Thursday, November 6, 2014

JAMAA ADAIWA KURUBUNI WAKE ZA WATU KINGONO ANASWA

Wakinamama (kushoto) wakimficha mwenzao (mke wa mtu) aliyenaswa kwenye ghetto la njemba mwenye asili ya Kiarabu, Hemed.

Mji wa Morogoro umekumbwa na matukio mfululizo ya mafumanizi ambapo baada ya ticha wa shule ya msingi kufumaniwa na dereva wa bodaboda kisha jamaa kubondwa kwa kukutwa akifanya ngono na mke wa mtu vichakani na denti wa upadri kufumaniwa, mwanzoni mwa wiki hii fumanizi lingine kiboko la njemba mwenye asili ya Kiarabu limetokea.Kwenye Kata ya Mazimbu mjini hapa mwanaume aliyefahamika kwa jina moja la Hemed, anadaiwa kunaswa laivu na mke wa mtu kwenye chumba anachoishi kilichopo Mtaa wa Boma mjini hapa.
Ikiwa kazini, Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers ilinyetishiwa kuwepo kwa ishu hiyo hivyo kufika eneo la tukio ndani ya dakika sifuri na kunasa tukio hilo likiwa bichi.
Wakinamama hao wakifanya juhudi kumtoa mke wa mtu (mwenye sidiria) eneo la tukio.
Katika fumanizi hilo lililojaza ‘inzi’ (umati), Hemed alidaiwa kuwa amekuwa na tabia ya kuwarubuni na kumwaga fedha mbuzi kwa wake za watu na kuserebuka nao ndani ya ‘geto’ lake jambo lililowafanya wenye wake zao kumwekea mtego ambao ulipofyatuka ukamnasa majira ya saa 3:00 asubuhi.
Akihojiwa na gazeti hili, mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo alisema kuwa, jamaa huyo alikuwa na mwanamke mzuri wa umbo aliyetajwa kwa jina moja la Husna ambaye alikutwa chumbani kwa Hemed.
Mashuhuda wa tukio hilo wakipiga chabo dirishani kwa mwarabu aliyenaswa.
Akizungumza na mwanahabari wetu kwenye eneo la tukio, mume wa Husna aliyejitambulisha kwa jina moja la Siri alikuwa na haya ya kusema:
“Nilimuaga mke wangu nakwenda Mwanza kwenye shughuli zangu za biashara. Nikiwa Mwanza nilijulishwa na majirani kwamba mke wangu kila siku anaacha watoto wetu kwa mama yake na kwenda kulala kwa Mwarabu.
Raia wenye Hasira kali wakiwa eneo la tukio.
“Ukweli kama mwanaume nilipatwa na hasira, nikatafuta ndege nikarudi hapa (Morogoro).
“Nimeelekezwa kwa Mwarabu na jamaa waliokuwa wamemwekea mtego, nilipofika nilichungulia dirishani, nikamuona mke wangu na Mwarabu wakiwa kitandani.
“Nilihisi kupooza mwili na roho ilikuwa inaniuma sana.”
Mwarabu(mwenye koti jekundu) aliyenaswa na mke wa mtu akiwa chini ya ulinzi.
Aliongeza: “Mimi na mke wangu tumefunga ndoa ya Kiislamu, tuna watoto wawili, mmoja ana umri wa miaka mitano na wa pili ana mwaka mmoja na miezi saba.
“Cha ajabu mtoto wa pili hadi sasa hatembei. Kwa tukio kama hili nahisi mke wangu amembembenda.”
Mtuhumiwa (mwarabu) akichukuliwa kwa mahojiano zaidi.
Kwa upande wake Husna ambaye alisitiriwa na wanawake wenzake waliokuwa wakimficha, alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo, alimjia juu mwanahabari wetu na kumtolea maneno ya shombo. 
Naye Mwarabu huyo alipohojiwa, pia alimtolea vitisho ‘kamanda’ wetu.
Kufuatia wingi wa watu, wawili hao walifungiwa chumbani lakini raia wenye hasira kali wakavunja mlango na kuwashushia kichapo.
Baadaye viongozi wa Kata ya Mazimbu wakiongozwa na Afisa Mtendaji, Brioht Sospeter na polisi mmoja walifika eneo la tukio wakawaondoa wawili hao na kuwapeleka ofisi ya kata kwa mahojiano zaidi.

No comments:

Post a Comment