Monday, September 15, 2014

MSTAHIKI MEYA JERRY SILAA AMLILIA IGP ERNEST MANGU.


MEYA wa Ilala, Jerry Silaa amemuomba Mkuu wa Jeshi la Polisi Ernest Mangu kutokubali askari wake kuwa wakala wa sheria za barabara.
 
Silaa alisema hayo katika uchaguzi wa Naibu Meya uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Alisema askari wengi wanajichukulia sheria mkononi kwa kuwakamata baadhi ya madereva kwa madai kuwa magari yao yamezidi viwango hivyo yanaharibu barabara pasipo kuzingatia sheria.

Pia Silaa ameitaka Mahakama ya Jiji kuacha kuwakamata wananchi kwa makosa yasiyofaa na ambayo hayana uhakika, kuwatoza faini zisizo na msingi na kuwaweka mahabusu bila hatia.

“Ninapigiwa simu na kupewa malalamiko mara kadhaa wananchi wanaonewa bila sababu za msingi na kuwafanya wajione sawa na wakimbizi katika nchi hii,” alisema Silaa.

Pamoja na hayo alisaini mkopo wa sh bilioni 1.2 kutoka Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) kwa ajili ya kununua magreda mawili ya kutengeneza miundombinu ya halmashauri.

MUNGU WA KIHINDI ATENGENEZEWA KITAMBULISHO.




Maafisa wa utawala nchini India, wanachunguza ambavyo kitambulisho cha elektroniki kimetengezwa kikiwa na picha ya Hanuman mungu wa kihindi na kutumwa kwa njia ya posta.
Kitambulisho hicho kina picha ya mtu anayejulikana kama Hanuman kutoka kwa kipindi kilichojuolikana kama Ramayana, akiwa amevalia mikufu ya dhahabu na taji la kifalme.Kitambulisho chenyewe kilipatikana wakati mfanyakazi wa posta alijaribu kukifikisha kwa mtu aliyetumiwa ila hangeweza kupata anwani ya mtu yeyote anayejulikana kama Hanuman.


Alipoangalia kwa picha , aligundua kuwa huenda ilikuwa mchezo wa danganya toto. Bado haijaulikana ni nani aliyeweka alama ya kidole kwenye kitambulisho hicho.

Hanuman alijulikana kama mtoto wa mungu wa kihindi aliyejulikana kama Pawan, na kitambulisho chenyewe kina namba ya simu na anwani ya sehemumoja katika jimbo la Rajasthan. Hanuman alijulikana kama mungu wa kihindi mwenye nguvu za ajabu na mtiifu sana 
Hanuman alijulikana kama mungu wa kihindi mwenye nguvu za ajabu na mtiifu sana.


 
Kwa kawaida Hanuman huonekana akiwa na uso wa Nyani pamoja na mkia. Kuna hekaya za kale kuhusu Hanuman kote nchini India.

Mfanyakazi huyo wa posta Heeralal Saini, alikirejesha kitambulisho hicho kwenye kituo cha posta baada ya kukosa kumpata mtu kwa jina la Hanuman.

'Hanuman ni nani?'
Hanuman ni mmoja wa miungu wanaobudiwa na watu nchini India na pia kuna hekaya nyingi tu kwenye vitabu vya kihindi kumhusu. Huonekana kama binadamu mwenye uso wa Nyani na mkia mrefu.

Mara kwa Mara yeye husemekana kuwa mtoto wa mungu mwingine wa kihindi Pawan na anasifika kwa kuwa mtiifu na mwaminifu pamoja na kuwa na nguvu

SERIKALI YATANGAZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KUFANYIKA DESEMBA 14





KIPENGA cha kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa, kinatarajiwa kupulizwa Novemba 30 mwaka huu na uchaguzi kufanyika Desemba 14 chini ya sheria zilizopo.
 
Taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), iliyotumwa katika vyombo vya habari jana, ilifafanua kuwa uchaguzi huo utafanyika kwa kuzingatia masharti ya sheria za serikali za mitaa na kanuni za uchaguzi huo.

 
Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyosainiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, sheria hizo zimetungwa na ofisi yake, baada ya kuwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu, asasi za kiraia na wadau mbalimbali.

 
Kwa uamuzi huo, wagombea wa nafasi zinazowaniwa za mwenyekiti wa mtaa, kijiji na kitongoji na nafasi za ujumbe wa serikali za vijiji na kamati za mitaa, wametakiwa wawe wanachama na wadhaminiwe na chama cha siasa chenye usajili wa kudumu.

 
Ratiba
Katika ratiba iliyotolewa sambamba na taarifa hiyo, wasimamizi wa uchaguzi wameelekezwa kutoa tangazo la majina na mipaka ya mitaa, vijiji na vitongoji, siku 50 kabla ya siku ya uchaguzi kwa kuzingatia Kanuni ya 6 ya Kanuni za Uchaguzi wa Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, ngazi ya vijiji, vitongoji na mitaa ya mwaka 2014.

 
Baada ya hatua hiyo, wasimamizi hao wa uchaguzi watateua majina ya wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi mara baada ya kusambazwa kwa kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa.

 
Katika eneo lake, msimamizi wa uchaguzi atatoa maelekezo ya uchaguzi siku zisizopungua 28 kabla ya siku ya uchaguzi kwa mujibu wa Kanuni ya 7(1), 8(1) ya kanuni za uchaguzi wa viongozi wa mamlaka za serikali za mitaa, ngazi ya vijiji, vitongoji na mitaa za mwaka 2014.

 
Aidha msimamizi wa uchaguzi atateua ofisa wa umma mwenye sifa na uadilifu, atakayeandikisha na kuandaa orodha ya wapiga kura siku 21 kabla ya siku ya uchaguzi kwa mujibu wa Kanuni 8 na 9 ya Kanuni za Uchaguzi wa Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa za mwaka 2014.

 
Uteuzi wagombea

 Baada ya hatua zote hizo za awali kufanyika, Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi atabandika orodha ya wapiga kura mahali pa matangazo ya uchaguzi na kutunza kumbukumbu zake, baada ya kusambazwa kwa kanuni za uchaguzi na kufanya uteuzi wa wagombea siku zisizopungua 20 kabla ya siku ya uchaguzi.

 
Ratiba iliyotolewa pia inaonesha kwamba Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, katika muda wa siku mbili tangu siku ya uteuzi kufanyika, atasikiliza na kutoa uamuzi katika muda usiozidi siku mbili kwa mapingamizi mbalimbali, kuanzia siku ya kupokea pingamizi husika.
Aidha kutakuwepo na Kamati ya Rufaa, ambayo wajumbe wake watateuliwa na Katibu Tawala wa Mkoa na katika uteuzi wake, Katibu Tawala atazingatia hali halisi ya watumishi wa umma walioko katika wilaya husika.

 
Kamati hiyo ya Rufaa, itateuliwa siku saba kabla ya siku za uteuzi wa wagombea kwa mujibu wa Kanuni ya 16(4) ya Kanuni za Uchaguzi wa Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa za mwaka 2014.

 
Kampeni
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, kampeni za uchaguzi zitafanyika wiki mbili za mwisho kabla ya siku ya uchaguzi na zitafanyika kwa muda wa siku 14 na zitamalizika siku moja kabla ya siku ya uchaguzi kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa za mwaka 2014.

 
Ili kufanikisha uchaguzi huo, wananchi wametakiwa kujiandikisha katika Rejista ya Wapigakura, itakayoandaliwa siku ishirini na moja kabla ya siku ya uchaguzi; na uchaguzi utafanywa kwa kutumia karatasi maalumu za kupigia kura.

 
Aidha kura zitapigwa na kutumbukizwa kwenye masanduku ya kupigia kura na kama kawaida, uchaguzi utafanyika katika ngazi ya kitongoji na mitaa katika sehemu ya faragha na hakutakuwa na mikutano ya uchaguzi katika ngazi za vijiji.

 
Uchaguzi uliopita

 Katika uchaguzi uliopita wa serikali za mitaa, CCM kilipata ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 90 ya kura zote zilizopigwa, hatua iliyochukuliwa na wachambuzi wengi kuwa ni dalili kuwa chama hicho kilikuwa kinakwenda kushinda Uchaguzi Mkuu wa 2010.

 
Uchaguzi wa mwaka huu, mbali na kuendelea kutumika kutoa ishara za uchaguzi mkuu ujao, pia utakuwa na umuhimu wa ziada katika kupima uimara wa makubaliano ya vyama vikubwa vya siasa, vilivyounda kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wakati wa mchakato wa Katiba mpya na kukubalika kwao kwa wananchi.

 
Tayari viongozi wa vyama hivyo, Chadema, CUF na NCCR Mageuzi, walishatoa kauli ya kuhoji kwa nini uchaguzi huo unachelewa, wakihofia kuwepo wanachoita mchezo mchafu wa kuwashitukiza.

 
Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe, alinukuliwa akidai Serikali imeshindwa kutangaza tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi huo, lakini pamoja na hitilafu hiyo, chama hicho kimeshatoa taarifa kwa wanachama wake kujiandaa kugombea.

 
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Magdalena Sakaya, alinukuliwa akidai kwa kuwa uchaguzi huo hufanyika Septemba kila mara na kwa kuwa mwaka huu kuna Bunge Maalumu la Katiba linalomalizika Oktoba, Serikali ilitakiwa kulitambua hilo na kutoa ratiba mapema.

 
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Chadema, John Mnyika alisema kutokana na mchakato wa kupata Katiba mpya kusuasua, vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi vinatakiwa kushirikiana ili kushinda viti vingi.

MBOWE ATANGAZA MAANDAMANO, MIGOMO ISIYOISHA.


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman Mbowe, akihutubia Mkutano Mkuu wa uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam jana.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe (pichani), ametangaza maandamano na migomo isiyokoma nchi nzima kushinikiza kuvunjwa Bunge Maalumu la Katiba, kwa madai kwamba limekuwa likitafuna fedha za umma huku wakijua kwamba Katiba haiwezi kupatikana.


Alitangaza hilo wakati akihutubia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chadema unaoendelea jijini Dar es Salaam jana uliojumuisha zaidi ya wajumbe 922 kati ya 1,049.

Wajumbe wa mkutano huo walitarajiwa kumchagua Mwenyekiti na viongozi wengine wa ngazi ya taifa wa chama hicho.

Hata hivyo, Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), hakusema maandamano na migomo hiyo itaanza lini, badala yake alitaka kila kiongozi wa wilaya kuwasilisha mkakati wa utekelezaji kwenye chama hicho taifa.

Viongozi wengine ambao vyama vyao vinaunda Ukawa waliohudhuria mkutano huo ni Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Mwenyekiti wa NLD, Dk. Emmanuel Makaidi. Alisema anaitaka serikali na uongozi wa Bunge kuahirisha Bunge hilo haraka iwezekanavyo, vinginevyo wanachama wa Chadema wataingia mtaani kwa kuwa na maandamano yasiyo na ukomo.

“Tusifanywe wajinga. Maoni ya Watanzania yanachakachuliwa, fedha zinaliwa...natangaza azimio la mkutano mkuu ni kushirikisha umma kwa maandamano na migomo kwa kibali cha polisi na bila kibali...siko tayari kwa mazungumzo tena, nchi haiwezi kubadilika kwa mazungumzo ambayo ni kuchezea fedha za umma,” alisema Mbowe.

Alisema viongozi mbalimbali, wananchi na mashirika binafsi wameongea kutaka Bunge lisitishwe, lakini limeendelea kutumia fedha za umma bila huruma, huku wakijua hakuna Katiba itakayopatikana.

Mbowe, ambaye anatetea nafasi ya Mwenyekiti baada ya kumaliza muda wake, alisema yapo mazingira yanayolazimisha kuvunja sheria ili kupenyezwa ukweli, ambao ni kutumia maandamano na migomo isiyo na kikomo.

“Najua watatumia nguvu na kututisha na silaha za moto. Lakini sisi tutasonga mbele,” alisema.
Alitangaza maazimio matano ya mkutano mkuu, ambayo ni mtandao wa chama na wananchi kushirikiana na Ukawa kila wilaya kufanya maandamano na migomo hiyo.

Wanasheria wote wa Ukawa wakutane na kuona uwezekano wa kufungua kesi dhidi ya wajumbe wa Bunge hilo.
Lingine ni kuwashambulia kisiasa wajumbe wa Bunge hilo, ambao ni wabunge katika majimbo yao kwa kuhakikisha hawarejei tena katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Azimio lingine ni kwa Mkoa wa Dodoma kufanya maandamano kuelekea kwenye kumbi za vikao vya Bunge ili kuwafanya wajumbe wasiendelee na Bunge hilo kwa kuwa kinachoendelea ni wizi, matusi na ukatili wa dhahiri dhidi ya Watanzania.

“Nawaagiza wajumbe wote wa mkutano mkuu kuleta mipango ya utekelezaji wa maazimio haya haraka kwa ajili ya kuanza utekelezaji,” alisema.
Mbowe, ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alisema mipango mingine ya kimkakati itaendelea baina ya viongozi wa Ukawa.

Alisema nchi iko kwa ajili ya mabadiliko, lakini tatizo kubwa ni uoga wa Watanzania, hivyo ni wajibu wa viongozi hao kuwaimarisha wananchi kwa kuwajenga kifikra.

“Sitaki fujo na wala sikusudii nchi iingie kwenye fujo. Tunataka haki ya wananchi. Tumeongea sana. Haitoshi kwa sasa. Sipo tayari kuzungumza, bali kuchukua hatua…wanaoendelea na vikao na kujitajirisha na fedha haramu ni wizi, ukatili na ubatili kwa mwenyekiti kubadili rasimu, sheria na kanuni atakavyo,” alisema Mbowe.

Aliongeza: “Napenda serikali ya Chama Cha Mapinduzi itambue katiba bora haipatikani kwa kuamuliwa kupiga kura au wingi, bali kwa maridhiano…viongozi wa dini, asasi na wananchi wamesema, lakini mwenyekiti anacheza na kodi zetu,” alisema Mbowe.

Rushwa
Mbowe alisema kiongozi yeyote wa Chadema ambaye atakamatwa na rushwa, atachukuliwa hatua, ikiwamo kufukuzwa uanachama na kuwataka wanachama kuacha kufikiri kuwa ndani ya chama hicho ni mahali pa kutoka kimaisha.

Alisema wanachama na viongozi wengi wa chama hicho wanajitolea kwa kuwa wana kiu ya mabadiliko na rushwa siyo sehemu ya maisha yao ya kila siku, bali kujali maisha ya kizazi cha sasa na kijacho.

Mbowe alisema ndani ya chama hicho hakuna ulaji, bali kufanya kazi kwa kujitolea zaidi na kwamba, chama hicho hakijiendeshi kwa kutegemea fedha za wahisani na hawajapewa fedha zozote kwa ajili ya mkutano huo.

HISTORIA YA CHADEMA
Mbowe alitumia mkutano huo kueleza historia ya chama hicho, huku akifananisha na treni inayokwenda Kigoma yenye vituo mbalimbali na katika kila kituo kutakuwa na abiria watakaoteremka na kupanda, huku wengine hawatateremka hadi wafike mwisho, ambako ni Ikulu.

“Jinsi chama kinavyozidi kukua, ndivyo kinavyozidi kushambuliwa…nia, uwezo na sababu tunayo. Hivyo, tunasonga mbele. Uzoefu wa miaka 23 umetosha. Sasa tunastahili kuingia Ikulu,” alisema.

“Hatutakubali msaliti kumuonea aibu. Hakuna mwenye sifa na umaarufu kuliko Chadema. Hiki ni chama kinachoundwa na damu, majeraha, uvumilivu na kujitoa kwa hali na mali kwa wanachama wake. Hivyo, hatutakubali kuvurugwa,” alisema.

Kwa mujibu wa Mbowe, kazi ya chama cha siasa ni kujenga fikra za wananchi na siyo kujenga maofisi na kwamba baada ya uchaguzi wa chama, wataanza mafunzo kwa viongozi.

DK. SLAA
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alitaka kuwekwa wazi kwa daftari la kudumu la wapigakura, ikiwa ni pamoja na wadau kushirikishwa kwa uwazi kuliko hali ilivyo sasa kwa chama kimoja kushirikishwa, huku vingine vikiachwa na kwamba hali iliyo itaondoa nchi kuingia kwenye machafuko.

Alitaka kuundwa kwa tume ya kimahakama kuchunguza vifo vya raia vilivyofanywa na polisi kwenye maeneo mbalimbali nchini, huku kukiwa na kesi nyingi zinazofunguliwa dhidi ya viongozi wa chama hicho.

DK. LWAITAMA
Mwanazuoni Exaveri Lwaitama, alisema Ukawa haihitaji kusajiliwa, bali ni mapambano ya mabadiliko ambayo yapo kichwani mwa Watanzania.
Aliwataka kutoangalia mtu mmoja mmoja kupata uongozi, bali uwezo wa mtu bila kujali chama anachotoka.


PROFESA LIPUMBA
Profesa Lipumba alisema tunu za kusimamia uwajibikaji zimeainishwa kwenye rasimu ya Katiba na kwamba baada ya CCM kuisoma na kuona inawawajibisha, wameamua kuchakachua kwa kuondoa mambo muhimu.

Alisema Ukawa imejenga kuaminiana na kuaminika kwa maoni ya Watanzania na kwamba Bunge linaendelea, huku wakijua hawawezi kupata katiba kwa kuhalalisha uwapo wao Dodoma, huku wakiendelea na matumizi mabaya ya fedha za umma.

“Lengo letu ni kufika mahali pa kufanya mkutano wa vyama vyote vya Ukawa na kupendekeza mgombea mmoja wa urais, tushirikiane. Vyama ni nyenzo katika kupata haki za raia kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa rasilimali zetu kutumika kwa manufaa ya wote,” alisema.

Alisema ni aibu kwa Tanzania kuwa na watoto wenye utapiamlo, kwani kati ya watoto 100, 42 wanakosa lishe bora na kina mama wakikosa huduma bora za afya.

MANGULA
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula, alisema siasa siyo chuki, bali ni tofauti za kisera, kiitikadi na falsafa na kwamba utaratibu wa kukutana mara kwa mara utawaweka pamoja.

MBATIA
Mbatia alisema Ukawa ni nyezo ya kurekebisha makosa ya nyuma na sasa wanasonga mbele bila woga na ni vyema CCM ikatambua kuwa nchi ni ya wote na siyo mali yao.

Alivitaka vyama vya CCM, Chadema na CUF kuzungumza kwa kuhakikisha mama ambaye ni Tanzania, anapewa upendo na kunyonyesha mtoto wake akue vizuri na kuacha mifarakano na kutupiana maneno.

Alisema kuendelea kwa Bunge hilo kwa kupoteza fedha za umma ni lazima waonyeshe chuki ya wazi na Ukawa wataendelea kushirikiana na kuaminiana.

DK. MAKAIDI.
Dk. Makaidi alisema Ukawa ni ligi ya kuleta maendeleo Tanzania na wataogelea na kuzama pamoja kwa kuwa ndilo tumaini kwa Watanzania.


Alisema ndani ya Ukawa kuna wapiganaji mahiri wanaoweza kuleta mabadiliko chanya na ni vyema kila chama kikatoa maazimio juu ya suala la uchaguzi wa serikali za mitaa ambao haueleweki.

JAJI MUTUNGI.
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, aliwapongeza Chadema kwa kudumisha demokrasia kwani chama kufanya mkutano mkuu ndiyo demokrasia.

Alisema hakwenda kwenye mkutano huo kama mtafiti au mchambuzi wa mkutano mkuu, bali kwa cheo chake.

TCD.
Mkurugenzi wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Daniel Loya, alisema demokrasia ndani ya vyama vya siasa ni tatizo kubwa na kufanya mkutano mkuu na kuchagua viongozi ni hatua kubwa ya kidemokrasia.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na baadhi ya Mabalozi wa nchi mbalimbali, viongozi wa dini, taasisi, wabunge wa chama cha ODM Kenya, vyama vya siasa kutoka nchi mbalimbali na mashirika ya kimataifa.

BABA WA FAMILIA AJIFUNGUA MTOTO: CHEKI PICHA HAPA



Familia inayoundwa na wanandoa Bianca na Nick Bowser, ni familia yenye furaha lakini iliyowashangaza wengi baada ya Nick ( baba wa familia) kupata ujauzito na kujifungua. 

Iko hivi; Nick ambaye ana umri wa miaka 27 hivi sasa, alizaliwa na jinsia ya kike na kupewa jina la Nicole na wazazi wake, lakini aliamua kubadilika na kuishi kama mwanaume (transgender/jike dume) tangu miaka saba iliyopita. Na hii ilichangiwa pia na sura na umbo la kiume alilokuwa nalo. 

Hali ilikuwa hivyo pia kwa Bianca ambaye ana umri wa miaka 32 hivi sasa, yeye alizaliwa mwanaume na kuitwa jina la Jason, lakini kutokana na kuwa na sura nzuri na umbo la kike, na hisia zake za kutaka kuishi kama mwanamke, alibadili aina ya maisha na kuishi kama mwanamke kamili. 
Wawili hao walikutana na kuamua kufunga ndoa huku wakiyabadilisha kabisa maisha ya wana ndoa, Nick akiwa baba wa familia anaevaa na kuishi kama mwanaume. Mkewe Bianca (ambaye ni mwanaume) yeye alibadili na kuishi kama mwanamke kamili akiihudumia familia yake na kuvaa mavazi ya kike kama mama siku zote.
Lakini kwa mujibu wa Bianca, wawili hao wamekuwa wakishiriki tendo la ndoa kama kawaida kwa kuwa wanaamini kubadili kwao mfumo wa maisha hakuwezi kubadili viungo vyao vya mwili. Matokeo yake, baba alipata ujauzito na kujifungua. Na hivi sasa wana watoto wawili.
Cha kushangaza ni kwamba wana ndoa hao hawawachanganyi majirani tu, lakini pia wamewaficha hadi watoto wao wadogo ambao wanaamini kabisa kuwa Bianca ndiye aliyewazaa na baba yao ni Nick. Lakini siri hii itakaa hadi lini ili hali majirani wanajua na wa wanandoa hao wameshaeleza kwenye vyombo vya habari? 
 Sifahamu lini tutaanza kuwaambia ukweli, labda wakati ambapo Kai (mtoto wao mkubwa) atakapokuwa na miaka sita hivi, lakini wanatakiwa kuwa na umri mkubwa wa kutosha kuelewa. Ni muhimu wakifahamu kwa kuwa ni siri kubwa ya kuwaficha watoto wako na kama wakifahamu kupitia njia nyingine watachukia sana.
Alisema Bianca. 

Biana aliendelea kujitetea kuwa kuwa jike dume/ dume jike haielezi jinsi ulivyo. Ni kama kuwa na rangi nyeupe, nyeusi, mnene au mwembamba haielezi kitu kuhusu jinsi ulivyo. 

Kwa upande wa Nick, anasema mara ya kwanza alipopata ujauzito wa Kai alibadilika na kuishi kama mwanamke, hivyo ikawa kama yeye na mumewe wote ni wanawake. Wengi walidhani wanacheza mchezo wa kusagana. 
Lakini alipopata ujauzito wa pili ndipo alipoamua kuishi maisha yake ya kawaida kama baba na kitumbo chake. Hali ilimnyima raha mbele za watu waliokuwa wanamshangaa sana.

MWANAMKE AWABAKA WATOTO WAWILI WA KIUME

Awalazimisha Wamuingilie Kimwili Usiku wa Manane

Vitendo vya ngono nchini Uganda vimesababish maambukizi makubwa ya UkimwiMwanamke wa miaka 37, Adong anashikiliwa na Polisi huko Gulu nchini Uganda kwa kosa la kuwaingilia watoto wawili wa kiume wenye umri wa miaka 14 na 15 ambao vilevile ni wenye undugu na yeye!Aliwaingilia watoto hao alipokwenda kuwatembelea wazazi wao na ndipo usiku akanyata na
kuingia chumbani mwao na kuwashawishi bila aibu wamle uroda!Ilitokea baba yao aliwasikia wanae wakijadili juu ya "utamu" na ndipo akaiarifu polis nao hawakuzubaa na kumtia ndani. Akitiwa hatiani anaweza kufungwa miaka 7 au maisha!Mambo hayo!

Friday, September 12, 2014

HII MPYAAAAAAAAAAAAA

KWA NINI WAHESHIMIWA WOTE HAWAONYESHI HAYA KAMA HUYU MHE.MWIGULU NCHEMBA??KAVUNJA REKODII..HEBU ANGALIA ALICHOFANYA


Nilifanikiwa kuonana na Mhe.Mwigulu hakuwa na mengi ila nakumbuka tu maana alianza kwa kuniambia hivi:

 Mwigulu Nchemba:

Namshukuru sana Mungu,Nimetimiza Miaka 10 ya NDOA yangu.Pongezi Nyingi sana Kwa Mama Joshua (Mke Wangu),Familia Yangu,Ndugu,Jamaa na Watanzania Wote kwa Maombi Yenu.
Yohana.13.34.Anasema pia jukumu la kulea watoto wetu ni letu wote ndiyo maana kwa mapenzi ya dhati nikiwa nyumbani natamani kumsaidia mke wangu kazi mbalimbali ikiwepo kukaa na watoto,kitu ambacho kwangu kinanipa furaha sana kwani muda mwingi nimebanwa na majukumu ya kitaifa na kimataifa..