Wednesday, August 13, 2014

TRENI YA ABIRIA YAPATA AJALI NCHINI USWISI


2
Treni lililobeba abiria zaidi ya 200 limepata ajali kwa kutereza pembeni ya reli na kusababisha baadhi ya mabehewa kuwa nje ya reli. Abiria waliokuwemo ndani ya treni hilo walilazimika kukimbilia upande wa pili wa treni hilo ili kuepuka lisidondoke kwenye maporomoko.Juhudi hizo zilisaidia na hakuna mtu aliyefariki kwenye hiyo ajali lakini watu 11 walipata majeraha na watano kati yao kupata majeraha makubwa.

Ajali hii imetokea kwenye mlima ya nchini Uswisi.
1
3
4
5
6
7

KIBONDE NA GADNER WAPANDISHWA KIZIMBANI

Watangazaji Ephraim Kibonde (wa kwanza kushoto) na mwenzake Gardner Habash (wa pili kulia) wakielekea kizimbani.
Watangazaji hao wakiongozwa na maofisa wa polisi kuelekea mahakamani.
...Wakiingia mahakamani.
MTANGAZAJI wa Clouds FM, Ephraim Kibonde na mwenzake, Gardner Habash wa Times FM leo wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa kusababisha ajali na kudharau amri ya polisi na kutoa lugha ya matusi.
Watangazaji hao wamesomewa mashitaka hayo na Wakili wa Serikali, Salim Mohammed mbele ya Hakimu Aniseta Wambura.
Kibonde na Gadna wanadaiwa kutenda makosa hayo Jumamosi ya Agosti 9, mwaka huu saa 12 asubuhi, katika eneo la Makumbusho, ambapo Kibonde akiwa anaendesha gari walilokuwa wamepanda aliligonga gari la raia mmoja wa kigeni (Mzungu) na kukimbia.
Kesi yao imeahirishwa mpaka Septemba 10 mwaka huu itakaposikilizwa tena.(Picha na Shakoor Jongo / GPL)

MADAKTARI HAWA NI BALAA:WAUNDA MASKIO NA KUMPA KIJANA ASIYE NA MASIKIO TANGU AZALIWE




Madaktari nchini Uingereza wameumba masikio kutokana na ubavu wa kijana (pichani kulia)aliyezaliwa bila ya viungo hivyo muhimu.

 Kijana huyo wa miaka tisa Kieran Sorkin alizaliwa bila masikio na madaktari wamekuwa wakifanya majaribio ya mbinu mpya ya matibabu katika hospitali ya Great Ormond Street iliyoko jijini London..

Takwimu nchini Uingereza zinaonesha kuwa takriban watoto 100 huzaliwa bila kiungo hicho muhimu nchini Uingereza .

 Madaktari wanaita ugonjwa huo microtia.

 Kieran aliyezaliwa kama kiziwi hakuwa na masikio alipozaliwa badala yake alizaliwa na shimo mbili na ndewe tu badala ya masikio.

 Tayari kieran anasikia baada ya upasuaji wa awali ambao ulimsaidia kupandikiza kifaa kinachomsaidia kupaza sauti ndani ya masikio yake.

 "Ningependa watu wakome kuniuliza kwanini unakaa tofauti hivi ", alisema Kieran akiwa katika mtaa wa Hertfordshire.
 "nimefurahishwa sana kufanana na marafiki zangu ''.
 "Hata mimi ninafurahi kuwa sasa nitaweza kuvaa miwani na vifaa vya kusikizia muziki."

 Mamake Kieran ,Louise Sorkin alisema kuwa kijana huyo ni mchangamfu sana na alikuwa anasubiri kwa hamu kufanyiwa upasuaji wa kupandikiza masikio hayo.

 "Sikuwa nafurahiwa watoto wenzake wakimkejeli kutokana na maumbile yake."

 Asubuhi ya siku ya upasuaji huo Neil Bulstrode aliumba masikio hayo na akapandikiza akitumia teknolojia ya kisasa ya kushona masikio hayo chini ya ngozi ya kichwa chake .

 Wanasayansi hao wanasema kuwa walitumia mbinu mpya ya kukuza viungo hivyo.
 Kieran alifurahishwa sana alipooeshwa masikio yake mapya siku tatu baada ya operesheni hiyo.
        via>> bbc swahili

SOMA HII NI MUHIMU KWAKO KUJUA NCHI INAKOKWENDA

TAARIFA KWA UMMA: UKAWA KUANDAMANA NCHI NZIMA

Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wanaunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).MCHAKATO WA KATIBA MPYA NA YANAYOENDELEA BUNGE MAALUM LA KATIBA
Ndugu wanahabari

Sote tunaelewa kuwa kwa matakwa ya CCM, Bunge Maalum la Katiba (BMK) limeendelea kufanya vikao vyake mjini Dodoma kuanzia Agosti 5 mwaka huu, kinyume kabisa na matarajio ya Watanzania, ambao kupitia fursa mbalimbali wamepaza sauti zao wakisisitiza maridhiano na mwafaka wa kitaifa kutangulizwa mbele badala ya maslahi ya watawala.
Tukiwa viongozi wa kisiasa ambao ni sehemu ya uongozi ndani ya jamii, wenye wajibu wa kuwa na maono chanya na muhimu kwa taifa letu, tumeendelea kufuatilia kwa karibu namna mchakato wa Katiba Mpya unavyoendelea kunajisiwa kupitia vikao hivyo vya BMK linaloendelea mjini Dodoma, likitumia rasilimali za taifa, zikiwemo kodi za Watanzania wanyonge, kujadili vitu visivyotokana na wananchi.



Mtu yeyote makini ataweza kubaini kuwa kwa namna mchakato wa Katiba Mpya unavyopelekwa au unavyokwenda kwa sasa ni matokeo ya kukosekana kwa uongozi wa kisiasa kwa Chama kinachoongoza Serikali, CCM.



Kuna ombwe kubwa la uongozi wa kisiasa katika jambo hili. Ni kama vile mchakato unajiendea tu wenyewe bila mwongozo wowote kutoka kwa watu walioko madarakani ambao wananchi walitarajia wangetumia mamlaka yao ya dhamana ya uongozi ili taifa lipite salama katika wakati huu mgumu na tupate Katiba Mpya na bora.



Vipo viashiria vingi tu vinavyoweka wazi hali hiyo ya ombwe la uongozi wa kisiasa katika mchakato huu wa kisiasa, ikiwa ni pamoja na kauli kinzani za viongozi wa Serikali na CCM yenyewe. 
Wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda akizungumza kama vile kunahitajika mazungumzo zaidi na kwamba suala la muundo wa serikali lilipaswa kupigiwa kura kabla, Mwenyekiti wa BMK anaendelea kuongoza bunge kama vile mchakato ni mali binafsi ya CCM na walioko madarakani.



Wakati baadhi ya viongozi wa Serikali ya CCM wakitoa kauli za kuhitaji kuwa makini na taratibu za kuendesha mchakato huu chama chao kinatoa kauli za kuzidi kuharamisha na kutia najisi mchakato mzima. Mchakato unakwama, nchi inayumba, Watanzania wako katika sintofahamu kwa sababu tu tumekosa uongozi wa kisiasa katika jambo hili.



Kiashiria kingine cha pengo hilo la uongozi wa kisiasa ambacho kwa kweli kwetu sisi kimetusikitisha zaidi kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kuendelea na ‘hamsini zake’ kama vile nchi haina tatizo lolote. 



Yaani wakati nchi na wananchi wako katika sintofahamu ya hatma ya Katiba Mpya itakayoweka misingi ya wao kujitawala na kuongozwa watakavyo, makundi mbalimbali yakipaza sauti zao, mataifa mengine yakituangalia kwa makini na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi wakifuatilia mchakato, Rais Kikwete anapata muda wa kutembelea ranch ya Rais Mstaafu wa Marekani George Bush! 



Wakati Rais Kikwete akiendelea kutalii dunia, wenzake wako mjini Dodoma wakichukua posho kwa kazi ambayo wananchi hawajui wanaifanya kwa maslahi ya nani!



Kwa ujumla mambo yote yanayoendelea sasa katika mchakato huu ni matokeo ya ombwe hilo kama tulivyosema. 



Inaonesha kuwa CCM wamelewa madaraka na viongozi wanaona dhamana ya uongozi iko juu ya wananchi hivyo hawajali umuhimu na nafasi ya mamlaka ya wananchi katika kuamua mstakabali wa taifa lao kwa ajili ya kizazi cha sasa na kuweka msingi wa vizazi vingi vijavyo.
Hivyo leo tungependa kuzungumza tena kuhusu Rasimu ya Katiba na mchakato wenyewe hapa ulipokwama;



Tunapenda kusema wazi kuwa tumeshangazwa sana na kitendo cha CCM na Serikali yake kulazimisha kuendelea kwa Bunge Maalum la Katiba Mpya, tena kwa mtindo ule ule wa kunajisi na kupuuza maoni ya wananchi yaliyomo kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya kama yalivyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.



Wamefanya hivyo pasi na kujali kilio cha wananchi kinachopazwa kutoka kila kona ya nchi, ambapo Watanzania mmoja mmoja na katika makundi mbalimbali wametaka maoni yao yazingatiwe kwa kujadiliwa, kuboreshwa na kisha kupitishwa na Bunge Maalum la Katiba kabla wao hawajayapigia kura ya maoni kwa ajili ya kuipitisha au kuikataa Rasimu ya Katiba Mpya.



Wajumbe wanaotokana na CCM pamoja na makada wengine wapatao 166 wa chama hicho ambao waliteuliwa kuingia kwenye bunge hilo kusimamia maslahi ya CCM kupitia kundi la wajumbe 201, wameamua bila haya mbele ya umma si tu kupuuza rasimu iliyotokana na maoni ya wananchi bali sasa wameamua kuingiza mambo yao waliyodhamiria tangu mwanzo kwa kadri ya maamuzi na maelekezo ya vikao vya chama hicho vikiongozwa na Mwenyekiti wao Jakaya Kikwete.



Bila kujali wala kuguswa na miito ya Watanzania mbalimbali wanaotaka jambo hili liongozwe na maridhiano kwa ajili ya mwafaka wa kitaifa badala ya kuweka matamanio ya watawala mbele, CCM na mawakala wao katika mchakato huu wameendelea pia kufuja na kutumia vibaya fedha za wananchi kupitia Bunge Maalum la Katiba kwa kujadili na kuingiza vitu visivyokuwemo au visiyotakiwa kuwa sehemu ya rasimu hii iliyopo sasa.



Hali hiyo imefanyika kwa namna kadhaa ikiwa ni pamoja na kutofuata sheria inayosimamia mchakato mzima, kubadili kanuni za uendeshaji wa BMK hasa katika taratibu za kujadili na kupitisha ibara na kubwa zaidi kuingiza masuala ya Tanganyika kwenye Rasimu ya Katiba ya Muungano.



Kimsingi masuala wanayoyajadili na kuyachomeka kinyemela kwenye Rasimu ya Pili ya Warioba, mathalan masuala ya Ardhi, Elimu, Maji, Kilimo, Uvuvi, Mifugo, Serikali za Mitaa nk ni masuala yanayopaswa kuandikwa kwa kina ndani ya Katiba ya Tanganyika na siyo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.



Ni vyema kukumbuka kuwa Zanzibar walijadili wenyewe mambo Yao ya Ndani na kutengeneza Katiba yao na hatuoni mantiki ya kuruhusu Wajumbe toka Zanzibar kujadili na kuamua mambo ya Tanganyika. BMK haina Sifa ya kujadili yasiyo ya Muungano.



Hivyo tofauti na wanavyotaka kujionesha katika jamii, CCM kupitia BMK wameamua kupindua kabisa rasimu nzima na kuweka maazimio ya vikao vyao kuwa ndiyo Katiba ya Tanzania. Jambo hili haliwezi kukubalika.



Kutokana na uchakachuaji huo wa Katiba Mpya unaoendelea kufanywa na CCM kupitia BMK, UKAWA tumefikia maamuzi yafuatayo;



· Tunamtaka Rais Jakaya Kikwete asitishe shughuli za BMK mara moja lisiendelee kuvuruga
na kuharibu mchakato wa Katiba Mpya na kuiweka nchi katika sintofahamu juu ya jambo hili
nyeti;
· Tunamtaka Rais Kikwete asitishe BMK ili lisiendelee kufuja fedha za Watanzania maskini
wanaopigania Katiba Mpya iwapatie matumaini ya kuongozwa na kujitawala wanavyotaka.



· Tunamtaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalum
kwenye matumizi ya fedha za BMK ambayo kuanzia Bunge la Bajeti lililopita tumebainisha
wazi kuwa yana uvundo mkubwa wa ufisadi na hayana maelezo sahihi.



· Iwapo Rais Kikwete atashindwa kutumia mamlaka yake kusitisha BMK na hivyo likaendelea
kinyume cha matakwa na maslahi ya wananchi kama lilivyofanya awali na linavyofanya sasa,
UKAWA tutawaongoza Watanzania kupaza sauti zaidi kupinga najisi inayotiwa kwenye maoni
yao, kupitia maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima.




Asanteni kwa kutusikiliza.




Prof. Ibrahim Haruna Lipumba
Mwenyekiti CUF




Freeman Aikaeli Mbowe
Mwenyekiti CHADEMA




James Francis Mbatia
Mwenyekiti NCCR Mageuzi




Wilbrod Peter Slaa
Kny Makatibu Wakuu, UKAWA.

BINTI MREMBO WA KAGAME ALIYEUZA SANA SURA MITANDAONI NI MJEDA


 
 





WATANZANIA TUMEFIKIA HAPA SASA DUUU

KAMATI YA WAZIRI WASSIRA YABARIKI ADHABU YA KIFO TANZANIA

WASIRA
LICHA ya sheria ya kunyonga kupigiwa kelele na jumuiya za kimataifa, wajumbe wa kamati namba sita ya Bunge Maalumu la Katiba wamependekeza iendelee kutumika nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma jana, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Steven Wassira, alisema hali hiyo ilijitokeza wakati wa kujadili Sura ya nne ya Rasimu ya Katiba.
“Wapo baadhi ya wajumbe walitaka adhabu ya kifo ifutwe, lakini wengi walipendekeza  adhabu hiyo iendelee, ingawa katika miaka ya hivi karibuni adhabu hiyo imekuwa ngumu kutekelezeka,” alisema.
Kwa upande wa suala la uraia wa nchi mbili, alisema wameliacha kiporo kutokana na kuwepo kwa mvutano miongoni mwa wajumbe.
Alisema kutokana na hali hiyo, kamati hiyo iliiacha kiporo sura hiyo na kuendelea kujadili sura nyingine.
“Kamati yetu hadi sasa imejadili sura ya pili, ya tatu na ya nne, Sura ya tano tuliiacha kiporo, hasa katika suala la uraia pacha,” alisema.
Alisema suala hilo halikufikia mwisho kutokana na kuwa na mjadala mkubwa kutokana na wajumbe kugawanyika na kwamba hata hivyo, suala hilo litapigiwa kura ili kupatiwa majibu.

“Maeneo mengi katika kamati yetu tumekubaliana, lakini yapo maeneo machache ambayo tunatofautiana,” alisema Wassira.
Alisema pamoja na kujadili sura hizo, kamati yake bado haijapiga kura kupitisha ibara za sura hizo ambayo kwa mujibu wa sheria inahitajika theluthi mbili ya wajumbe wote wakati wa kupitisha maamuzi.
Wassira alisisitiza kwamba Bunge la Katiba litaendelea na vikao vyake kama kawaida vya kutunga Katiba.
“Bunge hili haliwezi kuvunjwa kwa sababu watu wachache hawapo, kama ambavyo mnaona tunaendelea na vikao vyetu kama kawaida,” alisema.

NDOA YA MSANII LADY JAYDEE, GARDNER YADAIWA KUVUNJIKA!



Ndoa ya mwanamuziki Judith Wambura maarufu Lady Jaydee na mtangazaji mashuhuri wa radio Gardner G. Habash inasemekana imevunjika huku Gardner akihama Kimara alikokuwa akiishi na mkewe na kuhamia kwa mmoja wa ndugu zake wa karibu sana.
Chanzo cha kuvunjika ndoa hiyo bado hakijajulikana moja moja kwa moja ila wawili hao wamekuwa katika migogoro kwa muda sasa. Hii inaeelezwa kwamba siyo mara ya kwanza kutengana, lakini safari hii mambo yanaonekana kuwa magumu zaidi. 
Katika ukurasa wake wa Instgram, Jaydee ameandika: "Walking Away From Troubles" ambapo uchunguzi unaonyesha kwamba mambo si sawa hata kidogo.

Gardner kabla ya kumuoa Jide alikuwa tayari na mke halali wa ndoa na mtoto mmoja.

HIVI KUMBE HUWA YANATOKEA EEEEEEE!!!!!!!!!!!!!!

 
hizi ni picha za moja ya fumanizi iliyokuwa ya kushangaza sana kuliko ulizowahi kuona kama si kusikia pia. Daktari na mgojwa wake wafumaniwa wodini wakuvunja moja ya amri ya Mungu.  Si ajabu sana ukaona waimbaji na waigizaji wakionyesha ama kuimba kitu na kudhani ya kuwa kimetungwa vihwani mwao hivi vitu vipo. Bahati Bukuku mwimbaji wa nyimbo za injili alionyesha ya kuwa amepata mtoto baada ya kutembea na daktari ili mumewe atibiwe. sasa hii ni kali yaweza kuwa mgonjwa alikosa pesa ya kulipia gharama za matibabu. I hate sex bribe. wanawake wengi huwa wanakutana na majanga kama haya isipokuwa tuu wanashindwa kuwa wawazi lakini ikifanyika sensa na wakaamua kusema duuuuuuuu ni hatari
Binti akijaribu kujificha chini ya kitanda

Hivi ikitokea katika kuperuzi unakutana na picha kama hizi mtandaoni harafu muhusika ni ndugu yako, mkeo, jirani yako, ama vingine tuuu unajisikiaje? Huu ni udharirishaji sana. Hata kama mtu umemfumania si lazima uumlazimishe kupiga picha kama hivi tena eti kwa kumshika kwa nguvu na cha ajabuu wanadeal na mwanamke tuuu mwanaume aaaah wanafanya kumsitiri ili asidharirike. mwanamke aonekane. TGNP na wanaharakati wakipiga kelele mwajisikia vibaya.

BILL GATES ATUMIA MAMILIONI YA PESA

Katika boti hiyo helikopta zinamchukua Gates kumpeleke nchi kavu kucheza golf na kumrudisha Ni tajiri namba moja duniani mwenye utajiri unaofikia dola bilioni 79.2 hivyo kutumia shilingi bilioni nane kwa wiki si kitu kinachoweza kumpunguzia chochote Bill Gates. Na ndio maana Bill Gates yupo mapumzikoni ambayo tunategemea kwa mtu tajiri zaidi duniani ayafanye. Tajiri huyo amekodi meli binafsi maarufu yacht ambayo analipa dola milioni 5 (zaidi ya shilingi bilioni 8) kwa wiki.
  The Serene Gates yupo kwenye boti hiyo kubwa na mke wake Melinda na watoto wake Rory, Jennifer na Phoebe nchini Italia. Mwanzilishi huyo wa Microsoft ameamua kupumzika kwa kukodi yacht hiyo iitwayo The Serene yenye ukubwa wa futi 436 inayomilikiwa Yuri Scheffler.
Muonekano wa sehemu moja wapo ya ndani

KIBAKA AUWAWA KWA KUCHOMWA MOTO

 

Kijana ambaye jina lake na sehemu anayoishi haikufahamika mara moja ameuwawa kikatili kwa kuchomwa na moto na wananchi wenye hasira akidaiwa kuiba pikipiki maeneo ya katikati ya mji wa Morogoro.     
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo walisema pikipiki zaidi ya 20 zilikuwa zimeongozana na mojawapo ikiwa imembeba kijana huyo akiwa amefungwa kamba miguuni na mikononi huku nyingine ikiwa imebeba dumu la mafuta na kiroba cha majani makavu. "walipofika hapa walimlazimisha ashuke huku wakimpiga na aliposhuka walimuwashia moto juu yake mpaka waloporidhika ya kuwa kafa ndipo walipowasha pikipiki zao kwa mbwembwe na kuondoka"
mmoja wa mabodaboda haoalisema kuwa kibaka huyo walimkamata akitaka kupora pikipiki kwa bodaboda mwenzao ndipo walipo mtia mikononi na waliamua kumfanyia hivyo kwa kuwa wakipelekwa polisi wanaachiwa kwa dhamana na kuendeleza uhalifu wao mtaani hivyo waliamua kufana hivyo kama fundisho kwa vibaka wengine waache tabia mbaya



Baadhi ya mashuhuda wakitazama mwili wa kibaka aliyeuawa kwa kuchomwa moto baada ya kukutwa akipora pikipiki

MAMA TUNU PINDA BALOZI WA AMANI DUNIANI


205026
Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda  akiwa na Rais wa Universal Peace Federation (UPF), Dk. Thomas Walsh (kushoto) na Mwenyekiti wa UPF, Dk. Charles Yang mara baada ya kutunukiwa cheti cha kumtambua kama Balozi wa Amani Duniani katika hafla ya kufunga Mkutano wa Dunia kuhusu Amanina Usalama uliomalizika jana usiku (Agosti 12, 2014) jijini Seoul, KoreaKusini. (PICHA NA IRENE BWIRE WA OWM).

205215
Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda  (wa pili kulia mstari wa mbele) katika picha ya pamoja viongozi wenzake 10 waliotunukiwa vyeti vya kuwatambua kama Mabalozi wa Amani Duniani katika hafla ya kufunga Mkutano wa Dunia kuhusu Amani na Usalama uliomalizika jana usiku (Agosti 12, 2014) jijini Seoul, Korea Kusini. (PICHA NA IRENE BWIRE WA OWM).
205257
  Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda  (wa pili kulia mstari wa mbele) katika picha ya pamoja viongozi wengine waliotunukiwa vyeti vya kuwatambua kama Mabalozi wa Amani Duniani katika hafla ya kufunga Mkutano wa Dunia kuhusu Amani na Usalama uliomalizika jana usiku (Agosti 12, 2014) jijini Seoul, Korea Kusini. Walioshika vyeti kutoka kushoto ni Mke wa Rais wa visiwa vya Samoa, Bibi Filifilia Tamasese , Mke wa Rais wa visiwa vya Marshall, Bibi Lieom Anono Loeak na Mke wa Rais wa Fiji, Bibi Koila Nailatikau. (PICHA NA IRENE BWIRE WA OWM).