Friday, October 3, 2014
WABUNGE WALIVYOJIACHIA JANA BUNGENI
MKE, MUME WAVUANA NGUO WAKIZICHAPA HADHARANI
Hii ni
aibu kubwa! Njemba mmoja aliyefahamika kwa jina la Zeno na mkewe Mwajuma
Mtata, wakazi wa mtaa Mrefu, Kigogo-Luhanga jijini Dar wamenaswa
wakiangusha bonge la timbwili barabarani na kusababisha umati wa watu
kujikusanya eneo hilo kujionea ‘sinema’ ya bure.Timbwili zito likianza
kati ya njemba mmoja anayefahamika kwa jina la Zeno na mkewe Mwajuma
Mtata. Tukio hilo lililofananishwa na muvi ya kivita lilitokea usiku wa
Jumanne iliyopita ambapo chanzo kimedaiwa kuwa ni mwanamke huyo
kutelekeza jikoni kitoweo cha maini ya mbuzi na kwenda baa kupata
kilaji.
Kwa mujibu wa chanzo makini, siku ya tukio, Zeno alirudi nyumbani
mida ya jioni mkononi akiwa na kifurushi chenye maini ya mbuzi pamoja na
mazagazaga mengine zikiwemo ndimu, tangawizi, pilipili hoho, nyanya na
vitunguu kupokelewa na ‘mai waifu’ wake huyo.
MUME ATOKA KIDOGO
Baada ya Zeno kumkabidhi mkewe mazagazaga hayo kwa ajili ya mlo wa
usiku, alimuaga mkewe kuwa anakwenda kutembea ili akirudi akute msosi
uko tayari, wale, walale.
“Dakika kadhaa baada ya mumewe kutoka, nasikia bibie naye alichomoka na kwenda baa ya jirani ‘kusukutua mdomo’.
“Alipokaa sawa alibaini kuwa maini aliyoleta yalikuwa yameungua na
kuwa kama mkaa hali iliyompandisha hasira na kuanza kumsaka mkewe,”
kilidai chanzo hicho.
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwamba, Zeno akiwa katika
sakasaka yake ndipo alipombamba mkewe kwenye baa hiyo akimalizia
‘kunyonya’ kilevi kikali. ZACHAPWA
Bila kuuliza, Zeno alimkunja mkewe na kumtoa nje huku akimpa makofi
ndipo Mwajuma akaona kama anaonewa hivyo akamvizia mumewe na kumchota
mtama ambapo wote walikwenda chini kutokana na kuwa katika hali ya
kuzidiwa na kilaji.
Timbwili hilo liliendelea nje ya baa hiyo ambapo vijana wawili wa
mtaani hapo waliofahamika kwa majina ya Haidani na Kulwa walihofia
yangeweza kutokea machafuko zaidi wakakimbilia kwa mjumbe wa eneo hilo
aliyefahamika kwa jina la Shukuru lakini walimkuta mke wa mjumbe ambaye
aliwaambia mumewe alikuwa kazini.
Wapenzi hao baada ya kugaragazana vya kutosha ikiwa ni pamoja na
kuvuana nguo, mwanaume alianza kumburuza mkewe na kurudi nyumbani kwao
ambapo walipofika eneo la Kwamkoma walianza kutifuana tena kabla ya
kuamuliwa na wasamaria wema.
Taarifa tulizozipata wakati gazeti hili lilipokuwa linakwenda
mitamboni juzi, Jumatano, wawili hao walikuwa tayari wameshayamaliza na
wanaishi raha mustarehe baada ya kuombana msamaha.
Thursday, October 2, 2014
MABOMU YA MACHOZI YAENDELEA KUCHUKUA NAFASI YAKE RUNGWE
Wananchi wa
kata ya lwangwa Halmashauri
ya Busokelo wilayani Rungwe mkoani Mbeya wameandamana
kuanzia leo asubuhi
hadi katika ofisi za Halmashauri hiyo
wakishiniza serikali wilayani
humo kuwatoa watu
walio kamatwa baada ya kuhusiwa kuhusika na kifo cha
Gabriel Mwandemwa mwenye umri wa mika
{40} aliye uwawa na wananchi
katika siku za hivi karibuni kutokana na imani za kishirikina.
Wakizungumza
na yetu rungwe blog wakati
wa mandamano hayo wanachi
hao walisema hatua hiyo ilikuja
kufuatia jeshi la polisi wilayani humo
kuwakamata baadhi ya wananchi kwa madai ya
kuhusika na kifo cha kijana huyo
aliyefariki dunia siku za hivi karibuni
kutokana na vitendo vya
ushirikina.
Walisema
mnamo majila ya usiku wa kuamkia oktoba
moja jeshi la polisi liliwasili kinyemela katika maeneo hayo
kwa kuwakamata baadhi ya
wananchi bila kushirisha uongozi wa
maeneo husika kwa kufikishwa
kituoni, ambapo kutokana na
hali hiyo iliweza kupelekea wao kama
wanachi kuchukua hatua ya
kupinga kitendo hicho kwa
kuungana kwa pamoja
na kufanya maadamano ya amani
hadi katika ofisi ya mkurugezi
wa Halmashauri hiyo wakitaka
kutolewa kwa ndugu zao.
Hata
hivyo jeshi la polisi
liliwasili eneo la
tukio na kisha kunza kusaidia kuzuia gasia
hizo ikiwa ni pamoja
na kuwatia hatiani wale wote ambao walionekana kuanzisha vurugu hizo.
Diwani wa kata hiyo Robati Mwaibata alikili kuwapo kwa adha hiyo
na kusema mpaka sasa
wameshindwa kuongea na wananchi wake kutokana na
vurugu kuendelea kuchukua nafasi
yake.
Alisema chanzo
cha tukio hilo ni
baada ya jeshi la polisi kuwakamata
baadhi ya vijana wa eneo hilo
kwa tuhuma za
kuhusika na mauji
ya Gabriel Mwandemwa aliye
fariki dunia siku za hivi karibuni
kwa kukatwa na mapanga na kisha mwili wake kuchomwa moto.
Alisema mpaka sasa wanaendelea kutuliza gasia hizo kwa
ushirikiana na jeshi la polisi wilayani humo .
Hata
hivyo juhudi na malfa za
kutafuta mkuu wa wilaya ya rungwe krspini meela ziligonga mwamba mara
baada ya simu yake
kuita bila kupokelewa.
Siku
za hivi karibuni
wananchi wa kijiji cha Ikama
Mbande walimkamata Gabliel
Mwaibata walimkamata kwa kumwachia
kipigo na kisha kumchoma moto
baada ya kudaiwa kujihusisha
na vitendo vya kishjirikina.
KIJANA AFUMWA GESTI NA MKE WA KIGOGO
Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Marck Costantine (24), mkazi wa mtaa wa Kitangiri jijini Mwanza amenaswa ‘live’ gesti akiwa na mke wa kigogo mmoja (jina kapuni), aitwaye Mwanaidi wakijiandaa kuvunja amri ya sita.
Tukio hilo lilijiri Septemba 18, mwaka huu kwenye gesti moja maarufu
iliyoko mitaa ya Kitangiri baada ya kigogo huyo kupewa ‘ubuyu’ kwamba
anaibiwa mali yake ndipo akaandaa mtego na kufanikiwa kumnasa kijana
huyo alipokutwa kwenye chumba namba 4 cha gesti hiyo akijiandaa
kuserebuka.
“Kigogo alipopewa mchoro huo na wambea, siku ya tukio alimshtua Mwenyekiti wa Mtaa wa Kitangiri, Maginga Patroba, wakatia timu katika gesti hiyo, wakawakuta wachepukaji hao wakiwa kitandani huku Marck akiwa tayari ameshachojoa nguo, Mwanaidi akiwa bado,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Kigogo aliamuru wahudumu wagonge mlango ili wahusika wasishtuke,
walipofungua ndipo mwenyekiti sabamba na kigogo huyo wakazama ndani.”
Mwanaidi alipoona flashi za kamera ya wanahabari zikiwamulika, alianza kuangua kilio mbele ya mumewe kumuomba awasamehe lakini kigogo huyo alimtaka kijana huyo amlipe fidia ya shilingi milioni moja kama adhabu ya kutembea na mke wake.
Mwanaidi alipoona flashi za kamera ya wanahabari zikiwamulika, alianza kuangua kilio mbele ya mumewe kumuomba awasamehe lakini kigogo huyo alimtaka kijana huyo amlipe fidia ya shilingi milioni moja kama adhabu ya kutembea na mke wake.
Kutokana na hali ya uchumi ya kijana huyo
kutokuwa nzuri, hakuweza kulipa kiasi hicho cha pesa badala yake
aliomba kupewa muda wa kulipa pesa hizo.
Chini ya uangalizi wa mwenyekiti, Marck aliandika barua ya
makubaliano jinsi ya kulipwa kwa kiasi hicho cha pesa kwa kigogo huyo na
iwe kama fundisho kwake kuachana na tabia za kutembea na wake za watu.
Kwa upande mwingine, mwenyekiti Patroba alikiri kumfahamu Marck na
kudai ni kijana wa mtaani kwake na kumuonya asirudie mchezo huo mchafu.
“Namfahamu huyu kijana nimeshangazwa na kitendo hiki anachokifanya
kwani ni vitendo ambavyo havikubaliki katika jamii hivyo kama kiongozi
wa mtaa huu nitaendelea kutoa ushirikiano ili kuukomesha tabia kama hizi
za kuvunja miji ya watu,’’ alisema Patroba.
KATIBU MWENEZI (BAWACHA) KAWE AJIUNGA NA ACT
Mbunge wa Kawe Mh. Halima Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa BAWACHA taifa.
Kipimo Abdallah
ALIYEKUWA
Katibu Mwenezi wa Baraza la Wanawake Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
(BAWACHA) Jimbo la Kawe, Batuli Kivuma ambaye amejiunga na chama cha
Alliance for Change and Transparent (ACT-Tanzania amesema kilichomuondoa
CHADEMA ni ukabila ulioota mizizi kwa muda mrefu.
Kivuma
ambaye awali alikuwa mwanachama wa Chama Cha Wananchi CUF alisema
aliamini kuwa chama hicho kinasimamia demokrasia jambo ambalo
limeshindikana hasa ukiwa hotekei mkoa wa Kilimanjaro.
Alisema
tangu ajiunge katika chama hicho amekuwa na juhudi za kukijenga chama
hasa Kata ya Msasani na jimbo zima la Kawe ila juhudi zake zimekuwa
zikikwamishwa kwa misingi ya ukabila.
Katibu
Mwenezi huyo wa zamani wa BAWACHA alisema katika kudhihirisha hilo
alishiriki kwenye mchakato wa kugombea nafasi ya Udiwani viti maalum
mwaka 2010 ambapo alishinda ila aliondolewa kwa kigezo cha yeye ni Mdigo
na wakapewa nafasi hiyo Wachaga.
“Kusema
ukweli suala la kuhama vyama sio zuri ila inafikia mahali unashindwa
kuvumilia kwani nimekuwa nikionewa mara kwa mara katika chaguzi na
ukiangalia vizuri msingi wake ni ukabilia ambao unawabeba Wachaga” ,
alisema.
Kivuma
alisema alikuwa akikipenda sana chama hicho lakini ubaguzi uliopo
amefikia mwisho wa uvumilivu na kwamba anahitaji kuonyesha jitihada zake
kwingine.
Alisema
suala hilo la ukabila lilikidhiri katika uchaguzi mkuu ambao ulifanyika
hivi karibuni hasa katika upande wa BAWACHA ambapo juhudi zilifanywa
kuanzia ngazi ya chini hadi Taifa.
Mwenezi
huyo wa zamani wa BAWACHA alisema hata upatikanaji wa Mwenyekiti wa
BAWACHA wa sasa Halima Mdee ulitawaliwa na ukabila ikiwa ni agizo la
Mwenyekiti Taifa Freeman Mbowe.
“Unajua
hili neno demokrasia wanalielewa je bwana kwani kwa ufahamu wangu ni
kuhakikisha kuwa jamii inaacha pale inapofanya maamuzi yake ila huku ni
kinyume”, aliongezea Kivuma.
Kivuma alisema atahakikisha kuwa anakibomoa CHADEMA hasa katika Jimbo la Kawe ambapo amefanya kazi za kisiasa kwa muda mrefu.
Kwa
upande wake aliyekuwa Mjumbe wa Mtaa Serikali ya Mtaa wa Matofalini
Ujiji Kigoma Yassin Mohamed alisema ni vema vyama vikatambua kuwa hakuna
uadui baina yao na kuhama chama ni haki ya mtu.
Alitolea
mfano hali ya kisiasa ilivyokuwa siku za nyuma kati ya chama na CHADEMA
na CUF hali ambayo kwa sasa haipo na vinafanya kazi pamoja.
Mohamed alisema ameamua kujiunga na ACT-Tanzania na kuondoka CHADEMA ili kupata uhuru wa kupigania demokrasia ya kweli.
BARUA YA SITTA KUMJULISHA WAZIRI MKUU WAKUTANE HARAKA OFISINI KWAKE MAMBO MAGUMU NI BAADA YA MWANASHERIA WA Z’BAR KUPIGA KURA YA HAPANA ,YAVUJA
Hali ya Mwenyekiti wa Bunge lakatiba Samuel Sitta na gangi lake imekua ngumu mno baada ya Mwanasheria mkuu wa Zanzibar kupigilia msumari wa kura ya wazi ya kukataa.
Hali hii imemtia kiwewe Samuel Sitta na Wana Mapinduzi wa Rasimu ya katiba kuhaha na kuona sasa hali imekua ngumu na kusaka mbinu nyingine.
Sitta adiriki kumuandikia kiji notice Waziri mkuu Mizengo Pinda kumtaka ofisini kwake mara moja baada tu, ya Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar kupiga kura ya hapana.
Subscribe to:
Posts (Atom)






