Monday, September 29, 2014

MH. LOWASA AMKARIBISHA MONDULI BALOZI WA JAPAN NCHINI TANZANIA



 
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimkaribisha wilayani Monduli Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaki Okada wakati alipowasili wilayani humo jana Jumapili Septemba 28,2014 kwa ajili ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na nchi hiyo.Balozi huyo aliahidi kusaidia vifaa vya kisasa katika hospitali mpya ya kisasa inayojengwa wilayani humo.
Meneja wa Hoteli ya Emanyata mjini Monduli,Bi. Neema (kushoto) akimkaribisha Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaki Okada hotelini hapo.Pembeni kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Monduli,Bw. Twalib Mbasha.
Balozi wa Japan nchini,Mh. Masaki Okada (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri 
ya Wilaya ya Monduli,Twalib Mbasha (kulia) na Meneja wa Hoteli ya Emanyata mjini Monduli,Bi. Neema alikofikia balozi huyo na ujumbe wake katika ziara yake ya siku mbili wilayani humo.

UVCCM WAMVAA JAJI WARIOBA

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umemtaka aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba, aingie mtaani kupambana akiwa na chama cha siasa badala ya kuendelea kutumia mwamvuli wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Tamko hilo lilitolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar, Shaka Hamdu Shaka  alipozungumza na mjini Dodoma nje ya viwanja vya Bunge mjini hapa .

Shaka alisema anachokifanya sasa Jaji Warioba ni kinyume cha taratibu ziliozompa dhamana awe Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambapo sasa ni dhahiri matamshi yake yanatoa tafsiri ya kutaka ushindani na vyombo vya dola.

“Nampa ushauri wa bure usio na gharama mzee Warioba, akubali kuanzisha chama cha siasa ifahamike ana mchuano na Dola ilio chini ya Rais Kikwete, asitangaze kuingia mitaani kwa kukitumia kivuli cha Tume ya Rais iliofika ukomo wake kisheria”alisema Shaka.

Shaka alisema kimsingi ifahamike kwamba Jaji Warioba mwaka 2005 alijibanza chini ya  kivuli cha Taasisi ya Mwalimu Nyerere na kutoa kauli hasi dhidi ya viongozi wa serikali.

Shaka alisema si lazima kwa Jaji Warioba kuendelea kubaki kuwa CCM na kwamba ana haki ya kikatiba na kidemokrasia kutoka ili akipinge vizuri chama hicho

MCHUNGAJI AMSUGUA MATITI MUUMINI WAKE WAPATE UWEZO WA KUZAA


Kila Siku zinavyoenda Vioja vinavyofanywa na Wachungaji wa Dini Vinaibuka , Baada ya hivi Karibuni mchungaji mmoja kuwalisha Nyasi Wafuasi wake Mwingine Ameibuka Nchini Kenya Akidai kuwaponya Wanawake ambao hawapati watoto Kwa Kuwasugua Matiti yao Huko Akiwaombea Katika ofisi yake....

MASHEIKH WAIKATAA RASIMU YA KATIBA!


SHURA ya Maimamu Tanzania imetangaza hatua za kuikwamisha Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, kwa kwenda kuwaeleza waumini wa dini ya Kiislamu kupiga kura ya hapana.
Hatua hiyo imekuja baada ya Rasimu ya Katiba inayopendekezwa iliyowasilishwa mwishoni mwa wiki na Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge, kuiweka kando Mahakama ya Kadhi.Jana mara baada ya kumalizika kikao cha maimamu wanchi nzima, Msemaji wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Rajabu Katimba, alisema hatua ya kupiga kura ya hapana ni moja ya azimio lililoafikiwa na kikao hicho.
“Msimamo wetu kwa asilimia 100 ni hapana, hatuungi mkono, tunalaani vikali jinsi mchakato huu wa Katiba ulivyovurundwa kwa sababu maoni ya Waislamu hayakuzingatiwa. 
“Leo (jana) tulikuwa na kikao kilichojumuisha maimamu wote kutoka Tanzania na msimamo wetu katika hilo ni hapana,” alisema Sheikh Katimba.
Mbali na msimamo huo, Sheikh Katimba alisema mkutano huo pia umejadili mambo mengine mazito ambayo yatawekwa wazi hivi karibuni.
Sheikh huyo alisema wiki hii watakutana na vyombo vya habari ili kutoa tamko lao rasmi kuhusu Rasimu ya Katiba inayopendekezwa. 
Juzi na jana kumekuwa na ujumbe mfupi wa maneno (sms) uliokuwa ukisambazwa ambao ulisomeka hivi; ‘Assalam Alaykum, ndugu Muislam baada ya kukataliwa Mahakama ya Kadhi katika mchakato wa Katiba Mpya, Umoja wa Maimamu Tanzania (SHURA) wanakutana ili kujadili msimamo wa Waislamu kuipigia kura ya Ndiyo au Hapana mapendekezo ya Katiba Mpya’.
Chanzo kutoka ndani ya kikao hicho ambacho hakikutaka kutajwa jina lake, kilieleza masuala mengine mbali na azimio hilo la kukwamisha rasimu hiyo ya Katiba inayopendekezwa.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, kila imamu katika mkutano huo amepewa jukumu la kwenda kuzungumza na waumini wa msikiti wake na kuwaeleza ukandamizaji wa Rasimu ya Katiba inayopendekezwa.
“Pamoja na hali hii, lakini kila mmoja wetu sasa tunakwenda kuwasha moto mikoani maana hili Bunge la Katiba limebeba ajenda zote zenye masilahi yao kisiasa kuliko hali halisi.
“Kwa hali hii kuanzia sasa unyonge umefika mwisho, maana kila mara Serikali imekuwa ikitumia ngao ya Watanzania wanyonge hasa Waislamu kupitisha mambo yao…. Kwa sasa kwa Katiba hii tutaikwamisha tu,” kilisema chanzo hicho.

FROLA MBASHA NA MUMEWE WAANDAA SAPRAIZI KWA MASHABIKI WAO


 
Wawili hawa waandaa tamasha la uzinduzi wa fanya njia Bwana na kupanda katika jukwaa moja.

KUNDI LA WAMAREKANI WAJA NCHINI KUTIZAMA FURSA ZA UWEKEZAJI


Baadhi ya Marais,Wenyeviti na Wakurugenzi wa Makampuni mbalimbali ya nchini Marekani waliokuja nchini kwa lengo la kutizama fursa za uwekezaji.

Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Washington DC,Suleiman Saleh (katikati) akibadilishana mawazo na mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya kufua Umeme ya TANASI ,William Crawford.Ziara hiyo inayo ratibiwa na Ubalozi wa Tanzania,Washington DC ni ya siku ambapo wageni hao wataembelea sehemu mbalimbali kujionea fursa za uwekezaji.
Afisa Ubalozi wa Tanzaini ,washington DC ,Suleiman Saleh akizungumza juu ya ujio wa wageni hao 11 kutoka Marekani ambao wako nchini kwa ajili ya kutizama fursa ya uwekezaji.Hii ni mara ya tatu sasa Viongozi wa Makampuni mbalimbali ya  Marekani wanafika nchini ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa Rais Kikwete kutekeleza Dipromasia ya Uchumi.
Rais wa Kampuni ya Ahmed's Moving Express,Inc  ,Ahmed Issa,ambaye pia ni Balozi wa heshima akizungumza na waandishi wa habari katika hotel ya Mount Meru, jijini Arusha kuhusu ujio wa Marais,Wenyeviti na Wakurugenzi wa makampuni mbalimbali ya Marekani walioko Tanzania .Issa tayari ambaye ni ziara yake ya tatu sasa kuja Tanzania tayari ameanza uwekezaji katika sekta ya Utalii ikiwemo kufungua ofisi ya Utalii Carfonia Marekani iliyozindiliwa hivi karibuni na Rais JAkaya Kikiwete.
Mtaalamu wa Ujenzi wa nyumba za makazi ,Nishati Erick Nyaren akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ujio wao Tanzania .Nyaren yuko nchini kuangalia fursa katika uwekezaji katika sekta ya Ujenzi. na Miundo mbinu.

Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya kufua Umeme ya TANASI William Crawford akiwa na mjukuu wake Colin Machamsoc akizungumza na wanahabari kuhusu ziara yao ya siku sita nchini Tanzania ikiwemo kutembelea vivutio vya utalii vya ,Manyara,Serengeti na Ngorongoro.Crowford yuko nchini kutizama fursa ya uwekezaji inayopatikana katika sekta ya Kilimo.
Mhandisi wa vifaa vya matibabu,Bob Reynolds akizungumza na waandishi wa habari namna anavyofikiria kuwekeza katika sekta ya Afya hasa kwa kutizama upatikanaji wa vifaa tiba kama X Ray,Ultrasound na CT Scan.
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya kufua Umeme ya TANASI William Crawford akiwa na mjukuu wake Colin Machamsoc wakiwa katika pozi la Picha katika hotel ya Mount Meru.
Marais,Wenyeviti na Wakurugenzi wa Makampuni mbalimbali ya Marekani wakiwa katika picha ya pamoja katika hotel ya Mount Meru jijini Arusha.

KIJANA ACHOMWA MOTO HADI KUFA KWA WIZI


MTU mmoja mwenye umri kati ya miaka 25 na 30 ambaye jina lake halifahamiki, ameuawa baada ya kushindwa kujieleza juu ya pikipiki ambayo yeye na mwenzake walikuwa wanajaribu kuiuza Chalinze.
Watu hao walifika Chalinze wakidai kutokea Gairo wakitaka kuuza pikipiki aina ya Toyo yenye namba za usajili T 336 BZC. 
Lakini walipobanwa kuhusu kadi ya pikipiki walibabaika na hivyo kuanza kupigwa ambapo mmoja alitoroka na huyo mwingine kuuawa kwa kuchomwa moto baada ya kipigo. 
Tukio hilo limethibitishwa na kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Athuman Mwambalaswa.
Kamanda huyo alisema kwamba tukio hilo lilitokea Septemba 25 mwaka huu, majira ya saa 1 asubuhi eneo la Pera Chalinze wilaya ya Bagamoyo.
 
Kamanda huyo aliwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na kuwataka kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria, ikiwa ni pamoja na polisi ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.

“MSHINDO NYUMA SASA BASI” SARAH NDOSI



 WADAU WAISUBIRI KWA HAMU CD YAKE INAYOTARAJIWA KUTOKA MWEZI DECEMBER MWAKA HUU
 
Wapenzi wa muziki wa nyimbo za kikristo haswa wale wapendao kusikiliza na kuangalia waimbaji wanaoimba live yaani uimbaji bila ya mshindo nyuma wikiendi hii walipata burudani ya kutosha kutoka kwa mwanadada Sarah Ndosi, aliyefanya live recording katika ukumbi wa kanisa la VCCT mbezi jijini Dar.

Sarah aliyeonekana kuwa ni mzoefu wa uimbaji huo alizikonga nyoyo za mashabiki wake waliofika kushuhudia tukio zima alipo imba nyimbo sita (6) mfurulizo na kuwafanya watu kusimama na kushangilia huku wengine wakishikwa na mshangao wa aina ya muziki ambao mwanadada huyo aliimba.

“Kiukweli dada huyu anastahili tuzo tena ya heshima maana nyimbo anazoimba si za hapa, anaimba nyimbo za mbele (akimaanisha nyimbo zenye hadhi ya kimataifa) na atasaidia nyimbo za kitanzania kujulikana mbele (akimaanisha nje ya tanzania)yaani wanamuziki wangekuwa  wanaimba viwango hivi wanamuziki wakibongo (wanamuziki wakitanzania) wangekuwa mbali sana” alisikika shuhuda aliyejitambulisha kwa jina la Prezzor Fredy Chavala, The king

Hata hivyo watu wengi walipigwa na mshangao pale ambapo mwanadada huyo aliiimba Accapela ya aina yake ambayo kwa hakika iliwafanya watu kuinua mikono yao kuonyesha kwamba wamemkubali na kufurahia burudani waliyokuwa wakiipata ukumbini hapo.
“Aisee Sarah anaimba, hata sikutegemea kama angeimba hivi, mi nilikuja kuhakikisha kama kilichosemwa kuwa ni live ni kweli na kama kweli itakuwaje kwani ni wachache sana wanaweza kufanya hivi na kwa ubora unaotakiwa lakini Sarah ameweza” alisema mama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la mama Junior

Mwanadada Sarah ambaye alionyesha kipaji chake kwa kuanza kuimba kwa kurudisha mikogo ya enzi zile za kuimba kwa kupiga mabiti akiwaongoza waimbaji waliokuwa wakimsaidia katika uitikiaji kilinakshi tamasha hilo.

 
Sanjali na hilo Sarah alitoa zawadi kwa wanafunzi walioibuka kidedea katika shindano la Student Talent Vestival lililoshirikisha wanafunzi wa shule za secondary za jijini Dar es salaam ambaposhule 15 zilishiriki katika mashindano hayo na  mwanadada Ester  alishinda kwa upande wa wadada na Samwel Wilfred mwanafunzi wa Tambaza alishinda kwa upande wa wanaume wakati kikundi kutoka Jangwani kilishinda katika mchuano wa makundi bora.
Mwanamuziki huyo alisema kuwa ameamua kufanya mashindano hayo ili kuibua vipaji vilivyojificha mashuleni na kupata waimbaji wapya ambao watakuja na radha mpya katika muziki wa Injili ili kuleta changamoto katika tasnia ya muziki wa injili.

“watoto hawa wapo vizuri sana yaani wanajua kuimba kiukweli, wakipata waalimu wazuri wakuwaongoza katika uimbaji wao wanaweza wakaondoa majina ya baadhi wa waimbaji ambao tayari wanafahamika” alisema Sarah
 
Hata hivyo Sarah amesema kuwa mashindano hayo ya kutafuta vipaji mashuleni ni endelevu ambapo amesema kuwa yatakuwa yakifanyika kila mwaka ikiwa mwaka huundio ilikuwa mwanzo wake. Pia amewataka wanafunzi mashuleni kuweka juhudi katika masoyo yao ili kutowakatisha tama waalimu na wazazi katika kuwasapoti katika vipaji vyao. Hakuacha kuwasihi wazazi na waalimu kuwapa nguvu watoto ikiwa wanavipaji kwani hata yeye uimbaji wake aliuanzia akiwa shuleni na ndio imemfanya akafika hapo alipo katika uimbaji.

Sarah Ndosi amesema CD zake zitakuwa tayari sokoni ifikapo mwezi December mwisoni , hivyo amewaomba watu wote kumuunga mkono katika kazi yake hiyo ambapo amesema CD hizo zitauzwa kwa  Tsh 10000 kila moja.