Thursday, October 2, 2014

MABOMU YA MACHOZI YAENDELEA KUCHUKUA NAFASI YAKE RUNGWE


Wananchi wa    kata    ya lwangwa   Halmashauri  ya  Busokelo wilayani  Rungwe mkoani Mbeya  wameandamana   kuanzia     leo  asubuhi   hadi  katika ofisi za Halmashauri  hiyo    wakishiniza  serikali  wilayani  humo   kuwatoa  watu  walio kamatwa   baada  ya kuhusiwa kuhusika  na kifo cha  Gabriel Mwandemwa  mwenye  umri wa mika  {40} aliye  uwawa na  wananchi   katika  siku za   hivi karibuni kutokana na imani za  kishirikina.
 Wakizungumza  na   yetu rungwe  blog   wakati  wa  mandamano hayo  wanachi  hao   walisema hatua  hiyo ilikuja  kufuatia   jeshi  la polisi wilayani  humo  kuwakamata   baadhi ya wananchi   kwa madai ya  kuhusika na kifo  cha kijana  huyo  aliyefariki dunia siku za hivi karibuni  kutokana  na    vitendo vya  ushirikina. 
 
 Walisema  mnamo majila ya   usiku  wa kuamkia  oktoba   moja  jeshi la polisi  liliwasili kinyemela katika  maeneo hayo  kwa  kuwakamata  baadhi ya  wananchi    bila kushirisha  uongozi wa  maeneo husika   kwa  kufikishwa  kituoni,  ambapo kutokana na hali  hiyo   iliweza kupelekea  wao kama  wanachi kuchukua  hatua  ya  kupinga   kitendo hicho   kwa  kuungana  kwa  pamoja   na kufanya maadamano ya amani  hadi katika  ofisi  ya mkurugezi  wa Halmashauri hiyo  wakitaka kutolewa  kwa ndugu  zao.
   Hata  hivyo jeshi la  polisi liliwasili  eneo  la  tukio   na kisha kunza  kusaidia kuzuia    gasia  hizo   ikiwa  ni pamoja  na kuwatia  hatiani wale  wote ambao walionekana kuanzisha vurugu hizo.
   Diwani wa kata  hiyo Robati Mwaibata alikili kuwapo kwa  adha hiyo  na kusema  mpaka sasa wameshindwa  kuongea  na wananchi wake  kutokana na  vurugu kuendelea kuchukua nafasi  yake.
Alisema    chanzo   cha  tukio hilo ni  baada  ya jeshi la polisi  kuwakamata  baadhi ya  vijana wa  eneo hilo  kwa  tuhuma  za  kuhusika  na  mauji  ya    Gabriel Mwandemwa aliye fariki dunia siku za  hivi karibuni kwa   kukatwa na  mapanga na kisha mwili wake  kuchomwa moto.
 Alisema mpaka sasa wanaendelea  kutuliza gasia  hizo kwa  ushirikiana na jeshi la  polisi  wilayani humo .
 Hata  hivyo     juhudi na malfa za kutafuta mkuu wa wilaya ya rungwe krspini meela ziligonga mwamba   mara  baada  ya    simu yake  kuita bila kupokelewa.
 Siku  za  hivi  karibuni    wananchi wa  kijiji  cha Ikama  Mbande  walimkamata  Gabliel   Mwaibata  walimkamata kwa  kumwachia  kipigo na kisha   kumchoma moto baada ya  kudaiwa  kujihusisha  na vitendo  vya  kishjirikina.

KIJANA AFUMWA GESTI NA MKE WA KIGOGO


Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Marck Costantine (24), mkazi wa mtaa wa Kitangiri jijini Mwanza amenaswa ‘live’ gesti akiwa na mke wa kigogo mmoja (jina kapuni), aitwaye Mwanaidi wakijiandaa kuvunja amri ya sita.

Tukio hilo lilijiri Septemba 18, mwaka huu kwenye gesti moja maarufu iliyoko mitaa ya Kitangiri baada ya kigogo huyo kupewa ‘ubuyu’ kwamba anaibiwa mali yake ndipo akaandaa mtego na kufanikiwa kumnasa kijana huyo alipokutwa kwenye chumba namba 4 cha gesti hiyo akijiandaa kuserebuka.
Akisaini  kulipishwa faini
“Kigogo alipopewa mchoro huo na wambea, siku ya tukio alimshtua Mwenyekiti wa Mtaa wa Kitangiri, Maginga Patroba, wakatia timu katika gesti hiyo, wakawakuta wachepukaji hao wakiwa kitandani huku Marck akiwa tayari ameshachojoa nguo, Mwanaidi akiwa bado,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:

“Kigogo aliamuru wahudumu wagonge mlango ili wahusika wasishtuke, walipofungua ndipo mwenyekiti sabamba na kigogo huyo wakazama ndani.”

Mwanaidi alipoona flashi za kamera ya wanahabari zikiwamulika, alianza kuangua kilio mbele ya mumewe kumuomba awasamehe lakini kigogo huyo alimtaka kijana huyo amlipe fidia ya shilingi milioni moja kama adhabu ya kutembea na mke wake.
 
Kutokana na hali ya uchumi ya kijana huyo kutokuwa nzuri, hakuweza kulipa kiasi hicho cha pesa badala yake aliomba kupewa muda wa kulipa pesa hizo.
 
Chini ya uangalizi wa mwenyekiti, Marck aliandika barua ya makubaliano jinsi ya kulipwa kwa kiasi hicho cha pesa kwa kigogo huyo na iwe kama fundisho kwake kuachana na tabia za kutembea na wake za watu.
 
Kwa upande mwingine, mwenyekiti Patroba alikiri kumfahamu Marck na kudai ni kijana wa mtaani kwake na kumuonya asirudie mchezo huo mchafu.
“Namfahamu huyu kijana nimeshangazwa na kitendo hiki anachokifanya kwani ni vitendo ambavyo havikubaliki katika jamii hivyo kama kiongozi wa mtaa huu nitaendelea kutoa ushirikiano ili kuukomesha tabia kama hizi za kuvunja miji ya watu,’’ alisema Patroba.

KATIBU MWENEZI (BAWACHA) KAWE AJIUNGA NA ACT


index
Mbunge wa Kawe Mh. Halima Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa BAWACHA taifa.
Kipimo Abdallah
ALIYEKUWA Katibu Mwenezi wa Baraza la Wanawake Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) Jimbo la Kawe, Batuli Kivuma ambaye amejiunga na chama cha Alliance for Change and Transparent (ACT-Tanzania amesema kilichomuondoa CHADEMA ni ukabila ulioota mizizi kwa muda mrefu.
Kivuma ambaye awali alikuwa mwanachama wa Chama Cha Wananchi CUF alisema aliamini kuwa chama hicho kinasimamia demokrasia jambo ambalo limeshindikana hasa ukiwa hotekei mkoa wa Kilimanjaro.
Alisema tangu ajiunge katika chama hicho amekuwa na juhudi za kukijenga chama hasa Kata ya Msasani na jimbo zima la Kawe ila juhudi zake zimekuwa zikikwamishwa kwa misingi ya ukabila.
Katibu Mwenezi huyo wa zamani wa BAWACHA alisema katika kudhihirisha hilo alishiriki kwenye  mchakato wa kugombea nafasi ya Udiwani viti maalum mwaka 2010 ambapo alishinda ila aliondolewa kwa kigezo cha yeye ni Mdigo na wakapewa nafasi hiyo Wachaga.
“Kusema ukweli suala la kuhama vyama sio zuri ila inafikia mahali unashindwa kuvumilia kwani nimekuwa nikionewa mara kwa mara katika chaguzi na ukiangalia vizuri msingi wake ni ukabilia ambao unawabeba Wachaga” , alisema.
Kivuma  alisema alikuwa akikipenda sana chama hicho lakini ubaguzi uliopo amefikia mwisho wa uvumilivu na kwamba anahitaji kuonyesha jitihada zake kwingine.
Alisema suala hilo la ukabila lilikidhiri katika uchaguzi mkuu ambao ulifanyika hivi karibuni hasa katika upande wa BAWACHA ambapo juhudi zilifanywa kuanzia ngazi ya chini hadi Taifa.
Mwenezi huyo wa zamani wa BAWACHA alisema hata upatikanaji wa Mwenyekiti wa BAWACHA wa sasa Halima Mdee ulitawaliwa na ukabila ikiwa ni agizo la Mwenyekiti Taifa Freeman Mbowe.
“Unajua hili neno demokrasia wanalielewa je bwana kwani kwa ufahamu wangu ni kuhakikisha kuwa jamii inaacha pale inapofanya maamuzi yake ila huku ni kinyume”, aliongezea Kivuma.
Kivuma alisema atahakikisha kuwa anakibomoa CHADEMA hasa katika Jimbo la Kawe ambapo amefanya kazi za kisiasa kwa muda mrefu.
Kwa upande wake aliyekuwa Mjumbe wa Mtaa Serikali ya Mtaa wa Matofalini Ujiji Kigoma Yassin Mohamed alisema ni vema vyama vikatambua kuwa hakuna uadui baina yao na kuhama chama ni haki ya mtu.
Alitolea mfano hali ya kisiasa ilivyokuwa siku za nyuma kati ya chama na CHADEMA na CUF hali ambayo kwa sasa haipo na vinafanya kazi pamoja.
Mohamed alisema ameamua kujiunga na ACT-Tanzania na kuondoka CHADEMA ili kupata uhuru wa kupigania demokrasia ya kweli.

BARUA YA SITTA KUMJULISHA WAZIRI MKUU WAKUTANE HARAKA OFISINI KWAKE MAMBO MAGUMU NI BAADA YA MWANASHERIA WA Z’BAR KUPIGA KURA YA HAPANA ,YAVUJA

By3oIKGIcAAeU2u
Hali ya Mwenyekiti wa Bunge lakatiba Samuel Sitta na gangi lake imekua ngumu mno baada ya Mwanasheria mkuu wa Zanzibar kupigilia msumari wa kura ya wazi ya kukataa.

Hali hii imemtia kiwewe Samuel Sitta na Wana Mapinduzi wa Rasimu ya katiba kuhaha na kuona sasa hali imekua ngumu na kusaka mbinu nyingine.

Sitta adiriki kumuandikia kiji notice Waziri mkuu Mizengo Pinda kumtaka ofisini kwake mara moja baada tu, ya Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar kupiga kura ya hapana.

CHIPSI NI NOMA APEWA KIPIGO NA APOZWA NA CHIPSI

 



 
mwanakaka akienjoy chipsi baada ya kupewa kipigo