Wednesday, September 24, 2014

SIRI YA MANCHESTER KUFUNGWA GOLI 5 NA LEICESTER UNITED

KIPIGO CHA GOLI 5-3 ILICHOAMBULIA MANCHESTER UNITED SIRI YAFICHUKA

Siri ya kipigo kizito ilichokipata klabu ya Manchester United kutoka kwa klabu iliyopanda daraja msimu huu ya Leicester City imefichuka.
Taarifa zilizozagaa nchini Uingereza zinadai kuwa wachezaji na viongozi wa klabu ya Leicester City walifanyiwa maombi maalumu kutoka kwa mmoja kati ya viongozi wa dini ya Kibudha waliokuwepo uwanjani King Power Stadium kwaajili ya kazi hiyo maalumu. 
Wachezaji wa timu hiyo walifanyiwa maombi maalumu na kupewa mikono ya baraka ambayo inaaminika ndio iliyowasaidia kuupata ushindi huo wa kihistoria dhidi ya Manchester United kutoka kwa makasisi hao wa dini ya Kibudha waliofanya kazi hiyo kwenye dimba la King Power Stadium.

No comments:

Post a Comment