Friday, September 26, 2014

MAVAZI ALIYOVAA MREMBO HUYU YASABABISHA STEVE NYERERE KUZOMEWA


NYOTA wa kuigiza sauti za watu maarufu aliye pia mwigizaji wa sinema za Kibongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ wikiendi iliyopita alijikuta akiaibika kwa kuzomewa na kupopolewa kwa chupa za maji na mashabiki wa Klabu ya Simba baada ya kuingia uwanjani na demu aliyevaa ‘kihasarahasara’.Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’akiwa na mrembo huyo.Ishu hiyo ilijiri Jumamosi ya Septemba 20, 2014 ndani ya Uwanja wa Jamhuri mjini hapa wakati wa pambano kati ya Yanga na Mtibwa Sugar katika Ligi Kuu Tanzania Bara ambapo wenyeji walishinda 2-0. Steve alitinga uwanjani saa 11:00 jioni akiwa na demu huyo mrefu kwake,aliyetinga kipensi cha jinzi kifupi na tisheti ya njano na kijani (zinazotumiwa na Yanga).
Wakati wawili hao wakipita kwenye jukwaa la mashabiki wa Simba, ndipo walipozomewa na wengine kuwarushia chupa za maji kwa kile kilichodaiwa kuwa, demu huyo alivunja maadili ya Kitanzania kwa kuvaa kihasara hadharani.
Mrembo huyo akikatiza mbembezoni mwa uwanja.Baadaye mwandishi wetu alimfuta Steve na kuzungumza naye kuhusu tukio hilo ambapo alisema: “Wale kunizomea ni haki yao ila mimi na mwenzangu tumeona kama wametushangilia.” 
Alipoulizwa uhusiano wake na demu huyo,Steve aligoma kujibu badala yake alikimbilia kwa mwandishi mwingine na kuomba msaada. Mrembo huyo alipotakiwa kuzungumzia tukio hilola kuzomewa na sababu za yeye kuvaa vile, alijibu kwa mkato: “Kuzomea ni haki yao, mimi nawaona kama washamba tu.

No comments:

Post a Comment