Saturday, October 18, 2014

KADI YA RAIS OBAMA YAKATALIWA


BO II
Rais wa Marekani Barack Obama amejikuta katika wakati mgumu baada ya kadi yake ya muamana (credit card) kukataliwa katika mojawapo ya migahawa iliyopo jijini New York.Obama amekiri kukutana na mkasa huo alipokuwa akizunguma na waandishi wa habari baada ya kusaini agizo la rais litakalotumika kama sheria ya matumizi ya kadi za muamana ambayo itasaidia katika kuzuia wizi wa kadi hizo ambao umekithiri nchini humo.

Akizungumzia mkasa wa kukataliwa kadi yake, Obama amesema alifika katika mgahawa mmoja na baada ya kuhudumiwa vitafunwa, mara baada ya kadi kuingizwa katika mashine iligoma kufanya muamana, ndipo alipohisi kuwa kuna namna kadi hizo ‘zinachakachuliwa’, hivyo akalazimika kutumia kadi ya mkewe Michelle Obama kufanya muamana huo.
Tatizo la wizi wa kadi za muamana limeathiri watu takribani milioni 100 kwa mwaka jana, ambapo kusainiwa kwa agizo hilo la rais wa Marekani kutasaidia katika kuhakikisha usalama wa huduma za muamana na pia kuanzishwa kwa huduma ya dharura mtandaoni itakayowahudumia watumiaji waliopoteza kadi zao.
Marekani ni moja ya nchi zinazotoa huduma za kadi ya muamana ambapo mtumiaji wa huduma hiyo anakuwa na uwezo wa kupata huduma za malipo ya baada kwa manunuzi ya bidhaa na huduma mbali mbali.

SMBA AISHIYE NA BINADAMU BILA KUMDHURU


Kipande cha filamu ya Roar kikimuonyesha Tippi Hedren mama wa, Melanie Griffith's akicheza na simba anayeitwa Neil.
Melanie Griffith's akiwa amelala na Simba huyo kitandani mwake.
Melanie Griffith's akicheza na Simba.
Simba anayejulikana kwa jina la Neil akiwa amelala ndani ya nyumba.
Simba akiwa ameshika mguu wa Melanie Griffith's wakicheza nyumbani kwao Los Angeles, Marekani.
Tippi Hedren akipozi na Simba huyo.

Akiwa na miaka 14 mtoto aliyetambulika kama Melanie Griffth raia wa Los Angeles, Marekani aliweza kuishi na simba.
Akizungumza na gazeti la LIFE, mama wa Melanie, Tippi Hedren alieleza kuwa ilikuwa mwaka 1971 kipindi hicho Melanie alikuwa na miaka 14 ambapo walikuwa wakiishi kama familia na simba.
Simba huyo aliyekuwa amefundishwa kuishi na binadamu chini ya mtaalam wa wanyama, Ron Oxley, alikuwa na uwezo wa kula mlo mmoja kwa siku ambapo alikuwa akila nyama kilo 13.
 “Nilikuwa napenda kwa jinsi Neil alivyokuwa akiishi na mwanangu, alikuwa akilala naye katika kitanda kimoja.”

“Siku moja niliingia katika chumba cha mwanangu na kumkuta Neil akiwa amelala na mwanangu huku mikono yake ikiwa kwenye mdomo wa Neil, sikuogopa kwani amefundishwa jinsi ya kujiheshimu, hutakiwi kumshika eneo la puani mwake ama kumshtua ghafla kwa mikono katika uso wake,” alisema mama yake Melanie, Tippi.

Tayari kuna filamu imeshatengenezwa itakayojulikana kama Roar ambapo ndani yake kuna Neil pamoja na Melanie. Itatoka hivi karibuni.
Neil kwa sasa ana miaka 84 na amesharudishwa katika mbuga za kuhifadhia wanyama lijulikanalo kama Shambala lililopo California, Marekani na wanamchukulia kama mnyama wa kufugwa.

HATIMAYE LADY JAYDEE AVUNJA MKATABA NA GARDNER!


HABARI mpya kutoka kwa mastaa wanaodaiwa kuvunjika kwa ndoa yao, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ na Gardner G. Habash ‘Kaptaini’, inasemekana wamevunja mkataba wa kuendesha Mgahawa wa Nyumbani Lounge uliopo Ada Estate, Kinondoni jijini Dar. 
Mbongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’. Kwa mujibu wa mtoa habari wetu, wawili hao walidaiwa kufikia uamuzi wa kuvunja mkataba baada ya kuona ndoa yao inasuasua kutokana na migogoro.“Lady Jaydee au Jide alipoona mambo yanakwenda ndivyosivyo alimshauri Gardner wavunje
mkataba wa Nyumbani Lounge ili kila mmoja awe na businesses (biashara) zake. “Walimfuata mmiliki wa jengo, wakamwambia kwamba wanavunja, akawakubalia,” kilinyetisha chanzo makini. Chanzo hicho kilizidi kwenda mbali zaidi na kudai kuwa mgahawa huo kwa sasa unamilikiwa na mzungu. 
‘Lady Jaydee’ na Gardner G. Habash ‘Kaptaini’ wakati wakiwa pamoja. “Mgahawa kwa sasa unamilikiwa na Mzungu mmoja ambaye amenunua baadhi ya vitendea kazi walivyokuwa wakivitumia na Jaydee amekuwa akimsaidia mzungu huyo baadhi ya mambo kwa kuwa ni mgeni Bongo ila sasa Nyumbani Lounge itafunguliwa kwa jina jipya la M.O.G na Jaydee atafanya shoo ya ufunguzi kama msanii tu,” kilisema chanzo hicho. 
Baada ya kushibishwa maelezo hayo, mwanahabari wetu alimtafuta Jide bila mafanikio lakini Gardner alipopatikana, alijibu kwa kifupi.
“Siwezi kuzungumza chochote katika suala hilo.”
Jide na Gardner wanadaiwa kutengana na kila mmoja akiishi kivyake lakini wenyewe wamekuwa wakikanusha.
 

WAZUNGU WAKUTWA WAMEKUFA CHUMBANI JIJINI DAR.


Moja kati ya majeneza yaliyohifadhiwa miili ya marehemu yakitolewa ndani ya chumba hicho.Chanzo cha kuaminika kimeeleza kuwa wawili hao ambao walikuwa wakifanya kazi katika baa iitwayo Mashua iliyo ndani ya Slipway, huku mwanamke, aliyetajwa kwa jina la Hotsan, akiwa ndiye Meneja, walikutwa chumbani kwao wakiwa wamefariki baada ya kutoonekana kazini tokea Jumanne, siku ambayo Watanzania walikuwa wakikumbuka miaka 15 baada ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. 
WAZUNGU wawili ambao ni mume na mke wanaodaiwa kuwa ni raia wa Afrika Kusini, wamekutwa wamekufa chumbani kwao katika nyumba waliyokuwa wakiishi maeneo ya Slipway, Masaki jijini Dar es Salaam Jumatano hii.
Inadaiwa kuwa baada ya kutotokea kazini katika muda wa kawaida, wafanyakazi wenzao walijaribu kupiga simu zao za mikononi, lakini zote zilikuwa zikiita pasipo kupokelewa karibu mchana kutwa na hivyo kuwapa maswali mengi yasiyo na majibu. 
Siku iliyofuata, inadaiwa kuwa wafanyakazi wenzao walipojaribu tena kupiga namba hizo, simu zote mbili hazikupatikana
Jeneza lingine likitolewa ndani ya chumba hicho. Awali, walihisi huenda wenzao wameamua kuacha kazi baada ya kupata sehemu nyingine, lakini baadaye wakafikia uamuzi wa kuwafuatilia nyumbani kwao ili kujua kilichotokea. 
Walipofika, walikuta milango ikiwa imefungwa kwa ndani, kitu kilichowafanya waamini kuwa walikuwa ndani. Kwa kushirikiana na majirani, wafanyakazi hao waliamua kuvunja mlango wa chumba wanacholala wanandoa hao na kuwakuta wakiwa kitandani wamelala, kila mmoja akiwa amegeukia upande wake. 
Baada ya kuona tukio hilo la kushtusha, waliamua kuwaita Polisi ambao walipofika na kuiona miili hiyo, waliamua kuwaita wenzao wa kitengo maalum cha uchunguzi (Crime Investigation) ambao baada ya kufika, waliwataka raia na majirani waliokusanyika hapo kukaa mbali ili kuwapisha kufanya uchunguzi. 
Kamanda Suleiman Kova. Askari hao walikaa na miili ya marehemu kwa zaidi ya saa tatu wakiwafanyia uchunguzi na baada ya kukamilika kwa zoezi hili, miili hiyo ilichukuliwa kupelekwa hospitalini Muhimbili. 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja marehemu kuwa ni Roxxana Hilari na Hainess Hilton William na kwamba uchunguzi zaidi juu ya kilichowaua unaendelea.

NDEGE AGEUKA KUWA MWANADAMU

Kitendo hicho kiliwaacha wananchi vinywa wazi wasijue la kufanya huku wakibaki kupiga picha kwa kutumia simu zao za mikononi.Mapema wiki hii katika kijiji cha Oshindi nchini Nigeria wananchi walishuhudia sinema ya bure ambapo kamera zao zilikuwa macho yao na simu zao pale ndege aliyekuwa anapaa angani ghafla alianguka chini baada ya kudandia nyaya za umeme na kugeuka mwanamke.
Mwanamke huyo alionekana kuchubuka na kuwa na vidonda katika mwili wake hali iliyo kuwa inahuzunisha huku akiwa haongei (bubu).
Wananchi hao walimuuliza maswali mengi wakitaka kujua imekuaje hadi akageuka binadamu wakati yeye alikuwa ndege anapaa juu.
Mama huyo aliwajibu kuwa alikuwa anaenda kumtazama binti yake aliyekuwa amejifungua muda mchache.
Habari zinasema kuwa mwanamke huyo alikuwa mchawi na binti yake alikuwa anafanya sala wakati yule mama alikuwa anapaa. Inaelezwa kuwa wakati sala inaendelea ndipo mwanamama huyo aliyekuwa amejibadilisha na kuwa ndege akageuka binadamu.
Taarifa zinaarifu kuwa binti yake alikuwa kila akijifungua mtoto anafariki papo hapo.