Tuesday, November 4, 2014

ZITO KABWE AWASWEKA RUMANDE VIGOGO WA TPDC



01
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPDC, Michael Mwanda (mbele) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, James Andilile (nyuma yake), wakiongozwa na Polisi kuingia kwenye gari kwa ajili ya kupelekwa rumande baada ya kamati hiyo, kuwakuta na hatia ya kuidharau na kuinyima taarifa muhimu, wakati ilipokaa kama Mahakama katika kikao chake hicho.
02Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe, akifafanua jambo wakati akiwahoji Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Michael Mwanda na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, James Andilile wakati kamati hiyo, ilipokaa kama Mahakama katika kikao chake kilichofanyika jana, Ofisi za Bunge, Dar es Salaam. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Deo Filkunjombe.
03Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, James Andilile (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya TPDC, Michael Mwanda
04Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPDC, Michael Mwanda (mbele) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, James Andilile (nyuma yake), wakiongozwa na Polisi kwenda kuingia kwenye gari kwa ajili ya kupelekwa rumande baada ya kamati hiyo, kuwakuta na hatia ya kuidharau na kuinyima taarifa muhimu, wakati ilipokaa kama Mahakama katika kikao chake hicho.

No comments:

Post a Comment