Friday, November 21, 2014

WABUNGE WARUKA UKUTA KUINGIA BUNGENI...



Ukweli ni kwamba kuna story ambayo unaweza ukasimuliwa na rafiki yako ama mtu yoyote halafu ukaona kama ni uzushi na hakuna ukweli wowote.
Pata picha pale ambapo Spika wa Bunge pamoja na Wabunge wanafungiwa geti la kuingia ndani ya Ukumbi Bunge …
Nakupa story kutoka Nigeria, Spika wa Bunge la Nchi hiyo Aminu Tambuwal amelazimika kuingia ndani ya Bunge kupitia mlango mdogo wa dharura baada ya Polisi kufunga milango ya Bunge hilo kwa sababu za kiusalama.
Spika huyo alijitambulisha kwa Maafisa Usalama hao ili wamruhusu aingie lakini hakuna aliyeonekana kujali ombi lake wala kumjibu, japo baadaye walimruhusu aingie kupitia mlango mdogo wa dharura huku wabunge wengine wakizuiwa kuingia kitendo kilichowafanya waamue maamuzi magumu ya kuingia ndani ya Bunge kwa kuruka ukuta.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nigeria, Suleiman Abba amesema walilazimika kuzuia mtu yeyote kuingia ndani ya jengo hilo na kuweka ulinzi wa hali ya juu baada ya kupata taarifa kwamba kuna majambazi walipanga kuvamia Bunge hilo.Polisi waliwashambulia kwa gesi ya machozi Wabunge waliokaidi amri ya kutokuingia Bungeni, Wabunge wawili walipoteza fahamu katika vurugu hizo

KUNA BIASHARA YA WASANII WA KIKE WA MUVI INAENDELEA


Jokate Mwegelo akipozi.
 Stori:  Waandishi Wetu
Imefichuka! Kwa muda mrefu kumekuwa na taarifa za chini kwa chini kwamba baadhi ya mastaa wa kike Bongo, hasa wale wa filamu ‘Bongo Movies’ huuzwa kwa wanaume, mara nyingine kwa kujua au kutojua lakini wenyewe wamekuwa wakikanusha hivyo kutoa ‘kibarua’ kwa Ijumaa kuingia mzigoni kisha kumuibua mmoja wa wahusika (kuwadi) anayerahisisha biashara hiyo haramu ya ngono.

Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kwamba, kuwadi huyo huwa anajua dau la kila staa hivyo anapopata mwanaume hasa mapedeshee, wafanyabiashara na baadhi ya vigogo serikalini, huwaunganisha kwa kutoa namna ya mawasiliano au kuwaunganisha moja kwa moja.

Uchunguzi huo ulibaini uwepo wa madai mazito kwamba wapo baadhi ya mastaa wa kike wa Bongo Movies ambao hugombewa na makuwadi kwa sababu wana soko kubwa.
“Jaribu kufikiri msanii haonekani location (eneo la kuigizia sinema) wala sinema aliyocheza haijulikani lakini muda mwingi utamuona anatanua kwenye viwanja vya starehe, lazima ujiongeze kwamba kipato kinatoka wapi?
 
Staa wa filamu Bongo Aunt Lulu.
“Mimi nakwambia hii Bongo Movies imebaki jina tu, sioni mwanga mbeleni kwa sababu hawa mabinti hawapo serious zaidi ya kutafutiwa wanaume,” kilidai chanzo chetu ambacho ni mfuatiliaji wa karibu wa kazi za sanaa Bongo.

Madai mazito yaliendelea kushushwa kwamba wapo wanunuaji ambao huhonga magari (bila kadi) ambapo baadaye hukamatwa kimafia na kurejeshwa kwa mhongaji.
Ikazidi kufahamika kwamba, mastaa wenye sifa ya kuhongwa magari ni wale wenye majina makubwa.
Staa wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper Massawe.

Ilisemekana kwamba wapo mastaa wanaotajiwa dau kubwa kuanzia Sh. milioni tano na kuendelea na wapo wa chini ya hapo hadi buku hamsini (50,000).
Mpaka sasa kuna mastaa wanaowindwa na makuwadi kwa kuwa wana soko na bei zao kwenye mabano ni pamoja na Elizabeth Michael ‘Lulu’ (Mil. 5), Jokate Mwegelo (Mil. 5), Wema Isaac Sepetu (Mil. 5), Kajala Masanja (Mil. 5) na Jacqueline Wolper Massawe (Mil. 5).
 
Staa wa filamu Bongo, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’.
Wengine ni Baby Joseph Madaha (Mil. 5), Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ (Mil. 3), Aunty Ezekiel (Mil. 3), Jennifer Mwaipaja ‘Shumileta’ (Mil. 2) Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’ (Mil. 1), Lulu Mathias ‘Anti Lulu’ (Mil. 1), Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ (Mi. 1) na wengine kibao ambapo kwa sasa upepo umegeukia kwa wale wanaochipukia.
 
Katika kusaka ukweli juu ya skendo hiyo, jina la mmoja wa makuwadi hao ambaye ni mwigizaji wa kike Bongo, Lungi Maulanga (pichani) ilitajwa.
Staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Mbali na Lungi pia alitajwa mwigizaji mmoja wa kiume wa Bongo Movies na jamaa mwingine ambaye huwa ni mdandiaji wa ishu za mastaa (majina tunayo, tutayataja tukijiridhisha kisheria).

Baada ya kutajiwa jina la Lungi, gazeti hili lilimsaka mwigizaji huyo anayedaiwa kuwauza baadhi ya mastaa hao kwa wanaume ambapo alibanwa vilivyo hadi akaanika siri nzito nyuma ya biashara hiyo kubwa isiyo na kodi.
 
Staa wa filamu Bongo, Wema Sepetu.
Mbali na kukiri kuwakuwadia mastaa hao kipindi cha nyuma kabla ya kuacha, Lungi alifunguka kwamba amekuwa akisumbuliwa na wanaume wakware wakitaka awaunganishe na mastaa ambao alidai alishafanya nao kazi hiyo muda mrefu.
MSIKIE LUNGI Ijumaa: Habari yako Lungi... Lungi: Nzuri, mmekuja kufuata nini hapa (nyumbani kwake Kinondoni, Dar)? Ijumaa: Mbona unajihami? Tumekuja kukusomea mashitaka yako! Lungi: Mashitaka gani? Siku hizi nimetulia, sijichanganyi kama zamani, kulikoni tena? Ijumaa: Hapa kuna madai mazito...
 
Staa wa filamu Bongo, Vai wa Ukweli.
Lungi: Hebu semeni kilichowaleta, kwanza siku hizi sipendi kukutana na waandishi wa habari! Ijumaa: Kuna za chinichini kwamba wewe ndiye unayewauza mastaa wa Bongo na ndiyo biashara inayokuweka mjini kwa kuwa hata location huonekani. Je, ni kweli?
Lungi: (kwa hasira) yaani mimi niwekwe mjini na mastaa? Kwani hamjui anayeniweka mjini? Au mnataka niwafukuze na panga?Ijumaa: Kwa nini unakuwa mkali Lungi? Unachotakiwa kufanya ni kutoa majibu kwa sababu kuna shosti’ako ametutajia staa uliyemuuza juzi tu!
Staa wa filamu Bongo, Aunty Ezekiel akipozi.
Lungi: (bila kujua anarekodiwa) juzi! Sikieni, nawaheshimu sana, mimi nilikuwa nikifanya biashara hiyo siku nyingi na niliacha kwa sababu hao mastaa hawana maana, wakishapata wanajisikia na kusahau walipotoka.
“Huyo aliyewaambia ana ushahidi gani kama juzi nimeshamuuza staa? Ijumaa: Oke, tuache hilo! Unakumbuka dau kubwa ulilowahi kupewa wakati unawakuwadia? Lungi: (kwa mara ya kwanza anatabasamu) nilishawahi kupata hadi Sh. milioni tatu na kima cha chini laki tano, lakini jamani mbona ni siku nyingi?
 
Staa wa filamu Bongo, Lungi Maulanga.
“Kwanza mimi sitaki hizo habari kabisa. Nimechoka kusumbuliwa na wanaume kwa ishu hizo.”Ijumaa: Hilo dau kubwa ulilipata kwa mwanaume wa Dar, mikoani au nje ya nchi?Lungi: Watu wa mikoani ndiyo wanakata mkwanja mkubwa, hapa Dar longolongo tu. Hiyo Sh. milioni tatu niliipata kwa jamaa mmoja wa Arusha.

KIJANA SANDE MREMI AFARIKI DUNIA,NDEGE ZILIGOMA KUMSAFIRISHA

Sande Jacob Mremi amefariki Siku chache baada ya kukosa usafiri wa ndege ambapo alitakiwa kwenda nje ya nchi kupata matibabu.Kituo cha ITV kiliripoti kuhusu habari za kijana huyo kuumwa na kutokana na kusumbuliwa tatizo la uzito mkubwa nakushindwa kupata Ndege ya kumsafirisha kwenda kwenye matibabu India kijana huyo amefariki Dunia.Ndugu wa kijana huyo walilalamika kutoridhishwa na baadhi ya Mashirika ya Ndege kwa kushindwa kuwasaidia kumsafirisha ndugu yao.Katika mahojiano na ITV mama wa mtu huyo amesema; “..yaani kwa kweli mashirika ya Ndege hayakuweza kutufanyia haki kwa kweli, wametunyanyasa kwa sababu tulipokuwa tunapeleka maombi tunataka kumsafirisha mtoto wetu ilikuwa wao watusaidie na kutupa maelekezo tunatakiwa tufanye nini na nini, lakini baada ya kuona tunakosa msaada ndio tukaamua kuja ITV ili watusaidie, kwa hiyo yeye mwenyewe akaanza kupata presha kwa sababu presha alikuwa hana mpaka anapanga kusafiri alikuwa hana presha nilimpima vipimo vyote alikuwa hana tatizo lolote…”

Dada wa marehemu amesema; “..Ethiopia walitusaidia kwa kweli mpaka hatua ya mwisho na Jumapili kama Mungu angemuweka hai Ethiopia wangemsafirisha, na mashirika ya Ndege mengine yalitakiwa yatuelekeze hivi, lakini sasa kutokana na ile hali mara leo kapelekwa kesho anarudishwa mdogo wangu kesho kutwa kapelekwa amerudishwa mdogo wangu, msongo wa mawazo umemkaa rohoni anashindwa kuongea maskini ya Mungu, mawazo paka yamemfanya mdogo wangu alikuwa hana presha paka presha imekuja paka mdogo wangu anafariki.
sds
Baba wa Sande amesema; “…wakatumia sheria ya pili ya kunihusisha mimi wakaniambia bwana kumbe mtu huyu ni mkubwa sana tunatakiwa tuvunje viti tumbebe, nikawauliza nikulipeni bei gani? wakaniambia tulipe dola elfu saba mia tano na thelathini na nne, na mara ya kwanza tulilipa dola elfu sita miambili ishirini…”
Bado haijafahamika kama Shirika hilo la ndege litarudisha hela ambayo ililipwa na watu hao kwa ajili ya kumsafirisha ndugu yao.

WABUNGE WACHARUKA KASHFA AKAUNTI YA TEGETA-ESCROW

Hawa ndio wabunge waliofunguka wakitaka sakata hilo lijadiliwe bungeni
Naibu spika wa bunge Job Dungai, yeye ndiye kashikilia rungu, Ripoti " ijadiliwe au la"
Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za serikali, (PAC), Zitto Kabwe. Taarifa ya CAG kuhusu akaunti nya Tegeta Escrow, iko mikononi mwake
Mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu, (CHADEMA),akizunghumza bungeni mjini Dodoma jana, wakati lile sakata la IPTL, linalogubigwa na akauti iliyojichukulia umaarufu TEGETA ESCROW, lilipoibuka bungen i wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa waziri mkuu. Wabunge wanataka "ngoma" ijadiliwe bungeni, licha ya kashfa hiyo kuwa tayari mahakama kuu ya Tanzania
Mbunge wa Kigoma Kusini, (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, huyu ndiye aliyeibua kashfa ya akaunti ya Tegeta-Escrow
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mbunge wa Urambo, (CCM), Samwel Sitta
Mbunge wa Iringa mjini, (CHADEMA), Mchungaji Peter Msigwa
Mbunge wa kuteuliwa na Rais, ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-M,ageuzi, James Mbatia
Mbunge kijana, Esther Bulaya, (CCM)
Mbunge wa Longido,(CCM), Lekule Laizer,
Mbunge wa Kasulu mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali, ndiye aliyemchokoza Waziri mkuu kuhusu ripoti hiyo kujadiliwa bungeni
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, "Punguzeni jazba", akiwasihi wabunge kuwa serikali iko makini na inasubiri kwa hamu taarifa hiyo ili kila mtu hata yeye akibainika abebe msalaba wake, lakini akatahadharisha kuhusu umuhimu wa kuheshimu mihimili ya dola ikiwemo mahakama
Mbunge wa Kahama (CCM), James Lembeli

LORI LALIPUKA ENEO LA MIKUMI MKOANI MOROGORO


 Tumepokea picha ya tukio la ajali ya Lori lililokuwa limebeba mapipa ya lami ambalo limeshika moto mapema leo asubuhi maeneo ya Mikumi, Morogoro.chanzo cha mlipuko huo bado hakijafahamika mpaka sasa na bado hatujapata taarifa kama kuna aliepoteza maisha au kupatwa kwa majeruhi.Chini ni ujumbe kutoka kwa mdau wetu  alietuletea taswira hizi kuhusiana na hali ya barabara hiyo.
''Kama una safari ya kwenda Iringa-Mbeya au kama unapokwenda utapita mikumi basi sitisha safari kwani njia inefungwa tangu saa mbili asubuhi. Kuna lory linawaka moto mpaka sasa. Lilikuwa limebeba lami so lami bado inawaka na inesambaa sehemu kubwa''
Baadhi ya watu wakishudia tukio hilo la ajali.