mche mwingine).


Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi 2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara za arabika pamoja na ile ya Robusta Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa

Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi 2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara za arabika pamoja na ile ya Robusta Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho kinasababisa hasara kwa mkulima Pia TaCRI imetoa teknolojia za kuongeza tija na ubora wa kahawa aina mbili zinazotekelezeka za kuzalisha miche mipya bora ya aina hizi chotara ikiwa nipamoja na kutumia vikonyo, kupachika aina mpya juu ya mibuni ya zamani na kuzalisha kitaalamu miche kwa kutumia chupa ikifahamika kwa lugha ya kingereza ’Tissue culture au Somatic embryogenisis.’

Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi 2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara za arabika pamoja na ile ya Robusta Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho kinasababisa hasara kwa mkulima Pia TaCRI imetoa teknolojia za kuongeza tija na ubora wa kahawa aina mbili zinazotekelezeka za kuzalisha miche mipya bora ya aina hizi chotara ikiwa nipamoja na kutumia vikonyo, kupachika aina mpya juu ya mibuni ya zamani na kuzalisha kitaalamu miche kwa kutumia chupa ikifahamika kwa lugha ya kingereza ’Tissue culture au Somatic embryogenisis.’

Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi 2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara za arabika pamoja na ile ya Robusta Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho kinasababisa hasara kwa mkulima

Make Money at : http://bit.ly/copy_win

MCH: RWAKATARE AFIKISHWA POLISI KWA UHARIBIFU WA MALI

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mikocheni B Assemblies of God jijini Dar, Dk. Getrude Rwakatare (pichani) amefunguliwa mashitaka katika Kituo cha Polisi Wazo Hill kwa uharibifu wa mali inayodaiwa ina thamani ya shilingi milioni 20.
Bw. Grayson Justine anayelalamika kuvunjiwa nyumba yake na Mch. Getrude Rwakatare.
Taarifa zilizopatikana katika kituo hicho zenye Jalada la Kumbukumbu WH/RB/9029/2014 UHARIBIFU WA MALI na kuthibitishwa na mlalamikaji aliyejitambulisha kwa jina la Grayson Justine, zinaeleza mchungaji huyo alivunja nyumba ya Grayson kwa greda hali iliyomfanya mmiliki huyo kuzimia na kulazwa Zahanati ya Mico iliyopo Wazo Hill baada ya presha kupanda.
Katika mahojiano na waandishi wetu katika Ofisi za Global Publishers, Bamaga- Mwenge, Dar wiki iliyopita, Grayson alikuwa na haya ya kusema:
Nyumba ya Bw. Grayson wakati wa ujenzi.
“Kiwanja nilichojengea nyumba nilikinunua kwa Jumanne Rajab, Agosti 24, 2011 na makubaliano yalifanyika kwa kuandikishiana Ofisi za Serikali ya Mtaa wa Bunju ‘B’ na kila mmoja alikuwa na mashahidi wake.
“Kutokana na kuchoka katika kupangisha, niliamua kuchukua mkopo wa shilingi milioni 20 kazini ili nijenge haraka na kuhamia, ujenzi ulianza Septemba 21,  mwaka 2013 mpaka kufikia mwezi huu (Novemba) nilibakiza kupaua na nilitarajia kuhamia mwanzoni mwa mwaka kesho.
Mabaki ya matofali ndani ya uzio wa Nyumba ya Bw. Grayson Justine iliyobomolewa kwa greda.
“Baadaye nilikwenda Moshi kwenye msiba wa baba, niliporudi Dar nilimaliza siku moja tu, nikaripoti kazini. Nikiwa kazini Novemba 11, mwaka huu nikapigiwa simu na jirani kwamba nyumba yangu inabomolewa na greda, alifikiri kwamba nimeshaonana na Mchungaji Rwakatare na kukubaliana naye.
“Nilikwenda kule, kufika nikakuta hakuna jengo! Nilidondoka chini, sikujua kilichoendelea, nilipoteza fahamu, nilijitambua nikiwa Zahanati ya Mico.
“Kinachoniumiza sana ni kitendo cha kuvunjiwa nyumba yangu bila kushirikishwa, bora hata angenifungulia mashitaka kama anaona nilivamia kikwanja chake.”
“Yeye ana uwezo, ana ghorofa ya zaidi ya shilingi bilioni moja iweje anionee na kunivunjia mimi maskini niliyejenga kwa fedha za mkopo?
Mch. Getrude Rwakatare.
“Kituo cha polisi nilifika karibu mara nne lakini mpaka leo hii sijapewa mpelelezi wala hawajafika eneo la tukio, nataka sheria ichukue mkondo wake.”
Mwandishi alifika katika eneo la tukio na kushuhudia kifusi kinachodaiwa kuwa ni iliyokuwa nyumba ya Grayson iliyovunjwa na imezungushiwa ukuta na geti kupigwa kufuli.
Hata hivyo, Uwazi lilifika katika Ofisi za Serikali ya Mtaa wa Bunju ‘B’ na kuonana na mtendaji Abdallah Mkeyenge ambaye alikiri kuwepo kwa mvutano baina ya watu hao.“Hii barua ya makubaliano ya kuuziwa Grayson kiwanja inaonekana imetoka ofisini hapa lakini mimi kipindi hicho nilikuwa sijahamia ofisi hii.
Jumba la kifahari la Mch. Getrude Rwakatare.
“Ninachokumbuka kuna kipindi Mchungaji Rwakatare alikuja na milioni tano kuwapa Grayson na mtu mwingine yaani kuwapoza lakini walikataa kuzichukua,” alisema mtendaji huyo.
Mchungaji Rwakatare alipopigiwa simu kuhusiana na madai hayo alisema yupo bungeni hivyo alimwagiza msaidizi wake, Jerad Abeid kuzungumzia sakata hilo ambapo alisema eneo hilo mchungaji analimiliki  tangu mwaka 2005 na hati ziko ardhi Wilaya ya Kinondoni. Alibomoa nyumba ya Grayson akijua ni eneo lake la siku nyingi.
“Unajua katika maeneo hayo kuna watu walikuwa wakishirikiana na ofisi za mtaa kuuza kiwanja cha mchungaji kwa siri na tayari watu wanne walishauziwa lakini walikuwa hawajajenga,  mchungaji aliamua kuwapoza kiubinadamu na wameshaondoka bado watu wawili akiwemo huyo Grayson,” alisema Jerad.

SOMA JINSI ZITTO KABWE ALIVYOPANGUA MASHAMBULIZI YALIYODHAMILIA KUMUINGIZA KWENYE WIZI WA MABILIONI YA ESCROW


Nashambuliwa, tunashambuliwa! PAC tunasema “Hatutetereki”

Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya Kamati ninayoongoza ya PAC kuwasilisha Bungeni Taarifa Maalumu kuhusu ukaguzi maalumu wa akaunti ya Tegeta Escrow, kumekuwa na kampeni za chini chini zinazoendeshwa kwenye korido za Bunge na kwenye mitandao dhidi yangu binafsi na baadhi ya wabunge waliosimama kidete dhidi ya wizi wa fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania akaunti ya Escrow.

Baadhi ya tuhuma nimezipeleka kwenye vyombo vya dola ili zichunguzwe kwani zina vielelezo vya mahala pa kuanzia (kama leseni ya udereva ya mwanamke anajulikana kama Vivian Emmanuel Sirikwa na muhuri wa kampuni ya uwakili inayomilikiwa na Bwana Joseph Mkandege).

Baadhi ya Tuhuma

Baadhi ya tuhuma nitazijibu moja baada ya moja.
Waziri mmoja ambaye ni mtuhumiwa wa wizi wa fedha za Tegeta Escrow anazunguka kwa wabunge akisema tuhuma hizi kupikwa kama njia yake ya kuhamisha mjadala kutoka uporaji wa Tshs 200 bilioni kwenda kwenye masuala binafsi.

Tuhuma hizi zenye kichwa cha habari “Zitto na Filikunjombe wanatumiwa na Kenya na Uingereza kuvuruga na kudhoofisha Uwekezaji nchini mwetu” zinajibiwa hapa chini. Utaona ndugu Filikunjombe ametajwa kwa kichwa cha habari ili kumtaja tu bila sababu yeyote ile.

Tuhuma #1:

Zitto anaye rafiki yake Mkenya aitwae Rapahel Ongangi ambao kwa pamoja wameanzisha Gombe Advisors Co. Ltd (registered on 24 November 2011, Certificate No 87387) kwa ajili ya kufanya biashara na Makampuni ya Gesi na Mafuta yanayofanya kazi nchini hapa.

Majibu:

Gombe Advisors ni kampuni binafsi isiyofanya faida yaani ‘Company Limited by Guarantee’. Haina kazi na kampuni yoyote ya Gesi na Mafuta na wala yenyewe haijuhusishi na biashara hiyo. Gombe advisors haijafanya kazi yoyote ile na kampuni nyingine zaidi ya kusaidia wasanii wa kundi la Kigoma All stars. Upotoshaji hapa unalenga kupindisha mjadala.

Tuhuma #2:

Zitto amemsaidia Ongangi kupata uraia wa Tanzania na kwa sasa ni raia wa pasipoti. Zitto na Ongangi walimtafutia CEO wa Shell aitwae Axel Knospe nyumba na gari ya kukodi.

Majibu:

Raphael ni mtu binafsi ambaye anafanya shughuli zake hapa nchini, amesoma hapa nchini na ameoa na ana mtoto. Tuhuma hizi hazina msingi wowote ule maana ni uwongo. Wanaotoa tuhuma hizi waonyeshe hiyo pasipoti ya Bwana Ongangi kuthibitisha madai yao.

Tuhuma #3:

Mikataba ya STATOIL iliyokuwa inarushwa kwenye mitandao ya jamii na kuchapishwa kwenye magazeti ya Kenya ya hapa nchini (The Citizen na Mwananchi) mwandishi mkuu alikuwa huyo CEO wa Shell.

Majibu:

Mkataba uliovujishwa wa StatOil ulivujishwa na waandishi wa habari wa Norway. Uchambuzi wa mkataba huo nimeufanya mwenyewe kwa kutumia utaalamu wangu niliosomea wa kuchambua mifumo ya kodi kwenye sekta ya mafuta na gesi. Kwa namna yoyote ile, huyo anayetajwa kuwa CEO wa kampuni ya Shell hahusiki. Tuhuma hii wanaoitoa watoe ushahidi usio na chembe ya mashaka.

Ikumbukwe kuwa mkataba wa StatOil utaipotezea Tanzania mapato ya dola za Marekani bilioni 12 (takribani Tshs 20,400,000,000,000/=) katika kipindi cha miaka 15 baada ya gesi kuanza kuchimbwa.

Uamuzi wa Kamati ya PAC kutaka mikataba yote ya Gesi kuwa wazi una lengo la kuchambua kuona kama mikataba yote nchini haipotezi mapato kwa nchi. Uamuzi huo umewakasirisha sana baadhi ya waliohusika kuingia mikataba Serikalini maana wanajua kuna madudu kwenye mikataba na wanataka umma wa watanzania usijue!

Tuhuma #4:
Kampuni ya SHELL imechukizwa sana kucheleweshwa kwa kupata kibali cha kutafuta gesi na mafuta kule Pemba. Vilevile SHELL haina uwekezaji mkubwa Tanzania Bara kwani ilishindwa kwenye tenda zenye vitalu vyenye gesi nyingi upande wa Bara.

Majibu:

Ukweli ni kuwa Kampuni ya Shell ina vitalu 4 huko Zanzibar na tayari ina makubaliano na Serikali ya Zanzibar kuhusu utafutaji mafuta huko katika vitalu namba 9,10,11 na 12. Shell inafanya kazi na kampuni ya Petrobras ya Brazil kwenye kitalu namba 6 na namba 8. Taarifa hizi zipo wazi kwenye tovuti ya TPDC. Tuhuma nyepesi namna hii dhidi ya kampuni kubwa kama Shell zinaonyesha dharau na kiburi kinachotokana na uelewa mdogo wa mambo wa watu wanaotuhumu.

Tuhuma 5:

Ongangi anapokea maelekezo kutoka Serikali ya Kenya kuhujumu uwekezaji nchini mwetu.

Majibu:

Nazifahamu mbinu nyingi zinazotumika kufanya propaganda, lakini mbinu hii imeshindwa ikiwa mapema sana. Ni vema wanaotoa tuhuma hizi wazithibitishe vinginevyo ni mwendelezo wa propaganda zisozingatia diplomasia ndani yake dhidi ya jirani zetu wa Kenya. Hizi ni propaganda hatari ambazo hata hao wanaotuhumiwa wakisikia watatudharau sana.

Tuhuma #6 (juu ya Uingereza):

Uingereza imekuwa inamfadhili Zitto kwa miaka mingi kwa mambo yake ya kisiasa kwa hiyo sasa hivi Ubalozi wa Uingereza unamlipa Zitto na Kafulila kuhakikisha kwamba Standard Chartered ya Uingereza inalipwa deni lake lisilotambulika kisheria nchini mwetu.

Majibu:

Nimetangulia kusema hapo awali kuwa kuna propaganda ambazo haziangalii hata diplomasia; nyingine ni hii. Pamoja na kukanusha uzushi huu, ni vizuri wanaotoa tuhuma za namna hii kuthibitisha. Mimi binafsi sijawahi kufadhiliwa kisiasa na Taifa lolote lile. Inaelekea kuna wanasiasa wanaofadhiliwa na mataifa mengine ambao kwakuwa kwao ndiyo maisha wanaamini na wengine tupo kama walivyo.

Kwangu itikadi yangu ni ‘Uzalendo kwa nchi yangu’, ni jambo ambalo halina mbadala wake. Siku zote nasema “Right or wrong, my country first”.

Kurudia kurusha tuhuma kwa Ubalozi wa Uingereza nchini ni kudhihirisha kwa mara nyingine kiburi cha kuwa na mamlaka (arrogance of power) walicho nacho wanaotuma tuhuma hizi.

Aidha, wanatuhumu kuwa “Kafulila na Zitto wamehaidiwa 15% ya USD 150 million kama deni likilipwa”

Mtanzania anayeweza propaganda dhaifu kama hizi basi anatakiwa ajitafakari. Hata hivyo ni vema wanaotoa tuhuma hizi wathibitishe bila chembe ya mashaka.

Tuhuma #7:

Mbunge Mkono nae ameshikwa hasira kupoteza kazi ya uwakili pale TANESCO. Kafulila na Zitto wanalipwa na Mkono kuvuruga Serikali kwa hasira za kukosa fedha za kitapeli za TANESCO.

Majibu:

Hizi ni tuhuma ambazo sasa tumezizoea kutolewa. Mambo mepesi hayawezi kujibu mambo ya msingi kama tuhuma za wizi wa fedha zaidi ya Tshs bilioni 200 kutoka Benki kuu ya Tanzania. Kukusanya kila propaganda ili kuuhamisha umma ni kupungukiwa hekima na busara.

Aidha, wanaotuhumu wanadokeza kuwa “Naomba tuwe macho na Wabunge wetu achananeni na madai ya Zitto ya wizi. Huyu mtu anafanya biashara na Kampuni ya SHELL na inasemekana analipwa na Ubalozi wa Uingereza. Serikali ya Kenya na tapeli mkubwa Mbunge Mkono nae anawalipa Zitto na Kafulila”.

Watanzania, haya ni maneno ya hasira ya watu wanaokaribia kukamatwa kwa kushiriki wizi wa fedha katika Benki kuu ya Tanzania. Kamwe tuhuma kama hizi haziwezi kutukatisha tamaa katika kupambana ili ukweli ujulikane. Sisi tutapigana kwa ajili ya Taifa, kwa ajili ya mtanzania na tunachotaka ni umma uujue ukweli wa mambo.

Hasira hizi zinatokana na mambo mawili:

Moja ni uamuzi wa kamati ya PAC kuwasweka ndani baadhi ya watendaji wa TPDC kwa kushindwa kutekeleza maamuzi ya Kamati yanayohusu uwazi wa mikataba ya Gesi na Mafuta.

Pili, ni uamuzi wa PAC kuagiza ukaguzi maalumu wa mchakato mzima wa kuanzishwa na kufungwa kwa akaunti ya Tegeta Escrow ambapo zaidi ya shilingi bilioni 200 ziliporwa na zaidi ya shilingi bilioni 12 zinalipwa na TANESCO kila mwezi kwenda kampuni ya PAP inayomilikiwa na Harbinder Singh Seth (50%) na watu wasiojulikana kupitia kampuni ya Simba Trust iliyosajiliwa na kufichwa nchini Australia (50%).

Ieleweke kuwa PAP inalipwa shilingi milioni 400 kila siku kutoka TANESCO izalishe au isizalishe Umeme! Watanzania, PAP itaendelea kulipwa namna hiyo kwa miaka 20 ijayo. Kwa namna ambayo Seth analindwa na baadhi ya watendaji Serikalini na hasa ndani ya Wizara ya Nishati na Madini. Aidha, kuna fununu kuwa kuna maofisa serikalini wanaomiliki hizo 50% za kampuni ya PAP. Seth pia anamiliki kitalu cha gesi Mnazi bay Kaskazini kupitia kampuni ya HydroTanz.

Hasira hizi walizo nazo wanaonituhumu na Kamati yangu zimewapelekea kugushi nyaraka mbalimbali zinazonituhumu mimi na wenzangu ili kutuogopesha na kutukatisha tamaa katika kutafuta ukweli juu ya suala la uporaji wa fedha kutoka Benki kuu. Lengo lao ni kututoa kwenye mstari. Mimi na wenzangu hatutatoka kwenye mstari, tutashirikiana na wabunge wenzetu kuhakikisha ukweli unajulikana na wezi kuchukuliwa hatua kali.

Harbinder Singh Seth aliiangusha Serikali ya KANU nchini Kenya, sasa anachotaka kukifanya kinaweza kuiangusha Serikali ya CCM wakiendelea kumkumbatia.

Watanzania sio mabwege!

Zitto Kabwe
Mwenyekiti PAC
Dodoma, 9 Novemba 2014

Monday, December 1, 2014

WACHEZAJI WA SUNDERLAND WAKIWA WAMEVAA FULANA ZA KUITANGAZA TANZANIA KWENYE MECHI YAO DHIDI YA CHELSEA






Squad wear special warm-up t-shirts.
The players wore special t-shirts ahead of the home draw with Chelsea as part of the club's partnership with Tanzanian Tourist Board.
The Black Cats took to the field in the pre-game warm up sporting shirts emblazoned with the ‘Visit Tanzania’ logo as part of the partnership.
SAFC has already developed close links with Tanzania, through providing technical and practical support to the development of the football academy project, the first of its kind in the country.

The project will see thousands of youngsters benefit from a joined up approach combining football, education and community engagement, harnessing the knowledge and expertise of Sunderland AFC and its own successful Academy. 

RAIS KIKWETE AMTEUA PROF MUSSA ASSAD KUWA CAG MPYA, KUAPISHWA LEO

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS


PRESIDENT’S OFFICE,
STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Website : www.ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Mussa Juma Assad kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu, Desemba Mosi, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, inasema kuwa uteuzi wa Bwana Assad ulianza Novemba 5, mwaka huu, 2014.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa Bwana Assad ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 2, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.


Kabla ya uteuzi wake, Bwana Assad alikuwa Profesa Mshiriki, Idara ya Uhasibu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi ya Bwana Ludovick Utouh ambaye amestaafu kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma.

Profesa Assad ni msomi, mwenye weledi, ujuzi na uzoefu mkubwa wa uhasibu na udhibiti wa fedha ambaye ana Shahada ya Uzamivu wa Uhasibu (PHD in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Southampton, Uingereza mwaka 2001 na Shahada ya Uzamivu katika Udhibiti wa Fedha (MA in Financial Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City, Jamhuri ya Ireland mwaka 1991.

Profesa Assad pia ana Stashahada ya Kitaaluma ya Uhasibu (Professional Diploma in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City mwaka 1990 na Shahada ya Biashara (Bachelor of Commerce) ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam mwaka 1988.

Pamoja na uzoefu wa kitaaluma, Profesa Assad anao uzoefu mkubwa katika eneo la uhasibu na ukaguzi. Alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) kwa miaka saba (2007 - 2014); ni Rais na Mjumbe wa Chama cha Wahasibu Afrika (Pan African Federation of Accountants) tangu mwaka 2012; na ni mjumbe wa Bodi kadhaa za Wakurugenzi nchini Tanzania.

Katika kumteua Profesa Mussa Juma ASSAD kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Rais anayo imani kubwa kuwa elimu, weledi, ujuzi na uzoefu ambao Profesa Assad anao utamwezesha kutekeleza vema majukumu ya nafasi hiyo muhimu sana katika utawala bora wa nchi yetu.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.

1 Desemba,2014

WATANZANIA WENZETU WALIVYOTEKETEA KWA MOTO

INASIKITISHA NAMNA WATANZANIA WENZETU WALIVYOTEKETEA KWA MOTO
NI MPAKANI MWA ZAMBIA NA CONGO MARA BAADA YA LORI MOJA KULIPUKA MOTO NA MOTO HUO KUSAMBAA KWA KASI YA AJABU NA KUUNGUZA MAGARI MENGINE YALIYOKUWA KARIBU,BAADHI YA WATANZANIA WENZETU WALIOKUWA MADEREVA WA MALORI WAMEKUMBWA NA MKASA HUO ULIOPELEKEA MAJERUHI NA NA VIFOT0 
T1

MWANAJESHI ALEWA CHAKARI MPAKA KUZIMA


 Wananchi Iringa wakimtazama askari wa jeshi ambae jina halikuweza kufahamika aliyekuwa amezima kwa ulevi uliopinduki
 mjeshi huyo akiwa akiwa amezima
 Mjeshi huyo akiwa amepata fahamu baada ya kumwagiwa maji
Mjeshi akiwa amezima kwa kunywa pombe kupita kiasi
KATIKA hali isiyotegemewa askari mmoja wa jeshi la kujenga Taifa (JKT) anayesadikika kuwa na wa kambi ya Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa usiku wa juzi amenusurika kuvuliwa nguo za jeshi hadharani baada ya kukutwa amelewa chakali na kulala katika mfereji wa maji machafu eneo la nje ya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani mjini Iringa


Tukio hilo lilitokea muda wa saa 2 usiku baada ya wasamaria wema kumshusha askari huyo kutoka katika basi la Mgumba ambalo alikuwa amepanda kutoka Mafinga kuja mjini Iringa.

Akisimulia kisa na mkasa wa askari huyo kulewa chakali kiasi cha kushindwa kujitambua mmoja kati ya wasamaria wema aliyejitolea kumshusha katika basi hilo alisema kuwa askari huyo alipanda basi hilo Mafinga huku akiwa amelewa na wakati wote wa safari alionekana akinywa pombe kali kiasi cha kushindwa kujimudu na kuanza kutapika na kujisaidia haja ndogondani ya basi hilo.

Hata hivyo alisema baada ya kufika stendi ilikuwa ni vigumu kujitambua hivyo kupoteza fahamu na kulazimika kumpa msaada na kumzimua kwa maji kabla ya kupata fahamu kiasi na kujificha chini ya mfereji wa maji machafu .

Alisema kuwa mara baada ya kujitambua kiasi aliweza kutoa namba ya ndugu yake ambae ni askari wa FFU mjini Iringa aliyefika kumnusuru kuvuliwa nguo na kiongozi wake aliyefika eneo hilo na kumkutana akilishushia heshima jeshi kwa ulevi uliopitiliza

" Umelidhalilisha sana jeshi kwa askari kulewa hivi ukiwa katika sare .....sasa nataka kukuvua sare kisha nakupeleka kulala polisi kabla ya kesho kukuchukulia hatua zaidi " alisikika akisema kiongozi huyo ambae jina wala cheo chake hakukitaja
Maamuzi hayo ya kiongozi wake yaliwafanya mashuhuda kumuangukia na kumwomba amsamehe kwani bado ni kijana mdogo sana mambi ambayo aliyakubali na ndugu zake kumpakiza katika Taxi na kumpeleka eneo la Kihesa 
Ushauri wetu kwa askari wetu kujaribu kuheshimu nafasi hizo japo hakuna anayewakataza kunywa pombe ila watambue kuwa unywaji pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako ama chonde chonde ulevi noma.