KIPIGO CHA GOLI 5-3 ILICHOAMBULIA MANCHESTER UNITED SIRI YAFICHUKA
Siri ya kipigo kizito ilichokipata klabu ya Manchester United kutoka
kwa klabu iliyopanda daraja msimu huu ya Leicester City imefichuka.
Taarifa zilizozagaa nchini Uingereza zinadai kuwa wachezaji na
viongozi wa klabu ya Leicester City walifanyiwa maombi maalumu kutoka
kwa mmoja kati ya viongozi wa dini ya Kibudha waliokuwepo uwanjani King
Power Stadium kwaajili ya kazi hiyo maalumu.
Wachezaji wa timu hiyo walifanyiwa maombi maalumu na kupewa mikono ya
baraka ambayo inaaminika ndio iliyowasaidia kuupata ushindi huo wa
kihistoria dhidi ya Manchester United kutoka kwa makasisi hao wa dini ya
Kibudha waliofanya kazi hiyo kwenye dimba la King Power Stadium.
No comments:
Post a Comment