PATROBAS Paschal amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, (Bavicha).
Mwenyekiti huyo alichaguliwa katika
uchaguzi uliyofanyika juzi usiku katika ukumbi wa Mlimani City jijini
Dar es Salaam, kunakoendelea uchaguzi mkuu wa chama hicho Taifa.
Akitangaza matokeo hayo jana, Mwenyekiti
wa Baraza la Wazee Taifa ambaye ndiye msimamizi wa uchaguzi wa vijana,
Hashim Issa, alimtangaza Patrobas kuwa mshindi kwa kura 173..Mwenyekiti
mpya wa BAVICHA, Patrobas Paschal
Hata hivyo, uchaguzi huo ulifanyika katika awamu mbili ambako ya kwanza Upendo Peneza alipata kura 68 na Patrobas Paschal 61
Alifafanua kuwa kufanyika kwa uchaguzi wa awamu ya pili ni baada ya mshindi kutopata asilimia 50 ya kura alizopata.
Issa, alisema katika nafasi ya Makamu
Mwenyekiti Bara ilikuwa ikiwaniwa na wagombea 11 ilichukuliwa na Patrick
Ole Sosopi aliyepata kura 128 dhidi ya mpinzani wake Jesca Kisikwa
aliyepata kura 110.
Alisema kwa upande wa Zanzibar Makamu
Mwenyekiti iliyokuwa na wagombea watano, mshindi ni Zeudi Abdallah
aliyepata kura 126 dhidi ya Shabani Omary Shabani kura 69.
No comments:
Post a Comment