Tuesday, October 7, 2014

ROSE MUHANDO NDANI YA KASHFA NZITO


MSANII nyota wa nyimbo za Injili Bongo, Rose Muhando anadaiwa kuingia mitini na shilingi milioni moja alizolipwa kwa ajili ya kutumbuiza kwenye uzinduzi wa albamu ya Injili ya John Lisu iitwayo Uko Hapa, Jumapili iliyopita.
Msanii nyota wa nyimbo za Injili Bongo, Rose Muhando.Kwa mujibu wa chanzo makini, Rose alimegewa kiasi hicho cha pesa na Kampuni ya Msama Promotion iliyoandaa uzinduzi huo uliofanyika ndani ya Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar Jumapili iliyopita.
“Rose jamani ana mambo! Mnajua kama amemliza Msama (mkurugenzi wa Msama Promotion) shilingi milioni moja? Alipewa ili atumbuize kwenye uzinduzi wa albamu ya John Lisu lakini akaingia mitini.“Mbaya zaidi kila alipopigiwa simu kuulizwa kwa nini hajafika Dar ile Jumamosi ili Jumapili awepo ukumbini akawa hapokei simu.
Kikaendeela: “Rose ananishangaza sana, sikuwahi kufikiria kama anaweza kufanya hivyo, kikubwa kinachowaumiza wengi ni kutopokea simu na ingekuwa vizuri kama angetoa taarifa mapema kwa kutohudhuria kwake na sisi tungejua cha kufanya mapema,” kilisema chanzo hicho ambacho kipo ndani ya waandaaji hao. 
Chanzo hicho hakikuishia hapo, kiliendelea kuanika kuwa shutuma za aina hiyo zimekuwa zikimuandama sana mwanamuziki huyo kiasi cha kushindwa kuaminika na kudai kuwa hana njaa ya kutokomea na pesa hiyo kwani ni kiasi kidogo sana kwake.
Msanii nyota wa nyimbo za Injili Bongo, Rose Muhando akizungumza jambo.Risasi Mchanganyiko lilimsaka bosi wa Msama Promotion, Alex Msama ambaye alikiri Rose kutotokea kwenye uzinduzi huo licha ya kulipwa kiasi hicho cha pesa na kilichomuumiza zaidi ni kutopokea simu za wasaidizi wake waliotaka kujua nini kilimpata.
“Aliniangusha sana maana hata yeye nilimtangaza sana kwenye vyombo vya habari kwamba atakuwepo, lakini matokeo yake ikawa kimya, sijui nini kimempata lakini nitatoa tamko siku mbili hizi,” alisema Msama kwa masikitiko makubwa.
Alipopigiwa simu Rose Muhando alikacha kuongelea suala hili

No comments:

Post a Comment