Tuesday, September 23, 2014

WANANCHI WATAKA KUFANYA MAANDAMANO BAADA YA OFISI YAO KUWEKWA KWENYE KILABU CHA POMBE, RUNGWE,

WANANCHI wa Kata ya Kawetele Tarafa ya Tukuyu mjini wilayani Rungwe Mkoani Mbeya wanatarajia  kufanya maandamano  ya amani hadi kwenye ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kupinga hatua ya ofisi yao kuwekwa kwenye kirabu cha pombe.
Wakizungumza jana na  Yetu rungwe  blog kwa nyakati tofauti wamedai kitendo cha ofisi ya serikali kuwa katikati ya kirabu cha pombe na kumbi za starehe kimeshusha hadhi ya mji wa Tukuyu ambao ndiyo makao makuu ya wilaya hiyo.
Walida kuwa asilimia ishirini ya wananchi wa kata hiyo ni walokole hivyo wanakosa kupata huduma za kiofisi kutokana na mazingira mabaya ya kiofisi yalivyo hivyo hulazimika kupata huduma za kiofisi kwenye kata za mbali kinyume na taratibu.
Wananchi hao ambao hawakutaka majina yao yaandikwe gazetini walisema madai yao yakuomba ofisi kwa mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Veronika Kessy yamegonga mwamba na kudai kuwa wamepanga kufanya maandamano ya amani wakitaka kupatiwa ofisi.
Afisa mtendaji wa Kata hiyo Niklaus Kosama alikiri kuwepo na hali hiyo na kudai kuwa yeye ameletwa kufanya kazi katika kata hiyo  na hana mamlaka ya kupinga ofisi kuwepo mahali hapo.
Anyimike Mwasakilali diwani wa Kata hiyo mbali na kukiri kuwepo kwa hali hiyo pia alidai kuwa alipeleka maombi ya kupatiwa ofisi kwa mwenyekiti wa Halmashauri na mkurugenzi wa halmashauri hiyo  lakini alikuwa akipigwa dana dana
Alisema afisa utumishi wilayani humo alimueleza kuwa amempa barua ya kuhama mtumishi anayeishi nyumba no,RDC/RHB/BLD/08 kuwa mwezi wa 11 mwaka huu mtumishi huyo atahama na nyumba hiyo itafanyika kuwa ofisi ya kata.
 Yetu rungwe  ilimulika   hadi  kwenye nyumba hiyo kujiridhisha kana kwamba ni kweli mtumishi huyo wa Idara ya maji kama kapewa barua ya kuhama,ambapo alikanusha kuwa hajawahi kupewa barua ya kuhama na wala hata kwa mdomo.

Alfredy Mwakipiki mwenyekiti wa Halmasahuri hiyo kwa upande wake alisema anachokijua ni kuwa wananchi wa kata hiyo walifanya harambee ya kutaka fedha kwa ajili ya ununuzi wa uwanja na wao watawasapoti pindi watakapo jenga hadi mtambaa wa panya.
Alisema Halmashauri ya Rungwe magharibi inakata 20 na imekuwa ikishindwa kujenga kwa wakati ofisi za kata kutokana na bajeti ndogo,hivyo suala la ofisi katika kata hiyo litapewa kipawa mbele pindi wapatapo bajeti.  








































No comments:

Post a Comment