Tuesday, August 5, 2014

ADAM MALIMA ATOA CHANGAMOTO KWA WANASAYANSI NA SERIKALI WAKATI WA UZINDUZI WA RIPOTI YA ISAAA


Tanzania imezindua ripoti ya ISAAA ya mwaka 2013 inayoonyesha matumizi ya mazao yaliyozalishwa kwa kutumia biateknolojia duniani. Uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa tume ya sayansi na teknolojia (COSTECH) jijini Dar-es salaam, ulihudhuliwa na wanasayansi, waandishi wa habari, wakuu wa asasi mbali mbali za kilimo na naibu waziri wa fedha Bwana Adam Malima ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika usinduzi huo.

Naibu waziri wa fedha Adam Malima (katikati) akikata utepe kuzindua ripoti ya ISAAA ya mwaka 2013


Naibu waziri Adam Malima ambaye ndiye malezi wa jukwaa la bioteknolojia kwa maendeleo ya likimo OFAB Tanzania aliwataka wanasayansi kushirikiana kwa karibu na waandishi wa habari ili kufikisha matokeo ya tafiti zao kwa jamii wanayoitumikia. “Bila sayansi na teknolojia katika kilimo tutabakia kuvuna mazao machache katika eneo kubwa kitu ambacho ni tofauti na wenzetu, kinachotakiwa ni lazima mkulima aelezwe jinsi sayansi na teknolojia inavyofanya kazi na hii ninyi wanasayansi hamuwezi ila waandishi wa habari.”

Pia aliitaka serikali na tume ya taifa ya sayansi na teknolojia kuwajali wanasayansi waliopo nchini kama ambavyo wanajaliwa sana nje ya nchi kutokana na ubora wa kazi zao kitu ambacho ni tofauti hapa nchini. Hata hivyo naibu waziri huyo katika hotuba yake alisema kuna ongezeko kubwa la watu kuliko eneo la kilimo tulilo nalo, hivyo matumizi ya bioteknolojia katika kilimo ni lazima yatumike ili kwenda sambamba na ongezeko la watu pamoja na malengo ya milenia.

Pia alisema kukataza bioteknolojia ni kumnyima fursa ya maendeleo na kuendelea kumkandamiza mkulima ambaye maisha yake hutegamea kilimo na hutumia nguvu nyingi kulima lakini mavuno ni madogo. Aliendelea kwa kuwataka wanasayansi wote nchini tafiti zao zisiishie maofisini mwao kwni wanayo kazi kubwa katika jamii ya Tanzania, wajibu wao kwa watanzania ni kuhakikisha wanapata matokeo ya tafiti zao kwa wakati, kwani hakuna maendeleo bila ya utafiti kufanyika. “Najua ya kuwa wanasayansi wengi si waongeaji, lakini waandishi wa habari wapo kwa ajili yenu, tunataka wananchi wajue matokeo ya tafiti zenu haraka iwezekanavyo hasa zinazohusu kilimo ili tuweze kutoka tulipo” alisema.

Sanjali na hayo aliwasihi waandishi wa habari kutoa elimu itakayo msaidia mkulima kuelewa ukweli na umuhimu wa teknolojia katika kilimo. “Waandishi nyie ndio mnasikika sana na kuaminiwa sana na jamii chochote mtakachokiongea mnaaminika, na ndio maana watu wengi wanawatumia nyie kwenye mambo yao hivyo basi hata katika hili pigeni kelele ili wananchi wabadirike na kufuata kanuni za kilimo bora kwa ukombozi wa mkulima.”

Shirika la Kimataifa la Huduma za Kilimo cha Kibayoteki (ISAAA) hutoa ripoti kila mwaka kuonyesha hali ya biashara ya mazao ya bayotekinolojia duniani.

Ripoti ya Mwaka 2013, ambayo tayari imezinduliwa rasmi katika nchi kadhaa Ulimwenguni inaonyesha ongezeko la wakulima wadogo wanalima mazao ya kibayoteknolojia, mapato na mafanikio kiuchumi, uhifadhi wa mazingira na mchango wa kijamii hasa kuokoa maisha ya wakulima. Ripoti hiyo inaonyesha kuwa karibu asilimia mia (100%) ya wakulima waliojaribu kulima mazao ya kibioteknolojia wanaendelea kulima mazao hayo mwaka hadi mwaka, na karibu asilimia 90 ya wakulima waliolima mazao hayo ni wakulima wadogowadogo. Matokeo hayo yanaonyesha ukuwaji wa ufahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya kilimo.

Hata hivyo ripoti hiyo inaonyesha ukuwaji mkubwa wa uchumi kwa nchi zinazolima mazao hayo ikiwa ni nchi 27 zililima mazao hayo mwaka 2013 na kwa afrika, Afrika ya kusini imeongoza kwa kilimo hicho na nimiongoni mwa nchi 5 zinazoongoza duniani katika nchi zinazoendelea. Pia ripoti hiyo inaonyesha kuna ongezo kubwa la hekta za pamba aina ya BT cotton nchini Burkina faso na Sudani.

Mbali na hayo ripoti hiyo inaonyesha kuwa kuna majaribio ya mashambani ya pamba, mahindi na ndizi katika nchi zingine saba ambazo ni Kenya, Uganda, Cameroon, Malawi, Misri, Ghana na Nigeria wakati mradi wa mahindi yanayovumilia ukame wa WEMA unatarajiwa kukamillika kwaka 2017. Kilimo cha kibioteknolojia kimeonekana kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo duniani kwakuwa kilimo hicho kinalimwa katika eneo dogo mazao mengi hivyo kupunguza uharibifu wa mazingira wa kukata misitu kwa ajiri ya kutafuta maeneo ya kulima. Matumizi madogo ya dawa mashambani au kutotumia kabisa dawa kitu ambacho pia husaidia utunzaji wa mazingira, kumpunguzia mkulima bajeti ya matumizi katika kilimo na kulinda viumbe hai vingine ambavyo vingeathiriwa na matumizi ya madawa hizo.

Ripoti hiyo ambayo imetolewa kwa lugha ya kiingeleza imeweka bayana maendeleo ya Afrika katika matumizi ya bioteknolojia na Afrika mashariki imeonekana kuwa katika hatua nzuri za kimaendeleo ya teknolojia hiyo ambapo Uganda na Kenya zipo katika majaribio ya shambani katika mazao ya mihogo, mahindi na ndizi na Tanzania ipo katika hatua za uchunguzi wa maabara.


Japo kuwa kumekuwa na upinzani wa matumizi ya teknolojia hiyo hapa nchini kitu ambacho kimekuwa kikiwarudisha nyuma wakulima katika kuikubali, lakini uthibitisho wa kisayansi uliotolewa na wanasayansi wenyewe pamoja na mashirika makubwa duniani kama vile CODEX Alimentarius, European Food Safety Authority (ESFA) pamoja na shirika la afya duniani (WHO) yanaonyesha kuwa tangu teknolojia hii ianze kutumika hakuna ripoti yoyote iliyotolewa kuwa teknolojia hii inamadhara kwa binadamu, wanyama wala mazingira

Hivyo basi ripoti hii iwe chachu ya maendeleo kwa wakulima Tanzania, ipo fursa iwapo kuna nia. Uwezekano wa mkulima kuwa na maendeleo makubwa ipo kama kanuni za kilimo bora zitafuatwa.

Uzinduzi wa ripoti ya ISAAA haujafanyika Tanzania pekee pia ulifanyika Afrika ya kusini, Kenya, Burkina faso, uganda ikiwa hapa Tanzania uzinduzi huo uliandaliawa na tume ya sayansi na teknolojia Tanzania (COSTECH), ISAAA kushirikiana na OFAB Tanzania,

TAHA YATOA ELIMU KWA WAKULIMA WA MBOGAMBOGA KWENYE MAONYESHO YA NANENANE MKOANI MBEYA

Wananchi waa jijini Mbeya na mikoa ya jirani wamepata bahati ya kupata elimu ya bure ya kilimo cha mbogamboga, matunda na viungo kutoka kwa asasi isiyo ya kiserikali ya wakulima,wafanyabiashara na watoa huduma ya mazao ya horticulture tanzania (TAHA)
Elimu hiyo inayotolewa katika banda na vitalu vya maonyesho vilivyopo katika uwanja wa maonyesho wa nanenane wa John Mwakangale jijini Mbeya. Elimu iliyoambatana na  elimu lishe nia ikiwa kuwaelimisha wananchi umuhimu wa mbogamboga na matunda katika lishe na kujipatia kipato kwa kulima mbogamboga na matunda

Wakulima waliotembelea banda hilo wamenufaika na elimu hiyo inayotolewa na maafisa wa ufundi wa kilimo kutoka TAHA kwa ushirikiano na wale wa Barton Tanzania ambao kwa pamoja wapo katika viwanja hivyo ili kuhakikisha jamii ya wakulima wa mboga kutoka ukanda wa Nyanda za Juu Kusini wanapata elimu ya msingi bora ya uzalishaji wa mboga wenye tija. 


"Tumetembelewa na wakulima wasiopungua 500 na bado tunauhakika kuwa watakuja wengi kadiri siku zinavyokwenda kwani hawa waliotutembelea wamefurahia sama mafunzo haya hivyo natumaini watakwenda kupashana habari huko waendako kwani wote waliofika hapa wamefurahia elimu hii" alisema Afisa mawasiliano wa TAHA Likiti Thomas
Aliongeza kuwa wakulima wengi waliotembelea banda hilo wametaka sana  kujifunza mbinu na misingi ya awali ya uzalishaji wa mazao ya horticulture, hiyo ni ishara njema kwani inaonesha ni kiasi gani wananchi  wanatafuta mbinu fasaha inayoweza kuwakwamua kutoka katika uzalishaji wa mboga wa kawaida mpaka uzalishaji wa tija unaozingatia viwango vya kitaifa na kimataifa ili kujipatia manufaa zaidi ya hayo wayapatayo sasa kwani wengi wamegundua kuwa ipo fursa ya kujikwamua kimaishakwa kutumia kilimo
Mkuu wa mkoa wa Iringa  Mh. Dr. Christine Ishengoma akionyeshwa zao la nyanya katika moja ya vitalu vya TAHA


Nae mtaalamu wa kilimo Bwana Ringo amesema elimu itolewayo ni pamoja na matumizi ya mbegu bora (hybrid) pamoja na teknolojia za kisasa kwa ajili ya uzalishaji bora wa mazao. "katika maonyesho ya mwaka huu tupo kivitendo zaidi kwani mkulima anapata mafunzo kwa kusikiliza na kuona pia kwa kujenga imazi zaidi na kumpa mkulima hamasa ya kwenda kuyafanyia kazi mafunzo yetu"
 Vitalu vilivyotumiwa kwa ajili ya mafunzo kwa wakulima wa mbogamboga jijini Mbeya

 Mwananchi akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa TAHA
 Teknolojia ya umwagiliaji kwa mfumo wa kilimo cha matone (drip irrigation)ambao pia unaonesha utengenezaji bora wa matuta, nafasi na usafi ambayo huendana na mfumo wa kisayansi na teknolojia



kama ilivyo kauli mbiu ya TAHA ambayo ni "maono ya baadae ndiyo msingi na rasilimali zetu kuhakikisha ufanisi na mafanikio" ambapo nia ni kutaka mkulima kutumia rasilimali alizo nazo kujipatia kipato ikiwa ni pamoja na ardhi kwa ajili ya kilimo kwa kulima mazao tofauti tofauti kwa kutumia shamba moja

WAWILI WAFA MAJI WAKATI WA UBATIZO


Walikuwa wakibatizwa na mchungaji Nehemia Upendo wa kanisa la POOL of SILOAM jijini Mwanza katika ziwa la victoria ambapo maswahibu haya ya watu wawili kufariki baada ya kusombwa na wimbi lililokuja ghafla na kushindwa kujiokoa

Huu utaratibu wakubatiza ziwani bila kujali hali ya hewa usifumbiwe macho. kwani ilipaswa wao kufuata maelekezo kutoka kwenye mamlaka ya hali ya hewa kama nia ilikuwa kufanya ubatizo ndani ya ziwa hilo. sheria ni lazima ichukue mkondo wake kutokana na uzembe huu

Wakati watu wanabatizwa wakapigwa na wimbi.
Watu wawili wameripotiwa kufa.HIVYO watu musifanye mambo kwa mazoea wakati mwingine shetani nae hujichukulia umaarufu kwenye matukuo kama haya

DAWA YA UKIMWI MBIONI KUPATIKANA


KUMBE inawezekana! Wanasayansi wapatao 30 duniani waliokuna vichwa kutafuta dawa ya kutibu gonjwa hatari la Ukimwi wamesema hatua waliyofikia ni kujipongeza kwa asilimia mia moja.
Wataalam hao walikutana nchini Marekani hivi karibuni na kusema utafiti wao umeweza kutengeneza vidonge vya kudhibiti kasi ya ugonjwa huo kwenye mwili wa mwanadamu.

Wakiwa chini ya Chama cha Kimataifa cha Ukimwi na Jamii (International Aids Society au IAS), wamesema wanaamini miaka kadhaa mbele kutoka 2014 tiba ya uhakika itapatikana.
Mkurugenzi Mtendaji wa IAS, Dk. Bertrand Audoin alisema mafanikio yaliyopatikana kwa sasa ni dawa za kudhibiti virusi vya ugonjwa huo kuushambulia mwili wa binadamu hata kama virusi vitaendelea kuwepo mwilini.

Alisema kwa sasa wanatafiti namna ya kapata dawa itakayoweza kuangamiza kabisa virusi kwenye mwili wa binadamu.Kwa mujibu wa taarifa, dawa zaidi ya nane za chanjo ya ugonjwa huo zipo kwenye majaribio lakini wanasayansi hao hawajasema lini watazianika.

Mojawapo ya dawa iliyopo kwenye majaribio ni ya Niaid ya nchini humo ambayo ilifanikiwa kutambua chembechembe zinazoweza kidhibiti virusi vya ugonjwa huo hatari kwa zaidi ya asilimia 90.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na wataalam hao, kukutana kwao kwenye Jiji la Boston, Marekani ilikuwa ni kwa ajili ya kutoa tamko kwa jamii duniani kuhusu mafanikio waliyofikia.

Dk. Audoin amesema mkakati wao wa kwanza ulikuwa kuhakikisha dawa ya Ukimwi inapatikana katika kipindi cha mwaka 2010/2014 ambapo kweli matumaini yapo.Virusi vya Ukimwi viligunduliwa kwa mara ya kwanza kwenye maabara mwaka 1980 na kuua mamilioni ya watu kutokana na kutokuwa na tiba wala chanjo ya uhakika.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Uwazi lilipiga hodi Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kutaka kusikia wanasemaje kuhusu mafanikio ya chanjo na tiba ya Ukimwi yaliyoanza kupatikana lakini hakupatikana msemaji.

MCHUNGAJI GWAJIMA ANUNUA KELKOPTA KWA AJILI YA KUHUBILI IJILI


Habari ambazo zimethibitishwa na facebook page ya kanisa la Ufufuo na Uzima zinasema kuwa Helkopta hiyo imewasili nchini tayari na sasa inafanyiwa assembling kwaajili ya kuanza kuruka jumatatu hii. Tukio ambalo limelifanya kanisa hilo kuandaa ibada maalumu ya kumshukuru Mungu kwa kupokea helcopta hiyo itakayotumika kusambaza injili Tanzania.

http://api.ning.com/files/8QOPGYNO0th3hDpF3ZzAN6rfTh*W*jBrdgEoTYC0my1gOuhr1-Lx1*zIWR9nYs5jhHgYVwky3pRkLrtzGyAhnPH1bJZRRjQP/3.JPG Helcopta hiyo aina ya R44 ni mali ya kanisa la Glory of Christ T Church ambalo liko chini ya mch. Gwajima. Akiongea Jumapili iliyopita kanisani kwake Kawe Mch. Gwajima alisema huku akimsimamisha Mjapani mmoja ambaye kwa mujibu wa Mch huyo ndiye aliyefanikisha ununuzi wa helkopta hiyo ya kwanza nchini kutumika katika kusambaza injili.

http://api.ning.com/files/8QOPGYNO0tiUr8eYWK9Fm933U6QmLMwodxNtvp9FP-NNCrld48tPWB*ms1P3N2nchFGBo4UdflCTj82xU7Vzl3WYuKdJT0KI/8.JPG Aidha, Mchungaji Gwajima alitumia muda huo kutoa Ufafanuzi juu ya kuwepo kwa taarifa za yeye kushirikiana na Nabii maarufu GeorDavie kuzindua helcopta hiyo alisema, "Nabii GeorDavie amepanga kukodi helcopta aina sawa na yetu (R44) na atatua nayo kwenye kanisa lake (ambalo pia lipo maeneo ya Tanganyika Packers) akitokea Arusha. lakini mjue wote kuwa helkopta hiyo si ambayo kanisa la Ufufuo na Uzima imeinunua bali imekodiwa seacliff na wala hatujaandaa mkutano wa pamoja na Nabii huyo" mwisho wa kunukuu.

Hii inakuwa Helkopta ya kwanza kutumika kuhubiri injili ikiwa ni mali ya kanisa. Ibada ya shukrani kanisani Ufufuo na Uzima ilihudhuriwa na waimbaji kama Munishi akiwa na  Malebo (ameokoka), Rose Muhando, Bony mwaitege, John Lisu, Upendo Nkone, Flora Mbasha, Christina Shusho na wengine wengi..

na hivi ndivyo ilivyokuwa katika picha

 





http://api.ning.com/files/8QOPGYNO0thVD5Z2ZXMhFUd2-tjN-msoo1bW0pt2yGE-kYmD*13httGa-v9*TAdF5wFjat1sfQFqNhD24QHx6nPxPebcvnTw/5.JPGhttp://api.ning.com/files/8QOPGYNO0thAIrHwtmiffKtvs56VYEH*5kchDhsDlQI3EeohoBmpIY7JdeRz-wJSqdCOe8QSTnTN-jRcb2EGyPPkDYUYRqvt/6.JPG

MJUMBE WA UKAWA AWASALITI WENZIE KWA KWENDA BUNGENI DODOMA


Dodoma. Wakati wajumbe wa Bunge la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiendelea na msimamo wa kususia vikao vinavyotarajiwa kuanza leo mjini Dodoma, mmoja wa wajumbe wake jana aliripoti bungeni na kujiandikisha.

Mjumbe huyo, Clara Mwatuka ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), alionekana katika Viwanja vya Bunge saa 6:30 mchana akiwa ameongozana na wabunge kadhaa wa CCM wakiwamo Livingstone Lusinde (Mtera) na Jerome Bwanausi (Lulindi)


 CUF ni moja ya vyama vinavyounda Ukawa, pamoja na Chadema na NCCR Mageuzi na tayari viongozi wakuu wa vyama hivyo, Profesa Ibrahim Lipumba, Freeman Mbowe na James Mbatia wametangaza kwamba wajumbe wote wanaotokana na umoja wao hawatashiriki vikao vya Bunge hilo.

Mwatuka baada ya kujaza fomu maalumu za kujiandikisha, alielekea lango la Magharibi na kuingia kwenye gari la Bwanausi.

Awali, alipoulizwa kwenye Viwanja vya Bunge kuhusu kuwapo kwake Dodoma, alikataa kuzungumza lakini alikiri kujiandikisha bungeni

WATU HAWA SARE WANAZITOA WAPI?



 Askari feki wa Usalama Barabarani ambae Jina lake halikufahamika haraka akiwa chini ya Ulinzi mkali wa Askari Polisi (hayupo pichani) mara baada ya kukamatwa kwa kujifanya ni askari wa usalama barabarani huku akifahamu kuwa ni kosa kisheria. Inasemekana Mtuhumiwa aliwahi kuwa askari wa Usalama barabarani ambapo kituo chake cha Kazi kilikuwa Mkoa wa Pwani na ni mmoja kati ya askari waliofukuzwa kazi kwa kuenda kinyume na taratibu na sheria za Jeshi la Polisi Tanzania
 Askari Polisi ambae jina lake halikufahamika mara moja (Mwenye sweta) akimkamata kwa makini mtuhumiwa aliyejifanya askari wa usalama barabarani leo katika eneo la Chamazi Jijini Dar Es Salaam
Askari feki akishangaa na kuduwaa mara baada ya jeshi la Polisi Kumtia nguvuni leo Katika Eneo la Chamazi Jijini Dar Es Salaam Mapema leo.Picha Kwa Hisani ya Mdau.

MLEMAVU ATUMIA MGUU WAKE WA BANDIA KUHIFADHIA MADAWA YA KULEVYA


Kamishna Suleiman Kova akionesha namna mguu huo wa mtu mwenye ulemavu unavyotumika kutunzia dawa za kulevya.

KIJANA mmoja ambaye ni mlemavu wa mguu, Said Tindwa (36), mkazi wa Vijibweni Kigamboni jijini Dar, anashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kutumia mguu wake wa bandia kwa ajili ya kutunzia na kuuza dawa za kulevya.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum, Suleiman Kova alisema mlemavu huyo alitiwa nguvuni Agosti 1 mwaka huu kufuatia mtego uliowekwa na jeshi hilo. 
Alisema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa akitumia mbinu ya kuziuza dawa hizo kwa kuzificha kwenye mguu wake wa bandia. 
Aidha Kova alisema kuwa dawa alizokuwa akiziuza mlemavu huyo ni zile za viwandani kama vile cocaine, heroin na wakati mwingine bangi. 
“Katika mtego maalum uliowekwa na askari wa upelelezi ndipo mlemavu huyo alikamatwa akiuza dawa hizo kwa wateja wake baada ya kuzitoa alikozificha ambapo ni ndani ya mguu huo wa bandia” alisema Kova.