Saturday, November 1, 2014

ASKARI POLISI WA KIKE MWANZA AMKATA VIDOLE VINNE MFANYAKAZI WAKE KWA PANGA

JESHI la Polisi mkoani Mwanza linamshikilia askari wake WP Fatuma wa Kituo cha Polisi Igogo wilayani Nyamagana kwa kosa la kumjeruhi mtumishi wake wa ndani kwa mkumkata vidole vyake vinne vya mkono wa kulia kwa panga, akimtuhumu kumwibia Deki ya Video nyumbani kwake. 
Tukio hilo la kujeruhiwa kijana Steven Magessa (18), lilitokea Oktoba 20 mwaka huu katika kijiji cha Magange Mugumu wilayani Serengeti mkoani Mara nyumbani kwao kijana huyo aliyekuwa amekimbilia huko baada ya kudaiwa kumwibia mwajili wake nyumbani eneo la Igogo.
AKIONYESHA NAMNA ALIVYOJERUHIWA NA MAMA HUYO
Akizungumza na waandishi wa habari kijana huyo alieleza kuwa kufanya kazi kwa askari huyo kulikuja mara baada ya askari huyo kumfuata kijijini na kumuomba ridhaa ya wazazi wa kijana huyo kuambatana naye jijini Mwanza ili kumsaidia kazi za nyumbani ambapo walikubaliana malipo ya kiasi cha Sh 50,000/= kila mwezi jambo ambalo askari huyo alilikiuka na kushindwa kulitekeleza kwa muda wa miezi sita bila kumlipa mshahara.
“Nilipoona hajanilipa mshahara wangu kwa muda wa miezi sita huku kila ni kimwambia ananijia juu na kunitukana matusi basi nilimuomba ruhusa ya kwenda kijijini Oktoba 15 mwaka huu kumuona mama yangu mzazi aliyekuwa anaumwa ili kupata nafasi ya kurudi nyumbani” alisema.
Steven alieleza kuwa wakati akiwa kijijini askari huyo (Mwajili wake) alikuwa akimpigia simu kumtaka arudi Mwanza kuendelea na kazi na kudai kuwa atamlipa malimbikizo ya mshahara wake kiasi cha Sh 300,000/= zilizokuwa kama deni, Steven alikubali ombi hilo kwa kuomba atumiwe nauli na pesa kidogo ya kumwachia mama yake, jambo ambalo askari huyo alikaa kimya bila majibu.
“Siku ya Oktoba 20 mwaka huu majira ya saa 4:00 asubuhi alifika kijijini akiwa na askari watatu kwenye gari la Polisi (Difenda) wa Kituo cha Mugumu na kudai kuwa nipo chini ya ulinzi kisha kunifunga pingu, akidai kuwa nilimwibia Deki ya Video na kutoroka nyumbani kwake, walinipandisha kwenye Difenda kunipeleka kituoni “ alisema.
Kijana huyo alieleza kuwa baada ya kufikishwa kituoni Mugumu askari huyo na wenzake walianza kumuhoji huku wakimpa maneno ya vitisho, kijana huyo alipokataa kuwa hakuiba wala kutoroka, Sajenti Fatuma aliamuru kijana huyo kuvulishwa shati alilovaa na kisha akafungwa usoni na kuombwa anyooshe mkono mezani ili apewe 'Sapraizi'.
"Sekunde chache nilihisi kitu kikali kimenipitia kwenye vidole vyangu vinne vya mkono wa kulia na kufuatiwa na maumivu makali, niliusogeza mkono wangu mdomoni kuupoza kwa kuupuliza ndipo nilipo gundua kuwa nimekatwa kabisa vidole vyangu vinne vya mkono wangu wa kulia ikibakia dole gumba tu" kijana Steven alisimulia kwa uchungu.
“Niliangua kilio kutokana na maumizu na sijui vidole vyangu hadi sasa sijui vikowapi, askari wenzake baada ya kuona nimetokwa na damu nyingi walimshauri anipeleke hospitali ya Wilaya ya Mugumu ili nipatiwe matibabu kabla ya kuondoka kuja Mwanza,”alisisitiza.
Steven alisema baada ya kupatiwa matibabu, tulienda kupanda basi ili kuja Mwanza kwa madai kuwa amenifungulia kesi ya wizi wa Deki ya Video na tuliopfika alinipeleka kituo cha Polisi Kati Nyamagana na kuniweka Mahabusu akinituhumu wizi, lakini nilipochukuliwa maelezo nilikana tuhuma za wizi na kueleza ukweli wangu ili kupata msaada.
Huku taarifa zingine kutoka ndani ya jeshi zilizopatikana zilidai kuwa askari huyo alikusudia kufanya ukatili huo kutokana na udanganyifu ambao alifanya kwa uongozi wake akiomba kupatiwa silaha (SMG) kwa ajili ya kuitumia kwenye kazi za nje lakini lengo ikiwa ni kwenda na silaha hiyo kwa ajili ya kumkamata na kumtishia kijana huyo, jambo ambalo uongozi ulimgomea.
JESHI LA POLISI LINASEMAJE
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC), Valentino Mlowola, jana ofisini kwake amethibitisha kuwepo kwa taarifa za tukio hilo na kueleza kuwa tayari Jeshi hilo limechukuwa hatua madhubuti hatua ya awali ikiwa ni kumshikilia askari huyo kwa kufanya ukatili huo kwa kuvunja sheria na kujichukulia sheria mkononi kumjeruhi kijana huyo.
Mlowola alisema pamoja na kijana huyo awali kufunguliwa jarada la kutuhumiwa kufanya kosa la wizi (Jinai) na kudaiwa kutorokea kijijini kwao, bado askari huyo alitakiwa kufuata mfumo wa kiutawala na kisheria uliopo kushughulikia suala hilo badala ya kuamua kujichukulia maamuzi ya kumwadhibu mtuhumiwa kabla ya uthibitisho wa mashitaka yaliyokuwa yamefungulia.
“Nilipopokea taarifa hizi kwa mashangao na masikitiko makubwa na zimenisitua sana, si kitendo cha kiungwana hata kidogo kwa mtu ambaye anatakiwa kufuata taratibu za mfumo wa utawala na sheria katika utekelezaji wa kushughulikia kero na matatizo ya jamii, alitakiwa kutumia busara kwani tayari aliishamfungulia jarada la kumtuhumu kumwibia ikizingatiwa naye ni mzazi wa watoto watano ni lazima anaujua uchungu,”alisema. 
Kamanda Mlowola alieleza kufatia ukatili huo kufanywa na askari wake ameunda timu ya kikosi cha askari kwenda hadi kijijini Magange wilayani Serengeti mkoani Mara ili kufanya uchunguzi wa tukio hili ikiwa ni pamoja na kufanya mahojiano na familia, wananchi wa kijiji hicho kisha Hospitali ya Wilaya ya Serengeti alipopatiwa matibabu ya awali.
HIVI NDIVYO VIDOLE VILIVYOKATWA NA MAMA HUYO.
“Ili tupate ukweli wa jambo hili tumeunda timu hiyo, kwani kijana Steven tumemhoji ametueleza jinsi askari Fatuma alichomfanyia na kudai hakumwibia, lakini askri wetu pia amehojiwa awali amedai hakufanya kitendo hicho bali wananchi ndo walimfanyia ukatili huo hivyo ni mkanganyiko lakini ukweli utapatikana tu japo kuwa tukio hili halikufanyika Mwanza”alisisitiza.
Mlowola alisema kwamba tayari tunamshikiria askari huyu na kumfungulia jarada la uchunguzi kwa taratibu za kijeshi na ikibainika kutenda kosa hilo tutumfukuza kazi na kumfikisha katika vyombo vya sheria ili kuchukuliwa hatua zaidi kulingana na kosa alilofanya, lakini pia kijana Steven naye anashikiriwa kwa tuhuma alizonazo za wizi kufatia jarada lililopo.
“Hatuwezi kuendelea kucheka na kufumbia macho kitendo hiki ni jambo ambalo linamgusa kila mtu hata mimi ni mzazi ukiachana na utumishi wangu wa umma, ntahakikisha jambo hili nalishughulikia kwa umakini na kutoa taarifa kwa umma ili pia kueleza wananchi kuwa tukio hili limefanywa na mtumishi kama mtu si Taasisi ya Jeshi la Polisi na ahidi kutenda haki kwenye hili,”alisisitiza. 
Wito wangu kwa wananchi ni kuacha kujichukulia sheria mkononi na kuwaadhibu watuhumiwa mbalimbali kabla ya kuthibitika kwa makosa na tuhuma hizo, lakini wazingatie kufuata taratibu za kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria ili kushughulikia matatizo yao nawaomba waendelee kutoa ushirikiana na kufuata mfumo uliopo badala ya kujichukulia sheria mkononi.

ACHOMWA KISU BAADA YA KUFUMANIWA NA MKE WA MWALIMU

Mume wa mtu, Raphael Bernard (33) aliyechomana visu na mwalimu baada ya fumanizi.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, msala huo ulijiri juzikati nyumbani kwa ticha huyo, Kichangani ambapo mwalimu huyo alidaiwa kufumwa na mume wa mtu, Raphael Bernard (33) ambaye ni dereva wa bodaboda. 
KATIKA hali ya kutisha, fumanizi lililoambatana na bonge moja la mtiti linadaiwa kujiri nyumbani kwa mwalimu ‘ticha’ wa Shule ya Msingi ya Mafisa ‘A’, iliyopo Manispaa ya Morogoro mjini hapa aliyefahamika kwa jina la Rosemary Mkoba kisha watu wakachomana visu. 
Habari zilidai kwamba mwenye mume amekuwa akimfuatilia mumewe kwa muda mrefu, akagundua huwa anakwenda kujichimbia kwa ticha huyo huku akiacha familia ikilala njaa.
Ilisemekana kuwa, siku ya tukio, mwenye mume, akiwa na ‘jeshi’ lake, alimfuatilia mumewe hadi akamuona akiingia nyumbani kwa hawara wake huyo. 
Ikazidi kudaiwa kwamba baada ya kuhakikisha jamaa amelala kwa ticha huyo, mwanamke huyo na ‘skwadi’ yake waliondoka, asubuhi iliyofuata mishale ya saa 1:04 wakatia timu na kulianzisha timbwili huku mke huyo akidaiwa kumtishia ticha kuwa akipata ujauzito atazaa kwa mdomo.
Bw. Raphael Bernard akiuguza majeraha hospitalini. Habari zinadai kuwa, baada ya mke huyo na timu yake kuondoka, ticha huyo alimuwakia Raphael kwamba kumbe ana mke, kwa nini hakuwahi kumwambia? Ugomvi mwingine ukazuka hapo. 
MASHUHUDA SASA
Nao mashuhuda ambao ni majirani wa mwalimu huyo, Juma Hamis na Joyce Joseph, walipozungumza na paparazi wetu walisema siku hiyo walisikia vurugu kutoka ndani kwa mwalimu ambapo walikwenda kushuhudia.
Walisema walimkuta mwanaume huyo akipigana na ticha ambaye alikuwa akiendelea kulalamika kufichwa suala la mwanaume wake kuwa na mke. 
WACHOMANA VISU
“Unaambiwa mzozo huo ulipamba moto, maana yule mke aliyeondoka alidai amemfumania mumewe, mwalimu naye akadai alikuwa hajui.
“Katika purukushani hiyo huku wakipigana wao kwa wao ndipo wakachomana visu. Yaani mwanaume alijeruhiwa vibaya mno.
Mwalimu ‘ticha’ wa Shule ya Msingi ya Mafisa ‘A’ aliyechomana visu na Bw.Raphael Bernard. “Mwanaume alichomwa kisu utumbo ukatoka nje na kama siyo polisi kufika na kukimbizwa hospitalini, sasa hivi tungekuwa tunaimba ‘Parapanda Italia….Parapanda…’ kwani hali ilikuwa mbaya sana,” alisema Joyce kwa masikitiko. 
HOSPITALINI
Baada ya kuzungumza na majirani na mashuhuda wa tukio hilo, mwanahabari wetu alitia gia kwenye pikipiki yake aina ya ‘boksa’ hadi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.
Mwandishi wetu alizungumza na Kaimu Mganga Mfawidhi, Dk. Francis Semwene ambaye alikiri kuwapokea majeruhi hao.
“Mwanaume alikuwa amepasuka tumboni hivyo tunaendelea kumpa matibabu, yupo wodi namba moja na mwanamke ambaye naye amechomwa visu sehemu mbalimbali za mwili wake, naye tunaendelea kumpatia matibabu,” alisema Dk. Semwene. 
HUYU HAPA MWANAUME
Akizungumza na mwanahabari wetu kwa tabu huku polisi wakiwa wamempiga pingu kitandani, Raphael alisimulia kwa maumivu makali:
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Leonard Paul. “Mke wangu ni Veronica lbrahim ambaye tumeishi kwa miaka 6 na kujaliwa kupata mtoto mmoja.
“Mwezi wa tano mwaka huu, tuligombana, niliondoka nyumbani, kwa heshima ya mtoto wangu, sikuchukua kitu chochote zaidi ya nguo.
“Mwezi huohuo nilifanikiwa kuingia kwenye uhusiano na Mwalimu Rosemary ambapo baada ya penzi kukolea aliniambia nihamie kwake ili tulifaidi penzi letu tamu yaani mahaba motomoto na niliishi pale miezi mitano.” 
FUMANIZI?
Alipotakiwa kuelezea chanzo cha tukio la fumanizi, jamaa alifunguka: “Hamna. Ticha aliniamsha asubuhi akaniambia nimsaidie kufanya usafi na kumuogesha mwanaye. 
MADAWA YA KIENYEJI
“Nilipomaliza kumuogesha nilitaka kutandika kitanda, nilipoinua godoro niliona madawa ya kienyeji.
“Nilipomuuliza mwenzangu akawa mkali kama pilipili ndipo ugomvi mkubwa ukaanzia hapo.
“Baada ya mzozo mkali, ndugu zake walinivamia, akiwemo shemeji yangu wa kiume, namfahamu kwa jina la baba Dickson. 
MAUMIVU
“Wakati najitetea, nilishika kisu ambapo katika hekaheka ya kunyang’anyana na Rosemary kilinichoma mimi na yeye.” 
TICHA ARUHUSIWA
Mwandishi wetu alifika wodi namba tatu aliyolazwa ticha huyo na kuelezwa kuwa aliruhusiwa baada ya kupata nafuu ya majeraha mengi ya visu aliyoyapata sehemu mbalimbali za mwili wake hasa kichwani.
Baada ya kumkosa ticha huyo wodini, gazeti hili lilimfuata nyumbani kwake, alipobanwa alisema:
”Tukio hili limetokana na ushirikina wa mke wa zamani, alinitishia kuwa nikishika mimba nitajifungulia mdomoni akiapa kunifanyia kitu mbaya.
“Yaani hata sijui nini kimetokea, Raphael, mume wangu kipenzi amenichoma kisu na yeye kujichoma tumboni.” 
KAMANDA WA POLISI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Leonard Paul alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.
“Tukio hilo liliripotiwa Oktoba 27, mwaka huu, ambapo Raphael alikwenda kwa mpenzi wake, Rosemary ambako kulitokea ugomvi, wakaumizana kisa wivu wa kimapenzi, hivyo tunamshikilia mwanaume huyo huku uchunguzi ukiendelea,” alisema Kamanda Paul.

DENI LA PESA LAASABABISHA MAREHEMU KUGOMBEWA MAHALI PA KUZIKWA


Mtoto mwingine wa marehemu, Hassan Hatibu, akizungumza jambo na mtandao huu.

Ndugu na jamaa wakiwa katika mzozo huo. 
 
KIJANA mmoja aliyefahamika kwa jina la Mohamed Said ameingia katika mzozo mkali na ndugu zake wa upande wa mama yake kwa kugombea maiti ya mama yake mzazi.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, mzozo huo umeibuka baada ya kijana huyo kuwagomea ndugu zake kuuzika mwili wa marehemu mkoani Iringa mpaka hapo watakapomlipa shilingi laki tatu kama gharama za matibabu ya marehemu.

ASKOFU GEOR DAVIE AVUNJA NDOA YA SEKRETARI WAKE


Askofu Mkuu wa Huduma na Ngurumo ya Upako, George David ‘Geor Davie’.
Askofu Mkuu wa Huduma na Ngurumo ya Upako, George David ‘Geor Davie’ yenye makao makuu yake jijini Arusha ndiye aliyetajwa na mahakama hiyo kuwa ni chanzo cha kuvunjika kwa ndoa hiyo ya Pamella ambaye alikuwa ni sekretari wa kiongozi huyo wa dini baada ya ujumbe mfupi wa maneno (SMS) ukionesha mapenzi kunaswa kwenye simu ya mwanamke huyo ukitokea kwa Geor Davie.
KIMENUKA! Ndoa iliyodumu kwa miaka 15 kati ya Wiston Lotta (52) na Pamella Geofrey (40) imevunjwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kufuatia ushahidi mzito uliotolewa mahakamani hapo kumridhisha Hakimu Hawa Mghuruta.
Askofu Geor Davie akiwa na wasaidizi wake. Ushahidi uliotolewa na mwanaume ulidai kuwa mgogoro wa ndoa yake ulitokana na mkewe kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Askofu Geor Davie. 
Akisoma hukumu ya kesi hiyo Namba 01 ya mwaka 2012, Hakimu Mghuruta alisema kabla ya hukumu, mahakama ilizingatia ushahidi wa mashahidi watano wa upande wa mlalamikaji.Mke wa mtu Pamella Geofrey (katikati) anayedaiwa kutoka kimapenzi na boss wake, Askofu George David ‘Geor Davie’. 
Alimtaja mtoto wa kwanza wa wanandoa hao, Sifael Wiston (15) kwamba naye aliieleza mahakama hiyo namna mama yake alivyokuwa akizini nje ya ndoa kwa kukutana na Geor Davie ndani ya gari lake lenye rangi ya silva wakati wa usiku baba yake akiwa safarini. 
Mtoto huyo alianika kwamba, walikuwa wakipelekewa juisi na bajia ndani ya gari hilo lenye pazia kisha wao kufunga vioo kwa muda mrefu huku likionekana kutikisika, ushahidi ambao uliwashangaza waumini wa kanisa la askofu huyo.
Askofu George David ‘Geor Davie’ akitoa huduma ya maombezi kwa waumini. Wiston ambaye alikuwa msaidizi wa Geor Davie, alifungua kesi ya kudai talaka kwa Pamella ili kufikia ukomo wa shauri hilo ambalo lilianza kusikilizwa na Baraza la Usuluhishi wa Ndoa mwaka 2007 lakini ilishindikana kwa vile mkewe alipeleka sababu za uongo kuwa alikuwa akinyanyaswa hivyo kuikimbia nyumba. 
Hakimu Mghuruta ameamuru mali zote yakiwemo magari matatu, nyumba iliyopo Sakina na vitu vingine zibaki chini ya mlalamikaji lakini Pamella anaruhusiwa kwenda kuwasalimia watoto wake. Hata hivyo, mahakama ilimtaka Pamella kutowarubuni watoto hao kiasi cha kuathiri masomo yao

VICTOR MBAGGA MWANAMUZIKI WA INJILI ALIYEPANIA KUWAKOMBOA VIJANA WA TANZANIA .



Ni kijana mwenye makao yake mwanga mkoani kirimanjaro na alianza huduma ya uimbaji mwaka 2002 huku akiwa na nia ya kukiokoa kizazi cha vijana wasiojiweza.
Brother Victor Bagga kama anavyojulikana ameamua kujitolea kufanya kazi ya kumtangaza Kristo kwa watu ili kuwaweka huru waliofungwa kama lisemavyo neon la Mungu.
“ Nina mzigo mkubwa sana  moyoni mwangu wa kutaka wasiojiweza wajue kuwa wanatumaini kwa Yesu na si kwa mwanadamu, wapo vijana wengi sana wanamaisha yakusikitisha kisa hawajui yakuwa Kristo Yesu ndio tumaini kuu 
Kujitambua kwa kijana ni kitu muhimu sana lakini vijana wengi wameshindwa kujitambua kwa kuwa wanaishi nje ya mpango wa Mungu. " Ukishajua umezaliwa ili ufanye nini huwezi kuhangaika sana na dunia ila shetani hataki vijana wajitambue matokeo yake  amewatwisha mizigo mikubwa na ndio wanaoongoza kwa kilio cha maisha magumu." alisema Brother Victor


Pia alisema huwa anatumia kipaji chake cha uimbaji kuwatia moyo watoto watogo na walemavu kwani ni makundi ambayo yamesahaulika sana katika jamii yetu. "ukweli ni kwamba ukifanikiwa kuyafanya makundi haya yakatambua vipaji vyao mapema na wakavitumia kwa usahihi hawatahangaika kutafuta kazi za kuwainua kiuchumi, kwani kipaji cha mtu na elimu ndio njia pekee ya kumuondolea mtu umaskini kuliko kusubiri ajira kutoka kwa mtu mwingine kitu ambaho ni kilio kikubwa kwa vijana.


 



 

Hata hivyo anafurahia kuwa chini ya uangalizi wa kanisa la Mount Zion church kwa mchungajji H. Kimario ambaye amekuwa msaada mkubwa sana kwake katika huduma zake ili kuweza kutimiza maono yake ambayo ni kuwa mwimbaji wa kimataifa na kuweza kusaidia vijana wenye kupoteza mwelekeo wa ndoto zao haswa katika uimbaji na watoto walemavu.
 

 Brother Victor amesema katika huduma yake zipo changamoto ambazo akifanikiwa kuzitatua ataweza kuwahudumia vijana wengi ili nao waweze kuwasaidia wenzao


"Natamani sana huduma hii iwe ya kimataifa na itawezekana ikiwa nitaungwa mkono na watu wote kwani hatuwezi kuuondoa umaskini kwa makundi haya kwakuwa ni watu wasio na kitu na hata maandiko yanasema "asio na kitu hatapewa kitu na hata aliye na kidogo hicho nacho hunyang'anywa hupewa aliyenacho" hivyo nilazima tuwasaidie watu hawa kujua vipaji vyao pia ili viwasaidie wawe na kitu ili wapewe kitu" alisema Victor

Hivyo anaomba kuungwa mkono na watu wote katika kufanikisha maono yake na changamato hizo ni pamoja na vifaa vya Muziki, pesa pamoja na mahali pa kuwatunzia vijana hao kwani wengi hawapo mahali pamoja.

Victor Mbagga kijana mwenye asili ya Tanga ana albam mbili mpaka sasa na  anatarajia kuzizindua zote kwa mpigo mwezi ujao na anatamani sana kama atapata nafasi ya kufanya kazi pamoja na Christina Shusho, John Lisu pamoja na Upendo Kirahilo kwani ndio miongoni mwa waimbaji ambao wamekuwa kivutio sana kwake na kusaidia kukuza kipaji chake cha uimbaji. "ipo siku nitawashirikisha waimbaji hawa katika nyimbo zangu nasubiri kibali toka kwa Mungu tuu" alisema

Yupo tayari kwa mialiko popote duniani ili kuzidi kumtangaza Kristo Yesu. Mpigie +255766480206