Friday, October 10, 2014

AJALI ZA BARABARANI ZAZIDI KUWAMALIZA WATANZANIA








Gari ya Dar Xpress lifanyalo safari zake Kati ya Dar - Rombo likiwa limepata ajali jana jioni eneo la Marangu _Mamba. Watu kadhaa walijeruhiwa
 
 NA HUKO TABORA BASI LA NBS LAPINDUKA BAADA YA KUGONGA PUNDA

 

Habari zilizotufikia  kutoka mkoani Tabora ni kwamba basi la NBS lililokuwa linatoka jijini ,Mwanza kwenda Mpanda,limegonga punda leo asubuhi na kupinduka katika eneo la Nzega Ndogo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia ni kwamba mtu mmoja,ambaye ni kondakta wa basi hilo amefariki dunia na majeruhi wamekimbizwa katika hospitali ya wilaya ya Nzega.Inaelezwa kuwa majeruhi 12 wako mahututi

 

No comments:

Post a Comment