Sunday, August 17, 2014

TaCRI NA HRNS ZIMEFANYA KAZI YAKE, KAZI KWAO WAKULIMA.




 
Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi 2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara za arabika pamoja na ile ya Robusta
 Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa

 Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho kinasababisa hasara kwa mkulima 

Pia TaCRI imetoa teknolojia za kuongeza tija na ubora wa kahawa aina mbili zinazotekelezeka za kuzalisha miche mipya bora ya aina hizi chotara ikiwa nipamoja na kutumia vikonyo, kupachika aina mpya juu ya mibuni ya zamani na kuzalisha kitaalamu miche kwa kutumia chupa ikifahamika kwa lugha ya kingereza ’Tissue culture au Somatic embryogenisis.’

Taasisi hii ikiwa ndio uti wa mgongo katika sekta ya kahawa na sasa imefanikiwa kutoa teknolojia mpya ya kuongeza tija na ubora wa kahawa nchini kwa msaada mkubwa wa nchi za Ulaya pamoja na fedha kidogo inayopata kutoka kwenye mgawanyo wa bajeti ya serikali ya Tanzania kupitia wizara ya kilimo na chakula.
Ikiwa bado TaCRI imejipanga kufanya mambo makubwa katika sekta hii na kuikomboa Tanzania kiuchumi kwani kwa sasa kahawa inachangia asilimia 22 ya pato la Tanzania, serikali pia inatakiwa kuunga mkono kazi zinazofanywa na TaCRI kwa kuwekeza zaidi katika utafiti ili kupunguza makali ya kazi na kumuelemea mkulima atakapo kununua miche kutoka kwenye taasisi hiyo na hata kuiwezesha taasisi hiyo kifikia malengo kwa kuzalisha idadi kubwa ya miche chotara na kukikomboa kilimo cha kahawa Tanzania.

Akiongea na waandishi wa habari waliotembelae taasisi hiyo chini ya Bioscience For Farming in Africa (B4FA) ili
  kuona uhalisia wa utafiti unavyokwenda mmoja wa watafiti ambaye hakupenda jina lake litajwe asisema kuwa “hapo awali serikali ilitoa pesa za kutosha kwa ajili ya utafiti wa miche hiyo na walifanya kwa nguvu kubwa na mafanikio, lakini kwa sasa bajeti waipatayo kutoka  wizarani ni kidogo sana kiasi ambacho hakilingani kabisa na kazi tunayoifanya hapa, kwa mfano mwaka wa bajeti wa 2013/14 taasisi yetu imetengewa shilingi milioni mia moja ambayo ni kiasi kidogo sana kwa taasisi kama hii” alisema mtafiti huyo
Kwa kiwango ambacho kimefikiwa na TaCRI ni mafanikio makubwa katika tasnia hii ya kilimo na kubakia kazi kwa mkulima kuitikia wito kwa kuanza kupada miche bora au kupandikiza vikonyo kwenye miche ya zamani ili kuwa na kilimo chenye tija.

Ikiwa TaCRI wao wamejizatiti katika utafiti wa miche bora taasisi isiyo ya kiserikali ya Hanns R. Neumann Stiftung Tanzania (HRNS) ambayo pia ipo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro wao wamejito kuwaunga mkono wakulima wa kahawa kwa kutoa elimu ya kilimo cha kahawa hasa matuzi ya miche bora. Hivyo kwa kushirikiana na TaCRI katika kuhamasisha matumizi ya miche ya kahawa iliyoboreshwa wamewaunganisha wakulima katika vikundi na kuwawezesha wakulima kuanzisha bustani za miche ya kahawa ili kurahisisha upatikanaji wa miche hiyo.


HRNS wamekuwa watoaji elimu hii kwa vitendo kitu ambacho kimewasaidia wakulima wengi kuanza kulima kahawa upya kitu ambacho kilikuwa hakipo kutokana na wakulima wengi kukata tamaa kwa kuona kuwa kilimo cha kahawa ni cha hasara kutoka na miche ya zamani kuzeeka na kushambuliwa na magonjwa hivyo kutozaa matunda.


“Tumekuwa na mashamba darasa ambayo wakulima wengine wakiona matokea ya shamba huhamasika na wao kulima kahawa, pia tumekuwa tukitembelea vikundi na mashammba ya wakulima ili kuwashauli na kuona maendeleo ya mashamba yao
  ” alisema bwana Tadeus Moshiro ambaye ni meneja wa mradia wa HRNS

“Na kazi hizi tunafanya na mikoa yote inayolima kahawa bila kijali ni aina gani ya kahawa, na tumepata mafanikio makubwa sana mkoani Mbeya ambapo mwitikio wa wakulima ni mkubwa sana na mikoa mingine pia tunaona mwitikio huo japo wakulima wengi hulalamika bei kubwa ya bembejeo za kilimo” Tadeus alisema


Kutokana na pembejeo za kilimo kuwa juu wakulima wengi wamekuwa wanashindwa kumudu kilimo cha kahawa hivyo taasisi hii ya HRNS huwaunganisha wakulima wa kahawa ili waweze kupata mikopo katika mabenki yanayotoa mikopo kwa mkulima ili waweze kumudu kilimo na kupata mazao yenye tija kwa mkulima.


Hata hivyo HRNS imekuwa ikiwakujulisha wakulima bei ya kahawa kila mara ili kuwawezesha wakulima kujua hali halisi ya soko la hakawa kwa wakati.


Akizungumza kwa upande wa wakulima Bwana wa Moshi vijijini aliishukuru sana TaCRI kwa elimu waliyompa na kumuwezesha kutoka kwenye kilimo duni mpaka kumfikisha kwenye kilimo chenye tija na kuwa kama mfano wa kuigwa kijijini hapo, kwani ametoka kwenye uzalishaji wa gunia 1la kahawa mpaka kufikia kwenye magunia 6 ya kahawa kutokana na miche bora ya TaCRI.


Pia Bi Magdalena Temba Ambaye ni mtunza hazina wa kikundi cha Zinduka Farmer Group cha Kiruwa, Moshi ameshukuru HRNS kwa elimu waliyowapa na kuwawezesha wao kama kikundi kuwa na bustani yao ya miche bora ya kahawa ambayo huiuza kwa wakulima wenzao na kuwapatia kipato na kumuwezeza kila mwana kikundi kuwa na shamba lenye miche bora kitu ambacho si rahisi kwa mkulima mmoja mmoja kufanya hivyo kirahisi. Pia amewataka wakulima wa kahawa kote nchini kubadirisha miche ya kahawa kwa kupanda miche mipya iliyobora ama kupandikiza miche bora juu ya kikonyo cha kahawa ya zamani ili kupata faida zaidi katika kilimo. Na kushauri wakulima kujiunga katika vikundi ili kujikwamua kimaendeleo kwa kushirikiana na wakulima wengine


Licha ya bei ya kahawa kuwa chini na kuwafanya wakulima wengi kukata tama ya kuendelea na kilimo hicho na kufanya wakulima wengi kuanza kulima mazao mengine kama maharage, ndizi na mahindi, Bwana Tadeus Moshiro amewasihi wakulima kupanda miche mipya ya kahawa kwani inakuwa haraka na huchukua mda mfupi kuanza kutoa matunda ambapo nikipindi cha mwaka mpaka mwaka na nusu kuanza kuzaa. Na kwakufanya hivyo itamuwezesha mkulima kupata mazao mengi na yenye ubora wa juu hivyo kumuwezesha mkulima kuuza kahawa kwa bei nzuri zaidi yenye faida kwake na Taifa pia


Mbali na hayo yote wakulima wa kahawa mkoani Kilimanjaro wameiomba serikali ya Tanzania kuwa, kauli ya kilimo kwanza isiwe kwenye mahindi na mazao mengine ya chakula kwa kutoa ruzuku za pembejeo kwenye mazao hayo tuu bali kilimo kwanza itumike mpaka kwenye mazao ya biashara kama kahawa.

Hata hivyo kazi imebaki kwa mkulima kuitikia wito wa TaCRI  pamoja HRNS  kulima kahawa kwa kutumia miche mipya ya kahawa ili kujitoa kwenye kilimokisicho na tija na kulima kwa tija ili kujiongezea kipato cha mkulima mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

TUFAA LATOA AJIRA KWA VIJANA WA MJINI



              








“Asiyefanya kazi na asile” hii ni kauli ya Athumani Idd mfanya biashara wa matunda na mboga mboga Soweto jijini Mbeya. Alitoa kauli hiyo alipotembelewa na mwandishi dukani kwake jijini Mbeya.

 Athumani ni miongoni mwa wafanyabiashara wa maaatunda ya tufaa, embe, zabibu na machungwa na kwa upande wa mboga mboga huuza Uyoga, spinachi cornflower. Biashara hiyo aliibuni baada ya kutafuta ajira kwa mda mrefu bila mafanikio hivyo alianza kujihusisha na kilimo cha mboga mboga na kisha kuanza biashara hiyo aliyo nayo. Alisema “Vijana wengi wa mjini wamekuwa wakilalamikia ugumu wa maisha kutokana na ukosefu wa ajira ambapo imepelekea wengi wao kujihusisha katika vitendo vya uvunjifu wa sheria za nchi. Nimemaliza chuo cha UDSM (University of Dar es salaam) nimesomea mambo ya biashara, lakini sijabahatika kupata ajira hivyo nimeona nijiajiri mwenyewe kwenye kilimo cha mbogamboga na uuzaji wa matunda kitu ambacho sijutii kukifanya na Napata faida kubwa kuliko hata mshahara ambao ningelipwa. Na kati ya matunda yote niyauzayo tufaa linauzika sana kuliko mengine yote.

Mbali na Athumani Idd pia wapo vijana wengi sana ambao wamekuwa wakijishughulisha na biashara ya matunda hayo katika sehemu mbalimbali za nchi yetu haswa mijini. Hapo awali lilionekana ni tuda linaloliwa na watu wenye kipato kikubwa au watu wa mjini peke yao kitu ambaocho kimekuwa tofauti kwa sasa kutokana na uwingi wa matunda hayo na kuuzwa karibu kila mahalli hata barabarani kitu ambacho hapo awali haikuwa hivyo kwani hapo mwanzo tunda hili liliuzwa katika maduka makubwa pekee.

Mbali na biashara ya matunda ambayo imeenea sana sehemu za mijini, tufaa ni Tunda pekee ambalo limeonekana kutoa ajira kwa vijana wengi wanaojishughilisha na biashara hiyo. Na hiyo  ni kutokana na tunda lenyewe kupendwa na watu wengi pia upatikanaji wake hauna msimu maalum.
 
Kwa kuliongelea tunda hili ni tunda moja maarufu duniani ambalo hupendwa kuliwa na watu wote bila kujali lika la mtumiaji, hii inatokana na utamu, ulaini wake pamoja na faida za kiafya zinazopatikana kwa kula matufaa. Na wakati mwingine limekuwa likitumiwa na wapendanao ili kutoa ishara ya upendo baina yao

 Matunda haya hustawi zaidi kwenye nyanda za juu ambako joto sio kali, sehemu kama lushoto, mkoani Tanga, Arusha, miteremko ya Kilimanjaro, Mbeya, Iringa, Njombe, Songea na sehamu nyingine nyingi zenye hali ya hewa zinazofanana na hizo. Udongo unaofaa kwa kilimo cha tufaa ni wenye rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji.

Unaweza kupanda kwa kutumia mbegu au kwa kununua miche bora kutoka kwenye taasisiza kilimo mfano Uyole Mbeya kwa wakulima wa nyanda za juu, Tengeru kwa wakazi wa Arusha na SUA kwa wale wa Morogoro nk. kama utatumia mbegu basi ni bora kununua mbegu bora au ukikosa mbegu basi jaribu kutumia zile utakazopata kutoka kwenye tunda lenyewe kwa kufuata kanuni bora za kilimo

Kutokana na hilo ipo haja ya serikali ya nchi yetu kuona kwamba hiyo ni fursa tosha kwa wakulima kupewa mafunzo na kuwawezesha ili kujizatiti katika kilimo cha matunda pendwa kama tufaa ili kuinua uchumi wa mwananchi mmoja mmoja kama si kwa taifa zima

Kwa sasa matufaa mengi yaonekanayo barabarani huletwa Tanzania yakitokea Afrika ya kusini ambako ndiko mafanikio makubwa yamepatikana kwa kilimo cha matunda barani Afrika. Na kilimo cha tufaa nchini humo limefanikiwa baada ya utafiti wa mbegu bora (hybrid) kufanyika na tufaa ni miongoni mwa tunda ambalo lilifanyiwa utafiti huo na ndipo mafanikio yalipopatikana.

Akiongea kuhusu kuruhusu kuingia kwa matunda hayo meneja wa TFDA mkoani Mbeya Bwana Rodney Alananga, amesema kuwa wao kama TFDA wamechunguza kwa umakini na wamehakikisha kuwa matunda haya yanayotoka Afrika ya kusini hayana madhara kama ambavyo watu wengine wamekuwa wakidhani na kuogopa kula matunda hayo kwa dhana ambayo wengi wao wamekuwa wakisema yanamdhara kwa afya ya binadamu. “sisi kama TFDA huwa tunaruhusu chakula kuingia nchini kama hakina madhara hivyo wafanyabiashara wanatakiwa kufuata sheria za kibiashara mpakani kama vile kulipia ushuru  na vinginevyo watu wayatumie tuu kwani tunawahakikishia kuwa matufaa hayo hayana madhara ya aina yoyote” alisema meneja Rodney


Kwa upande wa wakulima wao wameiomba serikali kuchukua baadhi ya wakulima wanaotoka katika maeneo yanayolima matufaa na kuwapeleka Afika ya kusini ili kujifunza kwa vitendo jinsi ya ukulima bora wa matunda hayo ili wao pia waje kuwa mfano kwa wakulima wengine ili kuinua kilimo cha matunda hayo Tanzania. “sisi mpaka leo tunalima matufaa yaleyale ya zamani ambayo ukiyapeleka sokoni watu huyaita ya kienyeji  na wengi hawayapendi kwakuwa yana radha ya uchachu tofauti na yale ya kizungu” akimaanisha yale yatokayo Afrika kusini. alisema Yuda Nyamirandu mkulima wa njombe

“Mkulima hashawishiki mpaka ameona kwa macho ama sivyo utatumia nguvu kubwa sana kumshawishi mkulima kuwa mbegu Fulani inafaida na ndio maana wakulima wa mahindi wanawekewa shamba darasa ili waone na hii isiishie kwenye mahindi tuu” alisema Emmanuel Sanga

Akiongea kwa uchungu sana, Bwana Emmanuel alisema anasikitishwa sana na serikali ya Tanzania ambavyo haijaweka kipaumbele kujali kilimo kimatendo huku akitolea mfano jinsi wakulima ambavyo wanapata shida katika miundo mbinu, pamoja na teknolojia duni katika kilimo. “ Ndio maana vijana wanaona hakuna haja ya kujitesa kuingia katika sekta ya kilimo maana ni kazi ya mateso na ndio maana wanakimbilia mijini, lakini serikali ingejali sekta hii hakuna kijana ambaye angekwenda mjini wote tungebakia kwenye kilimo, lakini sasa matokeo yake hiyo kazi wanafanya wazee wasiokuwa na nguvu matokeo yake njaa inaikumba nchi”

Ikiwa kama kuna uwezekano wa vijana kupata elimu katika kilimo na kuwezeshwa kifedha ni hakika ya kwamba kilimo kwanza ikatimia kuliko kuiacha kauli hii ikaendelea kubebwa na wazee peke yao kama ilivyo sasa kwa vijana wengi kukimbilia mijini na kuwaacha wazee wakashughulika na kilimo. Na malengo haya yanaweza timia ikiwa kila mtanzania atasumama katika nafasi yake na kutimiza majukumu yake impasavyo.

Hata hivyo Tanzania bado hatujachelewa kwani taasisi za utafiti zipo na hivyo utafiti ukifanyika Tanzania yaweza kujikuta juu katika ramani ya wakulima bora duniani na kupata faida kubwa kama wazipatazo wenzetu. Kwani mbegu bora ni chanzo cha tija na mapato kwa wakulima na taifa kwa ujumla.

VIAZI LISHE MKOMBOZI WA UMASKINI JIJINI MWANZA


 
Kama ilivyo kawaida ya misemo ya watafiti wengi wasemao mbegu bora ndio tija kwa kilimo bora.  Msemo huu umekuwa ukitimia katika vituo mbalimbali vya utafiti katika kilimo kwa kujizatiti katika tafiti za mbegu bora zenye  manufaa kwa wakulima nchini.
Mkoani Mwanza kituo cha Ukiriguru Agricultural Research Institute kimefanya utafiti na kuja na mbegu mpya ya viazi vitamu vilivyopewa jina la viazi lishe. Mbegu hizi za viazi lishe vililetwa mwaka 2002 kutoka nchini Uganda na shirika la International Potato Centre  na kufanyiwa utafiti na hatimaye sasa kanda ya ziwa wameanza kufaidi matunda yake.
Viazi vitamu ni kati ya mazao makuu ya mizizi yanayozalishwa kwa wingi  na kutumiwa kama  chakula.

Mara zote zao hilo linapewa nafasi kubwa kuzalishwa na wakulima kwa sababu linavumilia ukame na linahesabiwa kuwa ni moja kati ya mazao ya kinga ya njaa kama ilivyo kilimo cha mihogo.
 


Mikoa inayoongoza kwa uzalishaji wa viazi vitamu ni Mwanza, Shinyanga, Dodoma, Morogoro, Kagera, Arusha na Ruvuma japo kuwa viazi vitamu hivi hilimwa karibu katika kila mkoa hapa Tanzania
Katika Mkoa wa Mwanza viazi lishe vimeonekana kuwa mkombozi baada ya TAHEA (Tanzania Home Economics Association) kuingilia kati na kuwasaidia wakulima kutambua umuhimu wa viazi hivyo. Kwa kushirikiana na taasisi ya utafiti ya Ukiriguru UARI (Ukiriguru Agricultural Research Institute), TAHEA waliamua kutoa mafunzo kwa wakulima ili waweze kujikwamua kimaendeleo na kiuchumi kupitia mbegu mpya za viazi lishe ambazo ni matokeo ya utafiti wa mbegu bora za viazi hivyo uliofanywa na UARI.
Wanawake ndio waliokuwa wakwanza kupata mafunzo hayo baada ya kuonekana wao ndio wakulima wa zao hilo kutokana na zana ya kwamba halina faida kibiashara hivyo kulimwa kwa matumizi ya chakula pekee.
Baada ya utafiti kufanyika na kupatikana aina tano ikiwa ni Ejumla, Karoti Dar, karoti C, Kabode na Jewel za mbegu mpya ambazo zimetofutiana matumizi na ustahimilivu wake, ndipo TAHEA ikawafundisha wanawakea hao kilimo bora, uvunaji bora pamoja na usindikaji ili kupata manufaa zaidi ambayo hapo awali hayakuwepo.
 
Pichani, Unga viazi lishe baada ya kuwekwa kwenye paketi tayari kwa kwenda sokoni 

Ramadhani Bundala ambaye ni afisa kilimo wa TAHEA akifafanua kazi kubwa ambayo wameifanya katika mradi huu wa kuwafundisha wakulima wa viazi kujikwamua kimaisha alisema kuwa“ wanawake wamekuwa wakielemewa sana na kazi za kulea familia huku wakijibakiza nyuma kuwa wao huwa wanalima mazao kwa ajili ya chakula hivyo tukaona ni bora tuwaelekeza wanawake hawa kuwa wanaweza wakalima viazi kama zao la biashara. Tukawaweka katika vikundi na kuwapa mbegu mpya kisha kuwafundisha kuanzia kuandaa shamba mpaka usindikaji. Huwezi amini kwa sasa kilimo hiki cha viazi kimevamiwa na wanaume baada ya kuona mafanikio walioyapata kwenye vikundi hivi.”
Bundala alisema kuwa mbali na kuwa chanzo cha mapato viazi lishe pia vina faida kubwa ikiwamo kuboresha afya hasa za watoto chini ya miaka mitano. Pia viazi lishe vyenye vitamin za aina nyingi ikiwamo vitamin A, vinasaidia watu wenye matatizo ya macho, kuboresha afya za akina mama wajawazito na wanaonyonyesha na kuongeza kinga ya mwili hasa kwa watu wanaoishi na maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi.
Kwa upande wao wakulima, wanakikundi cha Imala buhabi cha jijini mwanza wametoa shukrani zao kwa TAHEA pamoja na Ukiriguru kwa kuwafikisha walipo kwani wanamabadiriko makubwa kimaisha tofauti na hapo awali.

Naye Bi Mwanaidi  mjumbe wa kikundi hicho alisema kuwa japo kuwa yeye ni mjane anayelea familia anauwezo wa kuwapeleka watoto wake shule na kujenga nyumba nzuri ya familia kutokana na viazi lishe anavyolima.
Wakieleza kwa upande wa changamoto wakulima hao walisema kuwa pamoja na mafanikio hayo pia wakulima wa zao hilo wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo ni pamoja na ukosefu wa soko la uhakika na  ukosefu wa usafiri kutoka shambani kwenda sokoni.

Wameiomba serikali kushirikiana mashirika na kampuni binafsi kuwahamasisha wakulima  kuongeza jitihada katika kilimo hicho na kuongeza idadi ya maofisa ugani ili wawaongezee uwezo wa kuzalisha na kutafuta masoko zaidi. Na ikiwezekana serikali iwasaidie wakulima hawa kuwatangazia kazi zao katika soko la nje ili kuwaendeleza wakulima.

kwa mantiki hiyo basi Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA),  pia wanapaswa kuwafikia wakulima ili waweze kukagua kazi za wakulima, kuwaelimishe kwa lengo la kuwawezesha kuzalisha kwa ubora zaidi ili kuwapa uelewa wakulima ni jinsi gani wanaweza kuandaa bidhaa zao ili waweze kufika mbali zaidi na kujikwamua kutoka katika wimbi la kilimo duni na kufika mbali zaidi kama ilivyo katika kilimo cha mazao mengine kama vile kahawa, korosho na mazao mengine ambayo yapo kwenye ramani ya kuipatia pesa za kigeni nchi yetu.

Nae Robert Kileo afisa habari wa Ukiriguru amesema kuwa Kutokana na umuhimu wa viazi lishe Kituo cha utafiti wa Kilimo Ukiriguru  kikishirikiana na TAHEA kwa pamoja wamebuni mpango wa  kuhamasisha wakulima na wananchi kwa ujumla ili wafahamu umuhimu wa zao hilo.



Kileo alisema kwakuwa Tanzania ipo katika kufanya mapindizi ya kijani na kilimo kwanza inatakiwa kila sekta katika serikali kuunga mkono jitihada za wakulima ili kufanya kazi yakilimo iwe ajira kwa watanzania wengi ambao kilio chao kikubwa sasa ni ukosefu wa ajira nchini. 

Wataalam kutoka katika vituo hivyo wanasema kuwa, mbali na kuwaelimisha kuhusu faida zake pia wakulima wanaelimishwa umuhimu wa usindikaji wa viazi lishe na uendelezaji wa masoko katika mikoa ya kanda ya ziwa
Hivyo  serikali inapaswa kuingilia kati katika kuhamasisha wananchi kulima zao hilo, kutafuta masoko kwa ajili ya wakulima ambao wamekwishaanzisha kilimo hicho na kuwataka wananchi ambao bado hawajajiunga wafanye hivyo kwa manufaa yao na taifa kwa ujumla.

Ushauri mwingine kwa serikali ni kuhimiza matumizi ya teknolojia katika kukibadilisha kilimo cha viazi lishe ili kiwe cha kisasa na cha tija pamoja na kumwezesha mkulima mdogo kumiliki ardhi  na kuanzisha vituo vya kumsaidia.

Baadhi ya bidhaa zitokanazo na vizi lishe

ILIYOKUWA BAR SASA NI KANISA

 

Baa iliyopo Sinza-Lion jijini Dar ambayo imegeuzwa kuwa kanisa.
WAKATI matukio mengi ya kushangaza na kushtukiza yakiendelea kutokea kila siku duniani, neno la Mungu nalo linazidi kushika kasi kufuatia baa moja iliyopo Sinza-Lion jijini Dar kugeuzwa kuwa kanisa.Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa baa hiyo maarufu iitwayo The Don, ukumbi wake ambao ulikuwa ukitumika kwa watu kupiga ulabu, hivi sasa unatumiwa na waumini wa kanisa linalojukana kama Impact International Christian Centre kupata mahubiri. Lakini cha kushangaza ilibainika kwamba katika maandishi makubwa yanayolinadi jina la baa hiyo, chini yake ndipo limewekwa bango linaloonyesha kanisa hilo, kitu ambacho kwa mtu mgeni, ni vigumu kuelewa mara moja.

MWAAFUNZI WA TANZANIA AIBUKA KIDEDEA TUZO ZA ISHA SADC


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza mwanafunzi wa kidato cha nne Neema Steven Mtwanga(16) anayesoma katika shule ya sekondari Naboti Makambako,Njombe baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika utunzi wa insha katika shindano lililoandaliwa na Jumuiya ya uchumi ya maendeleo kusini mwa Afrika(SADC).Rais Kikwete alimpongeza mwanafunzi huyo wakati wa hafla ya ufunguzi wa mkutano wa 34 wa wakuu wa nchi za SADC unaofanyika katika mji wa kitalii wa Victoria Falls, nchini Zimbabwe ambapo mwanafunzi huyo aliandika insha inayohusu mabadiliko ya tabia nchi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wakuu na wawakilishi wa nchi za Jumuiya ya uchumi kusini mwa Afrika SADC muda mfupi baada ya ufunguzi wa mkutano wa 34 wa jumuiya hiyo uliofanyika katika hoteli ya Elephant Hills mjini Victoria Falls Zimbabwe leo.Katikati ji mwenyeji wa Mkutano huo Rais Robert Mugabe na mkewe Grace Mugabe(picha na Freddy Maro)

WATU WAWILI WAFARIKI PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA GARI ILIYOBEBA MAITI 10.


 Watu wawili wamefariki dunia papo hapo baada ya gari aina ya Land Cruser ilikuwa imebeba maiti 10 zikitokea hosiptali ya taifa Muhimbili kwenda hospitali ya St Francis Ifakara kugonga wapanda pikipiki katika eneo la Mtego wa simba Mikese mkoani Morogoro
Maiti zilizokuwa zinapelekwa hospitli ya St Fancis Ifakar kwa lengo la kufanya utafiti 

Gari lililosababisha ajali toyota Land Cruser 

 Mwili wa mmoja waliofariki katika ajali hiyo 
Pikipiki iliyosababishiwa ajali na kutoa uhai wa watu wawili waliokuwa wanakwenda shamba
Akizungumzia tukio hilo kwenye  eneo la tukio mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Bonifasi Mbao amesema gari hiyo ikiendeshwana dereva Pankrasi Pasco mkazi wa ifakara iliwagonga wapanda pikipiki Shaban Rajab na Ally Benulo wakazi wa Mikese na kufariki dunia papo hapo na chanzo cha ajali  mwendo kasi na dereva anashikiliwa na jeshi la polisi, kuhusu maiti 10 zilizokuwemo katika gari hiyo amesema zilikuwa zikipelekwa hospitli ya St Fancis Ifakar kwa lengo la kufanya utafiti na mafunzo ambapo wanafanya mawasilino ya kuzifikisha katika hospitali hiyo.
Nao wananchi walioshuhudia tukio hilo wameeleleza chanzo cha ajali hiyo ni mwendo  kasi huku wakilalamikia matukio ya ajali nyingi katika eneo hilo kutokana na kona na kuomba serikali kuweka matuta  na vibao vya tahadhari.

SAMAKI MKUBWA AVULIWA MTO AMAZO



Samaki aliye na urefu wa mita tatu aliyekuwa maarufu katika mto Amazon amevuliwa hadi ameangamia

Watafiti wamedhihirisha kuwa samaki huyo mkubwa hapatikani tena katika maeneo aliyokuwa maarufu.

Imebainika sasa kuwa samaki wa Arapaima alipatikana katika maeneo 8 kati ya 41 zilizofanyiwa utafiti, na idadi ya samaki huyo ilikuwa ndogo sana kuliko ilivyokuwa inatarajiwa.

Wavuvi walipewa mafunzo jinsi ya kuhesabu samaki hao ili kufanikisha utafiti huo mkubwa.

Watafiti walikata kauli kuwa athari za uvuvi kwa samaki wa kitropiki zilikuwa mbaya zaidi ya ilivyoaminika hapo awali.

Matokeo ya utafitihuo yaliripotiwa kwa shirika la uhifadhi wa mazingira yanayozalisha viumbe vya majini ''Aquatic Conservation: Freshwater and Marine Ecosystems''.

Arapaima huweza kuwa na uzani wa kilo 181 na ni mojawapo ya samaki wakubwa zaidi wanoishi katika maji yasiyo na chumvi.
 
 Samaki mkubwa zaidi wa maji matamu Arapaima. 

Samaki hao hupumua hewa sawa na binadamu, hivyo basi huibuka kutoka majini kupumua kila baada ya dakika kati ya 10-15 hivyo basi huwa ni rahisi kuwakamata.

Ukubwa wa Arapaima huvutia wavuvi kuwawinda na aghalabu huwanasa kwa kutumia chusa au nyavu za uvuvi.

Karne moja iliyopita, idadi ya Arapaima ilikuwa kubwa katika mto wa Amazon, lakini watafiti wanasema kuvua kupita kiasi kumesababisha idadi hiyo kupungua kwa kiwango kikubwa sana.

Hapo awali, utafiti nadharia ulitabiri kuwa uvuvi hauwezi kuangamiza aina fulani ya samaki majini kwani wavuvi huenda kuvua maeneo tofauti idadi ya samaki inapopungua katika eneo moja.

Wanasayansi, wakiongozwa na Leandro Castello, kutoka Virginia Marekani, walitaka kufahamu afya ya samaki wa Arapaima walioko eneo la chini la Amazon.

Aidha walitaka kugundua iwapo shughuli za uvuvi ziliunga mkono au kupinga utabiri wa nadharia tofauti.

Kuna nadharia zinazopendekeza kuwa samaki wakubwa, walio ghali, na ambao ni rahisi kukamatwa huweza kuvuliwa na kuisha majini, huku nadharia zingine zikipinga msimamo huo.

Watafiti hao walihoji wavuvi 182, walioaminika kuwa magwiji na wenzao, katika jamiii 81, zinazoishi katika eneo la kilomita 1,040, la Amazon.

Shughuli hiyo ilijumuishwa hesabu ya Kulifanywa ya samaki katika jamii 41 kati ya jamii zilizohojiwa.

Wavuvi nane walifunzwa kuhesabu idadi ya Arapaima pindi tu walipotokea majini.

Matokeo ya hesabu hiyo ni kuwa idadi ya Arapaima ilikuwa imepunguka katika asilimia 57% ya eneo la utafiti, Arapaima hawakuwepo katika asilimia 19% ya eneo hilo, na walivuliwa kupita kiasi katika asilimia 17% ya eneo hilo la utafiti, huku asilimia 5% tu wakifanya uvuvi unaokubalika.

Kwa 2% ya jamii zilizofanyiwa utafiti, samaki hao hawakuvuliwa.