Wakati
harakati mbali mbali za kukabiliana na ndoa na mimba za utotoni
zikiendelea na hasa katika nchi za Afrika, baadhi ya nchi barani humo
zinakabiliwa na changamoto hiyo kupita kiasi.
Ama kweli
ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni. Kesi ya kwanza na ya aina yake
imefanyika na hukumu yake kutolewa nchini Ivory Coast baada ya mwanamume
mmoja kumuoa binti yake wa umri wa miaka 11.
Kutokana na
kitendo cha mwanamume huyo kumuoa binti yake alihukumiwa kifungo cha
mwaka mmoja jela na faini ya dola za Kimarekani 700.
Mwendesha
mashtaka Rosine Kone amesema kwamba kesi hiyo ya aina yake itatuma
ujumbe mzito kwa raia wa nchi hiyo ili wanaume waache tamaa.
Nao Umoja wa
Mataifa unasema kwamba ndoa za utotoni nchini Ivory Coast si suala la
kushangaza, kwani mmoja kati ya mabinti watatu huolewa kabla ya
kufikisha umri wa miaka 18.
CREDIT: BBC
No comments:
Post a Comment