Tuesday, August 26, 2014

MAITI YAZIKWA KIMAAJABU DAR

Katika hali isiyokuwa  ya kawaida na kushangaza, wananchi wa Mbezi Msakuzi Wlaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, walisusa na kuondoka makaburini kwa kile kilichodaiwa kuwa maiti ya Michael Kisanto (pichani) waliyotarajia kuizika iliwekwa ndani ya  jeneza kimaajabu.

Mazishi ya Michael Krisanto yakiendelea.
Tukio hilo lilitokea hivi karibuni katika Makaburi ya Makamba Msakuzi, Mbezi jijini Dar es Salaam ambapo wananchi hao waligundua kuwa  maiti ya kijana huyo iliweka ndani ya jeneza kinyume na utaratibu uliozoeleka yaani kichwa chake kilielekezwa sehemu ya miguu na miguu ilielekezwa sehemu ya kichwa.
Msafara wa kuelekea makaburini kwa ajili ya mazishi ya Michael Krisanto.
\Kama hiyo haitoshi, maiti hiyo badala ya kuviringishwa sanda nyeupe, ilitumika sanda nyeusi kitu  kilicholeta tafsiri tofauti miongoni mwa waombolezaji. 
Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kuwa, kabla jeneza lenye mwili kutumbukizwa kwenye kaburi kulitokea mvutano mkubwa baina ya wanandugu na waombolezaji.

Waombolezaji wakizozana juu ya utaratibu wa mazishi ya Michael Krisanto.
Imeelezwa kuwa, waombolezaji hao waliwataka wanandugu wafuate taratibu zilizozoeleka katika jamii wakati wa kuzika.Hata hivyo, ndugu wa marehemu hawakuwasikiliza na kudai kwamba walikuwa wanafuata mila na tamaduni za kabila lao (jina la kabila linahifadhiwa kwa sababu maalum).
Mwili wa marehemu, Michael Krisanto ukishushwa kaburini.
Wanandugu hao wakaamua kushusha jeneza lenye mwili kaburini na walipoanza kuzika waombelezaji walikuja juu na kulitoa jeneza kaburini hali iliyosababisha kutokea kwa vurugu kubwa.
Wanandugu wa marehemu, Michael Krisanto wakiweka mishumaa pembezoni mwa kaburi la ndugu yao.
“Vurugu hizo zilisababisha wanawake waliokuwa makaburini kutimua mbio na wanaume wakasusa na kuwaacha wanandugu waendelee kumzika ndugu yao,” alisema shuhuda  wa tukio hilo kwa sharti la kutoandikwa jina lake gazetini.
Marehemu Michael Krisanto(kulia) enzi za uhai wake.
 Habari zinasema kuwa, kutokana na utata huo, hata mchungaji aliyepaswa kuendesha ibada ya mazishi aliondoka bila kutoa huduma ya kiroho. 

Mmoja wa wanandugu wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina moja la Victor, alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo hakuweza kusema chochote badala yake alikuwa akibubujikwa na machozi.

MKE WA MCHUNGAJI AJIFUNGUA HIRIZI HUKO BAGAMOYO


Wazee wetu walishawahi kuneno kwamba; Ukishangaa ya Mussa utayaona ya filauni! Ndivyo unavyoweza kuanza kusema kuhusiana na tukio la kushangaza lililotokea Kijiji cha Udindila Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani.

Mchungaji wa Kanisa la EAGT aliyetambulika kwa jina la Boniface Onesmo alijikuta akibubujikwa na machozi mara baada ya kushuhudia mkewe Bi. Benta Boniface akijifungua hirizi baada ya kushika mimba kwa kipindi cha miezi saba na nusu!

Akizungumza na mtangazaji wa Kipindi cha Hatua Tatu cha 100.5 Times Fm, Edson Mkisi Jr, Mchungaji huyo alisema kabla ya kutokea kwa tukio hilo mkewe amekuwa na matatizo ya kuharibika kwa mimba za mara kwa mara na tangu kuhamia kwa eneo hilo la Udingila Bagamoyo mkewe huyo hajawahi kuzaa mtoto hata mmoja angawa amekuwa akishika mimba kila walipohitaji kuzaa.

“Kwa hakika Mungu ni mwema na sitaacha kuendelea kumsifu na kumuabudu,” alianza kueleza Mchungaji Onesmo.

 “Zaidi ya mtoto huyu mmoja niliyemzaa kabla ya kuhamia hapa, hivi sasa kila ninapotaka kuzaa mtoto mimba za mke wangu zinaharibika na hadi muda huu mimba zaidi ya nne zimeshaharibika na hii nyingine ndio amezaa hirizi!” Mchungaji Onesmo alisimulia.

Aliezeza kuwa siku ya tukio, mkewe kipenzi alianza kusikia uchungu tangu saa nne asubuhi na kadri muda ulivyozidi kwenda ndivyo uchungu ulipozidi kuongezeka.
  
Hali iliendelea hivyo hadi saa nne usiku ambapo mkewe alihisi kabisa kupushi na mimi nilikuwa tayari kumsaidia lakini wakati anaendelea kupushi mkewangu akawa anatoa haja ndogo mara kwa mara na alitoa haja ndogo hadi ndoo nne ndogo zilijaa na kumwaga nje.

“Baada ya hapo aliendelea kusikia maumivu makali ya tumboni huku akihisi kuzaa lakini baadae aliposikia mtoto anakuja na mimi kujiweka tayari kumzalisha niliona kitu kinatoka kama mtoto kukivuta ikatoka hirisi ikiwa imefungwa kitambaa chenye rangi chekundu na nyeusi!” anasema.

Aidha, kwa upande wa mkewe, alisema kama siki hiyo kungekuwa na sumu ya panya angekunywa afe akapumzike.
Akizungumze huku akilia, mama Dotto (Benta), anasema siku ya tukio hilo roho yake ilinusa kaburi kama kama kungekuwa na hata mafuta ya taa kwenye kopo angekunywa ili afe.

Nilimuuliza mume wangu mara kadhaa kama kwenye kopo kuna mafuta ya taa lakini aliniambia yote aliweka kwenye kandiri (taa ya chemli) na hata nilipoangalia tunapoweka sumu sikuiona….kwa hakika kama ningekiona kimoja wapo ningekunywa nife! Nimetesema sana,” anasema mama Dotto.

Mama Dotto alisema pamoja na changamoto zote anazokutana nazo Bagamoyo lakini hajafikiria wala hafikirii kwenda kwa mganga wa kienyeji.

Siwezi kwenda kwa mganga wa kienyeji kwa sababu waganga ukienda wao huongeza tatizo kwa hiyo nitaendelea kumuomba Mungu hadi atakaposikia maombi yangu,” anasema huku akiangalia na mumewe pamoja na majirani waliofika kumjulia hali.

Akizungumza na Mkisi Jr, Mjumbe wa eneo hilo, Bw Hamza Adam, mbali na kuthibitisha kufahamu kutokea kwa tukio hilo, pia alibainisha kwamba mbali na tukio hilo ambalo hajawahi kukutana nalo tangu uhai wake, pia eneo hilo mifugo imekuwa ikifa hovyo bila kuwepo kwa ugonjwa wowote.

WANAJESHI WANNE WA NEPAL WAKAMATWA NCHINI JANA BILA KIBALI,YUMO PIA KOMANDO WAO



Wanajeshi hao wa jeshi la nchi ya NEPAL wakiwa wanaonyesha vyeti vyao vya uanajeshi wa jeshi hili

        Idara ya uhamiaji Jijini Dare s salaam imewakamata raia 12 wa kigeni waliokuja nchi kinyume na sheria wakiwemo wanajeshi wanne wa  jeshi la NEPAL pamoja na nane kutoka nchini india walioletwa nchini kinyume na sheria kwa kisingizio cha maisha magumu nchini kwao.
  
     Raia  hao wamekamatwa katika nyumba ya kulala wageni ya ESCOT iliyoko kijitonyama jijini Dar es salaam katika operation maalum iliyoendeshwa na idara ya uhamiaji Jijini baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wananchi wa maeneo hayo juu ya uwepo wa watu hao ambao waliwatilia mashaka.

Afisa uhamiaji wa jiji la Dar es salaam GRACE HOKORORO akizungumza na mtandao huu kuhusu sakata hilo
         Wanajeshi hao wanne wa jeshi la NEPAL yumo pia komando mmoja wa jeshi hilo ambao nao wamedai kuletwa nchini kwa ajili ya kutafutiwa ajira ya maswala ya ulinzi katika nchi za Africa hivyo wakashukia Tanzania kama kituo kwa ajili ya kufanikisha malengo yao.

        Akizungumza na mtandao huu muda mfupi uliopita afisa wa uhamiaji wa jiji la Dar es salaam GRACE HOKORORO amesema  kuwa wahamiaji hao wamekuwa wakipita katika nchi ya Tanzania na kupelekea nchi nyingine kama Africa ya kusini  kwa ajili ya kufanyishwa kazi zisizo halali



Picha mbili zikionyesha wanajeshi hao wakiwa katika nchi yao wakiwa wanalitumikia jeshi la nchi yao kabla ya kutimka na kuja nchini
      Aidha amesema kuwa watu hao wamekuwa wakiletwa na mawakala ambao wamekuwa wakiwatoa katika nchi zao kwa ahadi  la kuwatafutia kazi katika nchi hizi jambo ambalo amesema kuwa linatafsiriwa kama biashara ya binadamu ambapo mawakala waliowaleta watu hao hadi sasa hawajapatikana.
          
         Aidha Bi GRACE amewataka watanzania na watu wasamaria wema kuwafichia watu wanaowaficha watu kama hao kwani ni kinyume na sheria na baadae huleta madhara makubwa kama uhalifu na uuzwaji wa madawa ya kulevya.

KUNANI PERAMIHO?MTU MWINGINE AJINYONGA TENA (picha hizi si nzuri sana zinatisha)



Mwili wa Rashid Athuman ukiwa unaning’inia katika kitanzi ambacho alikifunga chooni kabla ya kujinyonga kasha kujifungia chooni.
Mwili wa Rashid Athuman ukishushwa na wasamaria wema kutoka kwenye kitanzi kwa kwa kushirikiana na Jeshi la polisi.


Mwili wa Rashid Athuman ukiwa unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhiwa maiti katika hospital ya Peramiho.
Hiki ni chumba  ambacho marehemu alikuwa amepanga na kinachoonekana ni kitanda ambacho alikuwa anatumia kulala yeye na mke wake .
Mke wa marehemu Lucy Adam (24) akiwa amembeba mtoto wake Yoweri Rashid (02) mgongoni.
--------------------------------

Ikiwa imepita siku moja tangu mazishi ya Fundi maabara mstaafu wa Hospitali ya Peramiho Bwana Frederick Mgaya (60) ambaye alifariki kwa  kujinyonga alhamisi iliyopita hapa Peramiho, mtu mwingine tena aliyetambulika kwa jina la Rashid Athuman (32) amekutwa amejinyonga katika  choo cha nyumba aliyokuwa akiishi.

Bwana Rashid Athuman ambaye ni mkazi wa Usangu Jijini Mbeya amejinyonga kwa kutumia shuka majira ya saa Saba za usiku baada ya kumuaga mke wake Bi Lucy Adam (24) kuwa anakwenda chooni kujisaidia ambapo alikwenda kukamilisha mpango wake huo.
Taarifa kutoka kwa mke wake huyo zinaeleza kuwa enzi za uhai wake Bwana Rashid Athuman alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua kikuu, tatizo lililowafanya wachukue uamuzi wa kuja Peramiho kwa ajili ya matibabu.
Bi Lucy anazidi kutanabaisha kuwa walifika Peramiho tarehe 19 Mwezi Julai  2014 na kupata chumba cha kupanga katika Kitongoji cha Namihoro jirani na Stendi Kuu ya Peramiho katika nyumba ya Cosmas Chidumule ambapo tangu wakati huo waliendelea na maisha yao wakiwa wakisaidiwa chakula na majirani waliokuwa na mapenzi mema.
“Tangu jana asubuhi nilishinda vizuri tu na marehemu mume wangu ambapo mishale ya saa tatu za usiku tulienda kulala. Muda mchache baadaye nilipitiwa na usingizi mpaka majira ya saa saba za usiku ambapo marehemu aliniamsha na kunieleza kuwa alikuwa anakwenda uani kujisaidia ambapo baada ya yeye kuelekea uani mimi niliendelea kulala” Alisema mke huyo wa marehemu.

“Baada ya muda mrefu kupita pasipo marehemu kurudi nikaamua kuamka na kutaka kuufungua mlango wa chumbani lengo hasa likiwa kwenda uani kujua sababu ya mume wangu kuchelewa kurudi. Nilishangaa kuona mlango umefungwa kwa nje na ikanibidi nitumie kisu ili kuweza kuufungua mlango huo ambapo nilifanikiwa na kwenda uani ambapo nilikuta mlango wa uani ukiwa umefungwa kwa ndani kitu kilichonifanya niusukume kwa nguvu na kumkuta mume wangu akiwa ananing’inia huku akiwa amekwishafariki” Alimalizia mjane huyo.

Mjane huyo ameishi na marehemu kwa muda wa miaka mitatu na kufanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume, Yoweri Rashidi (2) ambapo uchunguzi zaidi kuhusu chanzo cha kifo hicho bado unaendelea.