Wednesday, December 3, 2014
ZITTO AMTAMBULISHA MCHUMBA WAKE
Tuesday, December 2, 2014
BASI LAACHA NJIA NA KUTUMBUKIA KORONGONI MLIMA KITONGA
Basi
liitwalo Easy Bus lenye namba za usajili T 298 BLZ lililokuwa likitokea
Lilongwe Malawi likiwa katika mtaro wa Mlima Kitonga.


Foleni
kubwa iliyosababishwa na basi hilo baada ya kuingia mtaroni na kuziba
njia. Basi la abiria lenye namba za usajili T 298 BLZ likiwa linatolewa
katika mtaro wa Mlima Kitonga mapema leo baada ya kutumbukia. Hali hii
imesababisha foleni kubwa kwa magari huku mengine yakishindwa kuendelea
na safari zake. Kwa mujibu wa mashuhuda, chanzo cha gari hilo
kutumbukia mtaroni ni kufuatia kupata hitilafu na hatimaye uamuzi wa
kuliegesha kando ukafanyika kisha abiria wote wakashuka ili kusubiri
marekebisho hayo.
Haikupita
muda mrefu baada ya abiria kushuka gari lilikosa balansi, likaanza
kurudi kinyumenyume na kisha kuingia mtaroni. Hakuna mtu aliyefariki
dunia wala kujeruhiwa katika ajali hiyo.
RAIS KIKWETE AMWAPISHA CAG MPYA, PROF MUSA JUMA ASSAD IKULU JIJINI DAR
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali (CAG), Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam
Novemba 02, 2014.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akitia sahihi yake kwenye nyaraka baada ya
kumuapisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa
Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad nyaraka baada ya kumuapisha
Ikulu jijini Dar es salaa Novemba 02, 2014.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akimuangalia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad akiweka sahihi yake kwenye
nyaraka baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad na CAG Mstaafu Bw. Ludovick Utouh
Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 02, 2014.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali, Waziri
Mkuu Mhe Mizengo Pinda, Jaji Mkuu Mhe Mohamed Chande Othman, Spika Anne
makinda na Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es
salaam leo Novemba 02, 2014.

Rais
Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad na wafanyakazi
wa ofisi ya CAG Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na familia ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es
salaam Novemba 02, 2014.
(PICHA NA IKULU)
MZEE MSUYA AWASIHI WAKULIMU KUTOOGOPA NENO BIOTEKNOLOJIA
Kutokana na kuwepo kwa maneno
yanayowatishia na kuwakatisha tamaa wakulima kuwa mbegu za kisasa ni mbegu za
kibioteknolojia na hazifai kwa matumizi ya binadamuu, mzee Msuya amewasihi
wakulima kuwabeza watu hao na maneno yao na kutoliogopa neno bioteknolojia
kwani hilo ni neno la kisayansi ambalo halibadirishi uasili wa mmea wa aina
yoyote ile.
Aliyasema hayo baada ya kuwepo kwa
baadhi ya watu kumfuata na kumuuliza siri ya mafanikio yake katika kilimo na
anapowaambia kuhusu mbegu za kibioteknolojia huingiwa na mshangao na kuogopa
neno hilo
Mzee msuya ni miongoni mwa wazee
maarufu katika wilaya ya Vunjo kutokana na juhudi zake katika kilimo na ndio
wazee wenye pesa mjini hapo.
mzee huyo ambaye alisema siri ya
mafanikio yake aliipata baada ya kukubali kung'oa miche yake ya zamani ya
kahawa na kupanda miche mipya aliyoinunua katika taasisi ya utafiti wa kahawa
ya TaCRI baada ya kupata ushauri kutoka kwa mtaalamu wa kilimo wa taasisi hiyo.
"mtafiti alinishauri nitoe miche ya kahawa yote iliyokuwapo shambani na kunpambia nikanunue miche mipya ya TaCRI
kwani ni miche isiyokuwa na maambukizi ya magonjwa yanayosumbua zao la kahawa
sikuamini lakini baadaye nikakubali na nikafanya kama nilivyaambiwa na sasa
naitwa mchawi hapa kijijini kutokana na mazao ninayoyapata.
wanawake wakimsaidia mzee msuta kuchambua mahindi nyumbani kwake
Mzee huyo ambaye sasa amekuwa mwalimu wa wakulima wenzake alisema kuwa Tanzania kama nchi nyingine haiwezi kukwepa maendeleo ya bioteknolojia kutokana na utandawazi na maendeleo ambayo yapo duniani kote, kwa kuwa bioteknolojia ni nyenzo muhimu katika kuboresha kilimo, uzalishaji viwandani, kwenye afya, hifadhi ya mazingira pia kukuza uchumi nchini
mzee huyo ambaye alisema alikuwa anapata kilo 250 mpaka 1500 kwa msimu lakini tangu miche mipya ianze kuzaa matunda napata kilo 5000 mpaka 8000 kwa msimu na kwa ukubwa ule ule wa shamba. kitu ambacho akiwaeleza wenzie wanashangaa sana na kutoamini anachowaeleza.
Akifafanua kuhusu neno bioteknolojia alisema kwa madaha kuwa ni "taaluma ya kutumia michakato ya kibaolojia katika viumbe hai ili kupata mahitaji na huduma kwa maendeleo na maisha bora ya binadamu"
Msuya ambaye alisema hata sahau jinsi majirani zake walipomcheka na mumuita mpumbavu pale alipoamua kung'oa na kupanda miche mipya. Hata hivyo hakukatishwa tamaa na maneno yake bali alizingatia sana mafundisho aliyoyapata na kuyatendea kazi mpaka alipo fanikiwa na kubadirika kuwa mwalimu wa wengine
"Hivi sasa mimi nafuatwa na wakulima ili niwafundishe mbinu ninazotumia, lakini wengi wanashangaa ninapowaambia kuhusu mbegu mpya na utunzaji wa shamba vizuri wanaofuata ninayowaambia wanaona matunda yake.
shamba la kahawa la mzee msuya likiwa limechanganywa na zao la migomba
Mzee huyo alisema kuwa anajivunia sana elimu aliyoipata kutoka kwa watafiti kwani wamemfanya kutoka kwenye kilimo cha kutafuta chakula pekee na kuwa mkulima mfanyabiashara kwani mazao anayoyapata kwa sasa yanakidhi mahitaji yake ya chakula na kupata kiasi kikubwa kwa ajili ya kuyauza kwenye makampuni makubwa hapa nchini.
"TaCRI imeniondolea umaskini kwani walinifundisha elimu ya kutumia mbegu bora kwa kila zao ninalotaka kulima pamoja na matumizi ya samadi ya wanyama nilionao nyumbani hivyo kwamgu mimi kila kitu ni faida kwani mashamba yanategemea mifigo kwa mbolea wakati mifugo inategemea kilimo kwa chakula".
Hata hivyo aliwasii watafiti wote nchini kuwasaidia wakulima ili wapate elimu kuhusu matumizi ya mbegu bora ili kumkomboa mkulima kwani wakulima wengi wanadanganya na propaganda zinazoletwa na wafanyabiashara wengine wa bidhaa zao wakidai kuwa matumizi ya mbegu hizo si salama wakati ni uvumi usio wa kweli kabisa.
TaCRI ni taasisi ya utafiti wa kahawa nchini Tanzania na inafanya kazi kwa msaada wa nchi za ulaya, hufanya uzalishaji kwa njia ya Tissue Culture ( uzalishaji kwa njia ya chupa) na kuzalisha kwa kutumia vikonya (kupachika mche mmoja juu ya mche mwingine).
Taasisi ya Utafiti wa
Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi
2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara
za arabika pamoja na ile ya Robusta
Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa
katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina
za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata
zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya
majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa
Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Taasisi ya Utafiti wa
Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi
2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara
za arabika pamoja na ile ya Robusta
Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa
katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina
za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata
zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya
majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa
Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za
uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya
zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho
kinasababisa hasara kwa mkulima
Pia TaCRI imetoa teknolojia za kuongeza tija na ubora wa kahawa aina
mbili zinazotekelezeka za kuzalisha miche mipya bora ya aina hizi
chotara ikiwa nipamoja na kutumia vikonyo, kupachika aina mpya juu ya
mibuni ya zamani na kuzalisha kitaalamu miche kwa kutumia chupa
ikifahamika kwa lugha ya kingereza ’Tissue culture au Somatic
embryogenisis.’
Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Taasisi ya Utafiti wa
Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi
2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara
za arabika pamoja na ile ya Robusta
Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa
katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina
za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata
zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya
majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa
Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za
uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya
zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho
kinasababisa hasara kwa mkulima
Pia TaCRI imetoa teknolojia za kuongeza tija na ubora wa kahawa aina
mbili zinazotekelezeka za kuzalisha miche mipya bora ya aina hizi
chotara ikiwa nipamoja na kutumia vikonyo, kupachika aina mpya juu ya
mibuni ya zamani na kuzalisha kitaalamu miche kwa kutumia chupa
ikifahamika kwa lugha ya kingereza ’Tissue culture au Somatic
embryogenisis.’
Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Taasisi ya Utafiti wa
Kahawa Tanzania (TaCRI) iliyopo mkoani Kilimanjaro ilianza kazi rasmi
2001 na imepata mafanikio makubwa katika utafiti wa mbegu mpya chotara
za arabika pamoja na ile ya Robusta
Aina hizi za miche bora chotara za kahawa zimekuwa ni mkombozi mkubwa
katika sekta ya kahawa kwa kuwa zina tija ya hali ya juu zaidi ya aina
za zamani pia zina muonjo wa hali ya juu kama aina za zamani na hata
zaidi, na zina ukinzani na magojwa hatari ya chulebuni (CBD), kutu ya
majani (CLR) na mnyauko fuzari (CWD), (CBD) kutegemea aina ya kahawa
Kutokana na sifa hizo, aina hizo mpya zinampunguzia mkulima gharama za
uzalishaji, kati ya asilimia 50 na hata ukilinganisha na miche mingi ya
zamani ambayo mingi imezeeka na kushambuliwa na magojwa kitu ambacho
kinasababisa hasara kwa mkulima
Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Make Money at : http://bit.ly/copy_win
MCH: RWAKATARE AFIKISHWA POLISI KWA UHARIBIFU WA MALI
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mikocheni B Assemblies of God jijini Dar, Dk.
Getrude Rwakatare (pichani) amefunguliwa mashitaka katika Kituo cha
Polisi Wazo Hill kwa uharibifu wa mali inayodaiwa ina thamani ya
shilingi milioni 20.
Taarifa zilizopatikana katika kituo hicho zenye Jalada la Kumbukumbu WH/RB/9029/2014 UHARIBIFU WA MALI na kuthibitishwa na mlalamikaji aliyejitambulisha kwa jina la Grayson Justine, zinaeleza mchungaji huyo alivunja nyumba ya Grayson kwa greda hali iliyomfanya mmiliki huyo kuzimia na kulazwa Zahanati ya Mico iliyopo Wazo Hill baada ya presha kupanda.
Katika mahojiano na waandishi wetu katika Ofisi za Global Publishers, Bamaga- Mwenge, Dar wiki iliyopita, Grayson alikuwa na haya ya kusema:
“Kiwanja nilichojengea nyumba nilikinunua kwa Jumanne Rajab, Agosti 24, 2011 na makubaliano yalifanyika kwa kuandikishiana Ofisi za Serikali ya Mtaa wa Bunju ‘B’ na kila mmoja alikuwa na mashahidi wake.
“Kutokana na kuchoka katika kupangisha, niliamua kuchukua mkopo wa shilingi milioni 20 kazini ili nijenge haraka na kuhamia, ujenzi ulianza Septemba 21, mwaka 2013 mpaka kufikia mwezi huu (Novemba) nilibakiza kupaua na nilitarajia kuhamia mwanzoni mwa mwaka kesho.
“Baadaye nilikwenda Moshi kwenye msiba wa baba, niliporudi Dar nilimaliza siku moja tu, nikaripoti kazini. Nikiwa kazini Novemba 11, mwaka huu nikapigiwa simu na jirani kwamba nyumba yangu inabomolewa na greda, alifikiri kwamba nimeshaonana na Mchungaji Rwakatare na kukubaliana naye.
“Nilikwenda kule, kufika nikakuta hakuna jengo! Nilidondoka chini, sikujua kilichoendelea, nilipoteza fahamu, nilijitambua nikiwa Zahanati ya Mico.
Mwandishi alifika katika eneo la tukio na kushuhudia kifusi kinachodaiwa kuwa ni iliyokuwa nyumba ya Grayson iliyovunjwa na imezungushiwa ukuta na geti kupigwa kufuli.
Mchungaji Rwakatare alipopigiwa simu kuhusiana na madai hayo alisema yupo bungeni hivyo alimwagiza msaidizi wake, Jerad Abeid kuzungumzia sakata hilo ambapo alisema eneo hilo mchungaji analimiliki tangu mwaka 2005 na hati ziko ardhi Wilaya ya Kinondoni. Alibomoa nyumba ya Grayson akijua ni eneo lake la siku nyingi.
“Unajua katika maeneo hayo kuna watu walikuwa wakishirikiana na ofisi za mtaa kuuza kiwanja cha mchungaji kwa siri na tayari watu wanne walishauziwa lakini walikuwa hawajajenga, mchungaji aliamua kuwapoza kiubinadamu na wameshaondoka bado watu wawili akiwemo huyo Grayson,” alisema Jerad.
Taarifa zilizopatikana katika kituo hicho zenye Jalada la Kumbukumbu WH/RB/9029/2014 UHARIBIFU WA MALI na kuthibitishwa na mlalamikaji aliyejitambulisha kwa jina la Grayson Justine, zinaeleza mchungaji huyo alivunja nyumba ya Grayson kwa greda hali iliyomfanya mmiliki huyo kuzimia na kulazwa Zahanati ya Mico iliyopo Wazo Hill baada ya presha kupanda.
Katika mahojiano na waandishi wetu katika Ofisi za Global Publishers, Bamaga- Mwenge, Dar wiki iliyopita, Grayson alikuwa na haya ya kusema:
“Kiwanja nilichojengea nyumba nilikinunua kwa Jumanne Rajab, Agosti 24, 2011 na makubaliano yalifanyika kwa kuandikishiana Ofisi za Serikali ya Mtaa wa Bunju ‘B’ na kila mmoja alikuwa na mashahidi wake.
“Kutokana na kuchoka katika kupangisha, niliamua kuchukua mkopo wa shilingi milioni 20 kazini ili nijenge haraka na kuhamia, ujenzi ulianza Septemba 21, mwaka 2013 mpaka kufikia mwezi huu (Novemba) nilibakiza kupaua na nilitarajia kuhamia mwanzoni mwa mwaka kesho.
“Baadaye nilikwenda Moshi kwenye msiba wa baba, niliporudi Dar nilimaliza siku moja tu, nikaripoti kazini. Nikiwa kazini Novemba 11, mwaka huu nikapigiwa simu na jirani kwamba nyumba yangu inabomolewa na greda, alifikiri kwamba nimeshaonana na Mchungaji Rwakatare na kukubaliana naye.
“Nilikwenda kule, kufika nikakuta hakuna jengo! Nilidondoka chini, sikujua kilichoendelea, nilipoteza fahamu, nilijitambua nikiwa Zahanati ya Mico.
“Kinachoniumiza sana ni kitendo cha
kuvunjiwa nyumba yangu bila kushirikishwa, bora hata angenifungulia
mashitaka kama anaona nilivamia kikwanja chake.”
“Yeye ana uwezo, ana ghorofa ya zaidi ya shilingi bilioni moja iweje anionee na kunivunjia mimi maskini niliyejenga kwa fedha za mkopo?
“Kituo cha polisi nilifika karibu mara nne lakini mpaka leo hii
sijapewa mpelelezi wala hawajafika eneo la tukio, nataka sheria ichukue
mkondo wake.”“Yeye ana uwezo, ana ghorofa ya zaidi ya shilingi bilioni moja iweje anionee na kunivunjia mimi maskini niliyejenga kwa fedha za mkopo?
Mwandishi alifika katika eneo la tukio na kushuhudia kifusi kinachodaiwa kuwa ni iliyokuwa nyumba ya Grayson iliyovunjwa na imezungushiwa ukuta na geti kupigwa kufuli.
Hata hivyo, Uwazi lilifika katika Ofisi za
Serikali ya Mtaa wa Bunju ‘B’ na kuonana na mtendaji Abdallah Mkeyenge
ambaye alikiri kuwepo kwa mvutano baina ya watu hao.“Hii barua ya
makubaliano ya kuuziwa Grayson kiwanja inaonekana imetoka ofisini hapa
lakini mimi kipindi hicho nilikuwa sijahamia ofisi hii.
“Ninachokumbuka kuna kipindi Mchungaji Rwakatare alikuja na milioni
tano kuwapa Grayson na mtu mwingine yaani kuwapoza lakini walikataa
kuzichukua,” alisema mtendaji huyo.Mchungaji Rwakatare alipopigiwa simu kuhusiana na madai hayo alisema yupo bungeni hivyo alimwagiza msaidizi wake, Jerad Abeid kuzungumzia sakata hilo ambapo alisema eneo hilo mchungaji analimiliki tangu mwaka 2005 na hati ziko ardhi Wilaya ya Kinondoni. Alibomoa nyumba ya Grayson akijua ni eneo lake la siku nyingi.
“Unajua katika maeneo hayo kuna watu walikuwa wakishirikiana na ofisi za mtaa kuuza kiwanja cha mchungaji kwa siri na tayari watu wanne walishauziwa lakini walikuwa hawajajenga, mchungaji aliamua kuwapoza kiubinadamu na wameshaondoka bado watu wawili akiwemo huyo Grayson,” alisema Jerad.
SOMA JINSI ZITTO KABWE ALIVYOPANGUA MASHAMBULIZI YALIYODHAMILIA KUMUINGIZA KWENYE WIZI WA MABILIONI YA ESCROW

Nashambuliwa, tunashambuliwa! PAC tunasema “Hatutetereki”
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya Kamati ninayoongoza ya PAC kuwasilisha Bungeni Taarifa Maalumu kuhusu ukaguzi maalumu wa akaunti ya Tegeta Escrow, kumekuwa na kampeni za chini chini zinazoendeshwa kwenye korido za Bunge na kwenye mitandao dhidi yangu binafsi na baadhi ya wabunge waliosimama kidete dhidi ya wizi wa fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania akaunti ya Escrow.
Baadhi ya tuhuma nimezipeleka kwenye vyombo vya dola ili zichunguzwe kwani zina vielelezo vya mahala pa kuanzia (kama leseni ya udereva ya mwanamke anajulikana kama Vivian Emmanuel Sirikwa na muhuri wa kampuni ya uwakili inayomilikiwa na Bwana Joseph Mkandege).
Baadhi ya Tuhuma
Baadhi ya tuhuma nitazijibu moja baada ya moja.
Waziri mmoja ambaye ni mtuhumiwa wa wizi wa fedha za Tegeta Escrow anazunguka kwa wabunge akisema tuhuma hizi kupikwa kama njia yake ya kuhamisha mjadala kutoka uporaji wa Tshs 200 bilioni kwenda kwenye masuala binafsi.
Tuhuma hizi zenye kichwa cha habari “Zitto na Filikunjombe wanatumiwa na Kenya na Uingereza kuvuruga na kudhoofisha Uwekezaji nchini mwetu” zinajibiwa hapa chini. Utaona ndugu Filikunjombe ametajwa kwa kichwa cha habari ili kumtaja tu bila sababu yeyote ile.
Tuhuma #1:
Zitto anaye rafiki yake Mkenya aitwae Rapahel Ongangi ambao kwa pamoja wameanzisha Gombe Advisors Co. Ltd (registered on 24 November 2011, Certificate No 87387) kwa ajili ya kufanya biashara na Makampuni ya Gesi na Mafuta yanayofanya kazi nchini hapa.
Majibu:
Gombe Advisors ni kampuni binafsi isiyofanya faida yaani ‘Company Limited by Guarantee’. Haina kazi na kampuni yoyote ya Gesi na Mafuta na wala yenyewe haijuhusishi na biashara hiyo. Gombe advisors haijafanya kazi yoyote ile na kampuni nyingine zaidi ya kusaidia wasanii wa kundi la Kigoma All stars. Upotoshaji hapa unalenga kupindisha mjadala.
Tuhuma #2:
Zitto amemsaidia Ongangi kupata uraia wa Tanzania na kwa sasa ni raia wa pasipoti. Zitto na Ongangi walimtafutia CEO wa Shell aitwae Axel Knospe nyumba na gari ya kukodi.
Majibu:
Raphael ni mtu binafsi ambaye anafanya shughuli zake hapa nchini, amesoma hapa nchini na ameoa na ana mtoto. Tuhuma hizi hazina msingi wowote ule maana ni uwongo. Wanaotoa tuhuma hizi waonyeshe hiyo pasipoti ya Bwana Ongangi kuthibitisha madai yao.
Tuhuma #3:
Mikataba ya STATOIL iliyokuwa inarushwa kwenye mitandao ya jamii na kuchapishwa kwenye magazeti ya Kenya ya hapa nchini (The Citizen na Mwananchi) mwandishi mkuu alikuwa huyo CEO wa Shell.
Majibu:
Mkataba uliovujishwa wa StatOil ulivujishwa na waandishi wa habari wa Norway. Uchambuzi wa mkataba huo nimeufanya mwenyewe kwa kutumia utaalamu wangu niliosomea wa kuchambua mifumo ya kodi kwenye sekta ya mafuta na gesi. Kwa namna yoyote ile, huyo anayetajwa kuwa CEO wa kampuni ya Shell hahusiki. Tuhuma hii wanaoitoa watoe ushahidi usio na chembe ya mashaka.
Ikumbukwe kuwa mkataba wa StatOil utaipotezea Tanzania mapato ya dola za Marekani bilioni 12 (takribani Tshs 20,400,000,000,000/=) katika kipindi cha miaka 15 baada ya gesi kuanza kuchimbwa.
Uamuzi wa Kamati ya PAC kutaka mikataba yote ya Gesi kuwa wazi una lengo la kuchambua kuona kama mikataba yote nchini haipotezi mapato kwa nchi. Uamuzi huo umewakasirisha sana baadhi ya waliohusika kuingia mikataba Serikalini maana wanajua kuna madudu kwenye mikataba na wanataka umma wa watanzania usijue!
Tuhuma #4:
Kampuni ya SHELL imechukizwa sana kucheleweshwa kwa kupata kibali cha kutafuta gesi na mafuta kule Pemba. Vilevile SHELL haina uwekezaji mkubwa Tanzania Bara kwani ilishindwa kwenye tenda zenye vitalu vyenye gesi nyingi upande wa Bara.
Majibu:
Ukweli ni kuwa Kampuni ya Shell ina vitalu 4 huko Zanzibar na tayari ina makubaliano na Serikali ya Zanzibar kuhusu utafutaji mafuta huko katika vitalu namba 9,10,11 na 12. Shell inafanya kazi na kampuni ya Petrobras ya Brazil kwenye kitalu namba 6 na namba 8. Taarifa hizi zipo wazi kwenye tovuti ya TPDC. Tuhuma nyepesi namna hii dhidi ya kampuni kubwa kama Shell zinaonyesha dharau na kiburi kinachotokana na uelewa mdogo wa mambo wa watu wanaotuhumu.
Tuhuma 5:
Ongangi anapokea maelekezo kutoka Serikali ya Kenya kuhujumu uwekezaji nchini mwetu.
Majibu:
Nazifahamu mbinu nyingi zinazotumika kufanya propaganda, lakini mbinu hii imeshindwa ikiwa mapema sana. Ni vema wanaotoa tuhuma hizi wazithibitishe vinginevyo ni mwendelezo wa propaganda zisozingatia diplomasia ndani yake dhidi ya jirani zetu wa Kenya. Hizi ni propaganda hatari ambazo hata hao wanaotuhumiwa wakisikia watatudharau sana.
Tuhuma #6 (juu ya Uingereza):
Uingereza imekuwa inamfadhili Zitto kwa miaka mingi kwa mambo yake ya kisiasa kwa hiyo sasa hivi Ubalozi wa Uingereza unamlipa Zitto na Kafulila kuhakikisha kwamba Standard Chartered ya Uingereza inalipwa deni lake lisilotambulika kisheria nchini mwetu.
Majibu:
Nimetangulia kusema hapo awali kuwa kuna propaganda ambazo haziangalii hata diplomasia; nyingine ni hii. Pamoja na kukanusha uzushi huu, ni vizuri wanaotoa tuhuma za namna hii kuthibitisha. Mimi binafsi sijawahi kufadhiliwa kisiasa na Taifa lolote lile. Inaelekea kuna wanasiasa wanaofadhiliwa na mataifa mengine ambao kwakuwa kwao ndiyo maisha wanaamini na wengine tupo kama walivyo.
Kwangu itikadi yangu ni ‘Uzalendo kwa nchi yangu’, ni jambo ambalo halina mbadala wake. Siku zote nasema “Right or wrong, my country first”.
Kurudia kurusha tuhuma kwa Ubalozi wa Uingereza nchini ni kudhihirisha kwa mara nyingine kiburi cha kuwa na mamlaka (arrogance of power) walicho nacho wanaotuma tuhuma hizi.
Aidha, wanatuhumu kuwa “Kafulila na Zitto wamehaidiwa 15% ya USD 150 million kama deni likilipwa”
Mtanzania anayeweza propaganda dhaifu kama hizi basi anatakiwa ajitafakari. Hata hivyo ni vema wanaotoa tuhuma hizi wathibitishe bila chembe ya mashaka.
Tuhuma #7:
Mbunge Mkono nae ameshikwa hasira kupoteza kazi ya uwakili pale TANESCO. Kafulila na Zitto wanalipwa na Mkono kuvuruga Serikali kwa hasira za kukosa fedha za kitapeli za TANESCO.
Majibu:
Hizi ni tuhuma ambazo sasa tumezizoea kutolewa. Mambo mepesi hayawezi kujibu mambo ya msingi kama tuhuma za wizi wa fedha zaidi ya Tshs bilioni 200 kutoka Benki kuu ya Tanzania. Kukusanya kila propaganda ili kuuhamisha umma ni kupungukiwa hekima na busara.
Aidha, wanaotuhumu wanadokeza kuwa “Naomba tuwe macho na Wabunge wetu achananeni na madai ya Zitto ya wizi. Huyu mtu anafanya biashara na Kampuni ya SHELL na inasemekana analipwa na Ubalozi wa Uingereza. Serikali ya Kenya na tapeli mkubwa Mbunge Mkono nae anawalipa Zitto na Kafulila”.
Watanzania, haya ni maneno ya hasira ya watu wanaokaribia kukamatwa kwa kushiriki wizi wa fedha katika Benki kuu ya Tanzania. Kamwe tuhuma kama hizi haziwezi kutukatisha tamaa katika kupambana ili ukweli ujulikane. Sisi tutapigana kwa ajili ya Taifa, kwa ajili ya mtanzania na tunachotaka ni umma uujue ukweli wa mambo.
Hasira hizi zinatokana na mambo mawili:
Moja ni uamuzi wa kamati ya PAC kuwasweka ndani baadhi ya watendaji wa TPDC kwa kushindwa kutekeleza maamuzi ya Kamati yanayohusu uwazi wa mikataba ya Gesi na Mafuta.
Pili, ni uamuzi wa PAC kuagiza ukaguzi maalumu wa mchakato mzima wa kuanzishwa na kufungwa kwa akaunti ya Tegeta Escrow ambapo zaidi ya shilingi bilioni 200 ziliporwa na zaidi ya shilingi bilioni 12 zinalipwa na TANESCO kila mwezi kwenda kampuni ya PAP inayomilikiwa na Harbinder Singh Seth (50%) na watu wasiojulikana kupitia kampuni ya Simba Trust iliyosajiliwa na kufichwa nchini Australia (50%).
Ieleweke kuwa PAP inalipwa shilingi milioni 400 kila siku kutoka TANESCO izalishe au isizalishe Umeme! Watanzania, PAP itaendelea kulipwa namna hiyo kwa miaka 20 ijayo. Kwa namna ambayo Seth analindwa na baadhi ya watendaji Serikalini na hasa ndani ya Wizara ya Nishati na Madini. Aidha, kuna fununu kuwa kuna maofisa serikalini wanaomiliki hizo 50% za kampuni ya PAP. Seth pia anamiliki kitalu cha gesi Mnazi bay Kaskazini kupitia kampuni ya HydroTanz.
Hasira hizi walizo nazo wanaonituhumu na Kamati yangu zimewapelekea kugushi nyaraka mbalimbali zinazonituhumu mimi na wenzangu ili kutuogopesha na kutukatisha tamaa katika kutafuta ukweli juu ya suala la uporaji wa fedha kutoka Benki kuu. Lengo lao ni kututoa kwenye mstari. Mimi na wenzangu hatutatoka kwenye mstari, tutashirikiana na wabunge wenzetu kuhakikisha ukweli unajulikana na wezi kuchukuliwa hatua kali.
Harbinder Singh Seth aliiangusha Serikali ya KANU nchini Kenya, sasa anachotaka kukifanya kinaweza kuiangusha Serikali ya CCM wakiendelea kumkumbatia.
Watanzania sio mabwege!
Zitto Kabwe
Mwenyekiti PAC
Dodoma, 9 Novemba 2014
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya Kamati ninayoongoza ya PAC kuwasilisha Bungeni Taarifa Maalumu kuhusu ukaguzi maalumu wa akaunti ya Tegeta Escrow, kumekuwa na kampeni za chini chini zinazoendeshwa kwenye korido za Bunge na kwenye mitandao dhidi yangu binafsi na baadhi ya wabunge waliosimama kidete dhidi ya wizi wa fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania akaunti ya Escrow.
Baadhi ya tuhuma nimezipeleka kwenye vyombo vya dola ili zichunguzwe kwani zina vielelezo vya mahala pa kuanzia (kama leseni ya udereva ya mwanamke anajulikana kama Vivian Emmanuel Sirikwa na muhuri wa kampuni ya uwakili inayomilikiwa na Bwana Joseph Mkandege).
Baadhi ya Tuhuma
Baadhi ya tuhuma nitazijibu moja baada ya moja.
Waziri mmoja ambaye ni mtuhumiwa wa wizi wa fedha za Tegeta Escrow anazunguka kwa wabunge akisema tuhuma hizi kupikwa kama njia yake ya kuhamisha mjadala kutoka uporaji wa Tshs 200 bilioni kwenda kwenye masuala binafsi.
Tuhuma hizi zenye kichwa cha habari “Zitto na Filikunjombe wanatumiwa na Kenya na Uingereza kuvuruga na kudhoofisha Uwekezaji nchini mwetu” zinajibiwa hapa chini. Utaona ndugu Filikunjombe ametajwa kwa kichwa cha habari ili kumtaja tu bila sababu yeyote ile.
Tuhuma #1:
Zitto anaye rafiki yake Mkenya aitwae Rapahel Ongangi ambao kwa pamoja wameanzisha Gombe Advisors Co. Ltd (registered on 24 November 2011, Certificate No 87387) kwa ajili ya kufanya biashara na Makampuni ya Gesi na Mafuta yanayofanya kazi nchini hapa.
Majibu:
Gombe Advisors ni kampuni binafsi isiyofanya faida yaani ‘Company Limited by Guarantee’. Haina kazi na kampuni yoyote ya Gesi na Mafuta na wala yenyewe haijuhusishi na biashara hiyo. Gombe advisors haijafanya kazi yoyote ile na kampuni nyingine zaidi ya kusaidia wasanii wa kundi la Kigoma All stars. Upotoshaji hapa unalenga kupindisha mjadala.
Tuhuma #2:
Zitto amemsaidia Ongangi kupata uraia wa Tanzania na kwa sasa ni raia wa pasipoti. Zitto na Ongangi walimtafutia CEO wa Shell aitwae Axel Knospe nyumba na gari ya kukodi.
Majibu:
Raphael ni mtu binafsi ambaye anafanya shughuli zake hapa nchini, amesoma hapa nchini na ameoa na ana mtoto. Tuhuma hizi hazina msingi wowote ule maana ni uwongo. Wanaotoa tuhuma hizi waonyeshe hiyo pasipoti ya Bwana Ongangi kuthibitisha madai yao.
Tuhuma #3:
Mikataba ya STATOIL iliyokuwa inarushwa kwenye mitandao ya jamii na kuchapishwa kwenye magazeti ya Kenya ya hapa nchini (The Citizen na Mwananchi) mwandishi mkuu alikuwa huyo CEO wa Shell.
Majibu:
Mkataba uliovujishwa wa StatOil ulivujishwa na waandishi wa habari wa Norway. Uchambuzi wa mkataba huo nimeufanya mwenyewe kwa kutumia utaalamu wangu niliosomea wa kuchambua mifumo ya kodi kwenye sekta ya mafuta na gesi. Kwa namna yoyote ile, huyo anayetajwa kuwa CEO wa kampuni ya Shell hahusiki. Tuhuma hii wanaoitoa watoe ushahidi usio na chembe ya mashaka.
Ikumbukwe kuwa mkataba wa StatOil utaipotezea Tanzania mapato ya dola za Marekani bilioni 12 (takribani Tshs 20,400,000,000,000/=) katika kipindi cha miaka 15 baada ya gesi kuanza kuchimbwa.
Uamuzi wa Kamati ya PAC kutaka mikataba yote ya Gesi kuwa wazi una lengo la kuchambua kuona kama mikataba yote nchini haipotezi mapato kwa nchi. Uamuzi huo umewakasirisha sana baadhi ya waliohusika kuingia mikataba Serikalini maana wanajua kuna madudu kwenye mikataba na wanataka umma wa watanzania usijue!
Tuhuma #4:
Kampuni ya SHELL imechukizwa sana kucheleweshwa kwa kupata kibali cha kutafuta gesi na mafuta kule Pemba. Vilevile SHELL haina uwekezaji mkubwa Tanzania Bara kwani ilishindwa kwenye tenda zenye vitalu vyenye gesi nyingi upande wa Bara.
Majibu:
Ukweli ni kuwa Kampuni ya Shell ina vitalu 4 huko Zanzibar na tayari ina makubaliano na Serikali ya Zanzibar kuhusu utafutaji mafuta huko katika vitalu namba 9,10,11 na 12. Shell inafanya kazi na kampuni ya Petrobras ya Brazil kwenye kitalu namba 6 na namba 8. Taarifa hizi zipo wazi kwenye tovuti ya TPDC. Tuhuma nyepesi namna hii dhidi ya kampuni kubwa kama Shell zinaonyesha dharau na kiburi kinachotokana na uelewa mdogo wa mambo wa watu wanaotuhumu.
Tuhuma 5:
Ongangi anapokea maelekezo kutoka Serikali ya Kenya kuhujumu uwekezaji nchini mwetu.
Majibu:
Nazifahamu mbinu nyingi zinazotumika kufanya propaganda, lakini mbinu hii imeshindwa ikiwa mapema sana. Ni vema wanaotoa tuhuma hizi wazithibitishe vinginevyo ni mwendelezo wa propaganda zisozingatia diplomasia ndani yake dhidi ya jirani zetu wa Kenya. Hizi ni propaganda hatari ambazo hata hao wanaotuhumiwa wakisikia watatudharau sana.
Tuhuma #6 (juu ya Uingereza):
Uingereza imekuwa inamfadhili Zitto kwa miaka mingi kwa mambo yake ya kisiasa kwa hiyo sasa hivi Ubalozi wa Uingereza unamlipa Zitto na Kafulila kuhakikisha kwamba Standard Chartered ya Uingereza inalipwa deni lake lisilotambulika kisheria nchini mwetu.
Majibu:
Nimetangulia kusema hapo awali kuwa kuna propaganda ambazo haziangalii hata diplomasia; nyingine ni hii. Pamoja na kukanusha uzushi huu, ni vizuri wanaotoa tuhuma za namna hii kuthibitisha. Mimi binafsi sijawahi kufadhiliwa kisiasa na Taifa lolote lile. Inaelekea kuna wanasiasa wanaofadhiliwa na mataifa mengine ambao kwakuwa kwao ndiyo maisha wanaamini na wengine tupo kama walivyo.
Kwangu itikadi yangu ni ‘Uzalendo kwa nchi yangu’, ni jambo ambalo halina mbadala wake. Siku zote nasema “Right or wrong, my country first”.
Kurudia kurusha tuhuma kwa Ubalozi wa Uingereza nchini ni kudhihirisha kwa mara nyingine kiburi cha kuwa na mamlaka (arrogance of power) walicho nacho wanaotuma tuhuma hizi.
Aidha, wanatuhumu kuwa “Kafulila na Zitto wamehaidiwa 15% ya USD 150 million kama deni likilipwa”
Mtanzania anayeweza propaganda dhaifu kama hizi basi anatakiwa ajitafakari. Hata hivyo ni vema wanaotoa tuhuma hizi wathibitishe bila chembe ya mashaka.
Tuhuma #7:
Mbunge Mkono nae ameshikwa hasira kupoteza kazi ya uwakili pale TANESCO. Kafulila na Zitto wanalipwa na Mkono kuvuruga Serikali kwa hasira za kukosa fedha za kitapeli za TANESCO.
Majibu:
Hizi ni tuhuma ambazo sasa tumezizoea kutolewa. Mambo mepesi hayawezi kujibu mambo ya msingi kama tuhuma za wizi wa fedha zaidi ya Tshs bilioni 200 kutoka Benki kuu ya Tanzania. Kukusanya kila propaganda ili kuuhamisha umma ni kupungukiwa hekima na busara.
Aidha, wanaotuhumu wanadokeza kuwa “Naomba tuwe macho na Wabunge wetu achananeni na madai ya Zitto ya wizi. Huyu mtu anafanya biashara na Kampuni ya SHELL na inasemekana analipwa na Ubalozi wa Uingereza. Serikali ya Kenya na tapeli mkubwa Mbunge Mkono nae anawalipa Zitto na Kafulila”.
Watanzania, haya ni maneno ya hasira ya watu wanaokaribia kukamatwa kwa kushiriki wizi wa fedha katika Benki kuu ya Tanzania. Kamwe tuhuma kama hizi haziwezi kutukatisha tamaa katika kupambana ili ukweli ujulikane. Sisi tutapigana kwa ajili ya Taifa, kwa ajili ya mtanzania na tunachotaka ni umma uujue ukweli wa mambo.
Hasira hizi zinatokana na mambo mawili:
Moja ni uamuzi wa kamati ya PAC kuwasweka ndani baadhi ya watendaji wa TPDC kwa kushindwa kutekeleza maamuzi ya Kamati yanayohusu uwazi wa mikataba ya Gesi na Mafuta.
Pili, ni uamuzi wa PAC kuagiza ukaguzi maalumu wa mchakato mzima wa kuanzishwa na kufungwa kwa akaunti ya Tegeta Escrow ambapo zaidi ya shilingi bilioni 200 ziliporwa na zaidi ya shilingi bilioni 12 zinalipwa na TANESCO kila mwezi kwenda kampuni ya PAP inayomilikiwa na Harbinder Singh Seth (50%) na watu wasiojulikana kupitia kampuni ya Simba Trust iliyosajiliwa na kufichwa nchini Australia (50%).
Ieleweke kuwa PAP inalipwa shilingi milioni 400 kila siku kutoka TANESCO izalishe au isizalishe Umeme! Watanzania, PAP itaendelea kulipwa namna hiyo kwa miaka 20 ijayo. Kwa namna ambayo Seth analindwa na baadhi ya watendaji Serikalini na hasa ndani ya Wizara ya Nishati na Madini. Aidha, kuna fununu kuwa kuna maofisa serikalini wanaomiliki hizo 50% za kampuni ya PAP. Seth pia anamiliki kitalu cha gesi Mnazi bay Kaskazini kupitia kampuni ya HydroTanz.
Hasira hizi walizo nazo wanaonituhumu na Kamati yangu zimewapelekea kugushi nyaraka mbalimbali zinazonituhumu mimi na wenzangu ili kutuogopesha na kutukatisha tamaa katika kutafuta ukweli juu ya suala la uporaji wa fedha kutoka Benki kuu. Lengo lao ni kututoa kwenye mstari. Mimi na wenzangu hatutatoka kwenye mstari, tutashirikiana na wabunge wenzetu kuhakikisha ukweli unajulikana na wezi kuchukuliwa hatua kali.
Harbinder Singh Seth aliiangusha Serikali ya KANU nchini Kenya, sasa anachotaka kukifanya kinaweza kuiangusha Serikali ya CCM wakiendelea kumkumbatia.
Watanzania sio mabwege!
Zitto Kabwe
Mwenyekiti PAC
Dodoma, 9 Novemba 2014
Subscribe to:
Posts (Atom)
