Monday, May 2, 2016

VIJANA WAFUNGUKA MACHO KUHUSU KILIMO CHA MBOGA MBOGA NA MATUNDA





Japokuwa awamu ya tano ya uongozi wa Raisi John Pombe Magufuli umefanya mabadiriko mengi yanayokonga nyoyo za watanzania wengi bado kilimo kimebakia kuwa uti wa mgongo wa uchumiTanzania.
 
Hata hivyo mpaka sasa hajafanikiwa kuufuta usemi huu ambao umekuwa ukibakia kama ulivyo na ndivyo ilivyo kuwa kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania, kikichangia takribani nusu ya Pato zima la Taifa na robo tatu ya bidhaa zote zinazouzwa nje ya nchi. Pamoja na kuzalisha chakula, kilimo vilevile kinatoa ajira kwa asilimia 80 ya Watanzania. 

Sehemu kubwa ya kilimo Tanzania ni cha wakulima wadogo-wadogo (small-holder farmers) ambao wengi wao hawatumii njia za kisasa na wengine mpaka leo hawajawahi hata kuzijua.
Takwimu za Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, zinaonyesha kuwa Tanzania, wakulima wake hulima hekta milioni 5.1 nchi nzima kila mwaka, na kati ya hizo asimilia 85 ni kwa ajili ya mazao ya chakula ikiwa ni pamoja na mazao ya mbogamboga na matunda, ambayo huzalishwa kwa wingi karibu katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani. 



Kilimo cha mboga na matunda kimekuwa maarufu nchini kwa sasa kutokana na kuongezeka kwa mahitaji katika soko la ndani na nje, kuongezeka elimu kwa wakulima na watumiaji, upatikanaji kwa urahisi wa pembejeo na uwezeshaji unaofanywa na serikali pamoja na taasisi binafsi.

 Mikoa ya Kanda ya Kaskazini Arusha, Manyara, na Kilimanjaro kilimo hiki kimeanza kuwavuta kwa kasi makundi ya vijana na wanawake ambao sasa ndio wanaonekana kukivalia njuga  kilimo hicho hasa kufuatia uelimishaji na uhamasishaji unaofanywa na Taasisi zinazojishughulisha na utafiti na uuzaji wa pembejeo zinazohusu kilimo hicho.

Rijk zwaani imekuwa mstari mbele katika kuwapatia wakulima mafunzo ya kilimo cha mboga na matunda, pia kuwaaunga mkono wakulima wote wanapata mafunzo kwao kwa kuhakikisha wanapata mazao bora na masoko ya uhakika ya ndani na nje ya nchi, pembejeo na madawa muhimu na ushauri wa kitalaamu unaotolewa na maafisa ugani wa shirika hilo. 

Mbali na shirika hilo pia AVRDC pia wamekuwa mstari wambele kuendeleza utafiti wa mbegu mbali mbalii za mbogamboga na kutoa elimu kwa makundi tofauti tofauti ya wakulima kuhusu kilimo bora cha mbogamboga na hata wakati mwingine kutoa mbegu bure kwa makundi hayo ili kuyawezesha makundi hayo.

Licha ya hivyo SEVIA pia ndio limekuwa shilika la kimbilio la wakulima baada ya wao kujidhatiti katika kutoa mafunzo yajinsi ya kulima kwa kutumia kilimo cha kisasa ambacho imeonekana ndio njia pekee ya mkulima kujikwamua kutoka katika kilimo kisicho na tija na kuwa kilimo cha tija.

Ally Materu (30) ambaye ni mkazi wa Moshi Mkoani Kilimanjaro, amekuwa akijishughulisha na kazi ya kupanda mlima na watalii bila kujua kuwa anaweza akafanya shughuli nyingine mpaka alipojiunga na kikundi cha “kijana jikwamue” ambao hivi karibuni walitembelea Rikj zwaani na kupata mafunzo ya kilimo ndipo alipotambua kuwa kuna fursa ambayo anaweza akaifanya na ikampatia kipato kikubwa kuliko hiyo aifanyayo. 

“Leo nimetambua ya kuwa nilikuwa najicheleweshea maendeleo yangu mwenyewe kwa ajiri ya kutegemeo upandaji mlima wakati kumbe kilimo kinaweza kikanitoa kirahisi nikidhamilia” alisema Ally. 

 Nae mwalimu Ole Lengai (29) mkazi wa kijiji cha Olkokola Mkoani Arusha ambaye alibainisha kuwa kilimo hicho kimekuwa “dawa” ya tatizo sugu la ajira nchini ambalo linawakabili vijana wengi. “Nilianza kilimo hiki miaka miwili iliyopita, baada ya kujifunza kwa kutembelea shamba darasa la AVRDC, kwa kweli kiuchumi hali yangu imebadilika sana kutokana na mazao ninayozalisha kama nyanya, na aina nyingine tofauti za mboga kuuzika kwa haraka na kuwepo kwa soko la uhakika hasa baada ya wanunuzi kujua ubora wa mazao yangu alisema Ole. 

“Vijana wengi wanalalamika kuwa hawana mitaji ya kuanzisha shughuli za kilimo, malalamiko yao hayana mantiki sana kwasababu vijana wengi wanamiliki vitu vya bei ya juu kama simu, laptop, nguo za thamani na wakati mwingine wanapatikana sehemu za starehe wakitumia pesa za kutosha kuanzisha mradi wa kilimo”Alisema Ally. 

Kwa mujibu wa Ole, kilimo cha mboga ni rahisi sana kwa sababu hakihitaji eneo kubwa la ardhi, na pia mazao ya aina hiyo hukomaa ndani ya mda mfupi na mkulima anakuwa ameshapata fedha za mauzo na kurudisha gharama zake. 

Akijitolea mfano yeye mwenyewe alisema alihamasika sana baada ya kutembelea shamba darasa na kuona vijana wanaolima pembezoni mwa shirika la AVDRC na kupata shuhuda kutoka kwao akaamua kukata shauri ya kuondokana na maisha ya kupoteza mda kwa kukaa vijiweni.
“Nilianza kwa kulima matuta mawili ya mnafu na baada ya kuuza na kupata faida ndipo nilipoamua kujidhatiti katika kilimo, hivi sasa nina shamba la hekari moja ambalo nililinunua mwenyewe baada ya kupata faida ya mboga mboga na sasa nalima nyanya, mnavu pamoja na kabichi ambapo kilimo hiki kimenifanya mda mwingi kuwa shambani mpaka naambiwa naringa baada ya kuacha kuhudhuria vijiweni nilikokuwa nikienda kupoteza mda wa mafanikio haya niliyonayo sasa” aliongeza Ole

Hata hivyo wakulima wote wanalalamikia sana changamoto ya mbegu feki madukani pamoja na miundo mbinu ya barabara zisizopitika kabisa kwa gari hivyo wengi kushindwa kufikisha mazao yao katika masoko kwa muda na hata wakati mwingine imekuwa kikwazo cha kuwafanya wateja wao kushindwa kuwafikia kiurahisi pale wanapohitaji bidhaa kutoka kwao, hivyo wanalazimika kila wakati kuwapelekea sokoni 

 “Kama unavyoona hali ya barabara ni mbaya sana, hasa wakati wa masika barabara hazipitiki kabisa na hii ni changamoto kubwa sana kwa sisi wakulima, gharama zinaongezeka na matokeo yake faida pia inapungua”alisema mmoja wakulima wa nyanya.
”Serikali imesahau maeneo ya wakulima ambayo yanazalisha mazao ya biashara na chakula, tumelalamikia hali hii kwa muda mrefu na hata viongozi wetu yaani madiiwani na wabunge wanajua ila hakuna hatua zilizochukuliwa”. Aliongeza mkulima huyo

 Nae Abel kuley wa Rijk zwaan anabainisha kuwa mipango ya taasisi hiyo ni kuwafikia wakulima wengi zaidi katika maeneo yote ambayo kilimo cha mboga na matunda kinaweza kufanyika.
 “Sasa tunaelekeza nguvu zetu katika maeneo yote ambayo kilimo kinaweza kufanyika, malengo yetu ni kuwahusisha zaidi vijana na wanawake ambao ndio waathirika wakubwa wa tatizo la ajira nchini na tunadhani kwamba sekta hii inaweza kuwa mkombozi wa tatizo la ajira na kupunguza umaskini,”alisema. 

Nae Fekadu Fufa Dinssa kutoka, mzalishaji wa mbegu (vegetable breeder) AVRDC alisema kwa kushirikiana na serikali wanaweza kupunguza kabisa tatizo la ajira kama si kulimaliza kabisa ikiwa bei za pembejeo zitapunguzwa ili kuwapa fursa wakulima wengi kupata nafasi ya kujihusisha na kilimo bora

 Kwa mujibu wa taarifa ya Gavana wa Benki ya Tanzania, ya mwaka 2014 sekta ya kilimo imeonekana kupigwa kikumbo na sekta za utalii, dhahabu, viwanda na usafirishaji wa mizigo nje ya nchi. Kwa mujibu wa takwimu hizo sekta ya utalii iliingizia Taifa dola za Marekani bilioni mbili, dhahabu dola bilioni 1.7, viwanda dola bilioni 1.3  na kilimo kinachoingiza dola milioni 830 kwa mwaka. Hata hivyo bado kilimo kimebakia kuwa uti wa mgongo wa uchumi Tanzania.

Monday, January 18, 2016

TEKNOLOGIA YAZIDI KUSONGA MBELE KATIKA KILIMO


Wakati Tanzania ikijivunia kuwa kilimo ndio uti wa mgongo wa uchumi, juhudi nyingi zinafanyika ili kuona msemo huu haupitwi na wakati na kuendelea kumfanya mkulima kunufaika na kile anachokifanya. Wataalamu na watafiti wanajitahidi kila kukicha kubuni kila njia kufanya kilimo cha Tanzania kinainuka kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine ili kufikia viwango vya kimataifa kama zilivyo nchi nyingine.

Rijk zwaan ikiwa ni kampuni ya uzalishaji mbegu za mboga mboga nchini, wameamua kutumia njia za kisasa kuwafundisha wakulima jinsi ya kutumia mbegu za kisasa kwa njia ya mitandao ya kijamii ya Whats App na Facebook ambapo wamekuwa wakiwahimiza wakulima kutumia kilimo cha green house ili kuepukana na hasara zingine ambazo zingeweza kuepukika kwa kutumia kilimo hicho. Na kwakutumia njia hiyo imewarahisishia wakulima kushare uzoefu na mtaalamu kila wakati wanapohitaji msaada.

Kwa njia ya mitandao ya jamii tumefanikiwa sana, kwani kwa sasa teknolokia imekwenda mbali sana kitu ambacho kinatusaidia sisi kukutana na wakulima hata kabla ya kuonana nao ana kwa ana, na tumekuwa tukijivunia ubunifu huu kwani tumeona mwitikio wa wakulima kupasahana habari kuhusu shirika letu na bidhaa zetu wao kwa wao. Alisema Bwana Abel Kuley, meneja uzalishaji na maendeleo wa Rijk zwaan
Baadhi ya mbegu zilizooteshwa tayari kwa kupelekwa shambani 


Wakati tunaanza kuuza mbegu, tulianza na wakulima ambao wana ardhi lakini hawajui kitu cha kufanya hivyo tulianza kuwaeleza faida ya kilimo cha mbogamboga na namna ya kulima kilimo bora hivyo wale walioanza walianza kidogo kidogo lakini kila aliyeanza hakuna aliyejilaumu kuwa alifanya makosa kuingia katika kilimo hiki kwa kuwa wengi walijutia kwa nini hawakuijua siri hii tangu awali. Aliongeza Bwana Abel


Naye Bwana Hearald Peeters Mkurugenzi Mtendaji wa Rijk zwaak alisema wao wanatoa huduma ya mbegu za kisasa za mbogamboga kwa wakulima wadogo wadogo na wakubwa pia. Lakini tumekubali kufanya shughuli hii sisi wenyewe  kwa kuwafikia wakulima moja kwa moja kwani tunajua kuwa wateja wetu wametofautiana maeneo yao ya kilimo kwa maana ya hali ya hewa, udongo, pamoja na magonjwa ya mimea kutokana na eneo husika, hivyo hatutaki kuwauzia wakulima mbegu kana kwamba wote wanatoka sehemu moja. Alisema 
Hearald Peeters akiwa katika shamba la nyanya ndani ya Rijk Zwaan

Kila wakati tunapopata mteja mpya huwa tunamuuzia mbegu zetu lakini huwa hatumuachi hivyo hivyo kwani huwa tunamfundisha mfumo mzima wa jinsi ya kuzilima na kuzihudumia mpaka atakapovuna. Hata hivyo huwa hatumuuachii mkulima kuuza mwenyewe hivyo huwa tunatafuta masoko kwa ajilli yake japo wakulima wetu huwa wanapata wateja kabla hata hawajavuna, hivyo huwa tunapenda kumuhudumia mteja wetu na kumuacha akiwa na furaha na kwa mtindo huu wamekuwa wakipashana habari na kuongeza kasi ya kutumia mbegu zetu na kwa kufanya hivi wakulima wengi wamekuwa wataalamu wa kilimo hiki kwani huwa wanajifunza kwa vitendo kwa kusaidiana na wataalamu wa Rijk zwaan. Alisema Bwana Hearald


Hata hivyo Rijk zwaani wanawasihi wateja wao kuwa hakuna kampuni ya usambazaji wa mbegu waliyoingia nayo mkataba kwa kuuza mbegu zao kwakuwa wao wanatoa huduma ya uuzaji wao wenyewe ili kuhakikisha mkulima anapata mbegu halisi kutoka kwao

Nae Enock Nanyaro mkulima wa kikundi cha parokia ya familiaTakatifu, Njiro mkoani Arusha amesema tangu aanze kutumia mbegu za Rijki zwaan hajawahi kujuta kwani mafunzo aliyoyapata baada ya kununua mbegu zao yalimfanya kuvuna mazao mengi kuliko miaka yote aliyowahi kulima.
“Nawashukuru sana watu wa kampuni ya……. Maana wao ndiowaliotupeleka Rijk zwaan na kutukutanisha na wazalishaji wa mbegu hizi ambazo ndio nazitumia mpaka leo hii.  Sikuwhi kuwaza kuwa ipo siku moja nitakuwa mtaalamu wa kilimo cha kisasa lakini sasa Rijk zwaan wamenifikisha hapa nilipo leo alisema Bwana Enock



Enock Nanyaro akionyesha mmea uliooteshwa miaka miwili nyuma na bado unazaa matunda bora na yenye afya ikiwa ni mmoja ya mmea wa mfano ambao huutumia kuwaonyesha wakulima wenzake ambao humtembelea ikiwa yeye huita ni maajabu ya mbegu za Rikjzwaan. 


Renalda mlay wa Shant Town mjini Moshi Kirimanjaro, alikiri kuwa hakuwa na ndoto ya kuwa na shamba nyumbani kwake kutokana na eneo alilonalo, lakini mafunzo aliyoyapata kupitia Rijki zwaan aligundua ya kuwa anaweza akalima mboga mboga katika eneo alilonalo nyumbani na akapata faida kitu ambacho anakifanya sasa.

“Mimi nalima pilipili na nyanya kwenye green house nyumbani kwangu na ninapata faida mpaka watu wananishangaa. Nimeifanya hii ni ajira yangu baada ya kuacha kazi ya benki kwani kiwango cha pesa ninachozalisha kwa hili shamba ni zaidi ya mishahara ya baadhi ya watu wanayopata makazini.” Bi Renalda alisema

“Nikianza kueleza uzuri wa mbegu hizi unaweza ukaacha kazi na kuwa mkulima, kwani ukinunua mbegu za hii kampuni na kuziweka shambani hakuna hata moja ambayo haitaota,na uzaaji wake ni maajabu sana.” Alisema Bwana Deo Ryoba wa Moshono, Arusha
Bwana Ole Ngao yeye ni afisa kilimo wilayani simanjiro alisema kuwa wakulima wasilaumu kuhusu uzalishaji duni wa mbegu za kisasa tofauti na vile zinavyosifiwa isipo kuwa wanapasa kuilaumu serikali kwani ndio iliyoshindwa kutoa elimu ya kilimo kwa wananchi wake. Pia alisema kuwa wananchi wengi hawazingatii kile wanachoshauliwa na wataalamu wa kilimo kuhusu kilimo cha kisasa.

“zipo teknolojia nyingi sana ambazo zinatumika sasa katika kilimo, hali ya hewa na mabadiriko katika udongo yanayotokana na matumizi yamda mrefu kwa  kilimo yanamlazimu mkulima kuenenda na sayansi na teknolojia ili kupta faida katika kilimo” alisema Ole
 Hili ni jambo la kujifunza kuwa elimu kwa mkulima yaweza kutolewa hata kwa mitandao ya kijamii. Ipo  haja ya mkulima kubadiri mfumo katika kilimo kwani kwa hali ya sasa teknolojia inatumika kila mahali.

Pia serikali yetu ni lazima iunge mkono teknolojia ya kisasa katika kilimo kwani kumuhubilia mkulima kuhusu mabadiriko ya hali ya hewa bila kumwambia njia sahihi ya kuikabili ni kazi bure.
Hivyo basi ipo haja ya serikali kuitazama sera kwa jicho la tatu ili kuondoa zile sharia zinazowabana watafiti wa kilimo katika kukuza teknolojia katika kilimo Tanzania.

Rijk zwaani ni kampuni ya utafiti na uzalishaji mbegu za mbogamboga iliyopo Usa mkoani Arusha, iliyoanzishwa mwaka 2008  na nia ya kuanzishwa kwa kampuni hii ni kuboresha begu za mbogamboga ili kukuza kipato kwa mkulima wa kawaida kwa kushirikiana na mashirika mengine ya kilimo hapa nchini ikiwa ni SEVIA, AVRDC, TAHA na wakulima wenyewe.

Kwa kuhakikisha wanafikia malengo yao wamekuwa wakifanya mafunzo kwa vikundi vya wakulima pamoja na kushiriki katika maonyesho ya wakulima yanayofanyika kila mwaka hapa nchini na hata kushiriki maonyesho kama hayo yanayoandaliwa na baadhi ya wadau wa kilimo nchini.

Hearald Peeters akifafanua teknolojia mpya ya kilimo kifaacho kwa watu wasio na ardhi kwa waandishi wa habari walipotembelea Rijk zwaan Arusha








Sunday, July 12, 2015

RAIS KIKWETE AMSHUKURU ALLAH KWA MCHAKATO KWENDA SALAMA BILA MPASUKO.



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimempitisha Dk. John Pombe Magufuli kuwa mgombea urais kupitia chama hicho. Katika Mkutano Mkuu uliofanyika usiku wa kuamkia leo mjini Dodoma, Dk. Magufuli amechaguliwa kwa kura 1560 akifuatiwa na Asha-Rose Migiro aliyepata kura 702 huku Balozi Amina Salum Ali akipata kura 349.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya kikao hicho, Dk. Magufuli amepita kwa kura hizo kutokana na nguvu yake dhidi ya wagombea wengine.
“Hakukuwa na namna hapa kwa kuwa, wajumbe wanaamini katika mazingira haya magumu ya upinzani Dk. Magufuli anaaminika na kukubalika nje kuliko hawa wengine,” anasema mtoa taarifa na kuongeza;
“Baada ya kutemwa Membe (Bernard Membe) kwenye NEC kila mjumbe ambaye alikuwa upande wa Lowassa (Edward Lowassa) alipumua jambo lililomrahisishia Magufuli.”
Mkutano huo umehairishwa mpaka saa nne asubuhi, ambapo ndiyo muda ambao Dk. Magufuli ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Mashariki na Waziri wa Ujenzi atatangazwa rasmi kuwa mgombea wa Urais kupitia chama hicho.
Awali ndani ya ukumbi wa mkutano, kulidawa kuwepo kwa mpango wa wafuasi wa Lowassa kutaka kumpitisha Balozi Amina ili chama hicho kipate changamoto katika ‘kumuuza’ kwa wananchi ikiwa ni kulipiza kisasi kwa kukatwa mtu wao (Lowassa).
Katika Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya chama hicho, majina yaliyopitishwa yalikiwa ni Migiro, Magufuli, Balozi Amina, Membe na January Makamba.
Katika Halmashauri Kuu ya CCM yalipita majina matatu ya Dk. Magufuli, Dk. Migiro na Balozi Amina.



WAKATI CHAMA TAWALA WAKIFANYA UTEUZI, UKAWA WASHIRIKI FUTARI YA PAMOJA


  • Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Willibroad Slaa akishiriki futari iliyoandaliwa na Ofisi ya Kambi ya Upinzani Bungeni wakati wa kikao cha Viongozi Wakuu wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na wabunge wa umoja huo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam kujadili mikakati mbalimbali ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu. Kushoto kwake ni Mbunge wa CUF, Ali Khamis Seif (Mkoani) na kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa NLD Zanzibar, Ahmad Hemed.
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe akijadiliana jambo na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, Said Issa Mohamed (katikati) pamoja na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Ndelakindo Kessy (kushoto) huku wakishiriki futari iliyoandaliwa na Ofisi ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni wakati wa kikao cha Viongozi Wakuu wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na wabunge wa vyama vinavyounda umoja huo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam kujadili mikakati mbalimbali ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu.
Baadhi ya Wabunge wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kutoka kushoto, Naomi Kaihula (Viti Maalum CHADEMA), Salum Baruan (CUF- Lindi Mjini) na Mohamed Habib Mnyaa wakishiriki futari iliyoandaliwa jana jijini Dar es Salaam na Ofisi ya Kambi ya Upinzani Bungeni, wakati wabunge wa vyama vinavyounda umoja huo waliposhiriki kikao cha Viongozi Wakuu wa UKAWA (Summit) kilichojadili mikakati mbalimbali ya maandalizi ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu.(VICTOR)
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar Said Issa Mohamed akiwamiminia uji baadhi ya wabunge wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) wakati wa kula futari. Wabunge hao walikuwa wakihudhuria kikao cha Viongozi Wakuu wa UKAWA kilichofanyika juzi jijini Dar es Salaam kujadili mikakati mbalimbali ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu. Walioketi kutoka kushoto ni Seleman Bungala Bwege (CUF- Kilwa Kusini),Mohamed Habib Mnyaa (CUF-Mkanyageni) na Mama Riziki.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar Said Issa Mohamed akiwamiminia uji baadhi ya wabunge wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) wakati wa kula futari. Wabunge hao walikuwa wakihudhuria kikao cha Vioingozi Wakuu wa UKAWA kilichofanyika juzi jijini Dar es Salaam kujadili mikakati mbalimbali ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu. Walioketi kutoka kushoto ni Seleman Bungala Bwege (CUF- Kilwa Kusini) na Mohamed Habib Mnyaa (CUF-Mkanyageni).

MZEE KINGUNGE ATOA YAKE YA MOYONI MJINI DODOMA



MWANASIASA mkongwe nchini, mzee Kingunge Ngombale Mwiru, amekionya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutofanya dhihaka ya kumpendekeza kada yoyote kuwa mgombea wake wa urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, kwani kwa kufanya hivyo kitaanguka.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma Jumatano Julai 8, 2015, Kingunge ambaye ameshawahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini na ndani ya chama hicho alisema “ninatishwa na watu wanaotumia nguvu nyingi kwelikweli kupambana wenyewe kwa wenyewe ndani ya chama, badala ya kuelekeza nguvu hizo kupambana na wapinzani wetu, hii ni hatari.’, alionya
Amesema, CCM ni lazima ifuate katiba yake ili wajumbe wanaotarajiwa kutoa maamuzi watoe maamuzi sahihi na sio kupindisha katiba kwa kuanzisha utaratibu ambao sio utamaduni wa kidemokrasia.
“kuna kiongozi mmoja anasema, kada yeyote wa chama hicho aliyeomba kuteuliwa kuwania urais, endapo jina lake litakatwa hatakuwa na nafasi ya kukata rufaa, hii haijawahi kutokea na wala haipo kwenye katiba yetu.’ Amesema Mzee Kingunge.
"CCM lazima imteue mtu anayekubalika ndani na nje ya chama ili chama kiweze kushinda, kinyume na hapo, hii ni njama ya kukifanya kishindwe kwenye uchaguzi".

Hivi karibuni Katibu wa Halmashauri Kuu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, aliwaambia waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa hakutakuwa na nafasi ya kada wa chama hicho atakayeenguliwa kwenye mchujo kuweza kukata rufaa, kwani hakuna kanuni inayoelekeza kufanya hivyo.

Hata hivyo Kingunge amepinga kauli hiyo na kusema, inakwenda kinyume cha katiba ya CCM ambayo inaweka bayana kuwa maamuzi ya vikao vya chini yanaweza kukataliwa na vikao vya juu ikiwa ni pamoja na mwanachama ambaye anaona hakutendewa haki kuwa na nafasi ya kupinga uamuzi wa vikao vya chini.

Saturday, July 11, 2015

RESTLESS YAWAONYESHA NJIA YA KUPITA VIJANA



WENGI WAABADILI MTAZAMO WA URAIA

Vijana wakifuatilia kwa makini mafunzo

Vijana wengi wamekuwa walalamikaji wa mambo na wala si watendaji wa mambo wanayolalamikia, wakati huohuo vijana ndio nguvu kazi katika maendeleo ya jamii lakini si washiriki wa kuleta maendeleo hayo. 

Hayo yalisemwa na Kefar Mbogela ambaye ni mratibu msaidizi wa mradi wa Fahamu Ongea Sikiliza (FOS) ambao upo chini ya taasisi ya Restless Development nchini. Ambapo alisema lengo ni kutengeneza jamii bora ya vijana na kufanya vijana kuwa vioongozi bora katika jamii na wanakuwa wafanya maamuzi katika jamii.

Mradi wa Fahamu Ongea Sikilizwa unalenga kuwahamasisha, kuwaelimisha na kuwafanya vijana kushiriki katika shughuli za kiraia na hasa katika mchakato wa uchaguzi mkuu Tanzania. “Mraadi huu unawataka vijana wajitokeze kushiriki kwa wingi kujiandikisha, kupiga kura na kugombea kwani ni haki ya kila mtanzania mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea kwani kijana huyo  ana sifa za kupiga kura na kugombea pia. Alisema  Kefar

Akiongea kwa hamasa alisema kuwa vijana wengi wamekuwa hawashiriki katika shughuli za kimaendeleo kitu ambacho kimewafanya vijana hao kujinyima haki ya kimaendeleo kwa kutoshiriki kwao. “matatizo ya vijana wanayajua vijana wenyewe  na mengi yanaweza kutatuliwa na vijana wenyewe iwapo vijana wataashiriki kikamilifu katika nafasi za kuleta maendeleo kwani wao ndio nguvu kazi inayotegemewa katika kuleta maendeleo kuliko makundi mengine ya watu.  



Pia alisema ni vyema vijana wakawajibika kuyatimiza majukumu yao wenyewe badala ya kuendelea kuilaumu serikali huku wakiwa hawajitokezi katika shughuli za kiserikali wakidhani ya kuwa ni jukumu la serikali kufanya majukumu kwa ajiri ya vijana kitu ambacho ni kujidanganya na kuendelea kujicheleweshea maendeleo.

Wakati wa mafunzo hayo vijana walielezwa umuhimu wa vijana kushiriki katika kupanga maendeleo  kuanzia katika ngazi ya mtaa mpaka serikali kiujumla ili kuondoa dhana ya kuwaona vijana ni watu wasiofaa katika jamii kama ilivyo hivi sasa. Hivyo aliwasihi vijana hao kushiriki kikamilifu katika mchakato mzima wa kujiandikisha na kupiga kura kwa kuchagua viongozi sahihi.

Nae Bwana Abdul Lukanza ambaye ni afisa uhusiano wa vijana alieleza umuhimu wa nafasi ya vijana katika demokrasia kitu ambacho kiliamsha hisia za vijana wengi na kufanya maswali mengi kujitokeza miongoni mwa vijana hao.

Hata hivyo kitendo hicho kilitoa fursa kwa  Bwana Abdul kuelezea sifa na faida za demokrasia na kuwasihi vijana hao kufikisha elimu waliyoipata kwa vijana wengine ili Kuongeza uwezo na motisha kwa vijana kushiri katika mchakato wakujiandikisha, kupiga kura na kugombea nyadhifa mbalimbali, Kukuza ufahamu wa viongozi katika kazi na ni majukumu yao kuwasaidia wananchi kushiriki kikamilifu katika chaguzi zijazo.

Mafunzo hayo ambayo yalishirikisha vijana zaidi ya 50 kutoka mikoa ya Tanga, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Shinyanga yalifanyika mkoani Kilimanjaro, yaliwaacha vijana kuwa na hamu kubwa ya kwenda kutoa elimu hiyo baada ya kutambua kuwa vijana ndio chachu ya maendeleo.
 
“Elimu hii niliyoipata nitakwenda kuwapa vijana wenzangu ili nao fahamu zao ziweze kufumguka kama ambavyo ilivyo kwangu” alisema Salim Muhamed kutoka Manyara.
Wakati huohuo Lilian kutoka Tanga alisema kuwa elimu aliyoipata imemfungu ufahamu mkubwa na kumwezesha kutambua kuwa vijana wengi ni waongeji lakini si watendaji kitu ambacho mwisho wa siku wamebaki kuwa walalamikaji. “ Elimu hii ni lazima iwafikie vijana maana nimegundua kwamba watu wengi wanataka kufanyiwa mambo na si kufanya wenyewe ili kujikwamua kimaendeleo” AlisemaLilan

Restless ni taasisi ya maendeo ya vijana ambayo ilianzishwa mwaka 1985 nchini Uingereza kama SPW (Student Partnerships Worldwide) ambapo kwa tanzania shirika hili lilianza mwaka 1993 mjini Moshi mkoani Kirimanjaro na mwaka 1998 lilihamishia makao yake makuu mkoani Iringa ambapo lilikuwa likikusudia kutoa elimu ya afya ili kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi ambako ndiko makao makuu ya Restless yapo mpaka sasa.

Mradi huu wa OFS unatekelezwa katika mikoa kumi na nane (18) ya Tanzania Bara ambayo  imechaguliwa kwa vigezo maalumu vya uwakilishi wa kikanda. Mikoa hiyo ni; Mwanza,Kigoma,Manyara, Kilimanjaro,Dar es Salaam, Arusha,Mbeya, Iringa, Dodoma,Shinyanga, Mtwara, Lindi, Simiyu,Morogoro,Geita, Kagera, Tanga na Ruvuma.Katika mikoa yote hii wapo  vijana wakujitolea wanaotoa hamasa na mafunzo kwa mitandao ya vijana iliyoundwa na vijana wenyewe ili kutoa elimu ya uraia kote nchini.
 
Mbali na mradi huu pia Restdi wa lessDevelopmnt wanafanya mradi wa Mwanamke tunu, Vijana tung'are kazini, Dance for life na mingine mingi  kwa ajili ya vijana nchini

Raha ya ngoma uingie ucheze hivi ndivyo waswahili husema wakiwa wanamaanisha huwezi kukisemea kitu ikiwa hukijui na wala hujashiriki. Kwa mantiki hii vijana wanatakiwa kushiriki katika michakato ya kuleta maendeleo ya nchi tukianzia katika kuchagua viongozi

Sunday, December 14, 2014

ROSE MUHANDO HAYA NI YA KWELI


Mwimbaji nyota wa muziki wa Injili Bongo, Rose Muhando wakati akifanya yake.
Mapema wiki hii, chanzo kimoja kilipiga simu katika chumba chetu cha habari na kusimulia kuhusu habari hiyo, kwamba, Rose ambaye hana mume, amenasa na muda wowote kuanzia sasa anaweza kuitwa mama.

Madai ya chanzo hicho yalieleza kwamba, staa huyo amekuwa akijichimbia nyumbani kwake mkoani Dodoma tofauti na siku za nyuma ambapo alikuwa hakauki jijini Dar.
“Kama hamsadiki ninayowaambia, najua ninyi mmebobea kwenye habari za uchunguzi ‘so’ fanyeni yenu mtaniambia,” kilidai chanzo hicho kikiomba chondechonde kisichorwe jina gazetini.


Ili kujiridhisha na habari hiyo, pasipo kwanza kuwasiliana na Rose, moja kwa moja, gazeti hili lilimpigia simu mmoja wa watu wa karibu wa nyota huyo (jina linahifadhiwa), alipopatikana, aliulizwa kuhusu ishu hiyo na haya ndiyo aliyoyaeleza:

Rose Muhando akipafomu na madansa wake.


“Yaani hadi leo mlikuwa hamjapata hii habari? Mimi siku zote nilikuwa najua labda kwenu siyo habari kwa sababu ujauzito huu ni wa siku nyingi. “Hata sasa hivi ukimuona alivyo unajua wazi kuwa kuna kichanga tumboni kwani tumbo limechomoza hatari.”
Mtu huyo wa karibu alisema anapokuwa nyumbani Dodoma mara nyingi amekuwa mtu wa kukaa ndani tu kutokana na watu kumshangaa.Alisema Rose amekuwa akijificha kwa sababu ya kuogopa macho ya watu na uchovu unaotokana na hali aliyonayo ‘kuchoka’.

NANI MHUSIKA?
Juu ya nani mhusika wa mimba hiyo, mtu huyo wa karibu, ambaye anafahamu kila kinachofanywa na nyota huyo wa Wimbo wa Facebook alisema kuwa, inadhaniwa kuwa ni ya mcheza shoo wake (jina kapuni).


Inadaiwa kwamba, Rose, mara kadhaa amekuwa akisisitiza kuwa ni lazima amzalie mtoto jamaa huyo kwa jinsi anavyompenda.“Huyo mcheza shoo ana uhusiano naye kwa muda mrefu kidogo na ameshasema kwa watu wengi tu kwamba endapo Mungu atapenda basi atafurahi kama atamzalia mtoto.
“Mimi hajaniambia mimba hasa ni ya nani, lakini naziona dalili zote kuwa ni ya huyo kijana,” alisema mtu huyo.Rose Muhando na madansa wake wakitoa burudani.


Baada ya kujiridhisha na maelezo ya mtu wake wa karibu, gazeti hili lilianza kumtafuta Rose, mama wa watoto watatu ambao wote amezaa na wanaume tofauti, lakini katika hali ya kushangaza, simu yake iliita hadi kukatika bila kupokelewa, hata baada ya kupigwa mara kadhaa.

Likiamini huenda alikuwa katika shughuli au mahali panapombana kuzungumza, gazeti hili lilimtumia ujumbe mfupi wa maneno (SMS) na kumsomea mashitaka hayo ili atoe ufafanuzi, lakini pia hakuweza kujibu.
Likiamini huenda simu yake haisomeki kwa mtumishi huyo wa Mungu, gazeti hili lilitumia simu nyingine ambayo nayo iliita kwa muda mrefu hadi kukatika pasipo kupokelewa na hata pia alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu wenye maelezo kuhusu hali yake ya sasa, pia haukujibiwa hivyo jitihada zinaendelea.


Endapo itathibitika, ujauzito wa Rose utakuwa ni wa mtoto wa nne ambapo mara kadhaa staa huyo amekuwa akisema hayupo tayari kuolewa hivyo kuwaacha baadhi ya watumishi midomo wazi wakiamini mtu wa sampuli yake haifai kuzaa nje ya ndoa.