Tuesday, October 28, 2014

BONDIA FRANCIS CHEKA AONA NGUMI HAZILIPI, ARUDI KUOKOTA CHUPA NA MAKOPO MTAANI.


Nyumbani kwa bondia Francis ‘SMG’ Cheka hakuishi pilika ambazo zinatokana na kazi ya chupa za plastiki anayofanya bingwa huyo wa zamani wa dunia wa WBF.
Nje ya nyumba yake kuna mafurushi kila kona yakiwa na ‘bidhaa’ tofauti ikiwamo chupa za plastiki, chupa za konyagi, chibuku na plastiki ngumu (ndoo na madumu) yaliyopasuka.
Cheka anavyookota chupa
“Mimi ndiyo mwanzilishi wa biashara hii hapa Morogoro, niliianza 2004 baada ya kuamua kuingia mtaani kuokota na kuziuza mwenyewe, wakati huo kilo moja niliuza kwa Sh100 na nilikuwa nikizunguka kutwa nzima kutafuta chupa mtaani,” anasema Cheka.
Anasema wakati anaanza kuokota chupa alikuwa na miaka mitano tangu aingie kwenye ngumi za kulipwa, lakini hakuwa maarufu.
“Nilikuwa nina uwezo wa kuzunguka na kuokota hadi kilo 100 kwa siku, japo ilikuwa kazi ngumu, lakini nilipata fedha nikanunua kiwanja maeneo ya Kilimahewa na kujenga nyumba kwa kazi ya kuokota chupa.
“Pia niliweza kujiandalia mapambano peke yangu kwa kazi hii, ambayo yalinijenga na kunipa umaarufu kwenye ngumi, nimejiandalia mapambano zaidi ya 15 kwa fedha niliyopata kwa kuokota chupa,” anasema Cheka.
Anasema vijana wengi wa Morogoro walianza kuokota chupa baada ya kuona Cheka amejenga nyumba kwa kazi hiyo, hivyo hakuwa na hiyana aliwafundisha kazi hiyo na wengine aliingia nao mtaani kuokota.
“Nilipoanza kucheza mapambano ya ubingwa wa Afrika nilisimama kuokota chupa nikawaachia wengine na mimi kuelekeza nguvu zangu kwenye ngumi, kijiwe changu nikamweka mtu wa kufanya hiyo kazi na nikawa na nanunua kwa watu wengine kisha mimi nauza tena.
“Kwa kipindi chote ambacho nilikuwa nimebanwa na masuala ya ngumi, mradi wangu huu uliyumba kwani kila niliyemwachia alikuwa na fikra za kuniibia, ilifikia mahali nikakwama kwani nilikopa fedha benki kuongezea nguvu kwenye biashara yangu ya makopo hivyo nilipaswa kulipa,” anasema Cheka.
Anavyookota chupa mtaani
“Watu wanashangaa mtu kama mimi kuokota chupa, lakini ndiyo kazi inayoniweka mjini, wiki iliyopita nilikuwa Msamvu (stendi kuu ya Morogoro) nakusanya chupa kwa bahati nikakutana na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia alishangaa kuniona naokota Chupa.
Credit:Mwananchi.

MBWA WAKUTWA WAKISHAMBULIA MABAKI YA MWILI WA BINADAMU


 Mabaki ya mwili yaliyokutwa katika eneo la kijiji cha Lupapila wilaya ya songea mkoaniRuvuma yakikusanywa na wataaramu kutoka hospital ya mkoa wa Ruvuma.




Fuvu la kichwa likiwa linazolewa 

 MIFUPA ya masalia ya binadamu  wa jinsia ya kiume  ambaye hakuweza
kufahamika  jina na kukadiliwa kuwa na miaka (30) yamegundulika na Zaujia Pilly (70) mkazi wa kijiji cha Lupapila wilaya ya songea mkoani

Ruvuma  wakati akienda kuchimba dawa za kienyeji baada ya kuwaona mbwa
wakishambulia sehemu za mabaki hayo.



Akiongea na MTANDAO HUU ofisini kwake jana Kamanda wa polisi mkoa wa
Ruvuma Mihayo Msikhela alisema kuwa tukio hilo limetokea oktoba 26
mwaka huu majira ya saa 9:45  alasiri  huko katika kijiji cha Lupapila
mtaa wa Mahinya kata ya Subira nje kidogo ya manispaa ya Songea

Alisema kuwa  inadaiwa siku hiyo ya tukio kwenye msitu wa uwanja wa
ndege ilikutwa mifupa ya binadamu  wa jinsia ya kiume  ikiwemo fuvu la
 Kichwa, Mbavu, Mikono na Miguu wakati sehemu ya kiuno na mapaja ikiwa
imeharibika vibaya.


Alifafanua kuwa mabaki ya mwili huo yaligunduliwa na Zaujia Pilly
wakati akienda kuchimba dawa za kienyeji kwenye msitu huo ghafla
aliwaona Mbwa wakifukuzana kugombania mabaki ya mwili wa binadamu.


Alieleza zaidi kuwa  Zaujia baada ya kugundua tukio hilo alitoa
taarifa katika uongozi wa serikali ya Mtaa na kisha taarifa
zilipelekwa katika kituo kikuu cha polisi cha songea mjini ambako
baadaye polisi walifika eneo la tukio wakiwa wameongozana na Daktari
kutoka hospitgali ya Mkoa wa Ruvuma ambaye aliyafanyia uchunguzi
mabaki ya mwili huo na kubaini kuwa  marehemu alikuwa amepigwa na kitu
kizito kichwani kwenye eneo la kisogo kilichopelekea kifo chake.



Kamanda Msikhela alisema kuwa  kufuatia tukio hilo hakuna mtu yeyote
anayehusishwa na jeshi la polisi mkoani Ruvuma linaendelea kufanya
uchunguzi wa kina juu ya kifo hicho.

BABU WA MIAKA 62 AMBAKA MJUKUU WAKE WA MIAKA MITANO,,HEBU ANGALIA ILIVYOKUWA TU

Mzee wa miaka 62, Rashid Mbogo amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za kumbaka mjukuu wake mwenye umri wa miaka mitano.

Mtuhumiwa huyo, mkazi wa Kijiji cha Vikonge kilicho katika Kata ya Mpandandogo wilayani Mpanda, alifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Chiganga Ntengwa na kusomewa mashtaka na mwendesha mashtaka ambaye ni mkaguzi msaidizi wa polisi, Naathaniel Silomba.
Ilidaiwa na mwendesha mashtaka huyo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Oktoba 19, mwaka huu saa 2:00 usiku akiwa nyumbani kwake.
Mwendesha mashtaka huyo alidai kuwa siku ya tukio, mtuhumiwa akiwa anasubiria chakula cha usiku wakati kikiandaliwa na mkewe, alimwita mjukuu huyo na kisha kumpakata mapajani. Alidai kuwa baadaye alivua nguo na kuanza kumbaka huku mtoto huyo akipiga kelele za kuomba msaada kwa kitendo cha babu yake.
Mwendesha mashtaka huyo alidai kuwa baada ya kusikia mayowe hayo, bibi wa mtoto huyo na majirani waliingia ndani ya nyumba na kumkuta mtoto sebuleni akiwa anatokwa na damu nyingi sehemu zake za siri huku analia kutokana na maumivu makali aliyokuwa ameyapata.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mshtakiwa alikana mashtaka hayo ambayo alikuwa amesomewa na mwendesha mashtaka.
Hakimu Chiganga aliieleza mahakama kuwa dhamana ya mshtakiwa iko wazi endapo mshtakiwa atatimiza masharti.
Mshtakiwa alitakiwa awe na mdhamini mmoja mwenye mali isiyohamishika yenye thamani ya Sh5 milioni.
Hata hivyo, mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana, hivyo alipelekwa rumande.

JWTZ WATEGUA BOMU LILOTEGWA KATIKA ENEO LA KITUO CHA KURUSHIA MATANGAZO CHA TBC SONGEA‏



Bomu lililotengenezwa kienyeji  kama linavoonekana katika picha.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela akipata maelekezo kutoka kwa mtaaram wa mabomu ambaye ni kamanda wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) kabla ya kulitegua bomu hili.


Hili ni eneo la tukio ambalo limezungushiwa mkanda huu wa pilisi uliandikwa hairuhusiwi kupita eneo hili,Lakini chini ya huo mti kama inavoonekana katika picha kukiwa na udongo umetifuliwa ndipo mahara ambapo lilitegwa bomu hili la kutengenezwa kienyeji pia hapo ndipo huwa wanakaa askari wa Usalama barabarani kwa kujikinga na jua ama kupumzika pindi wanapokuwa kazini
Bomu lililotengenezwa kienyeji


Mtaaramu toka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania akiweka vifaa vyake vya kutegulia bomu hilo lililo tengenezwa kienyeji.
Mtaaramu toka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania akiwa anaonyesha umahili wake alionao aweze kulitegua bila kuleta madhara yoyote yale katika jamii
 Jeshi la polisi kwa kushirikiana na Jeshi la Ulinzi la wananchi Tanzania(JWTZ) wamefanikiwa kulipua bomu lililotegwa katika eneo la kituo cha kurushia matangazo kilichopo mshangano cha shirika la utangazaji Tanzania (TBC) Songea Mkoani Ruvuma siku ya jana majira ya saa moja jioni.

Bomu hili linalosadikiwa kutengenezwa kienyeji nawatu wasiojulikana lilitegwa hatua  zinazokadiliwa thelathini kutoka kitika kituo kilipo katika eneo ambalo askari wa usalama barabarani wanakaa kwa ajili kufanya kazi zao za kila siku.

 Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela amesema kwamujibu wa wataalamu wa milipuko kutoka jeshi la Ulinmzi la wananchi wa Tanzania bomu hili linaonekakana limetengenezwa kienyeji.
ameitaka jamii kutoa ushrikiano kwa jeshi la polisi ili liweze kuwabaini watu waliowalipua kwa bomu lililotengenezwa kienyeji askari polisi watatu  wakiwa katika doria katika kata ya misufini manispaa ya songea.

Msikhela amesema Jeshi la polisi linafanya jitihada za kuwapata watu hawa wanaohusika na mtandao huu wa utegaji wa mabomu na ulipuaji, Aidha ameitaka jamii kutoa ushrikiano kwa Jeshi la Polisi ili liweze kuwabaini watu wanaousika na matukio ya namana hii.

Na hii ni mara ya pili katika manispaa ya songea kutokea kwa matukio haya ambapo tarehe Oktoba 16 mwaka huu askari watatu wa jeshi la polisi katika wilaya ya Songea mkoani Ruvuma,  walijeruhiwa kwa kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu la kutupwa kwa mkono ambalo lilisadikiwa kutengenezwa kienyeji, katika eneo la matarawe mjini songea mkoani Ruvuma.

Askari hao walikutwa na mkasa huo saa moja na nusu usiku wakati wakiwa katika doria ambao ni WP Felista Abel, PC John Kaduma na PC Ramadhani Ally

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Joseph Mkirikiti akizungumza na mtandao huu wa demasho  kwa njia ya simu amesikitishwa na kitendo hicho cha utegeji wa Mabomu ikiwa nikutaka kuhatarisha amani iliyopo katika mkoa huu wa Ruvuma.
Aidha amesema serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama watahakikisha wanawasaka na kuwakamata walewote wanaohusika na vitendo hivi.

TASWIRA ZAIDI ZA MKUTANO WA UKAWA JANGWANI


 -Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wakionesha hati za waraka walizotiliana saini za ushirikiano katika viwanja vya Jangwani Dar es Salaam leo. Kutoka kulia ni, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalimu Seif Sharifu Hamad , Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CUF, Ibrahim Lipumba na Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
 Waendesha bodaboda ambao ni wafuasi wa Ukawa wakiingia kwa maandamano katika viwanja vya Jangwani.
 Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalimu Seif Sharifu Hamad , akihutubia kwenye mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Chama cha NLD, Dk. Emanuel Makaidi akihutubia kwenye hafla hiyo kabla ya kutiliana saini waraka wa ushirikiano.
 Makatibu wakuu wa vyama vinavyuunda Ukawa, wakionesha ishara ya mshikamano baada ya kusaini waraka huo wa ushirikiano. Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrord Slaa, Katibu Mkuu wa CUF, Maalimu, Seif Sharifu Hamad na Katibu Mkuu wa Chama NLD, Tozi Matwange.
 Wananchi wakiwa kwenye mkutano huo.
 Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Tundu Lisu (kulia), akimkaribisha Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Chama cha Wananchi (CUF), Ismail Jusa Ladhu, kuzungumza katika mkutano huo.
 Wafuasi wa ukawa wakionesha vidole vitatu juu wakimaanisha kuikubali serekali tatu inayotakiwa na Ukawa.
 Wafuasi wa Chama cha Wananchi (CUF), wakiwa 
kwenye mkutano huo.
Vijana wa chama cha chadema wakiwa juu ya gari wakifuatilia matukio mbalimba yaliyokuwa yakiendelea uwanjani hapo. Imeandaliwa na mtandao

Wednesday, October 22, 2014

MAMA ALIYEPIGWA MSHALE KISA MAHARI



Ghati Bunyige akiwa amekaa kwenye benchi akisubiri huduma ya matibabu katika kituo cha afya cha Sirari wilayani Tarime mkoani Mara.
UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni! Mwanamke mmoja, mkazi wa Kitongoji cha Buriba, Kijiji cha Sirari wilayani Tarime, Mara aitwaye Bunyige Chacha (25) amepigwa mshale kwenye makalio na mumewe, Ghati Nyamarandi kisa kikidaiwa kuanzia kwenye pesa ya mahari na watoto. Akisimulia mkasa wake mzito uliompata Oktoba 5, mwaka huu majira ya jioni, mwanamke huyo alisema siku hiyo, mumewe alirudi na kumuuliza walipo watoto wao wawili (hakuwataja majina) ambao aliwaondoa nyumbani siku kadhaa nyuma bila kumwambia.
Akasema, alipomuuliza hivyo tu, ndipo mumewe akamjia juu na kumshambulia kwa matusi huku akisema watoto aliwapeleka kuuzwa eneo linaloitwa Nyumba Ntobu. “Mume wangu alifika nyumbani, nilipomuuliza watoto wako wapi ndipo akanifungia ndani ya chumba na kunishambulia kwa matusi.
“Kwa bahati nzuri nilibahatika kutoroka na kukimbilia kwa majirani lakini wakati nikivuka uzio wa mlango nilianguka, akapata nafasi, akanirushia mshale ulionichoma sehemu ya makalio, chini ya mguu wa kulia,”alisema mwanamke huyo. 
Ghati Bunyige akiongea na mwandishi wa habari kuhusiana na mkasa aliokumbana nao. 
Mama huyo aliongeza kuwa, watoto wake wawili waliuzwa Nyumba Ntobu na baba huyo kuchukua mahari bila kumshirikisha mke suala ambalo lilizua mtafaruku ndani ya nyumba mwanamke akidai watoto wake kila siku.
“Kwanza mume wangu alimwachisha masomo binti yetu wa kwanza ambaye alikuwa akisoma darasa la tatu katika Shule ya Msingi Sirari, akamuoza Nyumba Ntobu na kupokea mahari yeye.
“Baadaye akamwachisha masomo binti yetu wa pili aliyekuwa akisoma darasa la pili katika Shule ya Msingi Nyamaraga, nchi jirani ya Kenya, akamwozesha hukohuko Nyumba Ntobu na akapokea mahari peke yake.“Baadaye nilikuja kugundua kuwa, alikuwa akipokea mahari kwa siri kwa sababu alitaka kulipia mahari ili na yeye aoe mke wa pili ambaye anaishi naye tayari, lakini ni mke wa mtu,” alisema mwanamke huyo. 
Picha ya mama huyo akiwa katika usafiri akipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu.
Hivi karibuni, Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania (Tamwa) kupitia kwa mkurugenzi wake mtendaji, Valarie Msoka alifika kumwona mwanamke huyo na kumpa pole kwa tukio lililompata. Alimtaka mama huyo kumshitaki mumewe ili akamatwe na sheria ichukue mkondo wake.
Msoka amekuwa mstari wa mbele katika kupigania haki ya mama na mtoto na kulaani vitendo vinavyofanywa na jamii vya ukatili wa kijinsia kwa madai kuwa nimila au desturi za makabila husika.
Kwa upande wake, mwanasheria msaidizi wa Kata ya Sirari, Zablani Zablani aliliambia gazeti hili kuwa, mwanamke huyo alifika ofisini kwake kuomba msaada wa kisheria baada ya kujeruhiwa kwa mshale na mumewe ambapo yeye alimpeleka Kituo cha Polisi cha Sirari ili kupata PF3 na kwenda kupata matibabu katika Zahanati ya Alpha iliyopo mji mdogo wa Sirari.

MH. MBOWE ATOLEA UFAFANUZI WA PICHA YAKE YA KIMAHABA ILIYOSAMBAA MITANDAONI!


Week iliyopita Picha hii ilienea mitandaoni ukimuonesha Freeman Mbowe na Mkewe Wakibusiana

“Kwanza mke wangu alikuwa anatimiza umri wa miaka 50 ya kuzaliwa, vilevile firstborn wetu Dudley alikuwa amemaliza shahada yake ya kwanza Chuo Kikuu cha Sussex, Uingereza, kwa mambo hayo mawili, tuliona ipo haja ya kufanya sherehe, ukizingatia watoto wetu wengine wawili Nicole na Denis walikuwa wamerejea nchini kwa sababu nao wanasoma nje ya nchi.

“Siku hiyo ya tukio ilikuwa Jumapili, tulianza kwa kwenda kanisani Azania Front tukatoa sadaka, baada ya hapo tulikwenda Serena Hotel kwenye Ukumbi wa Kivukoni ambako chakula cha mchana kilikuwa kimeandaliwa, tukajumuika na ndugu wengine pamoja na marafiki.