Thursday, September 11, 2014

KIJANA AUAWA AKITUHUMIWA USHIRIKINA MKOANI MBEYA

 Marehemu akipakiwa kwenye gari tayari kumpeleka chumba cha kuhifadhia maiti.

Ndugu na jamaa wakishiriki maziko ya marehemu, Gabriel Mwasyebule kijijini kwao ndembo lwangwa.
Marehemu Gabriel Mwasyebule enzi za uhai wake.
Nyumba ya marehemu, Gabriel Mwasyebule anayotuhumiwa kuijenga kwa uchawi.
Moja ya shamba la viazi vinavyo subiriwa kuvunwa mwezi huu, shamba la marehemu, Gabriel Mwasyebule, mashamba amabayo pia ni moja ya sababu ambazo wananchi wa lwangwa wanamtuhumu marehemu kuwa alikuwa anawalimisha watu kiuchawi na kuiba mazao ya mashamba mengine kiuchawi ili shamba lake liwe na mazao mengi na mazuri.
Hii ndio stoo kuwekea mazao mbalimbali ambayo marehemu alikuwa anatumia kutunzia mazao yake.
MATUKIO ya kujichukulia sheria mikononi bado yanazidi kuyakumba baadhi ya maeneo mkoani Mbeya ambapo katika tukio hili kijana Gabriel Mwasyebule miaka 39 ameuawa na wananchi wenye hasira kali wakimtuhumu kwa imani za kishirikina.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kumtaja marehemu aliyetambulika kwa jina la Gabriel Mwandemwa (Mwasyebule) mkazi wa kijiji cha Ikamambande (Lwangwa) Wilaya ya Rungwe aliuawa na watu wasiofahamika kwa kukatwa na vitu vyenye ncha kali sehemu za kichwani na kifuani.

Alisema tukio hilo lilitokea siku ya jumapili majira ya saa tano asubuhi huko katika Kijiji cha Ikamambande, kata ya Lwangwa, Tarafa ya Busokelo, Wilaya ya Rungwe, mkoaniMbeya

Alisema taarifa za awali zinadaiwa kuwa, uongozi wa kimila kijijini hapo uliitisha kikao cha dharura ukihusisha viongozi wa vitongoji na vijiji jirani na ndipo waliamua kumtafuta na kumlazimisha marehemu kuhudhuria katika kikao hicho na kisha kuanza kumpiga na kupelekea kifo chake.

Alisema marehemu alikuwa akituhumiwa kuwa ni mshirikina kijijini hapo kwa kuwa anawaroga watoto na kuwa anajipatia mazao mengi ya mavuno ya viazi na kujipatia pesa zilizowezesha ujenzi wa nyumba yake aliyoweka marumaru na Gipsam pia kumiliki pikipiki moja huku akitarajia baada ya mavuno mazuri ya mwaka huu kununua gari la kutembelea.

No comments:

Post a Comment