Wednesday, September 17, 2014

MKUU WA KITUO CHA POLISI NUSULA AUAWE NA WANANCHI BAADA YA KUFUMWA AKITAKA KUMBAKA MWANAFUNZI


Mkuu wa kituo cha polisi cha Nyamboge kilichopo katika kata ya Katoma wilayani Geita mkoani Geita amenusurika kuuawa na wananchi wenye  hasira kali  baada ya kukutwa akitaka kufanya mapenzi na mwanafunzi katika chumba anachoishi mwanafunzi huyo(Geto).

Tukio hilo limetokea juzi  Jumapili  majira ya saa tatu usiku ambapo wananchi wakiwa na marungu na mikuki waliweka mtego wa kumnasa mkuu huyo mwenye namba E 2837 Koplo Venance.

Akielezea tukio hilo binti huyo (jina linahifadhiwa)(19) anayesoma kidato cha nne alisema siku ya jumapili mkuu huyo wa kituo alituma maaskari wawili wiki jana wakaenda kumkamata.

"Hata sijui kosa langu,nilikamatwa nikalazimika kwenda na nilipofika alianza kunilazimisha natembea na mwalimu wangu,nilipokataa nilianza kupigwa na kulazimishwa kuandika maelezo",alisema mwanafunzi huyo.

Alisema baada ya kukataa kuandika maelezo alipelekwa rokapu na muda mfupi baadaye  alifuatwa na askari mmoja kati ya wale waliomfuata anapoishi, alianza kuandika maelezo na kumlazimisha kusaini.

Alisema  baada ya kugoma kuandika alipigwa sana na kuamua kusaini kutokana na kutishiwa kufungwa na baada ya kusaini aliitwa na OCS huyo na kumwambia aende nyumbani lakini arudi jioni ana shida naye ya muhimu sana lakini hakurudi kutokana na kuchoka na kipigo alichokipata kituoni hapo.

"Kutokana na mkuu huyo wa kituo kutuhumiwa na mwanafunzi kuwa anamtaka kimapenzi ilibidi awaambie wanafunzi wenzake na wananchi na baada ya hapo wakatengeneza mtego ili wamnase",walisema mashuhuda wa tukio hilo.

"Siku ya jumapili  mkuu huyo wa kituo alikwenda nyumbani kwa mwanafunzi huyo na kuomba wafanye mapenzi kwa kuwa wenzake anaoishi nao hawakuwepo lakini aligoma kufanya hiyo ",walisema mashuhuda wa tukio hilo  na  kuongeza:

"Kutokana na mtego wa wananzengo,muda mfupi   wananchi waliokuwa wamemuona OCS anakwenda kwa binti huyo walifika hapo na kufunga mlango kwa nje na kuanza kupiga mwano".
 

UKATILI DHIDI YA BINADAMU UNAOENDELEA NCHINI IRAQ NI HATARI


Hakika   binadamu   tumekuwa  kama  wanyama,   Angalia  mauaji  yanayofanywa  na  waasi  huko  iraq  hakika   yanatisha   sana
 






Huyu  ni  mwanajeshi  wa  serikali  ambaye  aliuwawa  na  waasi  wa   iraq
Hawa  ni   wanajehi   wa   Iraq  ambayo  waliuwawa  na   kikundi  cha  waasi  huko  iraq