Thursday, September 18, 2014

MASKINI NDOA HII JAMANI IMEFIKIA HAPA

Stori: Richard Bukos
PAMOJA na kutumia nguvu nyingi kukanusha kwenye mitandao kwamba ndoa yao haijavunjika, mtangazaji mahiri Bongo, Gardner Gabriel Habash ‘G. Habash’ na ‘mtalaka’ wake, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’, Jumamosi iliyopita walifanya tukio lililowashangaza watu kufuatia kila mmoja kuingia ukumbini akiwa na kampani yake na kukwepana kama paka na panya, Amani liliwanasa kwa vile lilikuwepo.

Tukio hilo lililoamsha minong’ono kwa watu waliosoma mchezo mzima, liliibukia ndani ya Ukumbi wa Ten Lounge (zamani Business Park) uliopo Makumbusho, Kijitonyama jijini Dar es Salaam ambako kulikuwa na uzinduzi wa albamu ya Bongo Fleva.

WALIVYOKAA
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Gardner alipoingia alikwenda kukaa kwenye meza na watu wengine watatu,  baadaye akafika Miss Mara 2000, Rashida Wanjara na kuunga ambapo walikuwa wakibadilishana mawazo na kufunguliana vinywaji kwa meno na kumiminiana kwenye glasi.

JIDE NAYE
Wakati Gardner ambaye pia hujulikana kwa jina la utani la Kapteni akiendelea kujipoza na Rashida na wengine, Jide yeye alikaa meza moja na kijana mmoja aliyevalia shati la kitenge la mtindo uliowahi kutamba miaka mitano nyuma, wengine huita Mackezie sanjari na wadada wawili.

WALICHOTAKA WATU
Baadhi ya watu walisikika wakishauri kwa sauti ushauri ambao haukuwafikia wawili hao ambapo walisema kama kweli ndoa hiyo haijavunjika, ni vyema Jide angeenda  kwenye meza aliyokaa Gardner na kusema chochote kisha kuondoka hali ambayo hakuwepo.

MAPACHA WALIOUNGANA MWILI WILAYANI MAKETE MKOANI NJOMBE KUHITIMU KIDATO CHA NNE MWAKA HUU



Hatua ya kwanza ya ndoto ya kuzama katika elimu ya mabinti pacha walioungana kiwiliwili, Consolata na Maria Mwakikuti (18) wa Kijiji cha Ikonda wilayani Makete  mkoa mpya wa Njombe, inatarajiwa kutimia Novemba mwaka huu, wakati mabinti hao watakapofanya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne.
 
Itakumbukwa kwamba walipokuwa wakimaliza elimu ya msingi mwaka 2009 kijijini kwao Ikonda, walikuwa na umri wa miaka 13 na katika ndoto zao kwa pamoja walisema wanataka kuwa wasomi waliobobea katika utaalamu wa kompyuta. Lakini, kwa sasa, wanasema wanatamani kufanya kazi ya Ukatibu Muhtasi.
 
Wanafunzi hao mwaka 2010 walichaguliwa kujiunga na Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Jangwani, Dar es Salaam.
 
Kwa sasa wanasoma katika Shule ya Sekondari ya Maria Consolata iliyopo Kidabaga wilayani Kilolo mkoani Iringa.
Shule hiyo inamilikiwa na Kituo cha Nyota ya Asubuhi ya Wamisionari Wakatoliki wa Italia, kinachosaidia kuwatunza watoto wanaotoka katika mazingira magumu.
 
Wakizungumza na mwandishi wa habari hii shuleni hapo hivi karibuni, walisema wanafurahi kuwa miongoni mwa watahiniwa watakaofanya mtihani huo wa kidato cha nne mwaka huu.
 
"Tunafurahi, tunajiandaa tunasoma kwa bidii, mtihani uko karibu tunataka tufaulu vizuri masomo yetu, ili ile ndoto yetu ya kuwa Makatibu Muhtasi itimie," walisema Maria na Consolata, ambao wanatumia baiskeli maalumu kuwapeleka darasani, ambako pia wana kiti maalumu.
 
Pacha hao wameshangaza watu wengi kwa jinsi walivyo, ambapo kila mmoja ana madaftari yake. Wakati wa kufanya mazoezi au kuandika kazi wanazopewa, mmoja huanza kuandika, akimaliza na mwingine huandika.
 
"Wala hatupati shida tumezoea, kila mmoja anafanya kazi yake, mimi naandika kwa mkono wa kushoto na Maria anaandika kwa mkono wa kulia," anasema Consolata, ambaye anaonekana kuwa mchangamfu zaidi.
Shule hiyo ina wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne. Ilianzishwa mwaka 2006 na hivi sasa ina jumla ya wanafunzi 183. Wote wanaishi kituoni hapo na wote wanatoka kwenye mazingira magumu.
 
Changamoto kubwa iliyokuwa shuleni hapo ni ukosefu wa nishati ya umeme, ambapo uongozi wa shule na kituo hicho unalazimika kutumia jenereta na umemejua, jambo ambalo mapema wiki hii Wakala wa Nishati ya Umeme Vijijini (REA), imewaondolea adha kwa kuwapelekea umeme.
 
Pacha hao walizaliwa mwaka 1996 wakiwa wameungana katika Hospitali ya Ikonda wilayani Makete mkoani Iringa.
 
Walifaulu mtihani wa darasa la saba mwaka 2010, ambapo kila mmoja alipata alama 151, ingawa walitofautiana ufaulu  kwenye masomo yao.
 
Katika somo la Maarifa ya Jamii, Consolata alipata alama 29 na Maria alama 25, kwenye somo la Kiingereza, Maria alipata alama 36 na kumzidi Consolata aliyepata alama 34, wakati kwenye somo la Sayansi, Maria alimzidi Consolata kwa kupata alama 31 dhidi ya 29.
 
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi iliwapanga pacha hao kujiunga na kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Jangwani jijini Dar es Salaam.
 
Hata hivyo hawakujiunga na sekondari hiyo, kutokana na hali yao na pia umbali kutoka Iringa hadi Dar es Salaam. Ndipo Wamisionari hao wakawachukua mwaka 2011 na kuanza kidato cha kwanza.
 
Walizaliwa kwenye Hospitali ya Misheni ya Ikonda mwaka 1996. Lakini, taarifa zao hazikufahamika hadi pale walipoandikishwa kuanza elimu ya msingi Ikonda na kutafutiwa mlezi wa kuwaangalia, baada ya wazazi wao kufariki dunia wakiwa bado wadogo.

UBAGUZI WA RANGI WAZIDI KUTIKISA ULIMWENGU WA SOKA

Na Saleh Ally
WAKATI mwingine nimekuwa najiuliza mambo maswali mengi sana kuhusiana na suala la ubaguzi wa rangi ambalo linaonekana wakati mwingine kulielemea Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Nianze na mkasa wa juzi ambao umemtokea kiungo nyota wa Brazil, Ronaldinho Gaucho ambaye hivi karibuni amejiunga na klabu ya Querétaro ya nchini Mexico ambako anaamini ndiyo atamalizia mpira wake.
Ronaldinho amebaguliwa, amedharauliwa na kuitwa sokwe, licha ya kwamba hakuwa na kosa hata punde.
Aliyembagua ni mwanasiasa maarufu wa chama kinachojulikana kama National Action Party (Pan) ambaye pia amewahi kuwa waziri wa serikari ya Mexico.
Jamaa anaitwa Carlos Manuel Treviño ambaye ameingia kwenye kundi la wapuuzi na wajinga wanaoamini ubaguzi wa rangi ni nyenzo.




Kisa cha kumbagua Ronaldinho ni kwa kuwa mwanasiasa huyo alikuwa akitokea katika mihangaiko yake anarejea nyumbani, kukawa na foleni kubwa sana njiani na mwisho aligundua inatokana na mashabiki wa klabu ya Queretaro waliokuwa wakitokea kwenye Uwanja wa Corregidora kumpokea kiungo huyo alipokuwa anatambulishwa.
Akaamua kuweka maneno ya kashfa kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook akimuita sokwe ambaye amesababisha yeye kuchelewa kufika nyumbani.


Mpira ni burudani kubwa lakini ni chombo bora kabisa cha kuwaunganisha watu mbalimbali wakiwemo wale waliogombana, wasiopendana au kutoelewana.
Nchi nyingi zilizoingia kwenye vita hasa vile vya wenyewe kwa wenyewe, mwisho zimetumia nguvu zaidi kwenye mchezo wa soka ili kurejesha hali ya utulivu.
Mfano mzuri ni Wanyarwanda ambao baada ya mauaji ya kimbari mwaka 1994, soka ndiyo chombo kilichosaidia kwa asilimia kubwa kuwaunganisha, pia kujitahidi kusahau mabaya na makali yaliyopita.

Sasa jiulize, wakati wengine wanatumia soka kama chombo unganishi, vipi hao wanatumia mchezo huo kama chombo tenganishi kwa lengo la kudharau, kuonea au kubeza bila hata sababu yoyote ya msingi.
Ninazungumzia Wazungu, ninazungumzia watu weupe wanaoamini ni bora kuliko Weusi hata kama heshima yao haiko juu kama wanavyofikiri.
Wakati mwingine unaweza kufikiri hata wao Fifa ni wababaishaji kwenye hili kwa kuwa hakuna adhabu kali zaidi kwa wanaofanya hivyo viwanjani.
Kuna kila sababu ya kuliangalia zaidi kwa kuwa wale wanaowabagua weusi, wanakuwa hawana heshima ya kimatendo au hata fedha dhidi yao.
Angalia waliombagua Samuel Eto’o au Yaya Toure kule Urusi. Mfano mwingine wale mashabiki ambao huwabagua wachezaji Waingereza au kule Hispania.
Ajabu hili linafanywa hata na wachezaji kwa wachezaji, nafikiri ndiyo ungekuwa mfano mzuri zaidi kuwaonya wabaguzi wengine.
Ikitokea mchezaji kambagua mwenzake, halafu ushahidi ukawa umepatikana kwa uhakika, basi afungiwe msimu mzima.
Wale mashabiki wanaweza kujifunza kupitia adhabu kali ambazo watapata wachezaji, makocha, viongozi na hata waamuzi ambao wataonyesha ubaguzi.
Nani kasema ngozi nyeupe au ngozi ya mzungu ndiyo akili? Upuuzi mtupu!
Tunajua Fifa ina Wazungu wengi kuliko Weusi, huenda linaonekana si suala kubwa sana na mapambano yake yako kwenye mapango tu bila ya vitendo.
Huenda adhabu ingekuwa kali sana kama Waafrika wangekuwa na nafasi ya kuwabagua Wazungu pia. Fifa bado inahusika na inapaswa kujua upole wake katika hilo, unazidi kufanya liendelee.
Wazungu wanaobagua Weusi ni wapuuzi, Fifa haipaswi kuacha upuuzi huo uendelee kwa kuwa si Weupe tu ndiyo wanaoujua kuucheza mpira na mfano mzuri wa kuwa Weusi wanaujua mpira, jikumbushe kwa Pele.
Wajinga kama mwanasiasa yule wa Mexico aliyembagua Ronaldinho ambaye sasa tayari yuko katika hali mbaya kisiasa kutokana na kusakamwa sana na mashabiki wa soka, wanapaswa wapate joto ya jiwe kama anayokutana nayo, la sivyo hawataacha.
Lakini kwa Fifa na mashirikisho ya soka Ulaya, nayo yapambane kuzuia hilo kwa kuwa inakuwa ajabu, hata Wazungu wenye njaa, nao wanawadharau Waafrika wenye mafanikio zaidi eti kisa ni Weupe. Huu ni upuuzi mkubwa.

MTOTO ALIYEZAMIA NDEGE: ATOWEKA TENA



Mtoto Happiness Rioba(10) aliyedaiwa kuzamia kwenye ndege kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar bila kugundulika, ametoweka tena nyumbani kwao baada ya kukutanishwa na mama yake mzazi Sara Zefhania.

Happiness ambaye ni mkazi wa eneo la Mkokozi, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani inadaiwa ametoweka katika mazingira ya kutatanisha.

Akizungumza na Mwananchi jana, Sara alisema mwanawe alitoweka jana saa sita mchana na kutokomea kusikojulikana.Alisema asubuhi mtoto wake aliamka salama bila tatizo lolote na muda wote walikuwa pamoja kwa kuwa alikuwa na wageni kutoka kituo cha televisheni cha ITV, waliomuahadi kumtembelea nyumbani kwa lengo la kumuona Happiness.

“Aliamka vizuri tu na muda wote alikuwapo nyumbani, lakini ilipofika saa sita mchana, nilipigiwa simu na waandishi wa habari wa ITV kuwa nikawachukue katika kituo cha daladala... kabla sijaondoka nilimwambia mwanangu nakwenda kupokea wageni, lakini niporejea nyumbani na wageni hatukumkuta,” alisema Sara.

Alisema baada ya kumkosa alianza kumtafuta akishirikiana na waandishi hao pamoja na majirani, lakini hawakufanikiwa kumpata ndipo alipotoa taarifa kwa mjumbe wa Serikali za Mitaa na kuwataarifu ndugu, jamaa na marafiki.

Aidha, aliongeza mwanawe alipokuwa Zanzibar alifanya mambo ya ajabu likiwamo kuongea na paka, kula chakula kwa kutumia mkono wa kushoto, kutokuongea na watu pamoja na kutoweka katika mazingira ya kutatanisha.

Alifafanua kuwa walipofika nyumbani wakitokea Zanzibar alianza kumdadisi kutaka kujua alifikaje huko na je kweli alipanda ndege, alisema baba yake ndiye alimuita ili akaishi naye huko.

CHAMA CHA ZITTO KABWE ACT,CHAFUNGUA OFISI ZILIPO OFISI ZA CHADEMA ARUSHA...


MAMA NA MWANAYE WAOANA BAADA YA KUWA NA MAHUSIANO YA JINSIA MOJA



"Mimi na Vertasha mwanangu tulianza mahusiano yetu wakat kipindi hicho akiwa na miaka 16 tu.Lakini nilisubiri mpaka afikishe miaka 18 ndipo tungeanza mapenzi kabisa kwa sababu ni umri ambao unaruhusiwa kisheria,sasa tunatembea out bila kificho chochote ili kuwa saidia watu wengine ambao wako kwenye uhusiano wa kishoga/mama na mwana/wasagaji ilio wajisikie huru.Tunataka watu watutambue kwamba sisi tuna mahusiano ya jinsia moja kama kawaida alisema mama huyo"

Sheria zinazuia mahusiano ya kindugu hasa suala la usagaji katika nchi nyingi za kiafrika..
 "Sisi ni wanawake kwa hiyo mimi Vertasha hatuwezi kuzaa watoto tena na tumeridhika na mahusiano yetu "

Vertasha anafurahia mahusiano hayo pia na anasema hivi...!!

"Mama yangu ni mama yangu anafanya vitu ambavyo ni wajibu wa mama kuvifanya,ananinunulia nguo ananinunulia chakula ananiambia nikatandike kitanda ,so imetokea tu tukawa tunafurahia mapenzi kwa pamoja"

MAMIA WAMSINDIKIZA MBOWE POLISI

 


Ulinzi mkali ukiwa umeimarishwa eneo la Makao Makuu ya Polisi wakati Freeman Mbowe akiwasili kuhojiwa.
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema Taifa (Bawacha), Halima Mdee akiwasili Makao Makuu ya Polisi jijini Dar leo.
Wananchi wakiwa Makao Makuu ya Polisi.
Mbowe amefika makao makuu hayo kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu kauli yake aliyoitoa Jumapili iliyopita ya kuitisha maandamano nchi nzima kushinikiza kusitishwa kwa Bunge Maalumu la Katiba.
Katika tukio hilo, baadhi ya waandishi wa habari wamekimbizwa na polisi waliokuwa na mbwa wakitakiwa kukaa umbali wa mita 200 kutoka katika makao makuu hayo ya polisi.
Mmoja wa wanachama ambaye alibishana na askari na kujikuta akipata kibano kidogo na baadae kuachiwa 
Mwenyekiti wa chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA mh FREMAN MBOWE leo amefanya shughuli za jiji la Dar es salaam kusimama kwa muda baada ya kufika makao makuu ya polisi jijini akiwa na wanasheria wa chama huku mamia ya wanachama wake wakiwa nyuma yake kutaka kujua kinachoendelea hapo ikiwa ni kuitikia wito wa jeshi hilo waliomtaka kufika kwa maelezo zaidi.
Baada ya mh MBOWE kufika makao makuu ya polisi aliingia ndani na kuhojiwa zaidi ya masaa manne na kisha mwanasheria wa chama hicho mh TUNDU LISSU kutoka na kauli kuwa mwenyekiti huyo ametuhumiwa kuwa makosa ya uchochezi alioufanya juzi jumapili wakati akihutubia wanachama wake ambapo alisema kuwa wataandamana na kufanya migomo nchi nzima kupinga bunge la katiba linaloendelea.
Hata hivyo kwa taarifa ya TUNDU LISSU ni kuwa mh MBOWE ameachiwa kwa dhamana kwa ajili ya kusubiri kesi yake hiyo.
Hata hivyo mh MBOWE alionekana kufichwa sana kiasi cha kutoikuwa rahisi kuonekana na wafuasi wake
Nje ya ofisi za jeshi la polisi wananchi ambao ni wafuasi wa CHADEMA walionekana kuwa na hamu ya kumwona mwenyekiti wao ambapo kwa mara kadhaa walisikika wakiimba na kupiga kelele ambapo polisi walianza kuwasukuma na kusogeza silaha zo karibu ila hali ikawa shwari.hadi mtendao huu unaondoka katika eneo la tukio wafuasi hao walikuwa wameondoka kwa maombi ya mwanasheria tundu lissu kuwa waondoke hapo ili kuepusha vurugu zisizo na msingi
Viongozi wa chama hicho walikuwepo kuhakikisha kuwa hali inakua shwari 
Mh TUNDU LISSU akizungumza na wananchi pamoja na wanahabari ambao aliwataka kuondoka katika maeneo hayo ili kuepusha vurugu ambazo zingeweza kuwaharibia zaidi katika kesi hiyo 

 

KAFULILA ATAKA PROFESA TIBAIJUKA ACHUNGUZWE: MABILIONI YA IPTL


 
MBUNGE wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi), ametaka viongozi wa Serikali, Bunge na Mahakama wanaotajwa kulipwa fedha za IPTL zilizokuwa kwenye Akaunti ya Escrow akiwamo Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka wahojiwe.

Alisema kuwa Profesa Tibaijuka ni mmoja wa viongozi wa Serikali ambaye amekiri kupewa fedha hizo, hivyo ni vyema vyombo vinavyohusika vikamuhoji.

“Vigogo wa Serikali, Bunge na Mahakama wanaotajwa kulipwa fedha kupitia akaunti ya VIP wanapaswa kuchunguzwa na PCCB (Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa), kwakuwa akaunti hiyo ilipokea fedha za Escrow. Hivyo ni wito wangu kwa PCCB imuhoji Profesa Tibaijuka kwakuwa amekiri kupokea fedha hizo,” alisema Kafulila alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.

Kafulila amesema pia kuwa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, akabidhi ripoti ya uchunguzi wa ufisadi wa Sh bilioni 200 kabla hajaacha ofisi Ijumaa.

“Hii ni kwa sababu yeye mwenyewe kabla hajaagizwa na Bunge aliomba siku 45 Machi 20, hadi leo ni zaidi ya siku 160 zimepita na hajakabidhi ripoti hiyo wala kutoa taarifa yoyote.

“Majibu anayotoa kuwa watafanya waliobaki, yanatia shaka hasa ukizingatia muda uliokwisha hadi sasa. Anaposema kazi hii ni sawa na majukumu mengine ya kawaida ni kielelezo cha kukimbia wajibu wake katika suala hili tete ambalo limesababisha hadi sasa nchi wahisani wasichangie bajeti kusubiri uchunguzi huu,” alisema Kafulila.

Alisema pia kuwa akauti ya VIP iliyopo Benki ya Mkombozi, ilipaswa kufungwa hadi uchunguzi ukamilike kwani ni mfaidika wa hela za Escrow zinazochunguzwa.

“Hiwezekani Benki ya Ulaya imesimamisha Akaunt ya VIP Uholanzi kwa shaka ya kupokea hela zinazochunguzwa za Escrow, lakini Tanzania bado VIP haijafungwa kusubiri uchunguzi,” alisema Kafulila.

Alisema pia kuwa taarifa zilizopo ni kwamba PCCB wameshakabidhi ripoti ya suala hilo Ikulu badala ya Bunge lililoomba kufanyika kwa uchunguzi huo.

“Hii ni kinyume cha utawala bora na ni mwanya wa uchakachuaji wa ripoti kama ilipotokea mwaka 2000 ambapo ripoti ya PCCB kuhusu wahusika walioingiza nchi kwenye mkataba mbovu wa IPTL walifichwa na Ikulu na kusababisha nchi kuendelea na mkataba wa kinyonyaji wa miaka 20,” alisema Kafulila.

Gazeti hili lilipomtafuta Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue, ili kuzungumzia suala hilo, alisema Ikulu haijapokea taarifa hiyo.

ZITTO
Naye Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, amesema suala hilo litazidi kuvuruga imani ya wananchi kwa utawala wa Rais Jakaya Kikwete kama wahusika wa suala hilo hawatachukuliwa hatua.

Alisema kutokana na hali hiyo, wanasiasa wanapaswa kuhamasisha ili kusaidia kuwafikisha waliotekeleza kashfa ya IPTL, PAP mbele ya sheria mara watakapokuwa wamepata vielelezo vinavyohitajika.

“Katika hali ya kawaida unaweza kujiuliza inakuwaje mtambo wa kufua umeme ulete mgogoro kisheria na katika vyombo vya habari kwa karibu miongo miwili na ukaruhusiwa kuvuruga vipaumbele vya uzalishaji umeme nchini.

“Pia inakuwaje mradi huu uchangie kutokea hasara kubwa kwa sekta ya umma na binafsi, hii inaonyesha kuwa mradi huu ni kielelezo cha utawala mbovu ndani ya Wizara ya Nishati,” alisema.

Kutokana na hali hiyo, alisema kuna maswali kadhaa ambayo hayajajibiwa ikiwa ni pamoja na kwanini Tanesco iliilipa IPTL kwa muda mrefu bila ya kuhoji malipo ya uwezo wa mitambo ni kwa muda gani mtambo wa IPTL ulikuwa haufanyi kazi na ni wakati gani ulipoanza tena, lakini pia wananchi wanapaswa kujiuliza kuwa nani alilipia matengenezo yake wakati ukiwa haufanyi kazi.

Alihoji pia kiasi cha fedha zilizobaki katika akaunti ya Escrow kama ni kweli ipo, IPTL inafanya kazi gani, nani anamiliki, hali yake ikoje, je hivi sasa inapata fedha za uendeshaji wa mitambo na ni kiasi gani, halafu kuna makubaliano gani kati ya kampuni hiyo na Tanesco.

KIKOSI KIPYA CHADEMA 2015



HATIMAYE Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeunda kikosi kazi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, baada ya makada nane kuchaguliwa na Baraza Kuu kuwa wajumbe wa Kamati Kuu.

Katika kikosi hicho, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika amevaa viatu vya aliyekuwa Makamu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, Zitto Kabwe.

Safu ya kikosi hicho ambacho kitaongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe, ilikamilika juzi usiku kwa Baraza Kuu kuchagua wajumbe nane wa Kamati Kuu, ikiwamo kuthibitisha uteuzi wa viongozi wa Kamati Tendaji kwa Bara na Zanzibar.

Katika safu ya Kamati Tendaji, mbali na Mnyika, chama hicho kimemteua mwanahabari, Salum Mwalimu Juma, kuwa Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, huku  nafasi ya Katibu Mkuu ikirudi kwa Dk. Willibrod Slaa.

Kwa upande wa wajumbe wa Kamati Kuu Bara, wanamume, waliorejea ni Profesa Mwesiga Baregu aliyepata kura 127 na Mabere Marando (164).

Sura mpya zilizoingia kwenye Kamati Kuu  Bara ni  Dk. Yared Fubusa aliyepata kura 127 na kwa upande wa Zanzibar, ilikwenda kwa Salum Mwalim Juma (112).

Wajumbe wa Kamati Kuu wanawake Bara, ilichukuliwa na sura mpya Catherine Vermand (97) na Suzan Kiwanga (93), wakati upande wa Zanzibar nafasi hiyo ilikwenda kwa Zainabu Musa Bakari (111) ambaye pia ni mpya.

Kazi ya kuchagua wajumbe nane ilihitimishwa kwa kuchaguliwa Elly Marco Macha kupitia nafasi ya watu wenye ulemavu iliyokuwa ikishikiliwa na marehemu mama mzazi wa Zitto, Shida Salum.

MAKAMU WENYEVITI
Nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bara imechukuliwa na Profesa  Abdallah Safari na kwa Zanzibar ni Said Issa Mohammed.

BARAZA LA WAZEE
Mwenyekiti wa baraza hilo, amechaguliwa Hashim Juma Issa, makamu wake ni Susan Lyimo, wakati  Makamu Mwenyekiti  Zanzibar ni Omar Masoud Omar, huku nafasi ya Katibu Mkuu ikienda kwa Rodrick Lutembeka.

BAWACHA
Nafasi ya Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHAa) ilikwenda kwa Halima Mdee na nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bara ilichukuliwa na Hawa Mwaifunga, huku Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar akiwa Hamida Abdallah.

BARAZA KUU BAWACHA
Nafasi hiyo kwa Zanzibar ilichukuliwa na Janeth Medadi Fusi, huku kwa upande wa Bara ilichukuliwa na mwandishi wa habari wa Gazeti la Tanzania Daima, Janeth J. Mjungu, Restuta Said Mjoka, Marietha Cosmas Chenyenge na Suzan Kiwanga.

BAVICHA
Nafasi ya Mwenyekiti  wa Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA) ilikwenda kwa Paschal Patrobas na nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bara ilikwenda kwa Patrick Sosopi na kwa upande wa Zanzibar, alichaguliwa Zeudi M. Abdallah.

VIGOGO WALIOANGUSHWA
Baadhi ya vigogo walioangushwa katika uchaguzi huo kwenye nafasi mbalimbali ni pamoja na Fred Mpendazoe, mwanaharakati Hebron Mwakagenda, aliyekuwa Katibu wa BAVICHA, Deogratius Mushi, Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Chiku Abwao, Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Ansbert Ngurumo, Mwenyekiti Mkoa wa Kinondoni, Henry Kilewo na Dk. Arcado Ntagazwa.

SIKITI WA HINDU WA MTAA WA KIBASILA JIJINI DAR WATEKETEA KWA MOTO,


 Kikosi cha zima moto kikifanya juhudi za kuzima moto huo.
MSIKITI wa madhehebu ya Wahindu uliopo maeneo ya Mtaa wa Kibasila karibu na shule ya Olimpia jijini Dar es Salaam, umeteketea kwa moto leo asubuhi ambapo baadhi ya mali zimeungua na mtu mmoja kukimbizwa hospitali kutokana na mshituko.


 Sehemu ya chumba cha msikiti kilichoungua.
Akizungumza na mtandao huu, shuhuda mmoja alisema moto huo umesababishwa na hitilafu ya umeme iliyoanzia kwenye mashine ya luku ambapo baadhi ya waumini walikuwa wakijiandaa  kuupamba msikiti huo.


 Wananchi wakiwa katika eneo la tukio wakisaidia kuokoa baadhi ya mali zilizopo ndani ya msikiti.
 Gari la kikosi cha zima moto likiwa eneo la tukio kuuzima moto.


Baadhi ya waumini wakiwa eneo la tukio.
Baadhi ya mali zilizookolewa.

MTUHUMIWA KESI YA UGAIDI AZIDI KUWAUMBUWA POLISI KWA MATESO YAO YA KUMMINYA SEHEMU ZAKE ZA SIRI

 Mtuhumiwa katika kesi ya ugaidi, Abdallah Maginga, ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, kumruhusu kutohudhuria siku za kesi na abaki magereza, kutokana na maumivu makali anayodai anayapata sehemu za siri alikominywa na polisi na kuingiziwa mti kwenye haja kubwa.
“Mheshimiwa Hakimu naomba mahakama yako inipe ruhusa ya kutohudhuria siku ya kesi, sababu ninapopanda gari napata maumivu makali sana sehemu za siri kunauma kwa sababu polisi walinitesa kwa kuniingizia mti kwenye haja kubwa na kuminya sehemu zangu za siri,”alisema.
Alisema mbele ya Wakili wa Serikali, Rose Sulle kuwa mbali na maumivu ya sehemu za siri, pia mguu wake uliokatwa hospitalini, bado unamsumbua kutokana na maumivu.

 
Maginga pia aliomba iagize Magereza wamruhusu akatibiwe hospitalini, kwani alitakiwa kwenda kupata matibabu Septemba 5 mwaka huu, ila alizuiwa hadi sasa.
 
Akijibu hoja hizo, Hakimu aliyesikiliza kesi hiyo, Devotha Msofe, alisema  suala la kuja mahakamani ni lazima na mahakama haiwezi kumpa ruhusa hiyo.
 
Pia, alimshauri mshitakiwa huyo kuwa kama ana maelezo mengi, amweleze hakimu anayesikiliza kesi yake, Mustapher Siyani ambaye kwa siku hiyo hakuwepo.
 
“Sikiliza Maginga suala la kuja mahakamani ni lazima na sio hiyari wala majadiliano, ila kuhusu kwenda hospitalini liwasilishe Magereza ndio mtaona kwa pamoja mnafanyaje,” alisema.
 
Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa washitakiwa  hao wameshitakiwa kwa makosa yaliyo chini ya Sheria ya Kuzuia ugaidi, ambapo Sheria Namba 22  ya Mwaka 2002 inasema upelelezi ukishakamilika, Mahakama Kuu ndiyo yenye mamlaka ya kuisikiliza na kutoa uamuzi.
 
Washitakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka ya kuua, kujaribu kuua, kusajili na kusafirisha vijana kujiunga na Al-Shabaab.
 
Mbali na mashitaka hayo, pia wanahusishwa na  tukio la  mlipuko wa bomu lilitokea baa ya  Arusha Night Park jijini Arusha na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine 16.
 
Watuhumiwa wengine wanaokabiliwa na mashitaka hayo ni Abdallah Athumani, Abdallah Thabiti, Ally Hamisi, Abdallah Wambura, Rajab Hemedi, Hassan Saidi, Ally Hamisi, Yassin Sanga, Shaaban Wawa, Swaleh Hamisi, Abdallah Yassin, Abdallah Maginga na Sudi Nassib Lusuma.
 
 Wengine walioongezwa katika shauri hilo ni Shaaban Mussa, Athuman Hussein, Mohammed Nuru, Jafari Lema, Abdul Mohammed na Said Michael Temba.

DIAMOND AWAFUNGUKIA WADADA


Diamond platnumz katika ururasa wake wa facebook amepost post ambayo ina mashiko sana kwa madada wa kibongo wanaojiona wao wako juu sana wanaona wakiza watapoteza mvuto kwa watu diamond akaamua kufunguka kiivi.Kwa mtazamo wangu mimi naona kuzaa hakumfanyi mtu azeeke au awe wa kizamani, ni tabia tu ya mtu mwenyewe.... na ndiomaana dada zetu kama Beyonce, Nancy sumary, Kim Kardashian na kadharika wana watoto na still wanafanya vizuri.....Au we mtazamo wako ukoje?
(I believe, bearing kid (s) doesn't transform a woman being old or being out of fashion.....it's her natural Behavior...my living proof are, Beyoncé, Nancy Sumary, Kim kardashan etc.... Isn't it??? Let me hear your views on this....)

MAMA AFUNGUKA MAAJABU ANAYOYAFANYA MWANAE NA KUSEMA NI MAZITO NA YANATISHA

Mtoto Happiness (10) anayedaiwa kuzua kizazaa mjini Zanzibar.

MTOTO Happiness (10) (pichani) ambaye mwishoni mwa wiki iliyopita  alizua kizazaa mjini Zanzibar baada ya kuonekana akizungumza na viumbe wa ajabu na wanyama, ametua jijini Dar kufuatia kufika kisiwani humo kimaajabu.Kwa mujibu wa mama mzazi wa mtoto huyo, Sarah Zefania, mwanaye Happiness alianza kuonesha maajabu Zenji tangu alipoonekana kwenye uwanja wa ndege kisiwani humo wiki iliyopita.
Alisema maofisa wa uwanja huo walipigwa butwaa baada ya kumwona mtoto huyo uwanjani amepita sehemu zote za ukaguzi ambazo abiria asiyekaguliwa nyaraka zake za kusafiria na mitambo maalum ya kuangalia vitu mbalimbali vikiwemo kemikali hatari, silaha na madawa ya kulevya hawezi kupita.
Kwa mujibu wa mama huyo, aliambiwa na maofisa wa uwanja huo kuwa sehemu hizo zote mtoto wake alipita bila kuonekana na kamera za uwanjani hapo wala kuacha kumbukumbu yoyote hali iliyozidi kuwaumiza vichwa maofisa wa uwanja huo.
Zefania alisema wakati maofisa hao wakitafakari hayo, ndipo msamaria mwema mmoja alijitokeza na kumchukua kwenda kumuhifadhi nyumbani kwake.Mtoto Happiness akiwa na mama yake mzazi, Sarah Zefania.

“Akiwa nyumbani kwa msamaria mwema huyo, nimeambiwa mwanangu alianza kumfanyia maajabu mbalimbali ikiwemo kuzungumza na wanyama na viumbe wengine wa ajabu au kutoka nje huku mlango umefungwa kwa ndani.
“Kuna muda alizungumza na viumbe wasioonekana ambapo aliwasiliana nao na kumletea vitu kadhaa alivyovitaka. Wakati mwingine alizungumza na wanyama wa mle ndani, kama kuku na paka ambao alikuwa akiwatuma kumfanyia yote aliyokuwa akiwaagiza.
“Hali hiyo ilimshtua yule msamaria mwema naye aliomba kupambazuke ili ampeleke mwanangu ustawi wa jamii. Yaani nahisi pengine angekuwa amemuokota sehemu bila kukabidhiwa mbele ya mashahidi pengine angemtupa usiku huohuo.
“Baada ya kushuhudia vituko hivyo, asubuhi iliyofuata alimkimbiza ustawi wa jamii ambako nako wameniambia alianza kuwafanyia vituko kama hivyo na kuwaambia kuwa angewatoroka muda wowote, kisha kuonekana akiparamia juu ya paa na kutaka kutoka.
“Yaani kwa muda mfupi waliokaa naye, maofisa wa ustawi wa jamii wanasema amewahenyesha vya kutosha ndipo walipofanya juhudi za kunitafuta na mimi nikaenda kumfuata,” alisema mama huyo muda mfupi baada ya kutua bandarini Dar.

Mtoto Happiness katika pozi.

Paparazi wetu alipomtaka mtoto huyo kuzungumza alikataa katakata na kujifanya bubu hali iliyomshangaza hata mama yake. “Nashangaa, sijui kwa nini hataki kuzungumza na wewe wakati ni mzungumzaji sana,” alisema mama Happiness.
Akizungumzia historia ya mtoto huyo, mama huyo alisema alimzalia Musoma, Mara na mwanaume mmoja aliyemtaja kwa jina la Juli ambaye walitengana na hawana mawasilino mazuri.
Mama huyo alisema alimpeleka mtoto wake shuleni lakini kila akifika harudi nyumbani na kutorokea anakokujua na kuonekana baada ya wiki mbili au tatu.
Kufuatia hali hiyo amewaomba wasamaria wema na viongozi wa dini kumwombea mtoto wake ili arudi katika hali ya kawaida kwani anajua kuna mkono wa mtu wa karibu uliyemharibu mtoto wake.