Saturday, December 13, 2014

WAZAZI WA MWOZESHA BINTI YAO KWA NGUVU BAADA YA KUFUMWA AKIFANYA TENDO LA NDOA

Na Baraka lusajo,
   Binti mmoja mkazi wa  kijiji   Lugombo  kata  ya Kandete  Wilayani Rungwe Mkoani  Mbeya  Getina   Karinga  miaka  {24} ameingia katika wakati  mgumu  baada ya kuozeshwa  ndoa  ya mkeka  kwa  nguvu na  wazazi  wake  baada  ya  kufuniwa   na  mwanaume  wakati  akifanya  tendo la ndoa  chumbani  kwao.

  Tukio  hilo  la kushangaza  limetokea  baada  ya  kijana  huyo kwenda  kwa  wazazi  wa  binti  huyo   kwa lengo la  maongezi ya  kawaida   na  kujikuta akiambulia   kipigo  kikali kutoka kwa  mama  mtu baada  ya kufumwa  wakati  akifanya  tendo  hilo chumbani kwa  mama yake  na binti.
 Hata hivyo  kutokana na     hali  hiyo
mama  huyo aliweza  kuangua  kilio kikubwa  baada  ya   vijana hao kuto onyesha  ishara  ya kuacghana  na kitendo  hicho mara baada  ya kufumwa  wakati  wakifanya kitendo hicho  na kwamba  kabla ya  tukio  mama  mtu alifika  na  kuwa muru  kuondoka mara  moja  lakini kutokana  na    wapendanao  kunogewa   na  tendo hilo  walijikuta wakiendelea  kufanya  bila kujari uwepo  wa  mama yao na kupelekea  mama mtu kupatwa  na hasira  na kuchukua   mfagio  na kuwachapa .
 Kwa mujibu  wa  mama  huyo ambaye  hakutaka  kutajwa  jina lake   hadharani  alisema  mnamo  majila ya  sambili za usiku akiwa ametokea  kwenye  shughuri  zake za kawaida  aliweza   kukuta milango ya   nyumba   yake ikiwa wazi  na kuamua  kuingia  lakini baada ya  kumwita  binti  yake  alijibiwa arudi  aliko tokea   , lakini aliamua  kupiga  moyo  konde  na  kuamua  kosogea  zaidi  na kumkuta mtoto wake akifanya  kitendo hicho  na kuamua   kuita watu.
         “Nimeona  aondoke  nyumbani kwangu kwani amekuwa akinidharau  bila kujari  kwamba    mimi ni mama yake  na  hadi kufikia hatua  ya  kufanya  mapenzi  na mwanaume mwingine  nyumbani kwangu kitu ambacho ni dharau  kubwa ,  na mpaka sasa nimemwozesha  na kutoa  baraka zangu  zote  kwani nimechoka   vitendo anavyo nifanyia   kwani  mda  wote amekuwa akifika nyumbani akiwa amelewa  pombe  kupita  kiasi  na  mda mwingine  nimekuwa  nikimfuma  kwa  macho  yangu akiwa  anavuta  bangi na sigara.” Alisema mama mtu.
 Kwa  upande  wa    binti huyo alisema   yuko  tayari  kuolewa  na kijana  huyo   na kwamba   anawashukuru wazazi  wake  kwa  hatua  walio fikia kutokana  na kwamba amekaa miaka  mingi sana akiwa  nyumbani  kwao bila  kuolewa na kwamba sasa  atakuwa  huru  katika  kumpatia mme  huduma yake  muhimu, na  huku mwanaume akifurahia  ndoa  hiyo  kutoikana  na kwamba  muda wote  walikuwa  wakimbania  mwanamke   huyo wakidai anatabia  mbaya  kitu amacho kwake    si kweli..
 Mtendaji wa  kata  hiyo  huruma mwakyusa  mbali  na kukili kutokea  kwa  tukio  hilo  alisema wameshindwa  kuendelea na  kesi hiyo kutokana na kwamba  wazazi  wa  binti  huyo  wamekataa  kumpokea binti  yao  kwa madai  ya kuwachafua na kuamua   kumuodhesha  bila  mahali.