Sunday, August 10, 2014

HADITHI YA KUNUSURIKA NA KIFO KWA DK SLAA NA MNYIKA


Madiwani walioasi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamerejea na kudai walirubuniwa na makada watano wa CCM kuhama kwenye chama hicho ili wawatumie kuwaua, Dk. Willbrod Slaa na John Mnyika.


Madiwani hao ni Sebastian Mzuka wa kata ya Ngokolo na Zacharia Martin wa kata ya Masekelo wote kutoka Shinganya mjini ambao wamewataja makada hao kuwa ni Naibu wa Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Wengine ni Naibu waziri wa Nishati na Madini, Steven Masele ambaye pia ni Mbunge wa Shinyanga mjini, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NEC, chama tawala, Nape Nnauye, na Habibu Mchange (aliyefukuzwa Chadema).

Wakizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam katika ofisi za chama hicho, madiwani hao walisema kuwa, mauaji hayo yalipangwa kutekelezwa kwa kiasi cha Sh. milioni 180.

Diwani Mzuka alisema wamefika kwenye ofisi hizo ili kueleza kinachoendelea kudhoofisha chama na kuomba toba baada ya kuhama.

Alisema mara baada ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kuvuliwa madaraka Chadema, Mchange alipewa kazi (dili) na CCM kutafuta viongozi na madiwani wa Chadema lengo likiwa ni kukidhoofisha.

Alisema Mchange aliwafuata Shinyanga kuzungumza nao kuhusu suala hilo.
Alisema Januari 27, mwaka huu alipewa kazi ya kulipua helkopta iliyokuwa ikitumiwa na Katibu Mkuu Chadema, Dk. Slaa, Mbunge wa Ubungo, Mnyika na Mwenyekiti wa kanda ya Mashariki katika ziara ya Kanda ya Ziwa.

“Aliniambia kuwa Masele ana dili la shilingi milioni 180, baada ya ujumbe huo nilipokea simu ya waziri huyo ambaye aliniambia nikifanikisha nitalipwa fedha hizo,” alisema.

Alisema kuwa Masele alimtaka aeleze helikopta hiyo itatua wapi, muda gani na kama kweli wahusika wamo ndani yake kisha ulipuaji ufanywe na watu walioandaliwa.

Alisema alijiandaa na kufuatilia ila hofu ya kimungu ilimuingia akahofia taifa litapokeaje tukio la kifo cha Dk. Slaa na yeye akihusika.

“Nilimweleza Masele lakini alimpigia simu mkuu wa wilaya ya Shinyanga Anna Rose Nyamubi, ambaye alimshauri kuwa sio vyema tukio hilo likafanyika wilayani kwake, baadaye nilikutanishwa na katibu mkuu wa umoja wa vijana ccm (UVCCM) Taifa , Sixtus Mapunda pamoja na mtu mmoja wa usalama, ” alisema.

Aidha, alisema aliwashauri badala ya kulipua watumie mabango na kurubuni vijana kuhujumu ziara ya Dk. Slaa ambapo walifanikisha hilo.

Alisema baadaye walikutana tena na Nape, Nchemba na kuombwa wawashawishi madiwani na viongozi wengine wahamie CCM kwa ahadi ya kupewa ukatibu wa Wilaya kwenye wilaya watakazoamua.

Alisema baadaye madiwani hao walienda Mwanza mjini ambapo huko walikutana na Nape ambaye alieleza kusikitishwa kitendo cha Chadema kumvua uwanachama Zitto.

KUONDOKA CHADEMA
Alisema Februari 26, mwaka huu waliondoka rasmi Chadema ambapo Nape alifika huko na kukutana naye hoteli ya Kalena ambapo katika mazungumzo alimhakikishia maisha mazuri pamoja na uongozi.

“Usiku ulipofika gari la mwenyekiti wa mkoa wa Mwanza iliwachukua na kuwapeleka uwanja wa ndege na kusafiri kuja Dar es Salaam kukutana na Nchemba ambaye naye aliwataka waelekee Dodoma na baadaye Kalenga,” alisema.

Aliongeza kuwa Dodoma walienda nyumbani kwa Kinana ambaye huko waliwakuta Masele, Nchemba na Mchange ambapo wakati wote Katibu Mkuu alisifu kitendo chao cha kuondoka Chadema.

Alisema katika mazungumzo makada hao walimwambia Nchange asichoke kwa kazi anayofanya.

ACT YATAJWA
Mzuka alisema makada hao walikubaliana mgogoro ndani ya Chadema lazima uboreshwe na kuahidi kugharamia fedha za kwenda mikoani na pia wakasema kuna chama kitasajiliwa.

Pia alisema makada hao walisema watahakikisha Msajili wa vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi anakipatia usajili wa kudumu kwa gharama yoyote chama cha ACT ili CCM ipate ushindi kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Alisema katika mazungumzo hayo, Kinana alisema ACT imeanzishwa kwa lengo maalum la kuipa CCM ushindi kwa kuwa hata huko duniani, ushindi wa chama tawala unatokana na usajili wa vyama vipya.

WABUNGE WANNE KUHUJUMIWA
Makada hao walikubaliana katika uchaguzi ujao mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, asirudi bungeni kwa sababu ameitia hasara serikali kuhusu hoja zake dhidi ya katiba.

“Katika jimbo la Lissu, ACT itafadhiliwa kusaidia kutoa mgombea CCM ambapo itagawa kura za jimbo,” alisema.

Diwani huyo alitaja wabunge wengine ambao wapo kwenye mtego huo kuwa ni mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema ambaye imeelezwa amesababisha kushuka kwa utalii.

Wengine ni mbunge wa Iringa mjini Mchugaji Peter Msigwa na mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi.

Kwa upande wa Lissu alisema kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa, Diwani akijiuzulu anatakiwa aandike barua rasmi kwa mwenyekiti wa Halmashauri na kuambatanisha na kiapo.

“Hawa hawakufanya hivyo kwa hiyo bado ni madiwani wa halmashauri ya mji wa Shinyanga,na uthibitisho kuwa hawajajiuzulu ni kuwa siku 90 zimepita bila kutangazwa uchaguzi, “ alisema.

MBUZI WASABABISHA VIFO OMKOANI LINDI




WATU wanane wamekufa papo hapo, wengine tisa wakijeruhiwa na kulazwa katika Hospitali ya Nyangao mkoani Lindi baada ya gari aina ya Land Rover, mali ya Halmashauri ya Mji Masasi kupata ajali katika kijiji cha Mtama wilaya ya Lindi Vijijini mkoani hapa.

Gari hilo lenye namba za usajili STL 1615, lilikuwa linatokea Lindi ambako maofisa wa Halmashauri ya Masasi walikuwa wanashiriki katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane) yaliyofanyika kitaifa katika Viwanja vya Ngongo, nje kidogo ya Manispaa ya Lindi.

Kutokea kwa ajali hiyo kulithibitishwa jana na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Lindi, Renatha Mzinga aliyesema ilitokea juzi majira ya saa 11.30 jioni katika kijiji cha Mtama.
http://4.bp.blogspot.com/-KDSyrLkmbaA/UTg43wefcwI/AAAAAAAAIbg/DwKqYhGpOLQ/s1600/3.jpg
Aliwataja waliokufa kuwa ni Issa Salumu (33), Malik Selemani (24), Juma Ausi (21), Rajab Khalfan (17), Said Mchora (24) na Fadhili Mchalasi (26) ambapo watu wawili hadi sasa hawajafahamika majina yao, na amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi.

Marehemu wote ni wakazi wa kijiji cha Mtama. Kwa mujibu wa Kamanda Mzinga, waliojeruhiwa kwenye ajali hiyo ni dereva wa gari hilo, Kessy Mwaijande (40).

Pia wamo madiwani watano wa Halmashauri ya Mji Masasi ambao ni Habiba Amlima, Maimuna Chiputa, Exaveria Mhagama, Asha Abbas na Blandina Nakajumo.

Wengine ni Abraham Mohammed, Shaabani Issa Kitemwe na Ally Adam, wote wakazi wa kijiji cha Mtama.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Lindi, Renatha Mzinga.

 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti mashuhuda wa ajali hiyo walisema kuwa majira ya jioni kwenye eneo hilo la tukio, waliliona gari hilo likiwa kwenye mwendo kasi, mazingira ambayo yalisababisha dereva wa gari hilo aliyekuwa akijaribu kukwepa mbuzi waliokuwa barabarani kushindwa kumiliki gari hilo na hatimaye kuacha njia na kuwagonga watu waliokuwa pembezoni mwa barabara hiyo, waliokuwa wakifanya biashara ndogo.

Hata hivyo, mmoja wa mashuhuda hao, Ahmad Mbonde aliiambia HabariLeo Jumapili kuwa, kama si kuwakwepa mbuzi, dereva wa gari hilo asingesababisha ajali.

Kutokana na tukio hilo, Kamanda Mzinga amewataka madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kunusuru maisha ya watu wanaoendelea kupoteza maisha na huku wengine wakibaki na ulemavu, mazingira ambayo hupunguza nguvu kazi ya

NYUMBA ZA RWAKATARE ZABOMOLEWA CHINI YA ULINZI MKALI

 Katapila likibomoa moja ya nyumba nne zinazomilikiwa na Mchungaji Getrude Rwakatare katika eneo la Mbezi Beach, Dar es Salaam jana.
WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Makazi jana imebomoa nyumba nne zilizojengwa ndani ya kiwanja namba 314 zilichopo eneo la Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam zinazomilikiwa na Mchungaji Getrude Rwakatare kwa tuhuma kuwa alivamia eneo hilo.

Kazi hiyo ya ubomoaji, ilitekelezwa chini ya ulinzi mkali wa Polisi na iliendeshwa kwa pamoja na maofisa wa Ardhi kutoka wizarani na Manispaa ya Kinondoni, waliodai wamepewa agizo hilo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Alphayo Kidata.


Mhandisi wa Manispaa ya Kinondoni, Baraka Mkuya alidai wamepewa agizo na Katibu huyo, kuvunja nyumba ndani ya kiwanja hicho, baada ya kubainika kuwa eneo hilo siyo mali ya Rwakatare, hivyo hastahili kujenga mahali hapo.
Mhandisi Mkuya alidai pamoja kutokuwa mmiliki halali wa eneo hilo, nyumba hizo pia zimejengwa bila utaratibu, ikiwemo kupata kibali cha ujenzi kutoka katika manispaa hiyo, suala linaloashiria kuwa kulikuwa na kitu kimejificha.
“Sisi kama manispaa tumekuja kutekeleza agizo la kubomoa kutoka kwa Katibu Mkuu, kinachoonyesha ni kuwa aliyejenga eneo hili alivamia eneo la mtu mwingine huku akijua wazi ni kinyume cha utaratibu” alidai Mkuya.
Alidai matatizo ya uvamizi wa viwanja, yamekuwa ni jambo la kawaida hasa katika Manispaa ya Kinondoni na kwamba wanaendelea kuyashughulikia kwa lengo la kuyapatia ufumbuzi wa haraka.
Awali, kazi hiyo ya ubomoaji ilitanguliwa na ‘vuta nikuvute’ baina ya mwanasheria aliyedai kuwa anamwakilisha Rwakatare, Emmanumuel Muganyizi na Mhandisi wa Manispaa ya Kinondoni, Baraka Mkuya kuhusu suala la kubomolewa kwa nyumba hizo, zinazodaiwa kujengwa ndani ya kipindi kisichozidi miezi miwili na kupauliwa kwa vigae.
Huku akiwa na nyaraka mbalimbali za kesi, alidai kesi bado ipo katika Mahakama ya Kinondoni. Muganyizi alisema anashangazwa na uamuzi huo uliochukuliwa kwa madai kuwa suala hilo, halijapatiwa ufumbuzi wa kisheria na Mahakama.
“Ninaamini hiki kinachoendelea hapa ni sawa na uvunjifu wa amani, kesi bado ipo mahakamani inapaswa iachwe iishe ndiyo uamuzi ufanyike. Kwa hili mnalofanya sasa siyo sawa kabisa,” alisema Muganyizi.
Mwanasheria huyo wa Rwakatare, awali aliingia katika mzozo na waandishi, akidai kushangazwa na kitendo chao cha kutaka kuandika habari hiyo.
Alidai habari hiyo haina manufaa kwa jamii, kwa kuwa inahusu madai ya mtu na mtu. Kwa upande wake, mtu anayedai kuwa mmiliki wa kiwanja hicho, aliyekuwepo wakati kazi ya uboaji ikiendelea, Janeth Kiwia, alidai kiwanja chake kilivamiwa na kuanza kujengwa mwishoni mwa mwaka jana wakati akiwa safarini kwa watoto wake nje ya nchi.
Alidai kabla ya kuvamia eneo hilo, kulikuwa na nyumba ya vyumba vinne, aliyokuwa akiijenga taratibu, ambayo hata hivyo ilibomolewa na msingi wake kutumika kujenga moja ya nyumba hizo.
“Tayari kulikuwa na nyumba iliyokuwa imefikia usawa wa rinta, lakini cha kushangaza walipovamia waliibomoa na kujenga ya kwao, namshukuru Mungu kwa kuwa haki imetendeka baada ya kuhangaika huku na kule kutafuta haki yangu,” alidai Janeth.
Alidai kitendo hicho, kimemfanya kujenga imani na Serikali kuwa inatenda haki, bila kujali kuwa aliyekuwa akiporwa na mnyonge, huku akiitaka kuwasafisha baadhi ya watendaji waliopo ndani ya wizara hiyo, wanaoshirikiana na watu wabaya kutaka kupora haki za watu.
“Nilikuwa sitarajii kama ningefanikiwa tena kupata kiwanja changu, namshukuru Mungu haki imetendeka bila hata mimi kutoa Shilingi moja, naomba tusife moyo na Serikali yetu kwa kuwa inafanya kazi,” alisisitiza Janeth.
Mwanasheria aliyekuwa akisimamia kesi ya Janeth, Howard Msechu kutoka Kampuni ya uwakili ya Homac, alidai mteja wake ndiye mmiliki halali wa kiwanja hicho.

HUYU NAE NI MWANAMKE


Mwanamama Power Black Nyati 'Jike Jeuri' akifanya vitu vyake ndani ya Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014.
'Jike Jeuri' akipiga 'push - up' ndani ya Uwanja wa Taifa.
'Jike Jeuri' akiwatoa jasho mabaunsa wawili walioshindwa kupeleka kidole chake chini.
Baada ya kuwatoa 'knock out' mabaunsa wawili, ilibidi aongezeke mwingine wawe watatu lakini bado walishindwa kupeleka kidole cha Jike Jeuri' chini.

HAWA NDIO MA LORE MODEL WA WATOTO WA JAMII YETU





Kwa mtindo huu huwezi kuwa kioo cha jamii, kwa skendo hii ni lazima utumie jahazi kujisafisha

Mtangazani Mahiri wa Redio 88.5 Clouds FM kupitia kipindi cha Jahazi, Ephrahim Kibonde akipingana na Askari wa Usalama barabarani wakati alipotakiwa kutii sheria bila shurti,mapema asubuhi hii jijini Dar es salaam.
Kibonde anadaiwa kusababisha ajali asubuhi hii eneo la Makumbusho, ikiwa gari aliyokuwa akiendesha kuigonga gari ya dereva mwingine kwa nyuma. Trafiki walifika eneo la tukio na kupima ajali, Kibonde alipoona hivyo akarudi nyuma na kuendesha gari lake kuondoka eneo la tukio bila kufuata taratibu za usalama barabarani,hali iliyomlazimu yule Trafiki kutumia gari lililogongwa kumfukuzia. 

Walifanikiwa kumkamata eneo la Mwenge na Trafiki aliingia katika gari lake na kumwomba arudi eneo la ajali ili wakapime na kuchora mchoro wa ajali. Kibonde aligoma na kumtaka trafiki ashuke katika gari lake,Trafiki naye hakutana kufanyi kwa maana ya kuwa aligoma kushuka na kumuamuru Kibonde arudi eneo la tukio. 

Kibonde aliondoa gari na kuendelea na safari yake huku yule Trafiki akiwa ndani ya gari hiyo, Trafiki aliwasiliana na wenzake ambao walianza kuifuatilia gari hiyo ya Kibonde kama walivyopewa maelekezo na mwenzao aliopo ndani ya Gari hiyo.

Mara Kibonde akatokea maeneo ya mataa ya Ubungo, hapo kulikuwa na Trafiki mwingine aliyekua eneo hilo akaipiga mkono gari ya Kibonde na ambapo inasemekekana hakusimama na badala yake ikaja gari nyingine na kuichomekea kwa mbele na hapo ndipo alipotiwa mbaroni! Aligoma kuendesha gari ikabidi livutwe hadi polisi Urafiki na yeye kuwekwa chini ya ulinzi na baadae akahamishiwa Kituo cha Oystabay ambako yupo mpaka sasa.

Inadaiwa kuwa Kibonde alikuwa amelewa sana,hali iliyopelekea kufanya hayo yote ikiwa ni pamoja na kuwajibu vibaya Askari hao


Kuna watoto na vijana wanaokuwa wanatamani sana kuwa kama Kibonde kwa vile wanavyomsikia  na kumtazama lakini kwa mtindo huu kaka unawaipoteza jamii. Japo kuwa ni kweli kwamba hakuna mwanadamu asiyefanya kosa lakini hili lisingefika hapa kama Kibonde angetii maelezo mpaka anaamua kuwa kituko namna hii.

Si lazima kila afanyacho upendaye ni lazima na wewe uyafanye kila kitu twajifunza kwa wakubwa lakini mkubwa akifanya ujinga mwachie wewe chukua lile lililozuri nenda nalo
 kuna wat


USIPOSTAAJABU YA MUSA UTAONA YA FILAUNI. HUYU NAE NI SAMAKI NA ANALIWA

Yaweza kuwa hujawahi kufikiri ipo siku utakula samaki kama huyu ila tuu ukae ukijua yakuwa samaki nguva yupo na analiwa hivyo kuwa makini na kila kitu unachokula kilichokuwa tayari kimeandaliwa