Thursday, October 16, 2014

AJALI YA LORI LA MAFUTA DAR LAANGUKA LAWAKA MOTO WATU WAPOTEZA MAISHA

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki (katikati) na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema wakimsikiliza miliki wa Nyumba ya kulala wageni United State na bar, Laurent Kasiga  iliyopo Mbagala Rangi tatu, Dar es Salaam ambayo iliteketea kwa moto uliotokana na roli la mafuta lililopinduka na kuwaka moto wakati vijana wakiiba mafuta.
 Mkuu wa Moa akikagua Nyumba hiyo ya kulala wageni iliyokuwa na vyumba 32.
 wananchi wakiangalia athari za moto huo.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akiangalia tenki la lori hilo.
 Lori hilo lilivyoteketea kwa moto uliosababishwa na mshumaa.
Moja ya maduka ya vifaa vya pikipiki lililoteketea 
 
Wafanyabiashara wa mchele waliokuwa na fremu katika eneo hilo wakiwa katika majonzi baada ya mzigo wao kuungua moto na kuharibika kabisa.

Mmoja wa majeruhi katika tukio hilo la moto akisimulia. 
Baadhi ya sehemu za mwili za watu walioungua. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadick, akiwa na mmoja wa wauguzi wa hospitali ya Temeke alipowatembelea waathirika wa ajali hiyo. WATU watatu wamefariki na wengine sita wakiwa katika hali mbaya Hospitali ya Muhimbili kufuatia tukio la moto uliolipuka kwenye gari la kubeba mafuta jana maeneo ya Mbagala jijini Dar es Salaam. 

AKizungumza Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Naibu Kamishna Mohammed Mpinga, alisema ajali hiyo haikuleta athari yoyote baada ya gari lile kupata ajali ila athari ilijitokeza baada ya watu kuvamia na kuanza kuiba mafuta na baadaye kujaribu kuiba betri ndipo cheche za moto zilipolipuka na kusababisha kuwaka kwa gari hilo. 

Wakati huohuo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mecky Sadick, amewataka wananchi kutokuwa na tabia ya kuvamia ama kuiba vitu pindi ajali zitokeapo.
Sadick alisema hayo alipotembelea hospitali ya Muhimbili na Temeke walipolazwa majeruhi hao.

No comments:

Post a Comment