Tuesday, December 2, 2014

MZEE MSUYA AWASIHI WAKULIMU KUTOOGOPA NENO BIOTEKNOLOJIA


Kutokana na kuwepo kwa maneno yanayowatishia na kuwakatisha tamaa wakulima kuwa mbegu za kisasa ni mbegu za kibioteknolojia na hazifai kwa matumizi ya binadamuu, mzee Msuya amewasihi wakulima kuwabeza watu hao na maneno yao na kutoliogopa neno bioteknolojia kwani hilo ni neno la kisayansi ambalo halibadirishi uasili wa mmea wa aina yoyote ile.
Aliyasema hayo baada ya kuwepo kwa baadhi ya watu kumfuata na kumuuliza siri ya mafanikio yake katika kilimo na anapowaambia kuhusu mbegu za kibioteknolojia huingiwa na mshangao na kuogopa neno hilo
Mzee msuya ni miongoni mwa wazee maarufu katika wilaya ya Vunjo kutokana na juhudi zake katika kilimo na ndio wazee wenye pesa mjini hapo.
mzee huyo ambaye alisema siri ya mafanikio yake aliipata baada ya kukubali kung'oa miche yake ya zamani ya kahawa na kupanda miche mipya aliyoinunua katika taasisi ya utafiti wa kahawa ya TaCRI baada ya kupata ushauri kutoka kwa mtaalamu wa kilimo wa taasisi hiyo.
"mtafiti alinishauri nitoe miche ya kahawa yote iliyokuwapo shambani na kunpambia nikanunue miche mipya ya TaCRI kwani ni miche isiyokuwa na maambukizi ya magonjwa yanayosumbua zao la kahawa sikuamini lakini baadaye nikakubali na nikafanya kama nilivyaambiwa na sasa naitwa mchawi hapa kijijini kutokana na mazao ninayoyapata.


wanawake wakimsaidia mzee msuta kuchambua mahindi nyumbani kwake 



Mzee huyo ambaye sasa amekuwa mwalimu wa wakulima wenzake alisema kuwa Tanzania kama nchi nyingine haiwezi kukwepa maendeleo ya bioteknolojia kutokana na utandawazi na maendeleo ambayo yapo duniani kote, kwa kuwa bioteknolojia ni nyenzo muhimu katika kuboresha kilimo, uzalishaji viwandani, kwenye afya, hifadhi ya mazingira pia kukuza uchumi nchini
mzee huyo ambaye alisema alikuwa anapata kilo 250 mpaka 1500 kwa msimu lakini tangu miche mipya ianze kuzaa matunda napata kilo 5000 mpaka 8000 kwa msimu na kwa ukubwa ule ule wa shamba. kitu ambacho akiwaeleza wenzie wanashangaa sana na kutoamini anachowaeleza.

Akifafanua kuhusu neno bioteknolojia alisema kwa madaha  kuwa ni "taaluma ya kutumia michakato ya kibaolojia katika  viumbe hai ili kupata mahitaji na huduma kwa maendeleo na maisha bora ya binadamu" 


 
Msuya ambaye alisema hata sahau jinsi majirani zake walipomcheka na mumuita mpumbavu pale alipoamua kung'oa na kupanda miche mipya. Hata hivyo hakukatishwa tamaa na maneno yake bali alizingatia sana mafundisho aliyoyapata na kuyatendea kazi mpaka alipo fanikiwa na kubadirika kuwa mwalimu wa wengine
"Hivi sasa mimi nafuatwa na wakulima ili niwafundishe mbinu ninazotumia, lakini wengi wanashangaa ninapowaambia kuhusu mbegu mpya na utunzaji wa shamba vizuri wanaofuata ninayowaambia wanaona matunda yake.


 shamba la kahawa la mzee msuya likiwa limechanganywa na zao la migomba

Mzee huyo alisema kuwa anajivunia sana elimu aliyoipata kutoka kwa watafiti kwani wamemfanya kutoka kwenye kilimo cha kutafuta chakula pekee na kuwa mkulima mfanyabiashara kwani mazao anayoyapata kwa sasa yanakidhi mahitaji yake ya chakula na kupata kiasi kikubwa kwa ajili ya kuyauza kwenye makampuni makubwa hapa nchini.
"TaCRI imeniondolea umaskini kwani walinifundisha elimu ya kutumia mbegu bora kwa kila zao ninalotaka kulima pamoja na matumizi ya samadi ya wanyama nilionao nyumbani hivyo kwamgu mimi kila kitu ni faida kwani mashamba yanategemea mifigo kwa mbolea wakati mifugo inategemea kilimo kwa chakula". 

Hata hivyo aliwasii watafiti wote nchini kuwasaidia wakulima ili wapate elimu kuhusu matumizi ya mbegu bora ili kumkomboa mkulima kwani wakulima wengi wanadanganya na propaganda zinazoletwa na wafanyabiashara wengine wa bidhaa zao wakidai kuwa matumizi ya mbegu hizo si salama wakati ni uvumi usio wa kweli kabisa.

TaCRI ni taasisi ya utafiti wa kahawa nchini Tanzania na inafanya kazi  kwa msaada wa nchi za ulaya, hufanya uzalishaji kwa njia ya Tissue Culture ( uzalishaji kwa njia ya chupa) na kuzalisha kwa kutumia vikonya (kupachika mche mmoja juu ya mche mwingine).


Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi 2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara za arabika pamoja na ile ya Robusta Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa

Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi 2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara za arabika pamoja na ile ya Robusta Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho kinasababisa hasara kwa mkulima Pia TaCRI imetoa teknolojia za kuongeza tija na ubora wa kahawa aina mbili zinazotekelezeka za kuzalisha miche mipya bora ya aina hizi chotara ikiwa nipamoja na kutumia vikonyo, kupachika aina mpya juu ya mibuni ya zamani na kuzalisha kitaalamu miche kwa kutumia chupa ikifahamika kwa lugha ya kingereza ’Tissue culture au Somatic embryogenisis.’

Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi 2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara za arabika pamoja na ile ya Robusta Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho kinasababisa hasara kwa mkulima Pia TaCRI imetoa teknolojia za kuongeza tija na ubora wa kahawa aina mbili zinazotekelezeka za kuzalisha miche mipya bora ya aina hizi chotara ikiwa nipamoja na kutumia vikonyo, kupachika aina mpya juu ya mibuni ya zamani na kuzalisha kitaalamu miche kwa kutumia chupa ikifahamika kwa lugha ya kingereza ’Tissue culture au Somatic embryogenisis.’

Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi 2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara za arabika pamoja na ile ya Robusta Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho kinasababisa hasara kwa mkulima

Make Money at : http://bit.ly/copy_win

No comments:

Post a Comment