Sunday, July 12, 2015

RAIS KIKWETE AMSHUKURU ALLAH KWA MCHAKATO KWENDA SALAMA BILA MPASUKO.



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimempitisha Dk. John Pombe Magufuli kuwa mgombea urais kupitia chama hicho. Katika Mkutano Mkuu uliofanyika usiku wa kuamkia leo mjini Dodoma, Dk. Magufuli amechaguliwa kwa kura 1560 akifuatiwa na Asha-Rose Migiro aliyepata kura 702 huku Balozi Amina Salum Ali akipata kura 349.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya kikao hicho, Dk. Magufuli amepita kwa kura hizo kutokana na nguvu yake dhidi ya wagombea wengine.
“Hakukuwa na namna hapa kwa kuwa, wajumbe wanaamini katika mazingira haya magumu ya upinzani Dk. Magufuli anaaminika na kukubalika nje kuliko hawa wengine,” anasema mtoa taarifa na kuongeza;
“Baada ya kutemwa Membe (Bernard Membe) kwenye NEC kila mjumbe ambaye alikuwa upande wa Lowassa (Edward Lowassa) alipumua jambo lililomrahisishia Magufuli.”
Mkutano huo umehairishwa mpaka saa nne asubuhi, ambapo ndiyo muda ambao Dk. Magufuli ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Mashariki na Waziri wa Ujenzi atatangazwa rasmi kuwa mgombea wa Urais kupitia chama hicho.
Awali ndani ya ukumbi wa mkutano, kulidawa kuwepo kwa mpango wa wafuasi wa Lowassa kutaka kumpitisha Balozi Amina ili chama hicho kipate changamoto katika ‘kumuuza’ kwa wananchi ikiwa ni kulipiza kisasi kwa kukatwa mtu wao (Lowassa).
Katika Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya chama hicho, majina yaliyopitishwa yalikiwa ni Migiro, Magufuli, Balozi Amina, Membe na January Makamba.
Katika Halmashauri Kuu ya CCM yalipita majina matatu ya Dk. Magufuli, Dk. Migiro na Balozi Amina.



WAKATI CHAMA TAWALA WAKIFANYA UTEUZI, UKAWA WASHIRIKI FUTARI YA PAMOJA


  • Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Willibroad Slaa akishiriki futari iliyoandaliwa na Ofisi ya Kambi ya Upinzani Bungeni wakati wa kikao cha Viongozi Wakuu wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na wabunge wa umoja huo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam kujadili mikakati mbalimbali ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu. Kushoto kwake ni Mbunge wa CUF, Ali Khamis Seif (Mkoani) na kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa NLD Zanzibar, Ahmad Hemed.
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe akijadiliana jambo na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, Said Issa Mohamed (katikati) pamoja na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Ndelakindo Kessy (kushoto) huku wakishiriki futari iliyoandaliwa na Ofisi ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni wakati wa kikao cha Viongozi Wakuu wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na wabunge wa vyama vinavyounda umoja huo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam kujadili mikakati mbalimbali ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu.
Baadhi ya Wabunge wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kutoka kushoto, Naomi Kaihula (Viti Maalum CHADEMA), Salum Baruan (CUF- Lindi Mjini) na Mohamed Habib Mnyaa wakishiriki futari iliyoandaliwa jana jijini Dar es Salaam na Ofisi ya Kambi ya Upinzani Bungeni, wakati wabunge wa vyama vinavyounda umoja huo waliposhiriki kikao cha Viongozi Wakuu wa UKAWA (Summit) kilichojadili mikakati mbalimbali ya maandalizi ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu.(VICTOR)
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar Said Issa Mohamed akiwamiminia uji baadhi ya wabunge wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) wakati wa kula futari. Wabunge hao walikuwa wakihudhuria kikao cha Viongozi Wakuu wa UKAWA kilichofanyika juzi jijini Dar es Salaam kujadili mikakati mbalimbali ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu. Walioketi kutoka kushoto ni Seleman Bungala Bwege (CUF- Kilwa Kusini),Mohamed Habib Mnyaa (CUF-Mkanyageni) na Mama Riziki.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar Said Issa Mohamed akiwamiminia uji baadhi ya wabunge wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) wakati wa kula futari. Wabunge hao walikuwa wakihudhuria kikao cha Vioingozi Wakuu wa UKAWA kilichofanyika juzi jijini Dar es Salaam kujadili mikakati mbalimbali ya ushindi kuelekea uchaguzi mkuu. Walioketi kutoka kushoto ni Seleman Bungala Bwege (CUF- Kilwa Kusini) na Mohamed Habib Mnyaa (CUF-Mkanyageni).

MZEE KINGUNGE ATOA YAKE YA MOYONI MJINI DODOMA



MWANASIASA mkongwe nchini, mzee Kingunge Ngombale Mwiru, amekionya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutofanya dhihaka ya kumpendekeza kada yoyote kuwa mgombea wake wa urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, kwani kwa kufanya hivyo kitaanguka.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma Jumatano Julai 8, 2015, Kingunge ambaye ameshawahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini na ndani ya chama hicho alisema “ninatishwa na watu wanaotumia nguvu nyingi kwelikweli kupambana wenyewe kwa wenyewe ndani ya chama, badala ya kuelekeza nguvu hizo kupambana na wapinzani wetu, hii ni hatari.’, alionya
Amesema, CCM ni lazima ifuate katiba yake ili wajumbe wanaotarajiwa kutoa maamuzi watoe maamuzi sahihi na sio kupindisha katiba kwa kuanzisha utaratibu ambao sio utamaduni wa kidemokrasia.
“kuna kiongozi mmoja anasema, kada yeyote wa chama hicho aliyeomba kuteuliwa kuwania urais, endapo jina lake litakatwa hatakuwa na nafasi ya kukata rufaa, hii haijawahi kutokea na wala haipo kwenye katiba yetu.’ Amesema Mzee Kingunge.
"CCM lazima imteue mtu anayekubalika ndani na nje ya chama ili chama kiweze kushinda, kinyume na hapo, hii ni njama ya kukifanya kishindwe kwenye uchaguzi".

Hivi karibuni Katibu wa Halmashauri Kuu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, aliwaambia waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa hakutakuwa na nafasi ya kada wa chama hicho atakayeenguliwa kwenye mchujo kuweza kukata rufaa, kwani hakuna kanuni inayoelekeza kufanya hivyo.

Hata hivyo Kingunge amepinga kauli hiyo na kusema, inakwenda kinyume cha katiba ya CCM ambayo inaweka bayana kuwa maamuzi ya vikao vya chini yanaweza kukataliwa na vikao vya juu ikiwa ni pamoja na mwanachama ambaye anaona hakutendewa haki kuwa na nafasi ya kupinga uamuzi wa vikao vya chini.

Saturday, July 11, 2015

RESTLESS YAWAONYESHA NJIA YA KUPITA VIJANA



WENGI WAABADILI MTAZAMO WA URAIA

Vijana wakifuatilia kwa makini mafunzo

Vijana wengi wamekuwa walalamikaji wa mambo na wala si watendaji wa mambo wanayolalamikia, wakati huohuo vijana ndio nguvu kazi katika maendeleo ya jamii lakini si washiriki wa kuleta maendeleo hayo. 

Hayo yalisemwa na Kefar Mbogela ambaye ni mratibu msaidizi wa mradi wa Fahamu Ongea Sikiliza (FOS) ambao upo chini ya taasisi ya Restless Development nchini. Ambapo alisema lengo ni kutengeneza jamii bora ya vijana na kufanya vijana kuwa vioongozi bora katika jamii na wanakuwa wafanya maamuzi katika jamii.

Mradi wa Fahamu Ongea Sikilizwa unalenga kuwahamasisha, kuwaelimisha na kuwafanya vijana kushiriki katika shughuli za kiraia na hasa katika mchakato wa uchaguzi mkuu Tanzania. “Mraadi huu unawataka vijana wajitokeze kushiriki kwa wingi kujiandikisha, kupiga kura na kugombea kwani ni haki ya kila mtanzania mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea kwani kijana huyo  ana sifa za kupiga kura na kugombea pia. Alisema  Kefar

Akiongea kwa hamasa alisema kuwa vijana wengi wamekuwa hawashiriki katika shughuli za kimaendeleo kitu ambacho kimewafanya vijana hao kujinyima haki ya kimaendeleo kwa kutoshiriki kwao. “matatizo ya vijana wanayajua vijana wenyewe  na mengi yanaweza kutatuliwa na vijana wenyewe iwapo vijana wataashiriki kikamilifu katika nafasi za kuleta maendeleo kwani wao ndio nguvu kazi inayotegemewa katika kuleta maendeleo kuliko makundi mengine ya watu.  



Pia alisema ni vyema vijana wakawajibika kuyatimiza majukumu yao wenyewe badala ya kuendelea kuilaumu serikali huku wakiwa hawajitokezi katika shughuli za kiserikali wakidhani ya kuwa ni jukumu la serikali kufanya majukumu kwa ajiri ya vijana kitu ambacho ni kujidanganya na kuendelea kujicheleweshea maendeleo.

Wakati wa mafunzo hayo vijana walielezwa umuhimu wa vijana kushiriki katika kupanga maendeleo  kuanzia katika ngazi ya mtaa mpaka serikali kiujumla ili kuondoa dhana ya kuwaona vijana ni watu wasiofaa katika jamii kama ilivyo hivi sasa. Hivyo aliwasihi vijana hao kushiriki kikamilifu katika mchakato mzima wa kujiandikisha na kupiga kura kwa kuchagua viongozi sahihi.

Nae Bwana Abdul Lukanza ambaye ni afisa uhusiano wa vijana alieleza umuhimu wa nafasi ya vijana katika demokrasia kitu ambacho kiliamsha hisia za vijana wengi na kufanya maswali mengi kujitokeza miongoni mwa vijana hao.

Hata hivyo kitendo hicho kilitoa fursa kwa  Bwana Abdul kuelezea sifa na faida za demokrasia na kuwasihi vijana hao kufikisha elimu waliyoipata kwa vijana wengine ili Kuongeza uwezo na motisha kwa vijana kushiri katika mchakato wakujiandikisha, kupiga kura na kugombea nyadhifa mbalimbali, Kukuza ufahamu wa viongozi katika kazi na ni majukumu yao kuwasaidia wananchi kushiriki kikamilifu katika chaguzi zijazo.

Mafunzo hayo ambayo yalishirikisha vijana zaidi ya 50 kutoka mikoa ya Tanga, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Shinyanga yalifanyika mkoani Kilimanjaro, yaliwaacha vijana kuwa na hamu kubwa ya kwenda kutoa elimu hiyo baada ya kutambua kuwa vijana ndio chachu ya maendeleo.
 
“Elimu hii niliyoipata nitakwenda kuwapa vijana wenzangu ili nao fahamu zao ziweze kufumguka kama ambavyo ilivyo kwangu” alisema Salim Muhamed kutoka Manyara.
Wakati huohuo Lilian kutoka Tanga alisema kuwa elimu aliyoipata imemfungu ufahamu mkubwa na kumwezesha kutambua kuwa vijana wengi ni waongeji lakini si watendaji kitu ambacho mwisho wa siku wamebaki kuwa walalamikaji. “ Elimu hii ni lazima iwafikie vijana maana nimegundua kwamba watu wengi wanataka kufanyiwa mambo na si kufanya wenyewe ili kujikwamua kimaendeleo” AlisemaLilan

Restless ni taasisi ya maendeo ya vijana ambayo ilianzishwa mwaka 1985 nchini Uingereza kama SPW (Student Partnerships Worldwide) ambapo kwa tanzania shirika hili lilianza mwaka 1993 mjini Moshi mkoani Kirimanjaro na mwaka 1998 lilihamishia makao yake makuu mkoani Iringa ambapo lilikuwa likikusudia kutoa elimu ya afya ili kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi ambako ndiko makao makuu ya Restless yapo mpaka sasa.

Mradi huu wa OFS unatekelezwa katika mikoa kumi na nane (18) ya Tanzania Bara ambayo  imechaguliwa kwa vigezo maalumu vya uwakilishi wa kikanda. Mikoa hiyo ni; Mwanza,Kigoma,Manyara, Kilimanjaro,Dar es Salaam, Arusha,Mbeya, Iringa, Dodoma,Shinyanga, Mtwara, Lindi, Simiyu,Morogoro,Geita, Kagera, Tanga na Ruvuma.Katika mikoa yote hii wapo  vijana wakujitolea wanaotoa hamasa na mafunzo kwa mitandao ya vijana iliyoundwa na vijana wenyewe ili kutoa elimu ya uraia kote nchini.
 
Mbali na mradi huu pia Restdi wa lessDevelopmnt wanafanya mradi wa Mwanamke tunu, Vijana tung'are kazini, Dance for life na mingine mingi  kwa ajili ya vijana nchini

Raha ya ngoma uingie ucheze hivi ndivyo waswahili husema wakiwa wanamaanisha huwezi kukisemea kitu ikiwa hukijui na wala hujashiriki. Kwa mantiki hii vijana wanatakiwa kushiriki katika michakato ya kuleta maendeleo ya nchi tukianzia katika kuchagua viongozi