Monday, December 1, 2014

WACHEZAJI WA SUNDERLAND WAKIWA WAMEVAA FULANA ZA KUITANGAZA TANZANIA KWENYE MECHI YAO DHIDI YA CHELSEA






Squad wear special warm-up t-shirts.
The players wore special t-shirts ahead of the home draw with Chelsea as part of the club's partnership with Tanzanian Tourist Board.
The Black Cats took to the field in the pre-game warm up sporting shirts emblazoned with the ‘Visit Tanzania’ logo as part of the partnership.
SAFC has already developed close links with Tanzania, through providing technical and practical support to the development of the football academy project, the first of its kind in the country.

The project will see thousands of youngsters benefit from a joined up approach combining football, education and community engagement, harnessing the knowledge and expertise of Sunderland AFC and its own successful Academy. 

RAIS KIKWETE AMTEUA PROF MUSSA ASSAD KUWA CAG MPYA, KUAPISHWA LEO

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS


PRESIDENT’S OFFICE,
STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Website : www.ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Mussa Juma Assad kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu, Desemba Mosi, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, inasema kuwa uteuzi wa Bwana Assad ulianza Novemba 5, mwaka huu, 2014.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa Bwana Assad ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 2, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.


Kabla ya uteuzi wake, Bwana Assad alikuwa Profesa Mshiriki, Idara ya Uhasibu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi ya Bwana Ludovick Utouh ambaye amestaafu kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma.

Profesa Assad ni msomi, mwenye weledi, ujuzi na uzoefu mkubwa wa uhasibu na udhibiti wa fedha ambaye ana Shahada ya Uzamivu wa Uhasibu (PHD in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Southampton, Uingereza mwaka 2001 na Shahada ya Uzamivu katika Udhibiti wa Fedha (MA in Financial Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City, Jamhuri ya Ireland mwaka 1991.

Profesa Assad pia ana Stashahada ya Kitaaluma ya Uhasibu (Professional Diploma in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City mwaka 1990 na Shahada ya Biashara (Bachelor of Commerce) ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam mwaka 1988.

Pamoja na uzoefu wa kitaaluma, Profesa Assad anao uzoefu mkubwa katika eneo la uhasibu na ukaguzi. Alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) kwa miaka saba (2007 - 2014); ni Rais na Mjumbe wa Chama cha Wahasibu Afrika (Pan African Federation of Accountants) tangu mwaka 2012; na ni mjumbe wa Bodi kadhaa za Wakurugenzi nchini Tanzania.

Katika kumteua Profesa Mussa Juma ASSAD kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Rais anayo imani kubwa kuwa elimu, weledi, ujuzi na uzoefu ambao Profesa Assad anao utamwezesha kutekeleza vema majukumu ya nafasi hiyo muhimu sana katika utawala bora wa nchi yetu.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.

1 Desemba,2014

WATANZANIA WENZETU WALIVYOTEKETEA KWA MOTO

INASIKITISHA NAMNA WATANZANIA WENZETU WALIVYOTEKETEA KWA MOTO
NI MPAKANI MWA ZAMBIA NA CONGO MARA BAADA YA LORI MOJA KULIPUKA MOTO NA MOTO HUO KUSAMBAA KWA KASI YA AJABU NA KUUNGUZA MAGARI MENGINE YALIYOKUWA KARIBU,BAADHI YA WATANZANIA WENZETU WALIOKUWA MADEREVA WA MALORI WAMEKUMBWA NA MKASA HUO ULIOPELEKEA MAJERUHI NA NA VIFOT0 
T1

MWANAJESHI ALEWA CHAKARI MPAKA KUZIMA


 Wananchi Iringa wakimtazama askari wa jeshi ambae jina halikuweza kufahamika aliyekuwa amezima kwa ulevi uliopinduki
 mjeshi huyo akiwa akiwa amezima
 Mjeshi huyo akiwa amepata fahamu baada ya kumwagiwa maji
Mjeshi akiwa amezima kwa kunywa pombe kupita kiasi
KATIKA hali isiyotegemewa askari mmoja wa jeshi la kujenga Taifa (JKT) anayesadikika kuwa na wa kambi ya Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa usiku wa juzi amenusurika kuvuliwa nguo za jeshi hadharani baada ya kukutwa amelewa chakali na kulala katika mfereji wa maji machafu eneo la nje ya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani mjini Iringa


Tukio hilo lilitokea muda wa saa 2 usiku baada ya wasamaria wema kumshusha askari huyo kutoka katika basi la Mgumba ambalo alikuwa amepanda kutoka Mafinga kuja mjini Iringa.

Akisimulia kisa na mkasa wa askari huyo kulewa chakali kiasi cha kushindwa kujitambua mmoja kati ya wasamaria wema aliyejitolea kumshusha katika basi hilo alisema kuwa askari huyo alipanda basi hilo Mafinga huku akiwa amelewa na wakati wote wa safari alionekana akinywa pombe kali kiasi cha kushindwa kujimudu na kuanza kutapika na kujisaidia haja ndogondani ya basi hilo.

Hata hivyo alisema baada ya kufika stendi ilikuwa ni vigumu kujitambua hivyo kupoteza fahamu na kulazimika kumpa msaada na kumzimua kwa maji kabla ya kupata fahamu kiasi na kujificha chini ya mfereji wa maji machafu .

Alisema kuwa mara baada ya kujitambua kiasi aliweza kutoa namba ya ndugu yake ambae ni askari wa FFU mjini Iringa aliyefika kumnusuru kuvuliwa nguo na kiongozi wake aliyefika eneo hilo na kumkutana akilishushia heshima jeshi kwa ulevi uliopitiliza

" Umelidhalilisha sana jeshi kwa askari kulewa hivi ukiwa katika sare .....sasa nataka kukuvua sare kisha nakupeleka kulala polisi kabla ya kesho kukuchukulia hatua zaidi " alisikika akisema kiongozi huyo ambae jina wala cheo chake hakukitaja
Maamuzi hayo ya kiongozi wake yaliwafanya mashuhuda kumuangukia na kumwomba amsamehe kwani bado ni kijana mdogo sana mambi ambayo aliyakubali na ndugu zake kumpakiza katika Taxi na kumpeleka eneo la Kihesa 
Ushauri wetu kwa askari wetu kujaribu kuheshimu nafasi hizo japo hakuna anayewakataza kunywa pombe ila watambue kuwa unywaji pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako ama chonde chonde ulevi noma.

SIRI IMEFICHUKA MSHAHARA NDIO SABABU YA HOUSE GIRL KUMTESA MTOTO

MSICHANA WA KAZI ALIYEMPIGA MTOTO AFUNGUKA MAZITO!

Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Duniani, leo kipo ambapo amekizungumza kwa mara ya kwanza tangu afanye kosa hilo baada ya jana kumuomba samahani mtoto huyo. Msichana huyo Jolly Tumuhiirwe ambaye kwa sasa amekamatwa na Polisi amesema sababu iliyomfanya amtese mtoto Arnella Kamanzi, ni kutokana na kuchanganyikiwa baada ya waajiri wake kutompatia pesa ili amtumie baba yake ambaye alikuwa anaumwa.

Amesema anajiona mwenye hatia kwa alichokifanya japo anadhani alifanya hivyo kama njia ya kumkanya mtoto huyo kwa kuwa alikuwa akimuona mama wa mtoto huyo alikuwa akimpiga kama njia ya kumkanya. 
 
Jolly amelalamika kuwa anajisikia vibaya pale ambapo wafungwa wenzake wamekuwa wakimtenga sana na kutaka kumpiga.

BI MWADAWA ALIITWA TAPELI ALIPOANZISHA KIKUNDI CHA VICOBA SASA AGEUKA KUWA MKOMBOZI

 Bi Mwadawa saidi ni mwanamke miongoni mwa wanawake wachache waliojitoa muhanga ili kupambana na umaskini na kujikwamua kutoka katika hali duni na kuwa mfano katia mji mdogo wa Mbezi luisi wilayani kinondoni jijini Dar.
Bi Mwadawa ambaye ni mratibu wa makazi katika VICOBA nchini amejitoa muhanga kuwa mwalimu wa wanawake na wanaume ambao wapo tayari kuondokana na umaskini kwa kuwakusanya pamoja na kuwafundisha jinsi ya kuondokana katika hali ya kuwa tegemezi na kuwa wajasiliamali. 

Mwanamke huyo ambaye amesema haikuwa kazi rahisi kwake kuwakusanya watu wa fikra tofauti na kuwafundisha kuhusu VICOBA endelevu kitu kilichopelekea yeye kuitwa tapeli na baadhi ya watu. Hata hivyo alisema kuwa hakukatishwa tamaa na watu hao badala yake alifanya juhudi kutoa elimu hiyo kwani alijua kitu anachokifanya. 
Bi Mwadawa ambaye sasa anavikundi 33 vya VICOBA na zaidi ya nusu ya vikundi hivyo vimeshajiunga kwenye mpango wa APPEX ambapo vikundi vyote vinauwezo wa kukopesheka kibenki na kujiendeleza.
Bi huyo na kikundi chake cha agape jana walizindua ofisi yao ya VICOBA cha MAKAZI iliyopo Mbezi Luisi na ilizinduliwa na Raisi wa VICOBA nchini Bi Devotha Likokola ambaye ndiye Mwasisi na mwanzilishi wa vikoba Tanzania.
kikundi hicho ambacho kilitimiza mwaka mmoja hapo jana kina zaidi ya Tsh 84,000,000 ambazo hukopeshana wao wenyewe kama wanakikundi. Na jana zilipatikana zaidi ya mil 3 katika harambee ya uboreshaji wa ofisi hiyo
 Mwadawa akiwa na rais wa vikoba Bi Devotha Likokola ndani ya ofisi mpya ya Makazi
 Raisi wa vikoba akikata utebe ikiwa na ishara ya uzinduzi wa ofosi ya Makazi Mbezi Jijini Dar jana
 Bi Devotha Likokola akiwaasa wanavicoba waliohudhuria uzinduzi huo 

VICOBA abavyo vilianzishwa na mwanasiasa ambaye ni mbunge wa viti maalum bi Devotha Likokola, alianzisha kwa nia ya kuwakomboa wanawake katika hali ya kuwa tegemezi na kuwafanya kuwa wajasiriamali kwa kuwafundisha mfumo endelevu wa kutegemezana kwa kuweka akiba na kukopa. Mfumo huo ambao umewanufaisha wananchi wengi na kuwafanya kuwa wamiliki wa mamilioni ya pesa kwa kununua hisa na kuweka mfuko wa jamii ambao umewasaidia wanachama wengi kuwasomesha watoto wao na wengine kununua nyumba zao wenyewe na magari kupitia VICOBA.

Bi Lilkokola ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa ofisi ya MAKAZI aliwaasa wanavicoba wote nchini kuachana na mfumo wa kuvunja vicoba kila ifikapo mwisho wa mwaka badala yake uwe mfumo endelevu ili kujikwamua zaidi. " huwezi ukawa unapanda mti halafu kila ifikapo mwisho wa mwaka unaukata, uwachekue ili uwe mkubwa ukuzalie matunda mengi baadae" alisema bi Likokola ambaye alifananisha vicoba na mti au mtoto.

mbunge huyo alisema kuwa VICOBA ni ubia wa hiari uliosajiliwa na BRELA kwa sheria ya ubia ili kuwawezesha wananchi kuwana haki ya umiliki wa fedha na mali kwani hii ni haki ya msingi kwa kila mwananchi na ili kutekeleza haki hii kwa urahisi ni vyema kila mwananchi akajiunga na vikundi vya Vicoba.

Ikiwa lengo kuu ni kumfanya mwanakicoba kuwa na maisha bora na ya furaha, thamani ya VICOBA ni kujitambua, uaminifu,kushirikisha na uwazi ili kukujitambua kujiwezesha kijasiriamali na kifedha.

Bi Likokola aliwahakikishia wanavioba kuwa ameanzisha VICOBA APPEX ambayo ni huduma ya kibenki inayotoa mikopa mikubwa kwa vikundi vya vicoba na muda si mrefu watakuwa na benki yao ambapo alisema hakutakuwa na benki yenye huduma bora na kumilikiwa na wananchi wenyewe Tanzania kama VICOBA.
VICOBA ambayo sasa imeenea nchi nzima na nchi zingine tano na wana nia ya kwenda mbali zaidi nia ikiwa kuenea dunia nziama
 Bwana Daudi Nkononki ambaye ni mwenyekititi wa kikundi cha Agape akisoma risala kwa mgani rasmi
 Mwenyekiti Daudi akikabidhi risala kwa Mheshimiwa Devotha Likokola
 wanavioba wakimzawadia Mbuzi Mh Likokola

 Mh: akifurahia moja ya picha aliyopewa kama zawadi na wanavikoba katika uzindizi huo
 mmoja wa wahudhuliaji katika uzinduzi huo akitoa ushuhuda jinsi naye alivyokuwa akidhani kuwa Bi Mwadawa ni tapeli wa pesa za watu. mzee huyo aliomba msamaha kwa bi Mwadawa na kumuahidi kujiunga na VICOBA pia aliwahimiza wazee pamoja na walemavu wengine kujiunga ili kuondokana na utegemezi na kuwa mizigo kwa ndugu na jamii kiujumla


Bwana Albet Njau Coordinator wa shirika la WAT ambalo ndilo linaloshirikiana na VICOBA kuwawezesha wanavicoba kumiliki makazi yao wenyewe. shirika hili linajishughulisha na ujenzi wa nyumba za aina yoyote hapa nchini.




WANANCHI WAASWA KUPANDA MICHE YA MATUNDA ILIYOBORESHWA





Kutokana na elimu ya kilimo kutolewa katika Nyanja mbalimbali watanzania wameonekana kuwa na mwamko wa kutumia mbegu na miche ya kisasa katika kilimo chao.

Hayo yamesemwa na msemaji wa BRIDEBABLE CONSULTANT LTD ya jijini Dar Mr Michael Lameck ambopo amesema wananchi wengi wamekuwa na muamko wa  kutumia mbegu bora katika kilimo, hivyo kuwaasa pia kutumia miche ya matunda iliyoboreshwa kiteknolojia zaidi.

msemaji huyo amesema kuwa upandaji wa miche ya matunda iliyo zalishwa kwa kutumia bioteknolojia ya uzalishaji kwa njia ya chupa na uzalishaji kwa kutumia vikonyo huleta tija katika kilimo cha matunda. kutokana na  watu kuwa na mwamko wa kula matunda pamoja na juisi za asili hivyo kumekuwa na uhitaji mkubwa wa matunda mijini hivyo amewaasa vijana kuchangangamkia tenda hii kwa kujikita katika kilimo

Ili kuepuka uagizaji wa matunda kutoka nje ya nchi kama ilivyo tunda la tufaa ambalo huletwa nchini kutoka nchi ya Afrika ya kusini amewataka vijana kujiajiri wenyewe katika kilimo kwa kulima matunda ambayo hayahitaji mkulima kuwa shambani wakati wote na hulimwa hata nyumbani kwa faida ya familia.

Bwana Michael akionyesha jinsi miche miwili ilivyounganishwa ili kupata mche mmoja 

Bridebable Consultant ni kampuni iliyoko jijini Dar inayouza miche bora ya matunda kwa wakulima nchini na nje ya nchi kulingana na mahitaji ya mkulima mwenyewe

Miche hii ambayo imeboreshwa na kituo cha utafiti na kilimo SUA ni miche ambayo hukua haraka na kuzaa matunda bora na kwa wingi. Miti hii ya matunda ni miti ambayo huchukua mda mfupi kuanza kuzaa matunda hivyo haimfanyi mkulima kusubiri mda mrefu kupata manufaa yake.

Bwana Michael alisema miche ya matunda ambayo inapendwa sana na watu wengi wa jiji la Dar ni pamoja embe aina ya Red Indian, Apple Mango, Alphonso, Cant, embe sindano na alizeti/dodo, pia kuna  Mapera, Minazi ya mda mfupi pamoja na machenza.

kilimo cha miti ya matunda yanaweza kupandwa nyumbani na kumnufaisha mtu kwa kula matunda na kutumia miti hiyo kama kivuli nyakati za jua kali, pia miti hupendezesha mazingira iwapo itapandwa katika utaratibu mzuri


 Baadhi ya miche inayouzwa na Bridebable

 Hata hivyo alisema kampuni yake inauza aina zote za miti japo kuwa kuna aina ya miti huuzwa kwa oda maalumu. hivyo yeyote mwenye mahitaji ya miti nyumbani au shambani kwake wasiliana nao kwa kuwapigia

+255 712545052, +255 784 647775 au waandikie  upambamichael@gmail.com


DIAMOND APETA TUZO ZA CHANNEL O AIBUKA NA TUZO 3


diamond  3diamond   19        Mwanamuzi wa kitanzania aitoa kimasomaso inchi yetu baada ya kufanya vizuri katika kinyang'anyiro cha tuzo za muziki Afrika. mwanamuziki Diamond amechukua tuzo 3 kati ya 4 na kuwaacha wenyemajina yao midomo wazi huku awaamini kama mkali wa kitanzania anaondoka na tuzo hizo.   
diamond   20
diamond  2Jumamosi Ya Nov  29 2014 Watanzania na wapenzi wa muziki wa bongo fleva walifuatilia kwa karibu sana tuzo za Video za Channel O zilizofanyika Johannesburg South Africa. Mtanzania mwenzetu Diamond Platnumz alikuwa akiwania tuzo nne kwenye vipengele tofauti.
Diamond Platnumz amefanikiwa kushinda tuzo tatu kati ya 4 alizokuwa anawania. Tuzo alizoshinda ni Most Gifted EastAfrica, Most Gifted Afro Pop na Most Gifted Newcomer.
Hizi ni picha za Diamond akiwa na mama yake mzazi, manager wake Bab Tale na Said Fela na Zari kutoka Uganda.
      diamond   4diamond   6diamond   8diamond   9diamond   10diamond   11diamond   13diamond  1
Kiukweli, haikuwa rahisi kabisa.. lakini kwa uwezo wa Mwenyez Mungu na support kubwa mliyonipa iliwezesha Bongo Flavour yetu kuandika Historia mpya kwenye Ramani ya mziki wa Africa…Hii inaonyesha ni jinsi gani Umoja ni nguvu na pia jins gani mziki wetu ukisupportiwa na kupewa kipaumbele unaweza kufika mbali zaidi… Shukran sana kwa @channeloafrica @channelotv kwa kuniona na kuthamini kipaji changu, My Family, Management, Media zote zilizokuwa zikinisupport, Watangazaji, Wasanii, Wadau na bila kuwasahau wapendwa wangu #TeamWasafi #TeamChibu #TeamPlatnumz #TeaMMondi toka instagram, Facebook, Whatsapp, Twitter na kadharika, wakiongozwa na kamanda langu @kifesi … Nawashkuruni sana sana

MFAHAMU SINGASINGA TAPELI WA ESCROW


POLISI ALIYEUA KIJANA MWEUSI AJIUZULU!


Daren Wilson Afisa wa polisi aliyempiga risasi na kumuua kijana mweusi nchini Marekani amejiuzulu. Wakili wa Darren Wilson ambaye ni afisa wa polisi aliyempiga risasi na kumuua kijana mweusi Michael Brown kwenye eneo la st Louis nchini Marekani mwezi Agosti anasema kuwa polisi huyo amejiuzulu.
Mapema wiki hii bwana Wilson aliondolewa mashtaka hatua iliyozua ghadhabu miongoni mwa waamerika weusi.Afisa huyo amekuwa likizoni tangu mauji hayo yafanyike, mauaji ambayo yalisababisha majuma kadha ya maandamano. 
Michael Brown,kijana mweusi nchini Marekani alipigwa risasi na kuuawa. Gazeti la St Louis limesema kuwa afisa huyo mwenye miaka 28 aliamua kujiuzulu baada ya kitengo chake cha polisi kupokea vitisho kwamba ghasia zitafutia iwapo ataendelea kuhudumu kama mfanyikazi.
Gazeti hilo lilichapisha kile lilichodai kuwa barua yake ya kujiuzulu ambayo ilisoma:''nimearifiwa kwamba iwapo nitaendelea kuwa mfanyikazi wa idara ya Polisi basi hatua hiyo itawachochea maafisa wa polisi na raia wa eneo la Furguson kuishi kwa hofu,hali ambayo siwezi kuikubali hata kidogo.''