Friday, October 3, 2014

WABUNGE WALIVYOJIACHIA JANA BUNGENI

1
2Wajumbe wa Bunge Maalum la katiba wakishangilia leo mjini Dodoma mara baada ya matokeo ya upigaji kura kuonyesha kuwa Theluthi mbili ya Zanzibar imepatikana.
3Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Anne Makinda akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa Bunge la Katiba na uongozi wao pamoja na uongozi wa nchi kabla ya bunge hilo kuvunjwa rasmi leo mjini Dodoma.
4Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, mhe. John Shibuda akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa Bunge la Katiba na uongozi wao pamoja na uongozi wa nchi kabla ya bunge hilo kuvunjwa rasmi leo mjini Dodoma.
5Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. John Cheyo akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa Bunge la Katiba na uongozi wao pamoja na uongozi wa nchi kabla ya bunge hilo kuvunjwa rasmi leo mjini Dodoma.
6Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar  ambaye pia ni mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Pandu Ameir Kificho akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa Bunge la Katiba na uongozi wao pamoja na uongozi wa nchi kabla ya bunge hilo kuvunjwa rasmi leo mjini Dodoma.
7Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Selemani Nchambi akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa Bunge la Katiba na uongozi wao pamoja na uongozi wa nchi kabla ya bunge hilo kuvunjwa rasmi leo mjini Dodoma.
8Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa Bunge la Katiba na uongozi wao pamoja na uongozi wa nchi kabla ya bunge hilo kuvunjwa rasmi leo mjini Dodoma.
10 (1)Makamu wa Pili wa Zanzibar ambaye pia alikuwa ni mjumbe wa Buge Maalum la Katiba, Mhe. Balozi Seif Ali Idd akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa Bunge la Katiba na uongozi wao pamoja na uongozi wa nchi kabla ya bunge hilo kuvunjwa rasmi leo mjini Dodoma.
11Aliyekuwa Makamu wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza bunge hilo mjini Dodoma wakati wa ufungaji wa bunge hilo leo 2 Septemba, 2014.
13Waziri Mkuu wa Tanzania ambaye pia alikuwa mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Mizengo Pinda akitoa akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa Bunge la Katiba na uongozi wao pamoja na uongozi wa nchi kabla ya bunge hilo kuvunjwa rasmi leo mjini Dodoma.
15Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta akiwashukuru wajumbe na Watanzania kabla ya kuvunja bunge hilo rsmi leo 2 Septemba, 2014 mjini Dodoma.
17 (1)Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wakitoa maneno ya shukurani kwa wajumbe na Watanzania kabla ya kuvunja bunge hilo rsmi leo 2 Septemba, 2014 mjini Dodoma.

MKE, MUME WAVUANA NGUO WAKIZICHAPA HADHARANI



Hii ni aibu kubwa! Njemba mmoja aliyefahamika kwa jina la Zeno na mkewe Mwajuma Mtata, wakazi wa mtaa Mrefu, Kigogo-Luhanga jijini Dar wamenaswa wakiangusha bonge la timbwili barabarani na kusababisha umati wa watu kujikusanya eneo hilo kujionea ‘sinema’ ya bure.Timbwili zito likianza kati ya njemba mmoja anayefahamika kwa jina la Zeno na mkewe Mwajuma Mtata. Tukio hilo lililofananishwa na muvi ya kivita lilitokea usiku wa Jumanne iliyopita ambapo chanzo kimedaiwa kuwa ni mwanamke huyo kutelekeza jikoni kitoweo cha maini ya mbuzi na kwenda baa kupata kilaji. 
Kwa mujibu wa chanzo makini, siku ya tukio, Zeno alirudi nyumbani mida ya jioni mkononi akiwa na kifurushi chenye maini ya mbuzi pamoja na mazagazaga mengine zikiwemo ndimu, tangawizi, pilipili hoho, nyanya na vitunguu kupokelewa na ‘mai waifu’ wake huyo.
 PICHA ZAIDI>>
Mke akimlia 'taimingi' kumbwaga mume wake kwa mweleka.
MUME ATOKA KIDOGO
Baada ya Zeno kumkabidhi mkewe mazagazaga hayo kwa ajili ya mlo wa usiku, alimuaga mkewe kuwa anakwenda kutembea ili akirudi akute msosi uko tayari, wale, walale.
“Dakika kadhaa baada ya mumewe kutoka, nasikia bibie naye alichomoka na kwenda baa ya jirani ‘kusukutua mdomo’.
Mara Puuuuu...!! wote chini “Sasa akiwa pale baa, alizidi kunogewa na masaa yalizidi kupotea ndipo Zeno alirudi nyumbani na kukuta mlango umeegeshwa na mkewe hayupo huku akisikia harufu kali ya kitu kuungua na kumfanya apige chafya.
“Alipokaa sawa alibaini kuwa maini aliyoleta yalikuwa yameungua na kuwa kama mkaa hali iliyompandisha hasira na kuanza kumsaka mkewe,” kilidai chanzo hicho.
Mume (Bw Zeno) akimburuta mkewe kwa ghadhabu. AMUIBUKIA BAA
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwamba, Zeno akiwa katika sakasaka yake ndipo alipombamba mkewe kwenye baa hiyo akimalizia ‘kunyonya’ kilevi kikali. ZACHAPWA 
Bila kuuliza, Zeno alimkunja mkewe na kumtoa nje huku akimpa makofi ndipo Mwajuma akaona kama anaonewa hivyo akamvizia mumewe na kumchota mtama ambapo wote walikwenda chini kutokana na kuwa katika hali ya kuzidiwa na kilaji.
Wote wakichukua uamuzi wa kuzima timbwili hilo. LAHAMIA NJE YA BAA
Timbwili hilo liliendelea nje ya baa hiyo ambapo vijana wawili wa mtaani hapo waliofahamika kwa majina ya Haidani na Kulwa walihofia yangeweza kutokea machafuko zaidi wakakimbilia kwa mjumbe wa eneo hilo aliyefahamika kwa jina la Shukuru lakini walimkuta mke wa mjumbe ambaye aliwaambia mumewe alikuwa kazini.
Mke(Bi Mwajuma Mtata) akijaribu kuzuia kupigwa picha na kamera za wanahabari. WARUDI NYUMBANI
Wapenzi hao baada ya kugaragazana vya kutosha ikiwa ni pamoja na kuvuana nguo, mwanaume alianza kumburuza mkewe na kurudi nyumbani kwao ambapo walipofika eneo la Kwamkoma walianza kutifuana tena kabla ya kuamuliwa na wasamaria wema.
Jirani akihoji kulikoni mpaka iwe hivi... ETI WAMEYAMALIZA!
Taarifa tulizozipata wakati gazeti hili lilipokuwa linakwenda mitamboni juzi, Jumatano, wawili hao walikuwa tayari wameshayamaliza na wanaishi raha mustarehe baada ya kuombana msamaha.

Thursday, October 2, 2014

MABOMU YA MACHOZI YAENDELEA KUCHUKUA NAFASI YAKE RUNGWE


Wananchi wa    kata    ya lwangwa   Halmashauri  ya  Busokelo wilayani  Rungwe mkoani Mbeya  wameandamana   kuanzia     leo  asubuhi   hadi  katika ofisi za Halmashauri  hiyo    wakishiniza  serikali  wilayani  humo   kuwatoa  watu  walio kamatwa   baada  ya kuhusiwa kuhusika  na kifo cha  Gabriel Mwandemwa  mwenye  umri wa mika  {40} aliye  uwawa na  wananchi   katika  siku za   hivi karibuni kutokana na imani za  kishirikina.
 Wakizungumza  na   yetu rungwe  blog   wakati  wa  mandamano hayo  wanachi  hao   walisema hatua  hiyo ilikuja  kufuatia   jeshi  la polisi wilayani  humo  kuwakamata   baadhi ya wananchi   kwa madai ya  kuhusika na kifo  cha kijana  huyo  aliyefariki dunia siku za hivi karibuni  kutokana  na    vitendo vya  ushirikina. 
 
 Walisema  mnamo majila ya   usiku  wa kuamkia  oktoba   moja  jeshi la polisi  liliwasili kinyemela katika  maeneo hayo  kwa  kuwakamata  baadhi ya  wananchi    bila kushirisha  uongozi wa  maeneo husika   kwa  kufikishwa  kituoni,  ambapo kutokana na hali  hiyo   iliweza kupelekea  wao kama  wanachi kuchukua  hatua  ya  kupinga   kitendo hicho   kwa  kuungana  kwa  pamoja   na kufanya maadamano ya amani  hadi katika  ofisi  ya mkurugezi  wa Halmashauri hiyo  wakitaka kutolewa  kwa ndugu  zao.
   Hata  hivyo jeshi la  polisi liliwasili  eneo  la  tukio   na kisha kunza  kusaidia kuzuia    gasia  hizo   ikiwa  ni pamoja  na kuwatia  hatiani wale  wote ambao walionekana kuanzisha vurugu hizo.
   Diwani wa kata  hiyo Robati Mwaibata alikili kuwapo kwa  adha hiyo  na kusema  mpaka sasa wameshindwa  kuongea  na wananchi wake  kutokana na  vurugu kuendelea kuchukua nafasi  yake.
Alisema    chanzo   cha  tukio hilo ni  baada  ya jeshi la polisi  kuwakamata  baadhi ya  vijana wa  eneo hilo  kwa  tuhuma  za  kuhusika  na  mauji  ya    Gabriel Mwandemwa aliye fariki dunia siku za  hivi karibuni kwa   kukatwa na  mapanga na kisha mwili wake  kuchomwa moto.
 Alisema mpaka sasa wanaendelea  kutuliza gasia  hizo kwa  ushirikiana na jeshi la  polisi  wilayani humo .
 Hata  hivyo     juhudi na malfa za kutafuta mkuu wa wilaya ya rungwe krspini meela ziligonga mwamba   mara  baada  ya    simu yake  kuita bila kupokelewa.
 Siku  za  hivi  karibuni    wananchi wa  kijiji  cha Ikama  Mbande  walimkamata  Gabliel   Mwaibata  walimkamata kwa  kumwachia  kipigo na kisha   kumchoma moto baada ya  kudaiwa  kujihusisha  na vitendo  vya  kishjirikina.

KIJANA AFUMWA GESTI NA MKE WA KIGOGO


Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Marck Costantine (24), mkazi wa mtaa wa Kitangiri jijini Mwanza amenaswa ‘live’ gesti akiwa na mke wa kigogo mmoja (jina kapuni), aitwaye Mwanaidi wakijiandaa kuvunja amri ya sita.

Tukio hilo lilijiri Septemba 18, mwaka huu kwenye gesti moja maarufu iliyoko mitaa ya Kitangiri baada ya kigogo huyo kupewa ‘ubuyu’ kwamba anaibiwa mali yake ndipo akaandaa mtego na kufanikiwa kumnasa kijana huyo alipokutwa kwenye chumba namba 4 cha gesti hiyo akijiandaa kuserebuka.
Akisaini  kulipishwa faini
“Kigogo alipopewa mchoro huo na wambea, siku ya tukio alimshtua Mwenyekiti wa Mtaa wa Kitangiri, Maginga Patroba, wakatia timu katika gesti hiyo, wakawakuta wachepukaji hao wakiwa kitandani huku Marck akiwa tayari ameshachojoa nguo, Mwanaidi akiwa bado,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:

“Kigogo aliamuru wahudumu wagonge mlango ili wahusika wasishtuke, walipofungua ndipo mwenyekiti sabamba na kigogo huyo wakazama ndani.”

Mwanaidi alipoona flashi za kamera ya wanahabari zikiwamulika, alianza kuangua kilio mbele ya mumewe kumuomba awasamehe lakini kigogo huyo alimtaka kijana huyo amlipe fidia ya shilingi milioni moja kama adhabu ya kutembea na mke wake.
 
Kutokana na hali ya uchumi ya kijana huyo kutokuwa nzuri, hakuweza kulipa kiasi hicho cha pesa badala yake aliomba kupewa muda wa kulipa pesa hizo.
 
Chini ya uangalizi wa mwenyekiti, Marck aliandika barua ya makubaliano jinsi ya kulipwa kwa kiasi hicho cha pesa kwa kigogo huyo na iwe kama fundisho kwake kuachana na tabia za kutembea na wake za watu.
 
Kwa upande mwingine, mwenyekiti Patroba alikiri kumfahamu Marck na kudai ni kijana wa mtaani kwake na kumuonya asirudie mchezo huo mchafu.
“Namfahamu huyu kijana nimeshangazwa na kitendo hiki anachokifanya kwani ni vitendo ambavyo havikubaliki katika jamii hivyo kama kiongozi wa mtaa huu nitaendelea kutoa ushirikiano ili kuukomesha tabia kama hizi za kuvunja miji ya watu,’’ alisema Patroba.

KATIBU MWENEZI (BAWACHA) KAWE AJIUNGA NA ACT


index
Mbunge wa Kawe Mh. Halima Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa BAWACHA taifa.
Kipimo Abdallah
ALIYEKUWA Katibu Mwenezi wa Baraza la Wanawake Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) Jimbo la Kawe, Batuli Kivuma ambaye amejiunga na chama cha Alliance for Change and Transparent (ACT-Tanzania amesema kilichomuondoa CHADEMA ni ukabila ulioota mizizi kwa muda mrefu.
Kivuma ambaye awali alikuwa mwanachama wa Chama Cha Wananchi CUF alisema aliamini kuwa chama hicho kinasimamia demokrasia jambo ambalo limeshindikana hasa ukiwa hotekei mkoa wa Kilimanjaro.
Alisema tangu ajiunge katika chama hicho amekuwa na juhudi za kukijenga chama hasa Kata ya Msasani na jimbo zima la Kawe ila juhudi zake zimekuwa zikikwamishwa kwa misingi ya ukabila.
Katibu Mwenezi huyo wa zamani wa BAWACHA alisema katika kudhihirisha hilo alishiriki kwenye  mchakato wa kugombea nafasi ya Udiwani viti maalum mwaka 2010 ambapo alishinda ila aliondolewa kwa kigezo cha yeye ni Mdigo na wakapewa nafasi hiyo Wachaga.
“Kusema ukweli suala la kuhama vyama sio zuri ila inafikia mahali unashindwa kuvumilia kwani nimekuwa nikionewa mara kwa mara katika chaguzi na ukiangalia vizuri msingi wake ni ukabilia ambao unawabeba Wachaga” , alisema.
Kivuma  alisema alikuwa akikipenda sana chama hicho lakini ubaguzi uliopo amefikia mwisho wa uvumilivu na kwamba anahitaji kuonyesha jitihada zake kwingine.
Alisema suala hilo la ukabila lilikidhiri katika uchaguzi mkuu ambao ulifanyika hivi karibuni hasa katika upande wa BAWACHA ambapo juhudi zilifanywa kuanzia ngazi ya chini hadi Taifa.
Mwenezi huyo wa zamani wa BAWACHA alisema hata upatikanaji wa Mwenyekiti wa BAWACHA wa sasa Halima Mdee ulitawaliwa na ukabila ikiwa ni agizo la Mwenyekiti Taifa Freeman Mbowe.
“Unajua hili neno demokrasia wanalielewa je bwana kwani kwa ufahamu wangu ni kuhakikisha kuwa jamii inaacha pale inapofanya maamuzi yake ila huku ni kinyume”, aliongezea Kivuma.
Kivuma alisema atahakikisha kuwa anakibomoa CHADEMA hasa katika Jimbo la Kawe ambapo amefanya kazi za kisiasa kwa muda mrefu.
Kwa upande wake aliyekuwa Mjumbe wa Mtaa Serikali ya Mtaa wa Matofalini Ujiji Kigoma Yassin Mohamed alisema ni vema vyama vikatambua kuwa hakuna uadui baina yao na kuhama chama ni haki ya mtu.
Alitolea mfano hali ya kisiasa ilivyokuwa siku za nyuma kati ya chama na CHADEMA na CUF hali ambayo kwa sasa haipo na vinafanya kazi pamoja.
Mohamed alisema ameamua kujiunga na ACT-Tanzania na kuondoka CHADEMA ili kupata uhuru wa kupigania demokrasia ya kweli.

BARUA YA SITTA KUMJULISHA WAZIRI MKUU WAKUTANE HARAKA OFISINI KWAKE MAMBO MAGUMU NI BAADA YA MWANASHERIA WA Z’BAR KUPIGA KURA YA HAPANA ,YAVUJA

By3oIKGIcAAeU2u
Hali ya Mwenyekiti wa Bunge lakatiba Samuel Sitta na gangi lake imekua ngumu mno baada ya Mwanasheria mkuu wa Zanzibar kupigilia msumari wa kura ya wazi ya kukataa.

Hali hii imemtia kiwewe Samuel Sitta na Wana Mapinduzi wa Rasimu ya katiba kuhaha na kuona sasa hali imekua ngumu na kusaka mbinu nyingine.

Sitta adiriki kumuandikia kiji notice Waziri mkuu Mizengo Pinda kumtaka ofisini kwake mara moja baada tu, ya Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar kupiga kura ya hapana.

CHIPSI NI NOMA APEWA KIPIGO NA APOZWA NA CHIPSI

 



 
mwanakaka akienjoy chipsi baada ya kupewa kipigo