Friday, October 17, 2014

KAMATI KUU YA CHADEMA YAKUTANA NA WANACHAMA WALIOWEKA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE UCHAGUZI MKUU 2015


 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akiingia katika ukumbi wa mkutano wakati wa Kikao cha Kamatii Kuu ya Chama hicho kilipokutana na Wanachama waliotia nia ya kugombea Ubunge katika Uchaguzi Mkuu 2015.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akiingia katika ukumbi wa mkutano wakati wa Kikao cha Kamatii Kuu ya Chama hicho kilipokutana na Wanachama waliotia nia ya kugombea Ubunge katika Uchaguzi Mkuu 2015.
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Joseph Haule 'Prof. J' (wa kwanza kushoto)akiwa katika Kikao cha Kamati Kuu ya Chadema pamoja na wajumbe wengine wakimkaribisha Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
Viongozi Wakuu wa Chadema wakiomba dua kabla ya kuanza Kikao.
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, Salum Mwalimu.
Salum Mwalim akifafanua jambo wakati wa Kikao hicho.
 Makamu Mwenyekiti wa Chadema Zanzibar,  Said Issa Mohamed akizungumza katika Kikao hicho.
 Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, John Mnyika akizungumza katika kikao hicho.
Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Prof. Abdalah Safari.
Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Wilbrod Slaa
 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akizungumza katika wakati wa Kikao cha Kamati Kuu ya Chama hicho ilipokutana na Wanachama waliotia nia ya kugombea Ubunge katika Uchaguzi Mkuu 2015.
Wabunge wa Chadema wakiwa katika kikao cha Kamati Kuu.
  
Baadhi ya viongozi wa Chadema.
Mustafa Muro akiwa katika Kikao hicho.
Wanachama wa Chadema.
Wanachama wakisikiliza hotuba ya Mwenyekiti wa Chadema.

Wanachama wa chama hicho.
Mwanamuziki wa kizazi kimpya Prof. J akiwa ni miongoni mwa watia nia.
Msanii wa bendi ya M4C akitumbuiza.

Thursday, October 16, 2014

AJALI YA LORI LA MAFUTA DAR LAANGUKA LAWAKA MOTO WATU WAPOTEZA MAISHA

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki (katikati) na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema wakimsikiliza miliki wa Nyumba ya kulala wageni United State na bar, Laurent Kasiga  iliyopo Mbagala Rangi tatu, Dar es Salaam ambayo iliteketea kwa moto uliotokana na roli la mafuta lililopinduka na kuwaka moto wakati vijana wakiiba mafuta.
 Mkuu wa Moa akikagua Nyumba hiyo ya kulala wageni iliyokuwa na vyumba 32.
 wananchi wakiangalia athari za moto huo.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akiangalia tenki la lori hilo.
 Lori hilo lilivyoteketea kwa moto uliosababishwa na mshumaa.
Moja ya maduka ya vifaa vya pikipiki lililoteketea 
 
Wafanyabiashara wa mchele waliokuwa na fremu katika eneo hilo wakiwa katika majonzi baada ya mzigo wao kuungua moto na kuharibika kabisa.

Mmoja wa majeruhi katika tukio hilo la moto akisimulia. 
Baadhi ya sehemu za mwili za watu walioungua. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadick, akiwa na mmoja wa wauguzi wa hospitali ya Temeke alipowatembelea waathirika wa ajali hiyo. WATU watatu wamefariki na wengine sita wakiwa katika hali mbaya Hospitali ya Muhimbili kufuatia tukio la moto uliolipuka kwenye gari la kubeba mafuta jana maeneo ya Mbagala jijini Dar es Salaam. 

AKizungumza Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Naibu Kamishna Mohammed Mpinga, alisema ajali hiyo haikuleta athari yoyote baada ya gari lile kupata ajali ila athari ilijitokeza baada ya watu kuvamia na kuanza kuiba mafuta na baadaye kujaribu kuiba betri ndipo cheche za moto zilipolipuka na kusababisha kuwaka kwa gari hilo. 

Wakati huohuo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mecky Sadick, amewataka wananchi kutokuwa na tabia ya kuvamia ama kuiba vitu pindi ajali zitokeapo.
Sadick alisema hayo alipotembelea hospitali ya Muhimbili na Temeke walipolazwa majeruhi hao.

MWANAJESHI ATOA ADHABU KALI KWA RAIA ALIYEVAA NGUO ZA JESHI KARIAKOO


Picha unazoona sio utani wala sinema ni raia wa kawaida akiogelea kwenye dimbwi kwa amri ya mwanajeshi.
Raia huyo alikutana na adhabu kali za mwanajeshi huyo baada ya kukutwa amevaa mavazi halisi ya jeshi la Tanzania maeneo ya Kariakoo Dar es Salaam.
Jamaa huyo alipokamatwa na kushindwa kutoa maelezo ya kuridhisha akaamriwa kuvua mavazi hayo na kisha kuaza kutumikia mazoezi ya hatari ..
Haya mavazi raia wanayapenda ila kwenda kutumikia jeshi hawataki ...ahahaaa jamaa alichokipata hawezi kutamani nguo za rangi ya kombat maisha yake yote.

HIZI NDIZO VURUGU KUBWA ILIYOTOKEA KWENYE MECHI BAINA YA SERBIA NA ALBANIA
















MCHUNGAJI AMTOROSHA MKE WA MTU AMBAYE NI MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI

MCHUNGAJI anayejiita nabii na mtume, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) aliyetajwa kwa jina moja la Emmanuel amejikuta ndani ya majanga kufuatia madai mazito kwamba amemtorosha mke wa mtu ambaye ni mwimbaji wa Nyimbo za Injili Bongo anayekuja juu kwa kasi, Janet Mrema.

Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Bongo anayekuja juu kwa kasi, Janet Mrema anayedaiwa kutoroshwa na mchungaji huyo. Kwa mujibu wa chanzo makini, mchungaji huyo alifika nyumbani kwa Jonas Mrema, mume wa Janet, maeneo ya Tegeta-Nyaishozi jijini Dar na kuishi kama mtumishi wa Mungu lakini polepole alianza mazoea tata na Janet. 
“Mume alianza kuhisi mabadiliko ya mkewe kwa mtumishi huyo, lakini nadhani aliona ni mawazo yake tu. Ndipo siku ya siku akashangaa mkewe na mchungaji huyo wameondoka nyumbani hapo. 
“Kwa sasa tangu tukio hilo litokee ni miezi kama mitatu. Mume alihangaika sana kumtafuta mkewe hadi jana (Jumatatu iliyopita) ndipo akampata wakiwa na mchungaji huyo kwenye nyumba moja ambako walikuwa wakiishi pamoja,” kilisema chanzo chetu.
Katibu wa Chama cha Waimba Injili Tanzania, Stela Joel akilizungumzia sakata hilo. Iliidaiwa kwamba, mchungaji huyo alipopekuliwa alikutwa na paspoti ya nchini Burundi wakati yeye ni Mkongo wa Uvira na alionekana kuishi nchini kinyume na sheria hivyo alifunguliwa jalada la kesi kwenye Kituo cha Polisi cha Wazo Hili, Tegeta lenye Kumbukumbu Na. WH/RB/7040/2014- KUISHI NCHINI BILA KIBALI. 
Juzi, Amani liliwasiliana na Katibu wa Chama cha Waimba Injili Tanzania, Stela Joel ambaye alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema tayari chama hicho kimemsimamisha uanachana Janet kwa kitendo chake hicho cha kumtoroka mumewe wa ndoa. 
“Ni kweli na Chama cha Waimba Injili Tanzania kimemsimamisha uanachama Janet. Hatuna mzaha katika maadili,” alisema Stela.Amani lilimpigia simu mume wa Janet, Jonas Mrema ambapo katika mazungumzo baada ya salamu alipewa pole kwa matatizo ya mkewe, alisema asante kisha alipoulizwa kuhusu hali ilivyo aliomba apige simu yeye baadaye kwa vile alikuwa kikaoni. 
Hata hivyo, baada ya saa mbili kupita bila kupiga, Amani lilimpigia tena simu ambapo iliita bila kupokelewa hivyo jitihada za kumpata zinaendelea.

Tuesday, October 14, 2014

KIJANA AKUTWA AMEFARIKI KORONGONI MKOANI KIGOMA



Mwili ukiwa bado eneo la tukio 
Katika hali ya kustajaabisha kijana mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Yusuph (Me) mkazi wa Buzebazeba Ujiji amekutwa amekufa katika korongo la Lebengera jirani na Ofisi za CCM mkoa katika manispaa ya Kigoma Ujiji huku akiwa amejaa damu katika paji lake la uso
Mara baada ya Jeshi la Polis kufika eneo la tukio walimpekua marehemu na kumkuta na fedha taslimu kama elfu tatu hivi na karatasi ambayo haikujulikana mara moja imeandikwa nini 
tukio hilo limetokea jana Oktoba13 eneo tajwa hapo juu huku umati mkubwa ukiwa umefurika ili kumtambua na kushuhudia tukio hilo, katika uchunguzi wa awali inasemekana tukio hilo limetokea jana usiku kwani kutwa nzima ya jana hapakuonekana mtu ambae amekufa eneo,akiongea na kibonajoro.com mmoja wa wananchi aliekuja kushuhudia tukio,na ambae ni mfanyakazi katika ofc moja jirani na eneo la tukio jina (....) amesema hii imekuwa ni mara ya pili kutokea tukio kama hili la mtu kukutwa ameuwawa na kutupwa katika korongo hili,hivyo tunaviomba vyombo vya usalama kuweka doria ya mara kwa mara eneo hili kwani eneo hili linakaribiana na Bar pamoja na Ofisi za Hazina Ndogo. 
Polisi wakichukua vielelezo katika picha 
Kutokana na eneo alilokutwa marehemu kuwa na miundombinu mibovu ya kumtoa walilazimika kutumia ngazi,hivyo waliomba msaaada wa ngazi kwa gali la emegency la Tanesco na hapa ngazi ilikuwa inashushwa tayari mwili kupandishwa juu kupelekwa eneo husika, 
Mwili ukitolewa tayari kupelekwa kwenye gari la Polisi 
Mwili ukiingizwa kwenye gali la Polis kuelekea Central Polis kwa taratibu zingine 
Mwili wa kijana Yusuph ukiwa ndani ya gari la Polisi,katika taarifa zingine zilizopotikana eneo la tukio zinasema kabla ya kugundulika kwa tukio hili kumetokea tukio lingine linalofanana na hili maeneo ya mwasenga usiku wa kuamkia leo mtu kukutwa ametupwa huku akiwa amepoteza maisha. 
Polisi wakiondoka eneo la tukio 
kwambali ndio eneo la ofisi za CCM mkoa ambapo kulia ndiko kumetokea tukio hili.