Friday, September 5, 2014

UKATILI KIASI HIKI

UKATILI WA KUTISHAMAMA ADAIWA KUMSULUBU MTOTO, APEWA KIBANO

HII ni too much! Jalada namba KW/RB/7565/2014-SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI lililopo kwenye Kituo cha Polisi cha Kawe, Dar, linamhusu mama aliyetajwa kwa jina moja la Teddy, mkazi wa Tegeta kwa madai ya kumtumikisha na kumtesa mtoto Magdalena Elisha (10) na kumsababishia majeraha na makovu ya vidonda sehemu mbalimbali mwilini.
Mama anayedaiwa kumsulubu mtoto huyo akilia baada ya kutiwa nguvunu na polisi.
Habari kutoka ndani ya jeshi la polisi zilidai kwamba, Teddy alimchukuwa mtoto huyo jijini Arusha kwa lengo la kumsaidia kukaa na mwanaye kwa kuwa familia ya mtoto huyo haina uwezo na ameishia darasa la tatu kwa kukosa vifaa vya shule.
Mtoto Magdalena Elisha anayedaiwa kusulubiwa na mama huyo.
Kwa mujibu wa Teddy, bila kujua kwamba ni kosa kumwajiri mtoto, aliamua kumwadhibu mtoto huyo kutokana na kutomsikiliza bosi wake hasa alipokuwa akionywa kuachana na tabia ambayo haikuwa ikimfurahisha.
Kwa upande wake Magdalena alidai kwamba alikuwa akipokea kipigo kila siku hasa wakati mama huyo alipokuwa akirejea nyumbani kutoka ‘jobu’ na kukuta mwanaye analia.
Sehemu ya majeraha aliyoyapata Magdalena Elisha baada ya kusulubiwa na mama huyo.
“Alikuwa akinipiga kila siku akikuta mtoto (wa miaka miwili) analia. Pia kuna siku alinipiga sana asubuhi, nikaona nikimbilie kwa mjumbe, ndiyo tukaenda kituo cha polisi, tukakutana naye akiwa anatoka polisi kutoa taarifa kuwa nimepotea, mimi naomba nisaidiwe nirudi kwa mama yangu Arusha,” alisema Magdalena na kumfanya bosi wake huyo apewe kibako na vyombo vya sheria.

No comments:

Post a Comment