Monday, November 10, 2014

KUMBUKUMBU YA NDEGE YA MALAYSIA MH17


Kumefanyika maadhimisho ya kuwakumbuka watu walipoteza uhai wao kwenye ndege ya shirika la ndege la Malaysia MH17, nchini Uholanzi,ambapo maua na mishumaa ipatayo mia mbili na tisini na nane vilinavyo wakilisha idadi ya abiria waliokuwa wakisafiri na ndege hiyo kabla ya ajali ambavyo viliwekwa na wanafunzi,ndege hiyo ilipopotelea Mashariki mwa Ukraine yapata miezi minne iliyopita.

mishumaa idadi sawa na abilia waliokuwepo ndani ya ndege iliyopotea ikiwa imewashwa kwa ajili ya kukumbuka vifo vya abilia 
Mfalme na malkia wa Uholanzi na mabalozi wa nje waliomo nchini humo walihudhuria hafla hiyo,ambapo majina ya walikufa katika ajali hiyo yalitajwa.
Ikiwa imetimia miezi minne leo, sababu za ajali hiyo mpaka sasa hazijajulikana,ingawa kikundi cha kigaidi cha Urusi kinashukiwa kuidungua ndege hiyo,ambayo ilikuwa ikifanya safari zake kutoka uwanja wa ndege wa Amsterdam kuelekea Kuala Lumpur Malaysia.
inasemekana ndege hiyo ilidunguliwa kwa kombora, na mara moja serikali mjini Moscow imekanusha taarifa hizo.
CREDIT: BBC

WANAUME KENYA KUSUSIA TENDO LA NDOA LEO!




Wanaume nchini Kenya wameelezea hisia mseto kuhusu wito wa kiongozi wa Shirika la Maendeleo la Wanaume nchini humo kwamba hapo kesho tarehe 11 wasusie tendo la ndoa na kuonyesha hisia za mapenzi kwa wanawake.

Wiki jana kiongozi huyo Nderitu Njoka amewataka wanaume nchini Kenya kufanya hivyo kuadhimisha siku ya kimataifa ya uhuru kwa wanaume inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 11 mwezi Novemba.
Bwana Nderitu amewataka wanaume wote kutojihusisha na wanawake kimwili , wawe wameoa au la kama ishara ya kuonyesha ghadhabu yao kwa ongezeko la dhuluma wanazotendewa wanaume pamoja na ongezeko la utumiaji wa dawa za kulevya na pombe miongoni mwa wanawake.
Wito huo hata hivyo umepuuzwa na baadhi ya wanaume ukitajwa kuwa njama ya bwana Nderitu kujipa umaarufu katika vyombo vya habari.
Hatua hiyo pia inatumiwa kjuonyesha kero la wanaume kutokana na hatua ya serikali kutenga shilingi bilioni mbili kwa mahitaji ya wasichana wakati ikikosa kutoa mchango kama huo katika kusadia wanaume wengi kufanyiwa tohara.
Njoka alinukuliwa akisema kuwa kidini wanaume ndio vipngozi wa familia lakini leo wamedhalilishwa huku wanawake wakitawala dunia.
CREDIT: BBC

UTATA MWINGINE WAIBUKA, MISS TZ MPYA ADAIWA SI RAIA WA TZ, ANKO LUNDENGA AFUNGUKA KIIVI!

Dar es Salaam. Baada ya taji la Miss Tanzania kuvishwa kwa mshindi wa pili, utata mwingine umeibuka baada ya mrithi huyo, Lilian Kamazima kudaiwa kuwa si raia. 
Jana kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kulikuwa na taarifa zinazodai kuwa Lilian siyo raia wa Tanzania na kwamba anatokea Rwanda.
Akizungumzia tuhuma hizo, Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ndiyo waandaaji wa mashindano ya Miss Tanzania, Hashim ‘Uncle’ Lundenga alisema tuhuma hizo kuhusu Lilian siyo kweli. 
“Sisi tunajua Lilian ni Mtanzania, tunaangalia cheti cha kuzaliwa alichotuletea kamati yetu ambacho kinaonyesha alizaliwa Tanzania, pia ni Mtanzania, hayo yanayosemwa kwamba Lilian siyo Mtanzania hatuyajui kabisa,” alisema Lundenga. 
Pia Lundenga alisema kitendo cha Sitti Mtemvu kujivua taji la Miss Tanzania 2014 kumemnyima sifa ya kuendelea kushikilia taji la Miss Temeke na lile la Kitongoji cha Chang’ombe. 

“Sitti amevua taji la Miss Tanzania maana yake ni kwamba hata lile la Miss Temeke 2014 na lile la Miss Chang’ombe 2014 ambayo ndiyo alikuwa mshindi kabla ya kushinda lile la taifa, ameyavua pia,” alisema Lundenga. 

Sitti aliingia katika kashfa ya tuhuma za kudanganya umri baada ya nyaraka zake mbalimbali kuonyesha amezaliwa 1989 na siyo 1991 kama alivyowasilisha kwenye kamati ya Miss Tanzania.

Kwa mujibu wa sheria za mashindano hayo, mshiriki anatakiwa awe na umri wa kuanzia miaka 18 na usiozidi miaka 24. 

Mwandaaji wa mashindano wa Miss Temeke, Ben Kisaka alisema, “Waliotoa taarifa ya Sitti kujivua taji ni kamati ya Miss Tanzania, hivyo wao ndiyo wanapaswa kutoa taarifa zingine kuhusu taji la Temeke.”

ASKOFU ANASWA NA MADAWA YA KULEVYA JIJINI DAR

Askofu Emeka Nwachukwu Mert raia wa Nigeria anayehusishwa na biashara ya madawa ya kulevya. 
Vigogo wa madawa ya kulevya wakiwemo viongozi wa dini sasa wanaanza kupukutika kutoka kwenye mstari wa siri huku baadhi yao wakikimbilia nje ya nchi kufuatia oparesheni kali inayofanywa na Kikosi cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulenya Tanzania kuwanasa kila kukicha. Hivi karibuni kikosi hicho kimemkamata askofu (mwangalizi mkuu wa kanisa) aliyetambulika kwa jina la Emeka Nwachukwu Mert raia wa Nigeria ambaye ana kanisa la kiroho maeneo ya Sinza jijini Dar.
Jina la kanisa hilo limedhibithiwa na vyombo husika kwa sababu ya uchunguzi zaidi na uhalali wake wa kuwepo nchini. 
Vyanzo vyetu makini ndani ya kikosi kazi vinaeleza kwamba, mchungaji huyo alikamatwa Oktoba 31, mwaka huu saa kumi usiku Tegeta wilayani Kinondoni, Dar es Salaam akiwa na madawa ya kulevya ‘unga’ aina ya heroine kilo 35. 
Habari za ndani kutoka kwenye oparesheni hiyo zinasema kuwa, endapo unga huo ungeingia sokoni na kununuliwa, basi mtumishi huyo wa Mungu angevuna kitita cha zaidi ya shilingi bilioni mbili. 


Mchungaji huyo ambaye serikali imeanza kazi ya kulichunguza kanisa lake, alidakwa na mzigo huo haramu kwenye makazi aliyopanga ambayo ni nyumba ya profesa mmoja wa chuo kikuu, Mbezi jijini Dar es Salaam.
Askofu akiwa chini ya ulinzi.WASHIRIKA NAO WADAKWA
Kwa mujibu wa chanzo, kamatakamata ya mchungaji huyo pia iliwakumba watuhumiwa wengine ambao ni Walyat Khan raia wa Pakistani, Chuksi Sylvester Agbazuo na Tony Olafor wote raia wa Nigeria na inadaiwa kwamba walikuwa wakikamatwa maeneo mbalimbali na kutoroka. 
a
Habari za siri ambazo Uwazi ilizinasa zinadai kuwa, watumishi wa Mungu waliokuwa kwenye orodha ya kunaswa walikuwa wengi lakini wamekimbilia nje ya nchi na kikosi hicho kimeshawasiliana na Polisi wa Kimataifa (Interpol) kwa ajili ya kuwasaka na kuwatia nguvuni. 
Taarifa zaidi zinaeleza kwamba, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya Tanzania, SACP Godfrey Nzowa amekabidhiwa majina ya vigogo wakiwemo viongozi wa dini ambao ni sugu katika biashara hiyo. Mbali na majina hayo, pia amepewa ratiba zao za safari za kibiashara hivyo kilichobaki ni kuwafuatilia na kuwakamata na ushahidi ili kuhakikisha kwamba hawawezi kupona mahakamani. 
Habari zaidi zinadai kuwa, siku za hivi karibuni, Kamanda Nzowa amekuwa akifumua mtandao wa watu wazito katika biashara hiyo na imebainika kuwa vigogo hao wana mtandao mkubwa serikalini ikiwemo wizara ya mambo ya ndani ambao wanawalinda kwa kupewa mamilioni ya pesa kwa ajili ya usimamizi wa upitishwaji wa biashara hiyo haramu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar. 
“Unajua zamani viongozi hao serikalini walikuwa wakimsumbua Kamanda Nzowa ili awaachie watuhumiwa waliokamatwa na unga bila mafanikio, lakini sasa wameshamsoma kiasi kwamba hata wakikamatwa hawampigii simu tena,” kilisema chanzo kingine.
Dawa za kulevya alizokutwa nazo askofu huyo.
 
Habari nyingine zinadai kuwa, Kamanda Nzowa pia ana majina ya watoto wa vigogo wa serikali wanaojihusisha na biashara hiyo na anayafanyia kazi. 
Kukamatwa kwa askofu huyo kumekuja baada ya kukamatwa kwa vigogo ambao ni viongozi wa dini katika makanisa ya kilokole.
Januari 11, mwaka huu, Askofu Moris Charles alidaiwa kukamatwa na polisi maeneo ya Chinga Mbili mkoani Lindi akiwa na kilo 210 za madawa ya kulevya aina ya heroine yenye thamani ya shilingi bilioni 9.4, kesi yake bado inaendelea mahakamani mkoani humo. Juni 8, 2011 polisi walifanikiwa kumkamata Mchungaji Kapupu Denis Okechuku wa kanisa la kilokole lililopo Kinondoni Biafra akiwa na kilo 81 za cocaine, kesi yao bado ipo Mahakama ya Kisutu, Dar.
Nyumba aliyokutwa askofu huyo.
 
KAMANDA NZOWA
  Kamanda Nzowa ofisini kwake juzi, alisema kuna watu wanne waliokamatwa Tegeta wakiwa na kilo 35 za madawa ya kulevya aina ya heroin na kuna wengine wanatafutwa kuhusiana na tukio hilo. 
“Kwa sasa nisingependa kuzungumzia sakata hilo kutokana na sababu za kiupelelezi kwani kuna wengine tunawatafuta na nitahakikisha wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria, nawashukuru wananchi kwa ushirikiano wao,” alisema Nzowa.

MAPYA YAIBUKA BAADA YA MISS TANZANIA 2014 KUJIVUA TAJI

Miss Tanzania 2014 aliyevuliwa taji, Sitti Abbas Mtemvu akipanda jukwaani kupata maombi ya Nabii Yaspi Bendera.
Stori: Chande Abdallah, Deogratius Mongela na Musa Mateja.
TENA! Saa chache tu baada ya Miss Tanzania 2014 aliyezua tafrani la kuchakachua umri kwa kujipunguzia miaka 2 ya kuzaliwa, Sitti Abbas Mtemvu kujisalimisha kwa kujivua taji mwenyewe, mapya yameibuka na Ijumaa Wikienda lina mzigo mkononi!
Mapya hayo yameibukia ndani ya Kanisa la Revelation Church lililopo Buza–Kipera jijini Dar kwa Nabii Yaspi Bendera ambaye amezungumzia ishu ya Sitti kujivua  taji mwenyewe.“Alikuja kwangu nikamwombea, akapata taji. Hata alipopata alikuja kushukuru, nilimwambia aendelee kudumu kwangu hadi atakapokwenda kwenye taji la dunia (Miss World) lakini hakufanya hivyo, akawa haji tena.“Hivi, nitoe mfano mmoja. Kama mtu akienda kwa mganga kuomba apewe dawa ili apate ujauzito, akishapata akaenda kwa mganga mwingine kuomba amfanyie dawa ili ujauzito huo usitoke. Je, siku ukitoka nani analaumiwa, mganga wa kwanza au wa pili?”
Aliyekuwa Miss Tanzania 2014 akipokea maombi ya nguvu kutoka kwa Nabii Yaspi Bendera 
TAFSIRI YAKE HAPA!
Kwa tafsiri rahisi sana ya mazungumzo ya nabii huyo, Sitti alikwenda kanisani kwake akaomba baraka ili ashinde taji la Miss Tanzania, akashinda lakini baadaye alihama kanisa na kwenda kusali kwingine mpaka alipovua taji.
Nabii Yaspi aliandelea kudai kwamba, kama Sitti angeendelea kudumu kwenye kanisa lake na kuombewa maombi ya nguvu, asingevua taji na angefanikiwa kwenda Miss World 2015 ambako pia angetwaa taji la dunia.
Lakini baada ya kutwaa taji alienda kanisa jingine akiwa na taji lake, matokeo yake mambo yakawa magumu mpaka alipolazimika kuvua taji hilo.
Nabii Yaspi Bendera akimkumbatia Sitti Abbas Mtemvu.
KUMBE ALISHAONYWA
Habari nyingine kutoka kwa mtu asiye msemaji wa kanisa hilo zinasema kuwa, baada ya kutwaa taji, Sitti alionywa na Nabii Yaspi kwamba kutaibuka vikwazo katika nafasi yake hiyo lakini alichotakiwa kufanya ni kudumu katika maombi ya kanisa hilo ili vikwazo hivyo vifutike lakini kwa sababu hakufanya hivyo matokeo yake ni hayo! 
SITTI AMEFIKAJE HAPA?
Siku chache baada ya Sitti kutwaa Taji la Miss Tanzania 2014 katika shindano lililochukua nafasi ndani ya Ukumbi wa Mlimani City, Dar, Oktoba 11, mwaka huu, yaliibuka madai kwamba, mrembo huyo alichakachua umri akidai ana miaka 23 wakati ana miaka 25.
Mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga akijibu hoja kutoka kwa wanahabari
Sheria za Miss Tanzania, mrembo mwenye miaka 25 haruhusiwi kushiriki mashindano hayo.
Katika madai hayo, ilisemekana kwamba, mrembo huyo alizaliwa Mei 31, 1989 kwenye Hospitali ya Aga Khan jijini Dar. Lakini yeye cheti alichokipeleka kwenye Kamati ya Miss Tanzania akidai alikipata kwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) kilionesha mlimbwende huyo alizaliwa Mei 31, 1991 hivyo ana miaka 23.
PASPOTI NDIYO CHANZO
Mazito yote yaliyompata Sitti, chanzo ni hati yake ya kusafiria (paspoti) ambayo ilibandikwa kwenye mitandao ya kijamii ikionesha mrembo huyo ambaye ni binti wa Mbunge wa Jimbo la Temeke kwa tiketi ya CCM, Abbas Mtemvu, alizaliwa Mei 31, 1989.
Mrithi wa Miss Tanzania 2014, Lillian Kamazima akiwa ni mwenye furaha.
KESI BADO MBICHI!
Katika barua yake kwa Kamati ya Miss Tanzania aliyoiandika Novemba 5, mwaka huu na kufika ofisi za kamati hiyo, Novemba 6, mwaka huu, saa 9:25 mchana, Sitti alisema ameamua kwa hiyari yake kuvua taji hilo baada ya kusakamwa na vyombo vya habari kwamba alichakachua umri.
“Leo nalivua taji rasmi nililopewa na binadamu lakini alilonipa mwenyezi Mungu bado ninalo. Mwisho naomba radhi Watanzania wote kwa uamuzi huo niliochukua,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo ya Sitti.
Nafasi ya Sitti imetwaliwa na mshindi wa pili, Lilian Kamazima aliyetokea Arusha.
Hata hivyo, kuna ushahidi wa kutosha kutoka Rita na Idara ya Uhamiaji kwamba, umri wa miaka 25 uliopo kwenye paspoti ya kusafiria ya Sitti ambayo imesambaa kwenye mitandao ya kijamii ndiyo sahihi!
Kwa maana hiyo, Sitti kujivua taji anakuwa amemalizana na kesi ya wananchi waliokuwa wakimkomalia, lakini kesi ya kughushi cheti cha kuzaliwa bado inamhusu kwa sababu kwa sheria za Tanzania, mtu akithibitika kudanganya umri kifungo chake ni miaka 3 jela na jamhuri inaweza kumshtaki kwa kusimamia kesi yenyewe.
Miss Lillian Kamazima akipozi.
NI HISTORIA KWA MISS TANZANIA
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya mashindano ya Miss Tanzania yaliyoanza nchini mwaka 1994 baada ya kufutwa awali ambapo mshindi wa kwanza anajivua taji ingawa pia haikuwahi kutokea mshiriki kuvuliwa taji kwa kosa lolote lile.
ILIWAHI KUTOKEA MISS KUDANGAYA SHULE
Mwaka 1995, Miss Tanzania alikuwa ni Emily Adolf, mwanafunzi wa kidato cha pili Shule ya Sekondari ya Central, Dodoma. Ushindi wake ulileta malumbano baada ya kubainika alishiriki akiwa mwanafunzi huku akidai alimaliza. Alifukuzwa shule lakini hakuvuliwa taji.



WEMA ALINUSURIKA NA UMRI
Mwaka 2006, Miss Tanzania, Wema Isaac Sepetu naye alinusurika kuvuliwa taji kwa madai kwamba alidanganya umri wake. Wema alidaiwa kushiriki mashindano hayo akiwa na miaka 17, yeye akadai ana 18 lakini vuguvugu la wananchi kumkomalia miaka hiyo haikuwa kama sasa.

ZIARA YA MH FREEMAN MBOWE MKOANI TABORA


Mweenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiwahutubia wananchi wa mji wa Nzega katika mkutano wa hadhara wa Oparesheni Delete CCM, uliofanyika kwenye Uwanja wa Paking jana.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiwatambulisha viuongozi wa ngazi ya Kata wa Chama cha Wananchi (CUF), kwenye mkutano wa hadhara wa Oparesheni Delete CCM, uliofanyika kwenye Uwanja wa Paking mjini Nzega jana. 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiagana na wananchi wa mji wa Nzega baada ya mkutano wa hadhara wa Oparesheni Delete CCM, uliofanyika kwenye Uwanja wa Paking jana.

AJALI YA NDEGE YACHUKUA UHAI WA DK MUNROE


Dk. Myles Munroea akiwa na mkewe Ruth enzi za uhai wao.
KIONGOZI wa Bahamas Faith Ministries, Dk. Myles Munroe, mkewe Ruth na watu wengine saba wamefariki dunia katika ajali ya ndege jana huko Bahamas.

Dk. Myles Munroe (kulia) wakati akiwa jijini Dar Oktaba mwaka huu akitazama vitabu vya mtunzi na mwalimu wa ujasiriamali ambaye pia ni Mkurugenzi wa Global Publishers Ltd, Eric Shigongo…

Dk. Myles Munroea akiwa na mkewe Ruth enzi za uhai wao.
KIONGOZI wa Bahamas Faith Ministries, Dk. Myles Munroe, mkewe Ruth na watu wengine saba wamefariki dunia katika ajali ya ndege jana huko Bahamas.

Dk. Myles Munroe (kulia) wakati akiwa jijini Dar Oktaba mwaka huu akitazama vitabu vya mtunzi na mwalimu wa ujasiriamali ambaye pia ni Mkurugenzi wa Global Publishers Ltd, Eric Shigongo (katikati). 
Katika ajali hiyo, ndege ndogo waliyokuwa wakisafiria iligonga winchi na kulipuka wakati ikiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Grand Bahama.
Dk. Myles Munroe wakati akiendesha mkutano wa viongozi wa serikali, wafanyabiashara na viongozi wa makanisa Oktoba mwaka huu jijini Dar.
Dk. Munroe ambaye pia alikuwa mzungumzaji maarufu wa mambo ya uongozi na biashara duniani, Oktoba 21, mwaka huu alitoa somo kwa viongozi mbalimbali nchini katika mkutano wake mkubwa uliofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar.

Dk. Munroe akiwa nchini Tanzania mwezi Oktoba mwaka huu.
Katika mkutano huo, Dk. Munroe kutoka Nassau, Bahamas, alifundisha mbinu za kuwafanya viongozi waweze kuchanganua mambo, kutimiza majukumu yao na hatimaye kufikia malengo makubwa ya kimafanikio ambayo yanaweza kuifanya nchi ipige hatua.
Dk. Myles Munroe akisalimiana na Eric Shigongo walipokutana katika Hoteli ya Serena jijini Dar, Oktoba mwaka huu.