Tuesday, November 4, 2014

MTOTO WA MIAKA 10 ABAKWA NA MZAZI WAKE

NA Baraka lusajo.
Kamati ya  ulinzi  na usalama ya  kijiji cha mwela  kata ya kandete  wilayani rungwe mkoani mbeya inamtafuta   geofrey mwasumbi   miaka  {36}  baada ya kumbaka mtoto wake   mwenye  umri  wa  miaka  {10}.
 Wakizungumza na kituo hiki mashuhuda wa tukio hilo wamesema tukio hilo la kushangaza limejitokeza  wakati mtoto  huyo akiwa amejituliza  katika makazi yao  na kijukuta akivamiwa  na baba mzazi kwa  kubakwa na kisha kuachiwa  maumivu  makali  katika sehemu zake  za siri.
  Kwa  upande wa mama  mzazi wa  mtoto  huyo  alisema  ,
    wakati  tukio  hili lina tokea  nilikuwa  shamba  lakini  baada  ya kulejea nilikuta  mtoto wangu akiwa anatokwa na  damu  na huku akishindwa  kutembea  ambapo  niliamua  kumkalisha  kitako   kwa kumhoji  na  badaye akaniambia  kuwa  alilazimishwa na baba yake kufanya  tendo  la ndoa  ambapo  niliamua  kutoa  taarifa  katika  uongozi wa kijiji   hicho na wao walitoa  taafa katika  uongozi wa    kata  na kisha  kumchukua  mtoto na kumpeleka katika kituo cha afya  cha mwakaleli kwa  matibabu zaidi.
Huruma mwakyusa afisa  mtendaji wa  kata  hiyo  mbali na kukili  kutokea  kwa  tukio hilo  alisema  mtuhumiwa alikimbia kwa kutomoea  kusiko julikana  mara  baada  ya  tukio  kufanyika  na kwamba juhudi za  kumtafuta  bado zinaendelea  jampo  mtoto  huyoamelazwa  katika kituo cha afya  cha  mwakaleli kwa matibabu.

    Diana  godwini  mratibu  wa  dawati la kijinsia   kupitia bonde la Mwakaleli   mbali na kukili kujitokeza kwa tukio hilo amesema   wametoa  taarifa  polisi  kwa lengo la kusaidia  kumsaka mtuhumiwa.
Aidha   gidwini alisema  vitendo vya  ubakaji katika maeneo  hayo  vimeendelea  kuchukua sera  mpya  kutokana  na uelewa   na  imani   za  kishirikina.
  Hata  hivyo judi na maalfa za  kumtafuta  mganga mkuu wa kituo  cha  afya  cha mwakaleli  Dr  edwini  mwakisisya  zimegonga mwamba  baaada  ya kukosekana  ofisini kwake.

RAIS KIKWETE AZUNGUMZA NA WAZEE WA MKOA WA DODOMA LEO


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wazee wa mji wa Dodoma leo Novemba 4, 2014 waliouitisha ili kuzungumza naye maswala kadhaa ya maendeleo.
 Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani wakati wa  Mazungumzo kati ya RaisJakaya Mrisho Kikwete na  wazee wa mji wa Dodoma leo Novemba 4, 2014 waliouitisha ili kuzungumza naye maswala kadhaa ya maendeleo

‘MTOTO WA NDEGE’ AOKOKA


Stori: Haruni Sanchawa na Denis Mtima
MTOTO Happiness Lyoba (10) ambaye aliripotiwa kuwa mwingi wa vituko vya maajabu, ikiwamo kuonekana akishuka katika ndege huko Zanzibar, ameripotiwa kuokoka katika Kijiji cha Mkokozi, wilayani Mkuranga, Pwani.
Mtoto Happiness Lyoba (10) akisoma Biblia.
Akizungumza na gazeti hili, mama wa mtoto huyo, Salah Zefania alisema mwanaye huyo alitoroka tena Septemba 16, mwaka huu na kukamatiwa eneo la Feri jijini Dar es Salaam, akidai kuwa ameitwa  na baba yake.
Baada ya kumkamata na kuanza kurejea naye kijijini Mkokozi ambako amehifadhiwa na msamaria mwema, alisema alipata simu nyingi za watu kumpa pole kwa tukio hilo, hali iliyomshangaza kwani hakuelewa watu hao walipataje habari hizo.
Mama mzazi wa mtoto Happiness Lyoba , Salah Zefania.
Miongoni mwa simu hizo ni pamoja na ya Mwinjilisti wa kanisa lao la Kisabato Mbagala aliyemtaja kwa jina la Jacob Mayala ambaye alihitaji kumuombea mtoto wake. ‘’Ni kweli Mwinjilisti huyo alifika Mkokozi na kufanya maombi maalumu yaliyoambatana na kufunga kwa siku kadhaa. Hali ya mwanangu kwa sasa ninakubaliana nayo maana amegeuka kuwa  binadamu ambaye  nilimtarajia, Happiness  hakuwa hivi maana alizidisha vituko vya maajabu,” alisema.
Mtoto Happiness Lyoba akiwa na mama yake.
Mama huyo amewaomba Watanzania wamsaidie mwanaye kusoma kwani hivi sasa anajitambua tofauti na huko nyuma.“Mimi kipato changu ni kidogo na huku niliko ni mbali sana, hakuna shule karibu, kazi yangu ni kilimo cha mbogamboga na tena hapa ninapoishi nimehifadhiwa tu, ninaomba msaada ili mtoto wangu aende shule,” alisema mama huyo akidai kuwa Ustawi wa Jamii ulimshauri kumweka binti yake mbali na maeneo aliyokuwa akiishi.
“Nilishauriwa asirudi  Kitunda kwa muda huu maana huko ndiko alikoanza kupatwa na hali ambayo naamini ilikuwa ni mapepo,” alisema.
Mtoto na mama wakisali pamoja.
HAPPINES  LYOBA
Kwa upande wake, Happines alisema anahitaji kusoma na kwamba matukio aliyokuwa akiyafanya hakujua yalivyotokea.

Mtu yeyote aliyeguswa na hali ya mtoto huyu ambaye akili yake imerejea kuwa ya kawaida kufuatia maombi ya kila siku, anaweza kuwasiliana na mama yake

ZITO KABWE AWASWEKA RUMANDE VIGOGO WA TPDC



01
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPDC, Michael Mwanda (mbele) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, James Andilile (nyuma yake), wakiongozwa na Polisi kuingia kwenye gari kwa ajili ya kupelekwa rumande baada ya kamati hiyo, kuwakuta na hatia ya kuidharau na kuinyima taarifa muhimu, wakati ilipokaa kama Mahakama katika kikao chake hicho.
02Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe, akifafanua jambo wakati akiwahoji Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Michael Mwanda na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, James Andilile wakati kamati hiyo, ilipokaa kama Mahakama katika kikao chake kilichofanyika jana, Ofisi za Bunge, Dar es Salaam. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Deo Filkunjombe.
03Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, James Andilile (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya TPDC, Michael Mwanda
04Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPDC, Michael Mwanda (mbele) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, James Andilile (nyuma yake), wakiongozwa na Polisi kwenda kuingia kwenye gari kwa ajili ya kupelekwa rumande baada ya kamati hiyo, kuwakuta na hatia ya kuidharau na kuinyima taarifa muhimu, wakati ilipokaa kama Mahakama katika kikao chake hicho.

HIVI NDIVYO VIJANA WALIVYOVURUGA MDAHALO UBUNGO PLAZA



Jaji Joseph Warioba akitoa mada. 
Mtoa mada katika mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa, Jaji Joseph Warioba akitoa mada kabla ya mkutano huo kuvunjika katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Saam.
Baadhi ya vijana walioingia na mabango ndani ya ukumbi wa mkutano wakiwa na mabango yaliyokuwa yakisomeka ‘Katiba inayopendekezwa tumeipokea tunaiunga mkono’.
Mlinzi wa Jaji Joseph Warioba (kushoto) akimkinga kwa mikono ili asipate madhara baada ya mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa kuvamiwa na kundi la vijana na kusababisha uvunjifu wa amani. 
Jaji Joseph Warioba akiangalia usalama wake kabla ya kuondolewa mlinzi wake katika ukumbi wa Ubungo Plaza ambapo mdahalo wa kuijadili Katiba inayopendekezwa ulikuwa ukifanyika kabla ya kuvunjika.
Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole akimzuia mmoja wa vijana aliyekuwa na jazba mara baada ya kutokea kwa vurugu katika mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekeza.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku (katikati) akisindikizwa kuingia katika chumba cha VIP mara baada ya kuvunjika kwa mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa. Mdahalo huo uliandalia na taasisi hiyo.
 Vijana wakiwa na mabango. 
 Mabango yakiwa juu. 
 Vujo zinaanza. 
 Mmoja wa vijana waliokuwa wakitoa maneno ya kashfa kwa Jaji Warioba akiwanyooshea vidole viongozi wa meza Kuu. 
 Baadhi ya viti vilivyovujwa. 
 Jaji Warioba akitoka katika ukumbi huku akisindikizwa na askari kanzu. 
 Jaji Warioba akisindikizwa na makachero wa Polisi. 
 Jaji Warioba akiwapungia mkono wananchi waliokuwa wamefurika nje ya jengo la Ubungo Plaza ambako mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa ulikuwa ukifanyika.Wananchi walikuwa nje ya jengo la Ubungo Plaza wakimshangilia Jaji Warioba wakati akitoka katika ukumbi wa mdahalo huku wakimuita 'Rais Rais'

Monday, November 3, 2014

ANGALIA TAARIFA KAMILI KUHUSU VURUGU ALIZOFANYIWA JAJI WARIOBA JANA JIJINI DAR ES SALAAM


 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba, jana alifanyiwa vurugu kubwa zilizosababisha kuvunjika kwa kongamano la kujadili mambo ya msingi ya kuangaliwa katika Katiba inayopendekezwa.
Kongamano hilo liliandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) na wazungumzaji wakuu walikuwa ni waliokuwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Miongoni mwao ni Joseph Butiku, Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Palamagamba Kabudi na Humphrey Polepole.

Jaji Warioba alipoanza kuzungumza, ndipo kikundi cha vijana kinachodaiwa kuwa kiliandaliwa dhidi ya kiongozi huyo kilipoanzisha vurugu hizo.

Vijana hao waliingia mapema katika ukumbi wa Ubungo Plaza, jijini Dar es Salaam, lakini baada ya Jaji Warioba kuanza kuzungumza waliibuka na mabango kisha kusogelea jukwaa alikokuwa amekaa Jaji Warioba na wajumbe wenzake.

Mabango mengi yalikuwa yakifanana kwa maudhui, aina ya wino uliotumika na pia hati ilionekana kufanana kwa kiasi kikubwa.

Mabango sita kati ya hayo, ambayo yalishikiliwa na vijana tofauti yaliandikwa kwa kalamu ya wino mzito mwekundu (marker pen) na matatu yalikuwa na ujumbe uliosomeka; "Katiba inayopendekezwa tumeipokea, tumeielewa na tunaiunga mkono."

Mengine matatu ya maandishi ya rangi ya bluu yalisomeka: "Katiba inayopendekezwa tumeipokea, na tunaiunga mkono."

Mengine yalisomeka “Fedha za Magharibi haziwezi kuibomoa nchi yetu, na Wananchi ndiyo wana maamuzi ya mwisho, Tume mnafanya kazi ya nani?”

Hali hiyo ilivunja utulivu ndani ya ukumbi kutokana waliokuwa na mabango kuendelea kuyainua juu huku kundi lingine likiwafuata kuwanyang’anya na kuyachana.

Hali hiyo pia ilisababisha watu waliokuwa ndani ya ukumbi kurushiana viti na kuwalazimisha wengine kutoka nje kuhofia usalama wao.

Kutokana na hali hiyo, Jaji Warioba na wenzake walitolewa katika ukumbi wa mikutano na kuingizwa katika chumba maalum kwa ajili ya usalama wao.

POLISI WAFYATUA MABOMU
Takribani dakika 10 baada ya kuibuka kwa vurugu hizo, polisi walifika katika eneo hilo na kufyatua mabomu ya kutoa machozi yaliyosababisha mamia ya watu waliokuwa katika eneo hilo kukimbia, kuanguka ovyo na wengine kujeruhiwa.

NIPASHE lilishuhudia polisi wakiwa wamewashikilia vijana wawili kwa kuhusishwa na vurugu hizo.

MWANDISHI APIGWA
Baadhi ya watu waliopigwa ni pamoja na Katibu wa Chipukizi na Uhamasishaji wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Paul Makonda na mwandishi wa BBC, Anold Kayanda, ambaye alijeruhiwa kichwani kutokana na vurugu za ukumbini baada ya kurushiwa kiti.

Awali, Jaji Warioba, alisema asilimia 81 ya ibara za Rasimu ya Tume yamo kwenye katiba inayopendekezwa, hata hivyo, maudhui yake yakitazamwa kwa makini mambo mengi ya msingi yametupwa. Aliyataja mambo manne ya msingi yenye kuleta mabadiliko ambayo yalipendekezwa na wananchi yaliyoondolewa kuwa ni tunu za maadili ambazo kwa mujibu wake, zilibadilishwa na kuwa urithi, madaraka ya wananchi, mgawanyo wa madaraka kutengenisha mihimili ya Serikali na Bunge na Muundo wa Muungano.
 
 
Alisema kuna baadhi ya mambo yaliyopo kwenye katiba inayopendekezwa yanatia shaka iwapo yatakuwa katika utekelezaji yakiwamo mgombea binafsi na asilimia 50 kwa 50 ya wabunge wanawake na wanaume.

Kuhusu kura ya maoni alisema ni lazima wananchi waandikishwe kwanza kwenye daftari la kupiga kura huku akiwataka kuwa makini kuyapigia kura mambo ya msingi.
Hata hivyo, mdahalo huo haukumalizika kutokana na hali hiyo na hatimaye kufungwa na Katibu Mtendaji wa MNF, Joseph Butiku.

Baadaye, Jaji Warioba alionekana akiondolewa eneo hilo kutoka chumba maalum alichokuwa amewekwa huku akiwa anasindikizwa na watu wa usalama akiwa mzima na kupanda kwenye gari lake na kuondoka eneo hilo.
CHANZO: NIPASHE