Thursday, October 9, 2014

AFARIKI DUNIA AKISHINDANA KUNYWA POMBE HARAMU TOKA MALAWI



NA BARAKA LUSAJO, MBEYA
KIJANA mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Wajibu Astofu (16) mkazi wa kijiji cha Lupata kata ya Ipoma katika Halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe Mbeya amepoteza maisha baada ya kushindana kunywa pombe haramu za viroba toka nchini Malawi zilizopigwa marufuku kuingizwa na kusambazwa nchini.
 
Akizungumza jana na waandishi wa habari mwenyekiti wa kijiji hicho Pius Dibile alisema kuwa kijana huyo aliweka mashindano na mwenzake ya kunywa pakiti kumi na moja pome hizo za viroba vyenye alcol 35 na kuwa atakayemaliza angepata zawadi.
Alisema kijana huyo ndiye alikuwa wa kwanza kuanza mashindano hayo na kufanikiwa kumaliza pakiti zote kumi na moja na ndipo alipoanza kuishiwa nguvu na kujipigapiga na kupelekea serikali ya kijiji na baadhi wa wanakijiji kufika eneo hilo na kufikia hatua ya kumkimbiza katika hospitali ya misheni ya Itete iliyokaribu na eneo hilo.
Dibile alisema kuwa alipofika katika hospitali hiyo madaktari wa zamu walijaribu kuokoa maisha yake kwa kumuwekea mashine ya kumsaidia kupumua lakini hali ikazidi kuwa mbaya na hatimaye akakata roho na kuwa viroba hivyo vilimkausha maji mwilini na kushindwa kupumua.

Aliongeza kuwa Serikali ya Kijiji hicho kiliitisha kikao cha dharula na kutaka kumuajibisha aliyedhamini mashindano hayo kwa kununua pombe hizo zilizopelekea umauti wa kijana Astofu na kuwa walikuwa wamechelewa kwa kuwa alikimbilia kusikojulikana na jitihada za kumpata zinaendelea.
Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chripin Meela aliwataka wananchi kutii agizo la Serikali na kwamba wao walipopiga marufuku waliona madhara ya pombe hizo kwa watumiaji ambapo bado wafanyabiashara wasio waaminifu wanaingizo pombe hizo na kuzisambazo kwa njia za panya na kusababisha maafa kwa wananchi.

 
Meela aliitaka serikali ya kijiji kumtafuta kijana huyo aliyedhamini mashindano ya pombe hizo na kumkamata ili afunguliwe kesi ya mauaji ili sheria ifuate mkondo wake na iwe fundisho kwa wengine na kuwa wananchi watoe ushirikiano pindi wawaonapo wafanyabiashara hao wanaposafirisha biashara hizo.


No comments:

Post a Comment