Tuesday, October 14, 2014

PAPAA MSOFE NA MAKONGORO WAENDELEA KUSOTA RUMANDE


Papaa Msofe (katikati) akishuka ngazi za Mahakama ya Kisutu. (Picha na maktaba yetu).
MFANYABIASHARA anayekabiliwa na kesi ya mauaji, Marijan Abubakar, maarufu kama Papa Msofe na mwenzake, Makongoro Joseph, wameendelea kusota rumande kutokana na kile kinachoelezwa kuwa upelelezi bado haujakamilika. 
Kesi ya watuhumiwa hao wawili imetajwa leo na mwendesha mashitaka wa serikali, Bi Hellen Moshi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam mbele ya Hakimu Mkazi, Hellen Liwa.
Msofe na Makongoro wanakabiliwa na kesi ya mauaji ya bwana Onesphory Kitoli.
Kesi hiyo imeahirishwa mpaka Oktaba 27, mwaka huu itakapotajwa tena.

No comments:

Post a Comment