Thursday, August 28, 2014

AGEUKA KUWA KICHAA KWA KUVAMIWA NA MAJIPU BAADA YA KUPIGIWA SIMU NA WATU WASIO FAHAMIKA

Na Baraka lusajo, Mbeya.
Binti mmoja mkazi wa  kijiji cha Ntete  kata ya lufingo wilayani Rungwe mkoani  mbeya Nelu  mwakasuri   ameingia katika wakati mgumu  baada ya  kupigiwa simu  na mtu /watu wasio fahamika na kugeuka kuwa  kichaa  kwa  ghafla.
 Akisimulia   kwa masikitiko makubwa   mama  mzazi wa binti huo  Eda  Nsiani alisema tukio  hilo la kuskisikitisha lilitokea   majila ya  sanane ya   usiku wakati  binti yake akiwa amelala   chumbani  kwake na mtoto wake  mwenye  umri wa mwezi mmoja na kushangaa  baada  ya  binti  yake  kuanza  kupiga makelele  ya kuomba msaada  akisema’’  Nisaidieni  nisaidieni   mwenzenu  nimepigiwa  simu sasa hivi  na mtu au  watu wasio fahamika lakini  sikio limeanza kuniuma kwa ghafla na  nahisi  kichwa changu  kung’oka nisaidieni tafadhar’’ alisema  mama mzazi,
 Alisema  baada  kufika  chumbani   kwake  nilikuta  binti  yangu akijitupa huku na kule ambapo  baada ya hali hiyo kuzidi kuchukua  sula mpya  niamua  kuchukua  hatua  ya  kuwaita  watumishi wa mungu   ambao walifika  muda  mfupi   na kuanza  kufanya maombi  usiku  mzima  lakini  pamoja na kufanyiwa  maombi   kote  bado hali iliendelea  kuwa  mbaya kupita  kiasi  kwani ilipo timu majila  ya  asubuhi niliamu kumwachia huru, lakini  cha kushangaza  nilikuta  akinza kukimbilia barabarani  na huku  akisema  anatafutwa  na  ndugu zake  kuzimu na kusema   ukichana  na kukimbilia  barabarani  mda  mwingine  anakuwa akichukua  kisu akitaka  kujiua  mwenyewe  na kupelekea  kumfungia ndani wakati  wote akiwa amefungwa  na kamba.
   Alisema   baada ya kukumbwa  na hali  hiyo     baada ya muda mfupi alianza  kuvamiwa na majipu  ya ajabu  kuzunguka  mkono wake wa  kushoto   ambao mpaka sasa  umevimba   vibaya kutokana na kuvamiwa na majipu hayo.
 Kwa  upande  wa wakazi wa maeneo hayo  walisikitishwa  na hali hiyo na  ukizingatia  kuwa  ni  tukio la  kwanza  kujitokeza kijijini hapa  na  kuwaomba  watumishi wa mungu kutoka  sehemu mbalimbali kufika  katika  eneo hilo kwa  lengo  kumuona  mgonjwa  mwadhirika  wa tukio hilo  ikiwa ni pamoja  na kumfanyia  maombi ili waweze kurudi katika  hali yake  ya kawaida. 



No comments:

Post a Comment