Friday, October 3, 2014

VITA YA WABUNGE MAMBO YAWEKWA PEUPEEEEE



Mbunge wa CCM kupitia kadi ya Umoja wa Vijana (UVCCM), Mkoa wa Arusha, Catherine Valentine Magige . IMEFICHUKA! Madai ya Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Geita, Vicky Paschal Kamata kuwatumia meseji za kashfa wabunge wenzake, Lucy Thomas Mayenga (CCM) na Catherine Valentine Magige (UVCCM)Mkoa wa Arusha sasa mambo hadharani.Kwa mujibu wa chanzo chetu, wabunge hao warembo wako katika vita baridi ikiendeshwa chini kwa chini kwa Cathy (pichani) na Lucy kudai kwamba wamekuwa wakitumiwa meseji zenye kejeli na kashfa nzito kutoka kwa mheshimiwa Vicky.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, licha ya sababu kutokuwa wazi sana, lakini madai ni kwamba wana bifu linalokimbilia mwezi wa nne sasa.
“Unajua si rahisi wao kuweka wazi bifu lao, lakini wenyewe watakuwa wanajua nini kiini, ukifuatilia utagundua kuwa maisha yao yamekuwa ni ya vikundivikundi, akina Lucy wana kundi lao na Vicky ana la kwake,” kilisema chanzo hicho.
Mbunge wa CCM kupitia tiketi ya Umoja wa Vijana, Lucy Thomas MayengaKWA NINI VICKY?
Chanzo kiliendelea kuanika kwamba, baada ya meseji zinazodaiwa kukosa staha kutumwa na asiyejulikana kwenda kwenye simu za mkononi za Cathy na Lucy, waheshimiwa hao hawakupembua sana mchele, moja kwa moja wanadaiwa kumtaja hasimu wao kwenye vyombo vya dola kuwa huenda anahusika na ‘utundu’ huo. 
POLISI WAFUATILIA MINARA YA SIMU
Duru za kipolisi zinadai kuwa kufuatia waheshimiwa hao kumlalamikia Vicky, wana usalama hao walianza kuchunguza mawasiliano yake ambapo walibaini mambo makuu mawili. 
KWANZA, baadhi ya meseji hizo zilionesha kutumwa kwa kupitia mnara wa simu uliopo maeneo ya bunge. PILI, kuna meseji iliwezeshwa kusafiri kwa nguvu ya mnara uliopo eneo linaloitwa Uwanja wa Ndege ambapo inadaiwa Mheshimiwa Vicky ndiko anakoishi.
 
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Geita, Vicky Paschal Kamata SERIAL NUMBER
Pia yapo madai kwamba, polisi hao walikwenda kitaalam zaidi na kubaini kwa kutumika namba zilizomo ndani ya simu eneo la kuwekea betri (serial number) ambazo zilionesha kuwa, laini iliyokuwa ikituma meseji za kuudhi kwa waheshimiwa hao pia imekuwa ikutumia na laini ambayo polisi walimjua mhusika, ingawa wasemaji wake wamesita kuthibitisha. 
POLISI NYUMBANI KWA VICKY
Habari zaidi zinadai kuwa, Jumanne iliyopita, polisi mkoani Dodoma walifika nyumbani kwa mheshimiwa Vicky na kufanya uchunguzi kama wanaweza kupata simu yenye laini iliyoripotiwa na akina Mayenga (pichani) kwamba imekuwa ikiwakashifu kwa meseji lakini hawakufanikiwa kukuta chochote. 
Alipotafutwa Vicky ili kujua undani wa meseji hiyo juzi, simu yake haikuwa hewani. Kwa upande wake Lucy ambaye alidai kutumiwa meseji za matusi katika gazeti moja (siyo la Global), naye simu yake iliita bila majibu, huku Cathy akishindwa kupatikana na kulifanya gazeti hili kuzidi kuchimba kwa kina sakata hili ili kupata mbivu na mbichi na kuzianika bila kusitasita.

No comments:

Post a Comment