Friday, August 29, 2014

WALAZIMIKA KUTEMBEA ZAIDI YA KILOMETA 4 KATIKA KUTAFUTA MAJI SAFI NA SALAMA.

 Na Baraka lusajo mbeya,
WANANCHI wa  kijiji  cha kyimo  kata   ya  kyimo  wilayani Rungwe mkoani  Mbeya  wamelazimika  kufukia mitalo ambayo ilikuwa imeandaliwa  na idala ya maji wilayani  humo  baada  ya wao  kukosa huduma hiyo kwa  muda mlefu na kulazimika  kutembeya  zaidi ya kilometa {4}  katika  kutafuta  maji  safi na salama 

 
Wakizungumza jana na  wandishi  wa  habari walipotembelea potembelea  kata hiyo mara baada ya kujurishwa uwepo  kwa ukosefu wa  huduma ya maji  kwa muda mlefu walisema kuwa Serikali kupitia benki ya Dunia {WBC} iliwapatia fedha kiasi  cha  Tsh,Mil,299   kwa ajiri ya ujenzi wa tenki  lamaji ambalo lilitegemewa  kujengwa  katika eneo hilo baada ya wao  kuto kuwa  na huduma hiyo kwa  muda mlefu  lakini  wanashangaa baada ya  huduma hiyo kukamilishwa na kuelekezwa  katika  kata ya jilani   ya lufingo  bila wao kunufaika  na huduma hiyo  na kupelekea  kuchukua  uamzi  wa  kufukia  mitalo ambayo ilikuwa imeandaliwa na idala ya  maji   wilayani humo   na huku wakishinikiza  idala hiyo  kuelekeza  maji kwanza kijijini kwao.
Omari Kajange mkazi wa kata hiyo alisema kuwa Mkuu wa mkoa huo Abasi Kandoro ndiye aliyewapa taarifa kuwepo kwa mradi huo na kuwa baada ya kuona mkandarasi amejenga chini ya kiwango walimpatia taarifa na yeye  kumuagiza mkandarasi huyo ajenge upya ndani ya siku 14.

Alisema kuwa mkandarasi huyoaliyejulikana kwa jina moja la Gulamali alikaidi agizo hilo ikiwa amefikisha zaidi ya miezi mitatu bila kujenga Tenki hilo na hakuna hatua iliyochukuliwa na wao wakiendelea kukosa huduma hiyo muhimu kwa kulazimika kutembea zaidi ya kilometa {4} katika kutafuta huduma hiyo. 

Kajange aliongeza kuwa kutokana na Serikali wilayani humo kushindwa kuchukua hatua waliamua kufanya mkutano mkuu uliowatuhumu  viongozi wa kata hiyo kushindwa kuwajibika na kutaka wapatiwe majibu juu ya hatua walizochukua kutokana na   ukosefu wa  huduma hiyo.

Akijibu hoja hizo diwani wa kata hiyo Frankson Mwaitalage alisema kuwa ni kweli jambo hilo lipo lakini lipo chini ya mkuu wa mkoa ambaye tayari ameanza kuchukua hatua juu ya uchakachuaji huo dhidi ya mkandarasi huyo.

Mwaitarage alisema kuwa Sekretalieti ya mkoa ndiyo iliyompa kazi injinia huyo na kuwa serikali ya kijiji ilitakiwa ipeleke lalamiko hilo mkoani kupitia kwa mkuu wa wilaya Chrispin Meela  na si kwangu.

“mimi mnanionea bule suala hili lipo chini ya mkuu wa mkoa,mimi sina mamlaka tulichokifanya ni kuukataa mradi huo maamuzi juu ya injinia huyo yatatolewa na mkuu wa mkoa na maji  yataanza  kupatikana mpaka mpale mladi  utakapo kuwa umekabidhiwa  na serikali kwa wanachi husika na  sivinginevyo ”alisema diwani huyo.

Mwaitolage alimaliza kwa kusema kuwa atamuagiza mwenyekiti wa kijiji hicho aitishe mkutano mkuu ili mambo yote yawekwe wazi kwa kuwa tatizo hilo la huduma ya  kmaji katika maeneo hayo lipo kwake na muhtasari wa mkutano huo yatapelekwa kwa mkuu wa mkoa kwa ajili ya maamuzi zaidi.

No comments:

Post a Comment