Monday, September 8, 2014

MBUNGE WA NZEGA AKITANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAIS WA TANZANIA MWAKANI.


1Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya serikali za Mitaa na Mbunge wa jimbo la Nzega Dr. Khamis Kigwangallah akiwasili katika hoteli ya Hyyat Kilimanjaro kwenye mkutano na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali ambapo leo ametangaza nia ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania unaotarajiwa kufanyika mwaka ujao 2015, Dk. Khamis Kigwangallah ameongozana na mke wake Dr. BayoumAwadh na watoto wake Sheila ambaye ni mkubwa Hawa na HK Junior
Mbunge wa Nzega CCM Dr. Hamis Kigwangalla,  akitangaza rasmi nia yake ya kugombea Urais kupitia tiketi ya CCM mwakani 2015
 amesema kutokea kuuza karanga na biggee mtaani mpaka kuwa Doctor Mbunge na Kiongozi wa CCM Taifa na kufikia na ndoto ya kutegemea kugombea Urais ina maana moja tu kwamba sera za CCM zina tija kwa Taifa na wananchi wake na yeye ni mfano wa kwanza mkubwa wa kuaminiwa kwamba sera hizo zinajali usawa kwa wananchi kwani pamoja na kupitia yote aliyopitia bado anaweza kutuhubutu kugombea Urais wa Tanzania kwa kukubaliwa na kuruhusiwa kikatiba na chama chake CCM na kuruhusiwa kisheria na Sheria za Jamhuri ya Tanzania.










No comments:

Post a Comment