Sunday, August 17, 2014

ILIYOKUWA BAR SASA NI KANISA

 

Baa iliyopo Sinza-Lion jijini Dar ambayo imegeuzwa kuwa kanisa.
WAKATI matukio mengi ya kushangaza na kushtukiza yakiendelea kutokea kila siku duniani, neno la Mungu nalo linazidi kushika kasi kufuatia baa moja iliyopo Sinza-Lion jijini Dar kugeuzwa kuwa kanisa.Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa baa hiyo maarufu iitwayo The Don, ukumbi wake ambao ulikuwa ukitumika kwa watu kupiga ulabu, hivi sasa unatumiwa na waumini wa kanisa linalojukana kama Impact International Christian Centre kupata mahubiri. Lakini cha kushangaza ilibainika kwamba katika maandishi makubwa yanayolinadi jina la baa hiyo, chini yake ndipo limewekwa bango linaloonyesha kanisa hilo, kitu ambacho kwa mtu mgeni, ni vigumu kuelewa mara moja.

No comments:

Post a Comment