Tuesday, October 14, 2014

PROFESA MAZRUI AFARIKI DUNIA


 

Profesa Ali Mazrui enzi za uhai wake.
MSOMI mashuhuri wa masuala ya kisiasa, utamaduni wa Kiafrika na dini ya kiisilamu wa nchini Kenya, Profesa Ali Mazrui ameaga dunia leo akiwa Marekani.
Mazrui alyekuwa anaishi nchini Marekani, amefariki akiwa na umri wa miaka 81baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Taarifa zinadai kuwa Profesa Mazrui atazikwa mjini Mombasa, Pwani ya Kenya alikozaliwa.
Enzi za uhai wake, marehemu alitoa ombi la kutaka kuzikwa Mombasa akisema angependa kuzikwa katika jumba la kihistoria la Fort Jesus.
Kabla ya kifo chake, Marehemu Mazrui alikuwa anafundisha katika Chuo Kikuu cha Binghamton mjini New York, Marekani.

No comments:

Post a Comment